Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Philémon 1.11
Bible en Swahili de l’est


Salutation et louange

1 Paulo, mfungwa wa Kristo Yesu, na Timotheo aliye ndugu yetu, kwa Filemoni mpendwa wetu, mtenda kazi pamoja nasi,
2 Corinthiens 1.1 Philémon 1.24 Colossiens 1.1 1 Thessaloniciens 3.2 Ephésiens 3.1
2 na kwa Afia, ndugu yetu, na kwa Arkipo askari mwenzetu, na kwa kanisa lililo katika nyumba yako.
Romains 16.5 Philippiens 2.25 Colossiens 4.17 Colossiens 4.15 2 Timothée 2.3-2.4
3 Neema na iwe kwenu, na amani, zitokazo kwa Mungu, Baba yetu, na kwa Bwana Yesu Kristo.
Romains 1.7 2 Corinthiens 13.14 Ephésiens 1.2
4 Namshukuru Mungu wangu sikuzote, nikikukumbuka katika maombi yangu;
Romains 1.8 2 Timothée 1.3 Ephésiens 1.16 1 Thessaloniciens 1.2 Philippiens 1.3
5 nikisikia habari za upendo wako na imani uliyo nayo kwa Bwana Yesu na kwa watakatifu wote;
Colossiens 1.4 Ephésiens 1.15 Philémon 1.7 1 Corinthiens 16.1 1 Jean 3.23
6 ili kwamba ushirika wa imani yako ufanye kazi yake, katika ujuzi wa kila kitu chema kilicho kwetu, katika Kristo.
Colossiens 1.9 Philippiens 1.9-1.11 1 Pierre 1.5-1.8 Jacques 2.14 Matthieu 5.16
7 Maana nalikuwa na furaha nyingi na faraja kwa sababu ya upendo wako, kwa kuwa mioyo ya watakatifu imeburudishwa nawe, ndugu yangu.
2 Corinthiens 7.13 2 Corinthiens 7.4 2 Timothée 1.16 Philémon 1.20 1 Thessaloniciens 2.19

Demande de Paul

8 Kwa hiyo, nijapokuwa nina ujasiri katika Kristo kukuagiza likupasalo;
1 Thessaloniciens 2.6 2 Corinthiens 3.12 2 Corinthiens 10.8 1 Thessaloniciens 2.2 2 Corinthiens 11.21
9 lakini, kwa ajili ya upendo nakusihi, kwa kuwa ni kama nilivyo, Paulo mzee, na sasa mfungwa wa Kristo Yesu pia.
Ephésiens 4.1 Romains 12.1 2 Corinthiens 6.1 Hébreux 13.19 2 Corinthiens 5.20
10 Nakusihi kwa ajili ya mtoto wangu niliyemzaa katika vifungo vyangu, yaani, Onesimo;
Colossiens 4.9 1 Corinthiens 4.15 Galates 4.19 2 Samuel 19.37-19.38 Marc 9.17
11 ambaye zamani alikuwa hakufai, bali sasa akufaa sana, wewe na mimi pia;
2 Timothée 4.11 Luc 17.10 Luc 15.32 Romains 3.12 1 Pierre 2.10
12 niliyemtuma kwako, yeye mwenyewe, maana ni moyo wangu hasa;
Matthieu 6.14-6.15 Marc 11.25 Luc 15.20 Ephésiens 4.32 Jérémie 31.20
13 ambaye mimi nalitaka akae kwangu, apate kunitumikia badala yako katika vifungo vya Injili.
1 Corinthiens 16.17 Ephésiens 3.1 Philémon 1.1 Philippiens 1.7 Philippiens 2.30
14 Lakini sikutaka kutenda neno lo lote isipokuwa kwa shauri lako, ili kwamba wema wako usiwe kama kwa lazima, bali kwa hiari.
2 Corinthiens 9.7 1 Pierre 5.2-5.3 1 Chroniques 29.17 1 Corinthiens 9.7 2 Corinthiens 1.24
15 Maana, labda ndiyo sababu alitengwa nawe kwa muda, ili uwe naye tena milele;
Genèse 45.5-45.8 Genèse 50.20 Actes 4.28 Esaïe 20.6 Psaumes 76.10
16 tokea sasa, si kama mtumwa, bali zaidi ya mtumwa, ndugu mpendwa; kwangu mimi sana, na kwako wewe zaidi sana, katika mwili na katika Bwana.
Matthieu 23.8 1 Timothée 6.2 Colossiens 3.22 1 Corinthiens 7.22 1 Pierre 1.22-1.23
17 Basi kama ukiniona mimi kuwa mshirika nawe, mpokee huyu kama mimi mwenyewe.
2 Corinthiens 8.23 Matthieu 10.40 1 Timothée 6.2 Matthieu 25.40 1 Jean 1.3
18 Na kama amekudhulumu, au unamwia kitu, ukiandike hicho juu yangu.
Esaïe 53.4-53.7
19 Mimi Paulo nimeandika kwa mkono wangu mwenyewe, mimi nitalipa. Sikuambii kwamba nakuwia hata nafsi yako.
Galates 5.2 1 Corinthiens 16.21-16.22 1 Corinthiens 9.1-9.2 Galates 6.11 2 Corinthiens 3.2
20 Naam, ndugu yangu, nipate faida kwako katika Bwana; uniburudishe moyo wangu katika Kristo.
Philémon 1.7 1 Thessaloniciens 3.7-3.9 1 Jean 3.17 3 Jean 1.4 Philémon 1.12
21 Kwa kuwa nakuamini kutii kwako ndiyo maana nimekuandikia, nikijua ya kuwa utafanya zaidi ya hayo nisemayo.
2 Corinthiens 2.3 2 Thessaloniciens 3.4 2 Corinthiens 8.22 2 Corinthiens 7.16 Galates 5.10
22 Na pamoja na hayo uniwekee tayari mahali pa kukaa; maana nataraji ya kwamba kwa maombi yenu mtajaliwa kunipata.
Philippiens 2.24 2 Corinthiens 1.11 Actes 28.23 2 Jean 1.12 Philippiens 1.19

Salutations

23 Epafra, aliyefungwa pamoja nami katika Kristo Yesu, akusalimu;
Colossiens 1.7 Romains 16.7 Colossiens 4.12 Colossiens 4.10
24 na Marko, na Aristarko, na Dema, na Luka, watendao kazi pamoja nami.
Colossiens 4.14 2 Timothée 4.10-4.11 Colossiens 4.10 Actes 19.29 Actes 12.12
25 Neema ya Bwana Yesu Kristo na iwe pamoja na roho zenu.
2 Timothée 4.22 Romains 16.20 Romains 16.23 Galates 6.18

Cette Bible est dans le domaine public.