Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Esaïe 19.7
Bible en Swahili de l’est


Prophétie sur l’Égypte

1 Ufunuo juu ya Misri. Tazama, Bwana amepanda juu ya wingu jepesi, anafika Misri; na sanamu za Misri zinatikisika mbele zake, na moyo wa Misri unayeyuka ndani yake.
Joël 3.19 Josué 2.11 Exode 12.12 Apocalypse 1.7 Ezéchiel 30.13
2 Nami nitawaamsha Wamisri juu ya Wamisri; nao watapigana, kila mtu na ndugu yake, na kila mtu na jirani yake, mji juu ya mji, na ufalme juu ya ufalme.
Juges 7.22 1 Samuel 14.20 Ezéchiel 38.21 Apocalypse 17.12-17.17 Matthieu 10.21
3 Na roho ya Misri itamwagika kabisa katikati yake, nami nitayabatilisha mashauri yake, nao watakwenda kwa sanamu zao, na kwa waganga, na kwa wapiga ramli, na kwa wachawi.
Esaïe 8.19 Daniel 2.2 1 Chroniques 10.13 Esaïe 15.2 Daniel 4.6-4.7
4 Nami nitawatoa hao Wamisri na kuwatia katika mikono ya bwana mgumu; na mfalme mkali atawatawala; asema Bwana, Bwana wa majeshi.
Ezéchiel 29.19 Jérémie 46.26 Esaïe 20.4 1 Samuel 23.7 Psaumes 31.8
5 Na maji ya baharini yatapunguka, na huo mto utakauka na kuwa pakavu.
Jérémie 51.36 Ezéchiel 30.12 Zacharie 10.11 Zacharie 14.18
6 Na vijito vya mto vitatoa uvundo, na mifereji ya Misri itakuwa haina maji mengi, itakauka; manyasi na mianzi itanyauka.
Esaïe 37.25 Exode 2.3 Job 8.11 Esaïe 15.6 Exode 7.18
7 Vitu vimeavyo karibu na Nile, katika ukingo wa Nile, na vyote vilivyopandwa karibu na Nile vitakauka na kuondolewa na kutoweka.
Esaïe 32.20 Jérémie 14.4 Joël 1.17-1.18 Esaïe 23.3 Ezéchiel 19.13
8 Na wavuvi wataugua, na wote wavuao kwa ndoana watahuzunika, nao watandao jarife juu ya maji watazimia.
Ezéchiel 47.10 Habakuk 1.15 Nombres 11.5 Exode 7.21
9 Tena wao wafanyao kazi ya kuchana kitani watafadhaika, na hao pia wafumao bafta.
Ezéchiel 27.7 Proverbes 7.16 1 Rois 10.28
10 Na nguzo za nchi zitavunjika vipande vipande, wote wafanyao kazi ya mshahara watahuzunika nafsini mwao.
Exode 7.19 Deutéronome 11.10 Exode 8.5
11 Wakuu wa Soani wamekuwa wapumbavu kabisa; washauri wenye hekima wa Farao, shauri lao limepumbazika; mwawezaje kumwambia Farao, Mimi ni mwana wa wenye hekima, ni mwana wa wafalme wa zamani?
Nombres 13.22 Psaumes 78.43 1 Rois 4.30 Esaïe 30.4 Actes 7.22
12 Wako wapi, basi, watu wako wenye hekima? Na wakuambie sasa; na wajue mambo aliyokusudia Bwana wa majeshi juu ya Misri.
1 Corinthiens 1.20 Esaïe 14.24 Esaïe 47.10-47.13 Romains 11.33-11.34 Job 11.6-11.7
13 Wakuu wa Soani wamekuwa wapumbavu, wakuu wa Nofu wamedanganyika; na hao walio mawe ya pembeni ya kabila zake wameikosesha Misri.
Ezéchiel 30.13 Jérémie 2.16 Jérémie 46.14 Zacharie 10.4 Jérémie 46.19
14 Yeye Bwana ametia roho ya ushupavu katika moyo wa Misri, nao wameikosesha Misri katika matendo yake yote, kama mlevi aendavyo huko na huko akitapika.
2 Thessaloniciens 2.11 Ezéchiel 14.7-14.9 1 Rois 22.20-22.23 Esaïe 47.10-47.11 Jérémie 25.27
15 Wala haitakuwako kazi yo yote katika Misri iwezayo kufanywa, ya kichwa au ya mkia, ya tawi au ya nyasi.
Esaïe 9.14-9.15 Habakuk 3.17 Aggée 1.11 1 Thessaloniciens 4.11-4.12 Proverbes 14.23
16 Katika siku hiyo Misri itakuwa kama wanawake; itatetemeka na kuogopa kwa sababu ya kutikiswa kwa mkono wa Bwana wa majeshi, autikisao juu yake.
Esaïe 11.15 Nahum 3.13 Jérémie 51.30 Jérémie 50.37 Esaïe 10.32
17 Na nchi ya Yuda itakuwa sababu ya utisho kwa Misri; kila mtu atakayeambiwa habari zake ataingiwa na woga, kwa sababu ya kusudi la Bwana wa majeshi, analolikusudia juu yake.
Esaïe 14.24 Daniel 4.35 Esaïe 20.2-20.5 Jérémie 25.19 Esaïe 46.10-46.11
18 Katika siku hiyo itakuwako miji mitano katika nchi ya Misri itumiayo lugha ya Kanaani, na kumwapia Bwana wa majeshi; mji mmoja utaitwa Mji wa uharibifu.
Sophonie 3.9 Zacharie 2.11 Esaïe 19.21 Esaïe 19.19 Esaïe 2.11
19 Katika siku hiyo itakuwako madhabahu katika nchi ya Misri kwa Bwana, na nguzo mpakani mwake kwa Bwana.
Genèse 28.18 Josué 22.10 Josué 22.26 Exode 24.4 Zacharie 6.15
20 Nayo itakuwa ishara na ushuhuda kwa Bwana wa majeshi katika nchi ya Misri; kwa maana watamlilia Bwana kwa sababu ya watu wawaoneao, naye atawapelekea mwokozi mwenye kuwatetea, naye atawaokoa.
Exode 2.23 Jacques 5.4 2 Rois 13.4-13.5 Esaïe 45.21-45.22 Esaïe 37.36
21 Na Bwana atajulikana na Misri, na Wamisri watamjua Bwana katika siku hiyo; naam watamtumikia kwa dhabihu na matoleo, nao watamwekea Bwana nadhiri, na kuzitekeleza.
Malachie 1.11 Esaïe 11.9 Habakuk 2.14 Ecclésiaste 5.4 Psaumes 98.2-98.3
22 Naye Bwana atapiga Misri, akipiga na kuponya; nao wakirudi kwa Bwana, atakubali maombi yao na kuwaponya.
Osée 14.1 Hébreux 12.11 Deutéronome 32.39 Esaïe 45.14 Esaïe 6.10
23 Katika siku hiyo itakuwako njia kuu itokayo Misri na kufika hata Ashuru; Mwashuri atafika Misri, na Mmisri atafika Ashuru, na Wamisri wataabudu pamoja na Waashuri.
Esaïe 11.16 Ephésiens 2.18-2.22 Esaïe 35.8-35.10 Esaïe 40.3-40.5 Esaïe 27.13
24 Katika siku hiyo Israeli atakuwa wa tatu pamoja na Misri na Ashuru, watakuwa baraka kati ya dunia;
Esaïe 65.8 Genèse 12.2 Esaïe 49.22 Zacharie 8.13 Esaïe 49.6
25 kwa kuwa Bwana wa majeshi amewabariki, akisema, Wabarikiwe watu wangu Misri; na wewe Ashuru, kazi ya mikono yangu; na wewe Israeli, urithi wangu.
Esaïe 29.23 Osée 2.23 Deutéronome 32.9 Esaïe 61.9 Psaumes 115.15

Cette Bible est dans le domaine public.