Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 31
Bible en Swahili de l’est


1 Nilifanya agano na macho yangu; Basi nawezaje kumwangalia msichana?
Jacques 1.14-1.15 Matthieu 5.28-5.29 Psaumes 119.37 Proverbes 6.25 Proverbes 4.25
2 Kwani sehemu ya Mungu itokayo juu ingekuwa nini, Na urithi wa Mwenyezi utokao juu?
Job 20.29 Hébreux 13.4 Job 27.13
3 Je! Siyo msiba kwa wasio haki, Na hasara kwao watendao uovu?
Job 21.30 Proverbes 1.27 Esaïe 28.21 2 Pierre 2.1 1 Thessaloniciens 5.3
4 Je! Yeye hazioni njia zangu, Na kuzihesabu hatua zangu zote?
Job 14.16 Proverbes 5.21 2 Chroniques 16.9 Job 34.21 Jérémie 16.17
5 Kwamba nimetembea katika ubatili, Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu;
Psaumes 44.20-44.21 Psaumes 7.3-7.5 Jérémie 2.5 Psaumes 12.2 Michée 2.11
6 (Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa, Ili Mungu aujue uelekevu wangu);
Psaumes 7.8-7.9 Daniel 5.27 Psaumes 17.2-17.3 Job 27.5-27.6 Psaumes 1.6
7 Kwamba hatua yangu imekengeuka na kuiacha njia, Na moyo wangu kuyaandama macho yangu, Tena kwamba kipaku cho chote kimeshikamana na mikono yangu;
Nombres 15.39 Ecclésiaste 11.9 Matthieu 5.29 Ezéchiel 14.7 Ezéchiel 14.3
8 Basi na nipande, mwingine ale; Naam, mazao ya shamba langu na yang’olewe.
Lévitique 26.16 Michée 6.15 Deutéronome 28.38 Job 15.30 Deutéronome 28.51
9 Kama moyo wangu ulishawishwa kwa mwanamke, Nami nimeotea mlangoni pa jirani yangu;
Ecclésiaste 7.26 Juges 16.5 Proverbes 2.16-2.19 Proverbes 7.21 Osée 7.4
10 Ndipo hapo mke wangu na asage kwa mwingine, Na wengine na wainame juu yake.
Jérémie 8.10 2 Samuel 12.11 Esaïe 47.2 Exode 11.5 Deutéronome 28.30
11 Kwani hilo lingekuwa kosa kuu; Naam, lingekuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi;
Lévitique 20.10 Job 31.28 Deutéronome 22.22-22.24 Genèse 38.24 Exode 20.14
12 Kwa kuwa ni moto uteketezao hata Uharibifu, Nao ungeyang’oa maongeo yangu yote.
Proverbes 6.27 Proverbes 3.33 Job 26.6 Job 15.30 Jérémie 5.7-5.9
13 Kama nimeidharau daawa ya mtumishi wangu, au ya kijakazi changu, Waliposhindana nami;
Lévitique 25.46 Exode 21.20-21.21 Ephésiens 6.9 Jérémie 34.14-34.17 Exode 21.26-21.27
14 Basi Mungu atakapoinuka nitafanya nini? Naye atakapozuru, nitamjibuje?
Michée 7.4 Job 9.32 Esaïe 10.3 Romains 3.19 Job 10.2
15 Je! Huyo aliyenifanya mimi ndani ya tumbo, siye aliyemfanya na yeye? Si yeye mmoja aliyetufinyanga tumboni?
Proverbes 14.31 Job 34.19 Proverbes 22.2 Néhémie 5.5 Esaïe 58.7
16 Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, Au kama nimeyatia kiwi macho ya mwanamke mjane;
Deutéronome 28.32 Job 20.19 Job 5.16 Lamentations 4.17 Psaumes 112.9
17 Au kama nimekula tonge langu peke yangu, Mayatima wasipate kulila;
Romains 12.13 Jacques 1.27 Ezéchiel 18.7 Actes 4.32 Deutéronome 15.14
18 (La, tangu ujana wangu alikua pamoja nami kama kwa baba; Nami nimekuwa ni kiongozi cha mjane tangu tumbo la mamangu);
19 Ikiwa nimemwona mtu kuangamia kwa kukosa nguo, Au wahitaji kukosa mavazi;
Job 22.6 Esaïe 58.7 2 Chroniques 28.15 Luc 3.11 Actes 9.39
20 Ikiwa viuno vyake havikunibarikia, Au kama hakupata moto kwa manyoya ya kondoo zangu;
Deutéronome 24.13 Job 29.11
21 Ikiwa nimewainulia mayatima mkono, Nilipoona msaada wangu langoni;
Job 22.9 Job 29.12 Job 24.9 Ezéchiel 22.7 Jérémie 5.28
22 Basi bega langu na lianguke kutoka mahali pake, Na mkono wangu uvunjike mfupani mwake.
Psaumes 137.6 Josué 22.22-22.23 Job 31.10 Psaumes 7.4-7.5 Job 38.15
23 Kwani msiba utokao kwa Mungu ulikuwa na kitisho kwangu, Na kwa sababu ya ukuu wake sikuweza kufanya neno.
Job 13.11 Psaumes 119.120 Job 42.5-42.6 Job 20.23 Joël 1.15
24 Ikiwa nimeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, Na kuiambia dhahabu safi, Wewe u tegemeo langu;
Psaumes 52.7 Psaumes 62.10 Psaumes 49.6-49.7 Genèse 31.1 Luc 12.15
25 Kama nilifurahi kwa kuwa mali yangu yalikuwa mengi, Na kwa sababu mkono wangu umepata vitu vingi;
Psaumes 62.10 Esther 5.11 Jérémie 9.23 Deutéronome 8.17-8.18 Esaïe 10.13-10.14
26 Kama nililitazama jua lilipoangaza, Au mwezi ukiendelea katika kung’aa;
Ezéchiel 8.16 Deutéronome 4.19 Deutéronome 17.3 2 Rois 23.5 2 Rois 23.11
27 Na moyo wangu umeshawishwa kwa siri, Na midomo yangu imeubusu mkono wangu;
Psaumes 2.12 Deutéronome 11.16 Romains 1.21 Romains 1.28 1 Rois 19.18
28 Hilo nalo lingekuwa uovu wa kuadhibiwa na waamuzi; Kwani ningemwambia uongo Mungu aliye juu.
Job 31.11 Deutéronome 17.2-17.7 Josué 24.27 Proverbes 30.9 Tite 1.16
29 Kama nilifurahi kwa kuangamia kwake huyo aliyenichukia, Au kujitukuza alipopatikana na maovu;
Proverbes 17.5 Proverbes 24.17-24.18 Psaumes 35.25-35.26 Psaumes 35.13-35.14 Abdias 1.12
30 (Naam, sikukiacha kinywa changu kufanya dhambi Kwa kuutaka uhai wake kwa kuapiza);
1 Pierre 3.9 Romains 12.14 Exode 23.4-23.5 Matthieu 5.22 Ecclésiaste 5.6
31 Kama watu wa hemani mwangu hawakunena, Ni nani awezaye kumpata mtu asiyeshibishwa na yeye kwa nyama?
Psaumes 35.25 2 Samuel 16.9-16.10 Job 19.22 1 Samuel 26.8 Luc 22.50-22.51
32 Mgeni hakulala njiani; Lakini nilimfungulia msafiri milango yangu;
Genèse 19.2-19.3 Juges 19.20-19.21 Hébreux 13.2 Romains 12.13 1 Pierre 4.9
33 Ikiwa kama mwanadamu nimeyafunika makosa yangu, Kwa kuuficha uovu wangu kifuani mwangu;
Proverbes 28.13 Osée 6.7 Genèse 3.12 1 Jean 1.8-1.10 Genèse 3.7-3.8
34 Kwa sababu niliwaogopa mkutano mkubwa, Na dharau la jamaa lilinitia hofu, Hata nilinyamaa kimya, nisitoke mlangoni-
Exode 23.2 Nombres 25.14-25.15 Esther 4.14 Néhémie 13.28 Amos 5.11-5.13
35 Laiti ningekuwa na mtu wa kunisikia! (Tazama, sahihi yangu ni hii, Mwenyezi na anijibu); Laiti ningekuwa na hayo mashitaka yaliyoandikwa na adui yangu!
Job 13.21-13.22 Job 19.23-19.24 Job 23.3-23.7 Job 38.1-38.3 Job 19.7
36 Hakika ningeyachukua mabegani; Ningejifungia mfano wa kilemba.
Esaïe 22.22 Job 29.14 Philippiens 4.1 Exode 28.12 Esaïe 62.3
37 Ningemwambia hesabu ya hatua zangu Ningemkaribia kama vile mkuu.
Ephésiens 3.12 Job 29.25 Job 42.3-42.6 1 Jean 3.19-3.21 Job 1.3
38 Kama nchi yangu yalia juu yangu, Na matuta yake hulia pamoja;
Jacques 5.4 Job 20.27 Psaumes 65.13 Habakuk 2.11
39 Kama nimeyala matunda yake pasipo kulipa, Au kama nimewafanya wenyewe kupotewa na uhai;
1 Rois 21.19 Jacques 5.4 Proverbes 1.19 Esaïe 26.21 Ezéchiel 22.6
40 Miiba na imee badala ya ngano, Na magugu badala ya shayiri. Maneno ya Ayubu yamekoma hapa.
Esaïe 7.23 Sophonie 2.9 Genèse 3.17-3.18 Psaumes 72.20 Malachie 1.3

Cette Bible est dans le domaine public.