Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 78.37
Bible en Swahili de l’est


Fidélité de Dieu au cours de l’histoire d’Israël

1 Enyi watu wangu, sikilizeni sheria yangu, Tegeni masikio kwa maneno ya kinywa changu.
Esaïe 51.4 Esaïe 55.3 Proverbes 8.4-8.6 Matthieu 13.9 Psaumes 51.4
2 Na nifunue kinywa changu kwa mithali, Niyatamke mafumbo ya kale.
Psaumes 49.4 Matthieu 13.34-13.35 Proverbes 1.6 Marc 4.34 Matthieu 13.11-13.13
3 Mambo tuliyoyasikia na kuyafahamu, Ambayo baba zetu walituambia.
Psaumes 44.1 Psaumes 48.8 Exode 13.8 Exode 13.14-13.15 Exode 12.26-12.27
4 Hayo hatutawaficha wana wao, Huku tukiwaambia kizazi kingine, Sifa za Bwana, na nguvu zake, Na mambo yake ya ajabu aliyoyafanya.
Deutéronome 11.19 Joël 1.3 Psaumes 145.4-145.6 Deutéronome 6.7 Josué 4.6-4.7
5 Maana alikaza ushuhuda katika Yakobo, Na sheria aliiweka katika Israeli. Aliyowaamuru baba zetu Wawajulishe wana wao,
Psaumes 81.5 Psaumes 147.19 Deutéronome 4.45 Ephésiens 6.4 Esaïe 8.20
6 Ili kizazi kingine wawe na habari, Ndio hao wana watakaozaliwa. Wasimame na kuwaambia wana wao
Psaumes 102.18 Psaumes 90.16 Psaumes 22.31 Psaumes 48.13 Josué 22.24-22.25
7 Wamwekee Mungu tumaini lao. Wala wasiyasahau matendo ya Mungu, Bali wazishike amri zake.
Deutéronome 5.29 Deutéronome 4.9 Deutéronome 6.12 1 Jean 3.22-3.24 Deutéronome 7.18-7.19
8 Naam, wasiwe kama baba zao, Kizazi cha ukaidi na uasi. Kizazi kisichojitengeneza moyo, Wala roho yake haikuwa amini kwa Mungu.
Psaumes 78.37 Exode 32.9 2 Rois 17.14 Ezéchiel 20.18 Deutéronome 31.27
9 Wale Waefraimu, wenye silaha, wapiga upinde, Walirudi nyuma siku ya vita.
1 Samuel 31.1 Deutéronome 1.41-1.44 Luc 22.33 Josué 17.16-17.18 Juges 9.38-9.40
10 Hawakulishika agano la Mungu; Wakakataa kuenenda katika sheria yake;
2 Rois 17.14-17.15 Juges 2.10-2.12 Deutéronome 31.16 Jérémie 31.32 Deutéronome 31.20
11 Wakayasahau matendo yake, Na mambo yake ya ajabu aliyowaonyesha.
Psaumes 106.13 Jérémie 2.32 Psaumes 78.7 Psaumes 106.21-106.22 Deutéronome 32.18
12 Mbele ya baba zao alifanya mambo ya ajabu, Katika nchi ya Misri, konde la Soani.
Nombres 13.22 Esaïe 19.11 Ezéchiel 30.14 Esaïe 19.13 Exode 7.1-12.51
13 Aliipasua bahari akawavusha; Aliyasimamisha maji mfano wa chungu.
Exode 15.8 Exode 14.21 Psaumes 38.7 Josué 3.16 Exode 14.1-14.15
14 Akawaongoza kwa wingu mchana, Na usiku kucha kwa nuru ya moto.
Psaumes 105.39 Exode 14.24 Néhémie 9.12 Néhémie 9.19 Exode 13.21-13.22
15 Akapasua miamba jangwani; Akawanywesha maji mengi kama maji ya vilindi.
1 Corinthiens 10.4 Psaumes 105.41 Nombres 20.11 Exode 17.6 Psaumes 114.8
16 Akatokeza na vijito gengeni, Akatelemsha maji kama mito.
Nombres 20.8 Deutéronome 8.15 Nombres 20.10-20.11 Psaumes 105.41 Deutéronome 9.21
17 Lakini wakazidi kumtenda dhambi, Walipomwasi Aliye juu katika nchi ya kiu.
Esaïe 63.10 Hébreux 3.16-3.19 Psaumes 106.13-106.32 Psaumes 78.32 Deutéronome 9.12-9.22
18 Wakamjaribu Mungu mioyoni mwao Kwa kutaka chakula kwa tamaa zao.
Nombres 11.4 1 Corinthiens 10.9 Exode 16.2-16.3 Psaumes 106.14-106.15 Jacques 4.2-4.3
19 Naam, walimwamba Mungu, wakasema, Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?
Nombres 21.5 Nombres 11.4 Psaumes 23.5 Exode 16.8-16.10 Nombres 11.13
20 Tazama, aliupiga mwamba; Maji yakabubujika, ikafurika mito. Pia aweza kutupa chakula? Atawaandalia watu wake nyama?
Nombres 20.11 Genèse 18.12-18.14 Exode 17.6-17.7 Psaumes 78.41 Nombres 11.18
21 Hivyo Bwana aliposikia akaghadhibika; Moto ukawashwa juu ya Yakobo, Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli.
Nombres 11.10 Deutéronome 32.22 Jude 1.5 1 Corinthiens 10.11 Nombres 11.1-11.3
22 Kwa kuwa hawakumwamini Mungu, Wala hawakuutumainia wokovu wake.
Hébreux 3.18-3.19 Jude 1.5 Deutéronome 1.32 Esaïe 7.9 Hébreux 11.6
23 Lakini aliyaamuru mawingu juu; Akaifungua milango ya mbinguni;
Malachie 3.10 Genèse 7.11 Psaumes 33.9 Esaïe 5.6 2 Rois 7.2
24 Akawanyeshea mana ili wale; Akawapa nafaka ya mbinguni.
Exode 16.4 Psaumes 105.40 Néhémie 9.15 Néhémie 9.20 Exode 16.14
25 Mwanadamu akala chakula cha mashujaa; Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha.
Psaumes 103.20 Matthieu 14.20 Matthieu 15.37 Exode 16.8
26 Aliuelekeza upepo wa mashariki mbinguni; Akaiongoza kusi kwa uweza wake.
Nombres 11.31 Psaumes 135.7
27 Akawanyeshea nyama kama mavumbi, Na ndege wenye mbawa, Kama mchanga wa bahari.
Nombres 11.32 Exode 16.12-16.13 Nombres 11.18-11.19
28 Akawaangusha kati ya matuo yao, Pande zote za maskani zao.
29 Wakala wakashiba sana; Maana aliwaletea walivyovitamani;
Psaumes 106.15 Nombres 11.19-11.20
30 Hawakuachana na matakwa yao. Ila chakula chao kikali ki vinywani mwao
Nombres 22.20-22.22 Nombres 11.33-11.34 Luc 16.19-16.23 Proverbes 1.32
31 Hasira ya Mungu ikapanda juu yao, Akawaua waliokuwa wanono; Akawaangusha chini vijana wa Israeli.
Esaïe 10.16
32 Pamoja na hayo wakazidi kutenda dhambi, Wala hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
Psaumes 78.22 Nombres 16.1-16.17 Nombres 14.1-14.45 Nombres 25.1-25.18 Luc 16.31
33 Kwa hiyo akazikomesha siku zao kama pumzi, Na miaka yao kwa hofu ya kuwasitusha.
Nombres 14.35 Nombres 14.29 Nombres 26.64-26.65 Job 14.1 Deutéronome 2.14-2.16
34 Alipowaua ndipo walipokuwa wakimtafuta; Wakarudi wakamtaka Mungu kwa bidii.
Osée 5.15 Nombres 21.7 Juges 3.8-3.9 Osée 7.14 Juges 4.3
35 Wakakumbuka kuwa Mungu ni mwamba wao, Na Mungu Aliye juu ni mkombozi wao.
Deutéronome 32.4 Exode 15.13 Esaïe 41.14 Deutéronome 32.15 Deutéronome 9.26
36 Lakini walimdanganya kwa vinywa vyao, Wakamwambia uongo kwa ndimi zao.
Ezéchiel 33.31 Esaïe 29.13 Esaïe 57.11 Osée 11.12 Psaumes 18.44
37 Kwa maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, Wala hawakuwa waaminifu katika agano lake.
Psaumes 78.8 Actes 8.21 Psaumes 51.10 Deutéronome 31.20 Osée 7.16-8.1
38 Lakini Yeye, kwa kuwa anayo rehema, Husamehe uovu wala haangamizi. Mara nyingi huipishia mbali ghadhabu yake, Wala haiwashi hasira yake yote.
Esaïe 48.9 Nombres 14.18-14.20 Psaumes 106.43-106.45 Esaïe 44.21-44.22 Ezéchiel 20.8-20.9
39 Akakumbuka ya kuwa wao ni kiwiliwili, Upepo upitao wala haurudi.
Genèse 6.3 Job 7.7 Jacques 4.14 Job 7.16 Psaumes 103.14-103.16
40 Walimwasi jangwani mara ngapi? Na kumhuzunisha nyikani!
Ephésiens 4.30 Psaumes 95.8-95.10 Esaïe 63.10 Hébreux 3.15-3.17 Psaumes 107.11
41 Wakarudi nyuma wakamjaribu Mungu; Wakampa mpaka Mtakatifu wa Israeli.
Nombres 14.22 Marc 5.35-5.36 2 Pierre 2.21-2.22 Deutéronome 6.16 Actes 7.39
42 Hawakuukumbuka mkono wake, Wala siku ile alipowakomboa na mtesi.
Juges 8.34 Exode 14.30-14.31 Psaumes 78.11 Jérémie 32.21 Esaïe 11.11
43 Alivyoziweka ishara zake katika Misri, Na miujiza yake katika konde la Soani.
Deutéronome 4.34 Néhémie 9.10 Deutéronome 6.22 Exode 7.3 Exode 4.21
44 Aligeuza damu mito yao, Na vijito wasipate kunywa.
Psaumes 105.29 Exode 7.17-7.21 Apocalypse 16.3-16.6
45 Aliwapelekea mainzi wakawala, Na vyura wakawaharibu.
Exode 8.21-8.24 Psaumes 105.30-105.31 Apocalypse 16.3 Exode 8.2-8.15
46 Akawapa tunutu mazao yao, Na nzige kazi yao.
Exode 10.12-10.15 Psaumes 105.34-105.35 Joël 2.25 Joël 1.4-1.7 Apocalypse 9.2-9.11
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe, Na mikuyu yao kwa mawe ya barafu.
Psaumes 105.32-105.33 Exode 9.18-9.34
48 Akaacha ng’ombe zao wapigwe kwa mvua ya mawe, Na makundi yao kwa umeme.
Exode 9.28 Exode 9.19
49 Akawapelekea ukali wa hasira yake, Ghadhabu, na uchungu, na taabu, Kundi la malaika waletao mabaya.
Exode 12.13 Romains 2.8-2.9 Lamentations 4.11 Job 1.12 2 Samuel 24.16
50 Akiifanyizia njia hasira yake; Wala hakuziepusha roho zao na mauti, Bali aliiachia tauni uhai wao;
Exode 9.3-9.6 Ezéchiel 7.9 Ezéchiel 8.18 Job 27.22 Ezéchiel 5.11
51 Akampiga kila mzaliwa wa kwanza wa Misri, Malimbuko ya nguvu katika hema za Hamu.
Psaumes 135.8 Psaumes 105.23 Psaumes 136.10 Psaumes 106.22 Psaumes 105.36
52 Bali aliwaongoza watu wake kama kondoo, Akawachunga kama kundi jangwani.
Psaumes 77.20 Néhémie 9.12 Jérémie 23.2-23.4 Luc 15.4-15.6 Psaumes 100.3
53 Hao akawachukua salama wala hawakuogopa, Bali bahari iliwafunikiza adui zao.
Exode 14.19-14.20 Exode 14.27-14.28 Exode 15.10 Exode 14.15 Hébreux 11.29
54 Akawapeleka hadi mpaka wake mtakatifu, Mlima alioununua kwa mkono wake wa kuume.
Exode 15.17 Psaumes 44.3 Psaumes 68.16 Daniel 9.16-9.20 Daniel 11.45
55 Akawafukuza mataifa mbele yao, Akawapimia urithi kwa kamba, Na kuwakalisha kabila za Israeli katika hema zao.
Psaumes 44.2 Josué 13.7 Josué 19.51 Psaumes 105.44-105.45 Psaumes 135.10-135.12
56 Lakini walimjaribu Mungu Aliye juu, wakamwasi, Wala hawakuzishika shuhuda zake.
Juges 2.11-2.12 Deutéronome 32.15-32.21 Psaumes 78.40-78.41 2 Rois 17.7-17.23 Ezéchiel 16.15-16.26
57 Bali walirudi nyuma, wakahaini kama baba zao; Wakaepea kama upinde usiofaa.
Osée 7.16 Ezéchiel 20.27-20.28 Psaumes 78.41 Juges 3.12 Juges 3.5-3.7
58 Wakamkasirisha kwa mahali pao pa juu, Wakamtia wivu kwa sanamu zao.
Deutéronome 32.21 Lévitique 26.30 1 Rois 12.31 1 Rois 11.7 Deutéronome 12.2
59 Mungu akasikia, akaghadhibika, Akamkataa Israeli kabisa.
Psaumes 106.40 Lamentations 2.7 Lévitique 20.23 Lévitique 26.44 Genèse 18.20-18.21
60 Akaiacha maskani ya Shilo, Hema aliyoiweka katikati ya wanadamu;
Josué 18.1 1 Samuel 4.4-4.11 Jérémie 26.6-26.9 Jérémie 7.12-7.14 1 Samuel 1.3
61 Akaziacha nguvu zake kutekwa, Na fahari yake mkononi mwa mtesi.
Psaumes 132.8 1 Samuel 4.21-5.2 Psaumes 24.7 2 Chroniques 6.41 1 Samuel 4.17
62 Akawatoa watu wake wapigwe kwa upanga; Akaughadhibikia urithi wake.
1 Samuel 4.2 Esaïe 64.9 Psaumes 89.38 1 Samuel 4.10-4.11
63 Moto ukawala vijana wao, Wanawali wao hawakuimbiwa nyimbo za arusi,
Jérémie 7.34 Jérémie 16.9 Jérémie 25.10 Esaïe 4.1 Deutéronome 32.22
64 Makuhani wao walianguka kwa upanga, Wala wajane wao hawakuomboleza.
1 Samuel 4.17 Job 27.15 Ezéchiel 24.23 1 Samuel 4.11 1 Samuel 22.18-22.19
65 Ndipo Bwana alipoamka kama aliyelala usingizi, Kama shujaa apigaye kelele sababu ya mvinyo;
Psaumes 44.23 Esaïe 51.9 Psaumes 7.6 Psaumes 73.20 Esaïe 42.13-42.14
66 Akawapiga watesi wake akawarudisha nyuma, Akawatia aibu ya milele.
1 Samuel 5.6 1 Samuel 6.4 Jérémie 23.40 Job 40.12
67 Ila akaikataa hema ya Yusufu; Wala hakuichagua kabila ya Efraimu.
2 Samuel 6.2 1 Samuel 6.21-7.1 2 Samuel 6.17
68 Bali aliichagua kabila ya Yuda, Mlima Sayuni alioupenda.
Psaumes 87.2 Genèse 49.8-49.10 Ruth 4.17-4.22 2 Chroniques 6.6 Psaumes 132.12-132.14
69 Akajenga patakatifu pake kama vilele, Kama dunia aliyoiweka imara milele.
Esaïe 51.6 Esaïe 48.13 Job 26.7 Psaumes 104.5 Psaumes 102.25
70 Akamchagua Daudi, mtumishi wake, Akamwondoa katika mazizi ya kondoo.
1 Samuel 16.11-16.12 Amos 7.14-7.15 2 Samuel 7.8 Actes 13.22 Exode 3.1
71 Nyuma ya kondoo wanyonyeshao alimwondoa, Awachunge Yakobo watu wake, na Israeli urithi wake.
2 Samuel 5.2 Psaumes 75.6-75.7 Genèse 33.13 1 Samuel 2.7-2.8 Psaumes 28.9
72 Akawalisha kwa ukamilifu wa moyo wake, Na kuwaongoza kwa busara ya mikono yake.
1 Rois 9.4 Actes 13.22 Esaïe 11.2-11.4 Psaumes 101.1-101.8 1 Rois 3.6-3.9

Cette Bible est dans le domaine public.