Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 31.16
Bible en Swahili de l’est


1 Nilifanya agano na macho yangu; Basi nawezaje kumwangalia msichana?
Jacques 1.14-1.15 Matthieu 5.28-5.29 Proverbes 4.25 1 Jean 2.16 Psaumes 119.37
2 Kwani sehemu ya Mungu itokayo juu ingekuwa nini, Na urithi wa Mwenyezi utokao juu?
Job 20.29 Hébreux 13.4 Job 27.13
3 Je! Siyo msiba kwa wasio haki, Na hasara kwao watendao uovu?
Job 21.30 Proverbes 10.29 Proverbes 21.15 Job 34.22 Proverbes 1.27
4 Je! Yeye hazioni njia zangu, Na kuzihesabu hatua zangu zote?
Job 14.16 2 Chroniques 16.9 Job 34.21 Proverbes 5.21 Jérémie 16.17
5 Kwamba nimetembea katika ubatili, Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu;
Ezéchiel 13.8 Proverbes 12.11 Psaumes 4.2 Psaumes 44.20-44.21 Psaumes 7.3-7.5
6 (Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa, Ili Mungu aujue uelekevu wangu);
Psaumes 7.8-7.9 Daniel 5.27 Psaumes 17.2-17.3 Proverbes 16.11 Psaumes 26.1
7 Kwamba hatua yangu imekengeuka na kuiacha njia, Na moyo wangu kuyaandama macho yangu, Tena kwamba kipaku cho chote kimeshikamana na mikono yangu;
Nombres 15.39 Ecclésiaste 11.9 Matthieu 5.29 Job 9.30 Psaumes 44.20-44.21
8 Basi na nipande, mwingine ale; Naam, mazao ya shamba langu na yang’olewe.
Lévitique 26.16 Michée 6.15 Deutéronome 28.38 Juges 6.3-6.6 Job 20.18
9 Kama moyo wangu ulishawishwa kwa mwanamke, Nami nimeotea mlangoni pa jirani yangu;
Ecclésiaste 7.26 Proverbes 6.25 1 Rois 11.4 Juges 16.5 Proverbes 2.16-2.19
10 Ndipo hapo mke wangu na asage kwa mwingine, Na wengine na wainame juu yake.
Jérémie 8.10 2 Samuel 12.11 Esaïe 47.2 Deutéronome 28.30 Exode 11.5
11 Kwani hilo lingekuwa kosa kuu; Naam, lingekuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi;
Lévitique 20.10 Job 31.28 Deutéronome 22.22-22.24 Genèse 38.24 Genèse 20.9
12 Kwa kuwa ni moto uteketezao hata Uharibifu, Nao ungeyang’oa maongeo yangu yote.
Proverbes 6.27 Malachie 3.5 Job 20.28 Hébreux 13.4 Proverbes 3.33
13 Kama nimeidharau daawa ya mtumishi wangu, au ya kijakazi changu, Waliposhindana nami;
Deutéronome 24.14-24.15 Colossiens 4.1 Deutéronome 15.12-15.15 Lévitique 25.46 Exode 21.20-21.21
14 Basi Mungu atakapoinuka nitafanya nini? Naye atakapozuru, nitamjibuje?
Psaumes 10.12-10.15 Psaumes 44.21 Psaumes 143.2 Psaumes 9.12 Michée 7.4
15 Je! Huyo aliyenifanya mimi ndani ya tumbo, siye aliyemfanya na yeye? Si yeye mmoja aliyetufinyanga tumboni?
Proverbes 14.31 Job 34.19 Proverbes 22.2 Psaumes 139.14-139.16 Néhémie 5.5
16 Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, Au kama nimeyatia kiwi macho ya mwanamke mjane;
Deutéronome 15.7-15.10 Esaïe 38.14 Actes 11.29 Deutéronome 28.32 Job 20.19
17 Au kama nimekula tonge langu peke yangu, Mayatima wasipate kulila;
Job 29.12-29.16 1 Jean 3.17 Deutéronome 15.11 Romains 12.13 Jacques 1.27
18 (La, tangu ujana wangu alikua pamoja nami kama kwa baba; Nami nimekuwa ni kiongozi cha mjane tangu tumbo la mamangu);
19 Ikiwa nimemwona mtu kuangamia kwa kukosa nguo, Au wahitaji kukosa mavazi;
Job 22.6 Matthieu 25.43 Matthieu 25.36 Jacques 2.16 Esaïe 58.7
20 Ikiwa viuno vyake havikunibarikia, Au kama hakupata moto kwa manyoya ya kondoo zangu;
Deutéronome 24.13 Job 29.11
21 Ikiwa nimewainulia mayatima mkono, Nilipoona msaada wangu langoni;
Job 22.9 Job 29.12 Michée 7.3 Michée 2.1-2.2 Proverbes 23.10-23.11
22 Basi bega langu na lianguke kutoka mahali pake, Na mkono wangu uvunjike mfupani mwake.
Psaumes 7.4-7.5 Job 38.15 Job 31.40 Psaumes 137.6 Josué 22.22-22.23
23 Kwani msiba utokao kwa Mungu ulikuwa na kitisho kwangu, Na kwa sababu ya ukuu wake sikuweza kufanya neno.
Job 13.11 Psaumes 119.120 Job 40.9 2 Corinthiens 5.11 Job 42.5-42.6
24 Ikiwa nimeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, Na kuiambia dhahabu safi, Wewe u tegemeo langu;
Psaumes 52.7 Deutéronome 8.12-8.14 Colossiens 3.5 Marc 10.24-10.25 Psaumes 62.10
25 Kama nilifurahi kwa kuwa mali yangu yalikuwa mengi, Na kwa sababu mkono wangu umepata vitu vingi;
Psaumes 62.10 Luc 12.19 Habakuk 1.16 Esther 5.11 Jérémie 9.23
26 Kama nililitazama jua lilipoangaza, Au mwezi ukiendelea katika kung’aa;
Ezéchiel 8.16 Deutéronome 4.19 Deutéronome 17.3 2 Rois 23.11 Jérémie 8.2
27 Na moyo wangu umeshawishwa kwa siri, Na midomo yangu imeubusu mkono wangu;
Osée 13.2 Deutéronome 13.6 Esaïe 44.20 Psaumes 2.12 Deutéronome 11.16
28 Hilo nalo lingekuwa uovu wa kuadhibiwa na waamuzi; Kwani ningemwambia uongo Mungu aliye juu.
Job 31.11 Deutéronome 17.2-17.7 Josué 24.27 Josué 24.23 Job 23.7
29 Kama nilifurahi kwa kuangamia kwake huyo aliyenichukia, Au kujitukuza alipopatikana na maovu;
Proverbes 17.5 Proverbes 24.17-24.18 Psaumes 35.13-35.14 Psaumes 35.25-35.26 2 Samuel 16.5-16.8
30 (Naam, sikukiacha kinywa changu kufanya dhambi Kwa kuutaka uhai wake kwa kuapiza);
1 Pierre 3.9 Romains 12.14 Matthieu 5.43-5.44 Exode 23.4-23.5 Matthieu 5.22
31 Kama watu wa hemani mwangu hawakunena, Ni nani awezaye kumpata mtu asiyeshibishwa na yeye kwa nyama?
Jérémie 40.15-40.16 Proverbes 1.18 Luc 9.54-9.55 Psaumes 35.25 2 Samuel 16.9-16.10
32 Mgeni hakulala njiani; Lakini nilimfungulia msafiri milango yangu;
Genèse 19.2-19.3 Hébreux 13.2 Juges 19.20-19.21 Romains 12.13 1 Pierre 4.9
33 Ikiwa kama mwanadamu nimeyafunika makosa yangu, Kwa kuuficha uovu wangu kifuani mwangu;
Proverbes 28.13 Osée 6.7 Genèse 3.12 Actes 5.8 Josué 7.11
34 Kwa sababu niliwaogopa mkutano mkubwa, Na dharau la jamaa lilinitia hofu, Hata nilinyamaa kimya, nisitoke mlangoni-
Exode 23.2 Esther 4.11 Matthieu 27.20-27.26 Néhémie 13.4-13.8 Job 34.19
35 Laiti ningekuwa na mtu wa kunisikia! (Tazama, sahihi yangu ni hii, Mwenyezi na anijibu); Laiti ningekuwa na hayo mashitaka yaliyoandikwa na adui yangu!
Job 13.21-13.22 Job 23.3-23.7 Job 19.23-19.24 Job 17.3 Job 27.7
36 Hakika ningeyachukua mabegani; Ningejifungia mfano wa kilemba.
Esaïe 22.22 Exode 28.12 Esaïe 62.3 Job 29.14 Philippiens 4.1
37 Ningemwambia hesabu ya hatua zangu Ningemkaribia kama vile mkuu.
Job 13.15 Genèse 32.28 Job 9.3 Ephésiens 3.12 Job 29.25
38 Kama nchi yangu yalia juu yangu, Na matuta yake hulia pamoja;
Job 20.27 Psaumes 65.13 Habakuk 2.11 Jacques 5.4
39 Kama nimeyala matunda yake pasipo kulipa, Au kama nimewafanya wenyewe kupotewa na uhai;
1 Rois 21.19 Jacques 5.4 Ezéchiel 22.12-22.13 Proverbes 1.19 Esaïe 26.21
40 Miiba na imee badala ya ngano, Na magugu badala ya shayiri. Maneno ya Ayubu yamekoma hapa.
Genèse 3.17-3.18 Psaumes 72.20 Malachie 1.3 Esaïe 7.23 Sophonie 2.9

Cette Bible est dans le domaine public.