Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 23.13
Bible en Swahili de l’est


1 Utakapoketi kwa chakula pamoja na mtawala, Mwangalie sana yeye aliye mbele yako.
Jude 1.12 Genèse 43.32-43.34
2 Tena ujitie kisu kooni, Kama ukiwa mlafi.
1 Corinthiens 9.27 Philippiens 3.19 Matthieu 18.8-18.9
3 Usivitamani vyakula vyake vya anasa; Kwa maana ni vyakula vya hila.
Proverbes 23.6 Psaumes 141.4 Ephésiens 4.22 Luc 21.34 Daniel 1.8
4 Usijitaabishe ili kupata utajiri; Acha kuzitegemea akili zako mwenyewe.
Proverbes 3.5 Proverbes 28.20 Hébreux 13.5 Romains 12.16 Proverbes 26.12
5 Je! Utavikazia macho vile ambavyo si kitu? Maana bila shaka mali hujifanyia mabawa, Kama tai arukaye mbinguni.
Proverbes 27.24 1 Timothée 6.17 Jérémie 22.17 Psaumes 119.36-119.37 Genèse 42.36
6 Usile mkate wa mtu mwenye husuda; Wala usivitamani vyakula vyake vya anasa;
Psaumes 141.4 Deutéronome 15.9 Proverbes 23.3 Daniel 1.8-1.10 Proverbes 22.9
7 Maana aonavyo nafsini mwake, ndivyo alivyo. Akuambia, Haya, kula, kunywa; Lakini moyo wake hauwi pamoja nawe.
Psaumes 12.2 Juges 16.15 Psaumes 55.21 Luc 11.37-11.54 Luc 7.39
8 Tonge lile ulilokula utalitapika, Na maneno yako matamu yatakupotea.
9 Usiseme masikioni mwa mpumbavu; Maana atadharau hekima ya maneno yako.
Matthieu 7.6 Proverbes 26.4-26.5 Esaïe 36.21 1 Corinthiens 4.10-4.13 Jean 10.20
10 Usiiondoe alama ya mpaka wa zamani; Wala usiingie katika mashamba ya yatima;
Proverbes 22.28 Jérémie 22.3 Deutéronome 19.14 Zacharie 7.10 Job 24.9
11 Kwa sababu mkombozi wao ana nguvu; Atawatetea juu yako.
Proverbes 22.23 Job 19.25 Exode 22.22-22.24 Deutéronome 27.19 Jérémie 51.36
12 Elekeza moyo wako kusikiliza mafundisho; Tega masikio yako kusikia maneno ya maarifa.
Proverbes 2.2-2.6 Jacques 1.21-1.25 Ezéchiel 33.31 Matthieu 13.52 Proverbes 22.17
13 Usimnyime mtoto wako mapigo; Maana ukimpiga kwa fimbo hatakufa.
Proverbes 13.24 Proverbes 19.18 Proverbes 29.17 Proverbes 29.15
14 Utampiga kwa fimbo, Na kumwokoa nafsi yake na Kuzimu.
1 Corinthiens 5.5 1 Corinthiens 11.32 Proverbes 22.15

Appels d’un père à son fils

15 Mwanangu, kama moyo wako una hekima, Moyo wangu utafurahi, naam, moyo wangu;
Proverbes 23.24-23.25 Proverbes 29.3 3 Jean 1.3-1.4 2 Jean 1.4 Jean 21.5
16 Naam, viuno vyangu vitafurahi, Midomo yako inenapo maneno mema.
Proverbes 8.6 Ephésiens 4.29 Ephésiens 5.4 Colossiens 4.4 Jacques 3.2
17 Moyo wako usiwahusudu wenye dhambi; Bali mche Bwana mchana kutwa;
Proverbes 28.14 Proverbes 3.31 Proverbes 24.1 2 Corinthiens 7.1 Actes 9.31
18 Maana bila shaka iko thawabu; Na tumaini lako halitabatilika.
Jérémie 29.11 Proverbes 24.14 Psaumes 9.18 Psaumes 37.37 Philippiens 1.20
19 Sikia, mwanangu, uwe na hekima, Na kuuongoza moyo wako katika njia njema.
Proverbes 4.10-4.23 Proverbes 9.6 Proverbes 6.6 Proverbes 23.12 Proverbes 23.26
20 Usiwe miongoni mwao wanywao mvinyo; Miongoni mwao walao nyama kwa pupa.
Esaïe 5.22 Ephésiens 5.18 Romains 13.13 Proverbes 28.7 Esaïe 5.11
21 Kwa maana mlevi na mlafi huingia umaskini, Na utepetevu humvika mtu nguo mbovu.
Proverbes 21.17 Philippiens 3.19 Deutéronome 21.20 Proverbes 24.30-24.34 Joël 1.5
22 Msikilize baba yako aliyekuzaa, Wala usimdharau mama yako akiwa mzee.
Proverbes 1.8 Jean 19.26-19.27 Proverbes 6.20 Ephésiens 6.1-6.2 Proverbes 30.17
23 Inunue kweli, wala usiiuze; Naam, hekima, na mafundisho, na ufahamu.
Proverbes 18.15 Matthieu 13.44 Proverbes 16.16 Psaumes 119.72 Matthieu 13.46
24 Baba yake mwenye haki atashangilia; Naye amzaaye mtoto mwenye hekima atamfurahia.
Proverbes 10.1 Proverbes 15.20 Proverbes 23.15-23.16 1 Rois 1.48 Philémon 1.20
25 Na wafurahi baba yako na mama yako; Na afurahi aliyekuzaa.
Proverbes 17.25 Luc 1.31-1.33 Luc 1.58 Luc 1.40-1.47 1 Chroniques 4.9-4.10
26 Mwanangu, nipe moyo wako; Macho yako yapendezwe na njia zangu.
Psaumes 119.2 Matthieu 10.37-10.38 Psaumes 107.43 Psaumes 119.9-119.11 Deutéronome 6.5
27 Kwa maana kahaba ni shimo refu; Na malaya ni rima jembamba.
Proverbes 22.14
28 Naam, huotea kama mnyang’anyi; Huwaongeza wenye hila katika wanadamu.
Ecclésiaste 7.26 Proverbes 7.12 Jérémie 3.2 1 Corinthiens 10.8 Proverbes 9.18
29 Ni nani apigaye, Yowe? Ni nani aliaye, Ole? Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani mwenye mguno? Ni nani aliye na jeraha zisizo na sababu? Ni nani aliye na macho mekundu?
Esaïe 5.11 Esaïe 5.22 Ephésiens 5.18 Proverbes 23.21 2 Samuel 13.28
30 Ni wale wakaao sana kwenye mvinyo; Waendao kutafuta divai iliyochanganyika.
Psaumes 75.8 Esaïe 5.11 Ephésiens 5.18 Proverbes 9.2 Proverbes 20.1
31 Usiitazame mvinyo iwapo ni nyekundu; Iitiapo bilauri rangi yake, ishukapo taratibu;
Psaumes 119.37 Matthieu 5.28-5.30 2 Samuel 11.2 1 Jean 2.16 Proverbes 6.25
32 Mwisho wake huuma kama nyoka; Huchoma kama fira.
Amos 9.3 Job 20.16 Esaïe 59.5 Exode 7.5-7.6 Esaïe 28.3
33 Macho yako yataona mambo mageni; Na moyo wako utatoa yaliyopotoka.
Osée 7.5 Jude 1.12-1.13 Proverbes 2.12 Psaumes 69.12 Proverbes 31.5
34 Naam, utakuwa kama alalaye katikati ya bahari; Au kama yeye asinziaye juu ya mlingoti.
1 Thessaloniciens 5.2-5.7 1 Rois 20.16-20.22 Exode 15.8 2 Samuel 13.28 Luc 17.27-17.29
35 Utasema, Wamenichapa wala sikuumia; Wamenipiga wala sina habari; Nitaamka lini, nitazidi kuitafuta tena.
Esaïe 56.12 Jérémie 5.3 Proverbes 27.22 Proverbes 26.11 2 Pierre 2.22

Cette Bible est dans le domaine public.