Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Job 31.12
Bible en Swahili de l’est


1 Nilifanya agano na macho yangu; Basi nawezaje kumwangalia msichana?
Jacques 1.14-1.15 Matthieu 5.28-5.29 Proverbes 4.25 1 Jean 2.16 Psaumes 119.37
2 Kwani sehemu ya Mungu itokayo juu ingekuwa nini, Na urithi wa Mwenyezi utokao juu?
Job 20.29 Hébreux 13.4 Job 27.13
3 Je! Siyo msiba kwa wasio haki, Na hasara kwao watendao uovu?
Job 21.30 Proverbes 21.15 Job 34.22 Proverbes 1.27 Esaïe 28.21
4 Je! Yeye hazioni njia zangu, Na kuzihesabu hatua zangu zote?
Job 14.16 Job 34.21 Proverbes 5.21 2 Chroniques 16.9 Jérémie 16.17
5 Kwamba nimetembea katika ubatili, Na mguu wangu umeukimbilia udanganyifu;
Proverbes 12.11 Psaumes 4.2 Psaumes 44.20-44.21 Psaumes 7.3-7.5 Jérémie 2.5
6 (Na nipimwe katika mizani iliyo sawasawa, Ili Mungu aujue uelekevu wangu);
Psaumes 7.8-7.9 Daniel 5.27 Psaumes 17.2-17.3 Psaumes 26.1 Psaumes 139.23
7 Kwamba hatua yangu imekengeuka na kuiacha njia, Na moyo wangu kuyaandama macho yangu, Tena kwamba kipaku cho chote kimeshikamana na mikono yangu;
Nombres 15.39 Ecclésiaste 11.9 Matthieu 5.29 Psaumes 44.20-44.21 Esaïe 33.15
8 Basi na nipande, mwingine ale; Naam, mazao ya shamba langu na yang’olewe.
Lévitique 26.16 Michée 6.15 Deutéronome 28.38 Job 20.18 Psaumes 109.13
9 Kama moyo wangu ulishawishwa kwa mwanamke, Nami nimeotea mlangoni pa jirani yangu;
Ecclésiaste 7.26 Proverbes 6.25 1 Rois 11.4 Juges 16.5 Proverbes 2.16-2.19
10 Ndipo hapo mke wangu na asage kwa mwingine, Na wengine na wainame juu yake.
Jérémie 8.10 Esaïe 47.2 2 Samuel 12.11 Deutéronome 28.30 Exode 11.5
11 Kwani hilo lingekuwa kosa kuu; Naam, lingekuwa ni uovu wa kuadhibiwa na waamuzi;
Lévitique 20.10 Job 31.28 Deutéronome 22.22-22.24 Genèse 38.24 Proverbes 6.29-6.33
12 Kwa kuwa ni moto uteketezao hata Uharibifu, Nao ungeyang’oa maongeo yangu yote.
Proverbes 6.27 Job 20.28 Hébreux 13.4 Proverbes 3.33 Job 26.6
13 Kama nimeidharau daawa ya mtumishi wangu, au ya kijakazi changu, Waliposhindana nami;
Colossiens 4.1 Deutéronome 15.12-15.15 Lévitique 25.46 Exode 21.20-21.21 Ephésiens 6.9
14 Basi Mungu atakapoinuka nitafanya nini? Naye atakapozuru, nitamjibuje?
Psaumes 143.2 Psaumes 9.12 Michée 7.4 Job 9.32 Esaïe 10.3
15 Je! Huyo aliyenifanya mimi ndani ya tumbo, siye aliyemfanya na yeye? Si yeye mmoja aliyetufinyanga tumboni?
Proverbes 14.31 Proverbes 22.2 Job 34.19 Psaumes 139.14-139.16 Néhémie 5.5
16 Ikiwa nimewanyima maskini haja zao, Au kama nimeyatia kiwi macho ya mwanamke mjane;
Esaïe 38.14 Actes 11.29 Deutéronome 28.32 Job 20.19 Job 5.16
17 Au kama nimekula tonge langu peke yangu, Mayatima wasipate kulila;
1 Jean 3.17 Deutéronome 15.11 Romains 12.13 Jacques 1.27 Ezéchiel 18.7
18 (La, tangu ujana wangu alikua pamoja nami kama kwa baba; Nami nimekuwa ni kiongozi cha mjane tangu tumbo la mamangu);
19 Ikiwa nimemwona mtu kuangamia kwa kukosa nguo, Au wahitaji kukosa mavazi;
Job 22.6 Matthieu 25.36 Jacques 2.16 Esaïe 58.7 2 Chroniques 28.15
20 Ikiwa viuno vyake havikunibarikia, Au kama hakupata moto kwa manyoya ya kondoo zangu;
Deutéronome 24.13 Job 29.11
21 Ikiwa nimewainulia mayatima mkono, Nilipoona msaada wangu langoni;
Job 22.9 Job 29.12 Michée 2.1-2.2 Proverbes 23.10-23.11 Job 24.9
22 Basi bega langu na lianguke kutoka mahali pake, Na mkono wangu uvunjike mfupani mwake.
Job 38.15 Job 31.40 Psaumes 137.6 Josué 22.22-22.23 Job 31.10
23 Kwani msiba utokao kwa Mungu ulikuwa na kitisho kwangu, Na kwa sababu ya ukuu wake sikuweza kufanya neno.
Job 13.11 Psaumes 119.120 Job 40.9 2 Corinthiens 5.11 Job 42.5-42.6
24 Ikiwa nimeifanya dhahabu kuwa tumaini langu, Na kuiambia dhahabu safi, Wewe u tegemeo langu;
Psaumes 52.7 Colossiens 3.5 Marc 10.24-10.25 Psaumes 62.10 Psaumes 49.6-49.7
25 Kama nilifurahi kwa kuwa mali yangu yalikuwa mengi, Na kwa sababu mkono wangu umepata vitu vingi;
Psaumes 62.10 Habakuk 1.16 Esther 5.11 Jérémie 9.23 Deutéronome 8.17-8.18
26 Kama nililitazama jua lilipoangaza, Au mwezi ukiendelea katika kung’aa;
Ezéchiel 8.16 Deutéronome 4.19 Deutéronome 17.3 Jérémie 8.2 Jérémie 44.17
27 Na moyo wangu umeshawishwa kwa siri, Na midomo yangu imeubusu mkono wangu;
Deutéronome 13.6 Esaïe 44.20 Psaumes 2.12 Deutéronome 11.16 Romains 1.21
28 Hilo nalo lingekuwa uovu wa kuadhibiwa na waamuzi; Kwani ningemwambia uongo Mungu aliye juu.
Job 31.11 Deutéronome 17.2-17.7 Josué 24.27 Job 23.7 Juges 11.27
29 Kama nilifurahi kwa kuangamia kwake huyo aliyenichukia, Au kujitukuza alipopatikana na maovu;
Proverbes 17.5 Proverbes 24.17-24.18 Psaumes 35.25-35.26 Psaumes 35.13-35.14 2 Samuel 16.5-16.8
30 (Naam, sikukiacha kinywa changu kufanya dhambi Kwa kuutaka uhai wake kwa kuapiza);
Romains 12.14 1 Pierre 3.9 Matthieu 5.43-5.44 Exode 23.4-23.5 Matthieu 5.22
31 Kama watu wa hemani mwangu hawakunena, Ni nani awezaye kumpata mtu asiyeshibishwa na yeye kwa nyama?
Proverbes 1.18 Luc 9.54-9.55 Psaumes 35.25 2 Samuel 16.9-16.10 Job 19.22
32 Mgeni hakulala njiani; Lakini nilimfungulia msafiri milango yangu;
Genèse 19.2-19.3 Hébreux 13.2 Juges 19.20-19.21 Romains 12.13 1 Pierre 4.9
33 Ikiwa kama mwanadamu nimeyafunika makosa yangu, Kwa kuuficha uovu wangu kifuani mwangu;
Proverbes 28.13 Osée 6.7 Genèse 3.12 Josué 7.11 1 Jean 1.8-1.10
34 Kwa sababu niliwaogopa mkutano mkubwa, Na dharau la jamaa lilinitia hofu, Hata nilinyamaa kimya, nisitoke mlangoni-
Exode 23.2 Job 34.19 2 Corinthiens 5.16 Exode 32.27 Jérémie 38.16
35 Laiti ningekuwa na mtu wa kunisikia! (Tazama, sahihi yangu ni hii, Mwenyezi na anijibu); Laiti ningekuwa na hayo mashitaka yaliyoandikwa na adui yangu!
Job 13.21-13.22 Job 19.23-19.24 Job 23.3-23.7 Job 33.6 Job 13.24
36 Hakika ningeyachukua mabegani; Ningejifungia mfano wa kilemba.
Esaïe 22.22 Esaïe 62.3 Job 29.14 Philippiens 4.1 Exode 28.12
37 Ningemwambia hesabu ya hatua zangu Ningemkaribia kama vile mkuu.
Genèse 32.28 Job 9.3 Ephésiens 3.12 Job 29.25 Job 42.3-42.6
38 Kama nchi yangu yalia juu yangu, Na matuta yake hulia pamoja;
Psaumes 65.13 Habakuk 2.11 Jacques 5.4 Job 20.27
39 Kama nimeyala matunda yake pasipo kulipa, Au kama nimewafanya wenyewe kupotewa na uhai;
1 Rois 21.19 Jacques 5.4 Ezéchiel 22.12-22.13 Proverbes 1.19 Esaïe 26.21
40 Miiba na imee badala ya ngano, Na magugu badala ya shayiri. Maneno ya Ayubu yamekoma hapa.
Psaumes 72.20 Malachie 1.3 Esaïe 7.23 Sophonie 2.9 Genèse 3.17-3.18

Cette Bible est dans le domaine public.