Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Accueil  /  Bible  /  Bible en Swahili de l’est  / Luc 7     

Luc 7
Bible en Swahili de l’est


Guérison d’un esclave à Capernaüm

1 Alipokwisha kuyamaliza maneno yake yote masikioni mwa watu, aliingia Kapernaumu.
Matthieu 8.5-8.13 Luc 7.1-7.10 Matthieu 7.28-7.29
2 Na mtumwa wake akida mmoja alikuwa hawezi, karibu na kufa; naye ni mtu aliyempenda sana.
Job 31.5 Actes 10.7 Colossiens 3.22-4.1 Jean 4.46-4.47 Genèse 35.8
3 Aliposikia habari za Yesu, alituma wazee wa Wayahudi kwake kumwomba aje amponye mtumwa wake.
Matthieu 8.5 Jean 4.47 Luc 9.38 Philémon 1.10 Luc 8.41
4 Nao walipofika kwa Yesu, walimsihi sana wakisema, Amestahili huyu umtendee neno hili;
Matthieu 10.13 Matthieu 10.37-10.38 Apocalypse 3.4 Matthieu 10.11 Luc 7.6-7.7
5 maana, analipenda taifa letu, naye alitujengea sinagogi.
Esdras 7.27-7.28 1 Jean 3.14 1 Jean 3.18-3.19 1 Chroniques 29.3-29.9 1 Rois 5.1
6 Basi Yesu akaenda pamoja nao. Hata alipokuwa si mbali na nyumba yake, yule akida alituma rafiki kwake, akamwambia, Bwana, usijisumbue, maana mimi sistahili wewe uingie chini ya dari yangu;
Luc 8.49 Matthieu 20.28 Luc 5.8 Luc 15.19-15.21 Genèse 32.10
7 kwa hiyo nilijiona sistahili mwenyewe kuja kwako; lakini, sema neno tu, na mtumwa wangu atapona.
Psaumes 107.20 Luc 4.36 Exode 15.26 Marc 1.27 Deutéronome 32.39
8 Kwa maana mimi nami ni mtu niliyewekwa chini ya mamlaka, mwenye askari chini yangu; nikimwambia huyu, Nenda, huenda; na huyu, Njoo, huja; na mtumwa wangu, Fanya hivi, hufanya.
Actes 24.23 Actes 23.26 Actes 23.23 Actes 23.17 Actes 25.26
9 Yesu aliposikia hayo alimstaajabia, akaugeukia mkutano uliokuwa ukimfuata, akasema, Nawaambia, hata katika Israeli sijaona imani kubwa namna hii.
Matthieu 8.10 Matthieu 15.28 Matthieu 9.33 Romains 3.1-3.3 Romains 9.4-9.5
10 Na wale waliotumwa waliporudi nyumbani, wakamkuta yule mtumwa ni mzima.
Marc 9.23 Matthieu 8.13 Matthieu 15.28 Jean 4.50-4.53

Résurrection à Naïn

11 Baadaye kidogo alikwenda mpaka mji mmoja uitwao Naini, na wanafunzi wake walifuatana naye pamoja na mkutano mkubwa.
12 Na alipolikaribia lango la mji, hapo palikuwa na maiti anachukuliwa nje, ni mwana pekee wa mamaye ambaye ni mjane, na watu wa mjini wengi walikuwa pamoja naye.
Luc 8.42 1 Rois 17.18 2 Rois 4.16 Jacques 1.27 Jean 11.19
13 Bwana alipomwona alimwonea huruma, akamwambia, Usilie.
Jérémie 31.20 Hébreux 4.15 Luc 8.52 Juges 10.16 Marc 8.2
14 Akakaribia, akaligusa jeneza; wale waliokuwa wakilichukua wakasimama. Akasema, Kijana, nakuambia, Inuka.
Jean 5.25 Esaïe 26.19 Actes 9.40-9.41 Jean 11.25 Luc 8.54-8.55
15 Yule maiti akainuka, akaketi, akaanza kusema. Akampa mama yake.
1 Rois 17.23-17.24 2 Rois 4.32-4.37 2 Rois 13.21
16 Hofu ikawashika wote, wakamtukuza Mungu, wakisema, Nabii mkuu ametokea kwetu; na, Mungu amewaangalia watu wake.
Matthieu 9.8 Luc 7.39 Luc 1.68 Luc 1.65 Psaumes 65.9
17 Habari hii yake ikaenea katika Uyahudi wote, na katika nchi zote za kando kando.
Luc 7.14 Marc 1.28 Matthieu 9.26 Matthieu 4.24 Matthieu 9.31

Jean-Baptiste vu par Jésus

18 Wanafunzi wa Yohana wakamletea habari za hayo yote.
Jean 3.26 Matthieu 11.2-11.19
19 Ndipo Yohana alipowaita wawili katika wanafunzi wake, akawatuma kwa Yesu akiuliza, Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine?
Luc 10.1 Jean 4.25 Jérémie 23.5-23.6 Esaïe 40.10-40.11 Genèse 3.15
20 Nao walipofika kwake, walisema, Yohana Mbatizaji ametutuma kwako, akisema, Wewe ndiwe yule ajaye, au tumtazamie mwingine?
Luc 7.19
21 Na saa ile ile aliwaponya wengi magonjwa yao, na misiba, na pepo wabaya; na vipofu wengi aliwakirimia kuona.
Marc 3.10 Marc 5.34 1 Corinthiens 11.30-11.32 Marc 5.29 Jacques 5.14-5.15
22 Ndipo alipojibu, akawaambia, Nendeni mkamweleze Yohana hayo mliyoyaona na kuyasikia; vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakasika, viziwi wanasikia, wafu wanafufuliwa, maskini wanahubiriwa habari njema.
Esaïe 35.5-35.6 Luc 4.18 Esaïe 29.18-29.19 Esaïe 61.1-61.3 Jacques 2.5
23 Naye heri mtu ye yote asiyechukizwa nami.
Esaïe 8.14-8.15 1 Corinthiens 2.14 1 Corinthiens 1.21-1.28 1 Pierre 2.7-2.8 Jean 6.60-6.66
24 Basi, wajumbe wa Yohana walipokwisha ondoka, alianza kuwaambia makutano habari za Yohana, Mlitoka kwenda nyikani kutazama nini? Unyasi ukitikiswa na upepo?
Ephésiens 4.14 Luc 1.80 Luc 3.2 2 Corinthiens 1.17-1.20 Jacques 1.6-1.8
25 Lakini mlitoka kwenda kuona nini? Mtu aliyevikwa mavazi mororo? Jueni, watu wenye mavazi ya utukufu, wanaokula raha, wamo katika majumba ya kifalme.
Esaïe 59.17 Matthieu 6.29 Esther 5.1 1 Pierre 3.3-3.4 Esther 1.11
26 Lakini, mlitoka kwenda kuona nini? Nabii? Naam, nawaambia, na aliye zaidi ya nabii.
Luc 20.6 Luc 1.76 Matthieu 11.9-11.14 Jean 3.26-3.30 Luc 16.16
27 Huyo ndiye aliyeandikiwa haya, Tazama, namtuma mjumbe wangu Mbele ya uso wako, Atakayeitengeneza njia yako mbele yako.
Malachie 3.1 Luc 1.76 Marc 1.2 Jean 1.23 Esaïe 40.3
28 Nami nawaambia, Katika wale waliozaliwa na wanawake hakuna aliye mkuu kuliko Yohana; lakini aliye mdogo katika ufalme wa Mungu ni mkuu kuliko yeye.
Matthieu 11.11 Luc 9.48 Luc 3.16 1 Pierre 1.10-1.12 Matthieu 13.16-13.17
29 Na watu wote na watoza ushuru waliposikia hayo, waliikiri haki ya Mungu, kwa kuwa wamebatizwa kwa ubatizo wa Yohana.
Luc 3.12 Luc 7.35 Romains 3.4-3.6 Actes 19.3 Matthieu 3.5-3.6
30 Lakini, Mafarisayo na wana-sheria walilipinga shauri la Mungu juu yao, kwa kuwa hawakubatizwa naye.
Matthieu 22.35 Luc 13.34 Jérémie 8.8 Ephésiens 1.11 Galates 2.21
31 Bwana akasema, Niwafananishe na nini watu wa kizazi hiki? Nao wamefanana na nini?
Matthieu 11.16-11.19 Lamentations 2.13 Marc 4.30
32 Wamefanana na watoto walioketi sokoni na kuitana, wakisema, Tuliwapigia filimbi wala hamkucheza; tuliomboleza, wala hamkulia.
Matthieu 11.16-11.19 Esaïe 28.9-28.13 Esaïe 29.11-29.12 Jérémie 5.3-5.5 Zacharie 8.5
33 Kwa kuwa Yohana Mbatizaji alikuja, hali mkate wala hanywi divai, nanyi mwasema, Ana pepo.
Luc 1.15 Marc 1.6 Jérémie 16.8-16.10 Matthieu 10.25 Jean 10.20
34 Mwana wa Adamu amekuja, anakula na kunywa; nanyi mwasema, Tazama, mlafi huyu, na mnywaji wa divai, rafiki wao watoza ushuru na wenye dhambi.
Luc 15.2 Luc 19.7 Matthieu 9.11 Jean 12.2 Luc 14.1
35 Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.
Proverbes 8.32-8.36 Luc 7.29 Matthieu 11.19 Proverbes 17.16 Osée 14.9

Une femme verse du parfum sur Jésus

36 Mtu mmoja katika Mafarisayo alimwalika ale chakula kwake; akaingia katika nyumba yake yule Farisayo, akaketi chakulani.
Marc 14.3-14.9 Matthieu 26.5-26.6 Luc 14.1 Luc 11.37 Luc 7.34
37 Na tazama, mwanamke mmoja wa mji ule, aliyekuwa mwenye dhambi, alipopata habari ya kuwa ameketi chakulani katika nyumba ya yule Farisayo, alileta chupa ya marimari yenye marhamu.
1 Timothée 1.9 Jean 12.1-12.8 1 Pierre 4.18 1 Timothée 1.15 Luc 7.37-7.39
38 Akasimama nyuma karibu na miguu yake, akilia, akaanza kumdondoshea miguu machozi yake, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake, akiibusu-busu miguu yake na kuipaka yale marhamu.
Ecclésiaste 9.8 Psaumes 126.5-126.6 Psaumes 6.6-6.8 Genèse 18.4 Jérémie 31.9
39 Basi, yule Farisayo aliyemwalika alipoona vile, alisema moyoni mwake, Mtu huyu kama angekuwa nabii, angemtambua mwanamke huyu amgusaye, ni nani, naye ni wa namna gani, ya kwamba ni mwenye dhambi.
Luc 7.16 Marc 7.21 Luc 15.2 Matthieu 9.12-9.13 Matthieu 20.16
40 Yesu akajibu akamwambia, Simoni, nina neno nitakalo kukuambia. Akasema, Mwalimu, nena.
Luc 18.18 Matthieu 26.49 Luc 6.8 Jean 16.30 Matthieu 7.22
41 Akasema, Mtu mmoja mkopeshaji alikuwa na wadeni wawili; mmoja amwia dinari mia tano, na wa pili hamsini.
Matthieu 18.28 Romains 5.20 Luc 12.48 Luc 11.4 1 Jean 1.8-1.10
42 Nao walipokuwa hawana cha kumlipa, aliwasamehe wote wawili. Katika hao wawili ni yupi atakayempenda zaidi?
Psaumes 32.1-32.5 Galates 3.10 Jérémie 31.33-31.34 Ephésiens 4.32 Matthieu 6.12
43 Simoni akajibu akasema, Nadhani ni yule ambaye alimsamehe nyingi. Akamwambia, Umeamua haki.
Luc 10.38 2 Corinthiens 5.14-5.15 1 Timothée 1.13-1.16 Marc 12.34 1 Corinthiens 15.9-15.10
44 Akamgeukia yule mwanamke, akamwambia Simoni, Wamwona mwanamke huyu? Niliingia nyumbani kwako, hukunipa maji kwa miguu yangu; bali huyu amenidondoshea machozi miguu yangu, na kuipangusa kwa nywele za kichwa chake.
1 Timothée 5.10 Juges 19.21 Genèse 19.2 Genèse 18.4 1 Samuel 25.41
45 Wewe hukunibusu; lakini huyu tangu nilipoingia hakuacha kunibusu sana miguu yangu.
2 Samuel 15.5 Romains 16.16 2 Samuel 19.39 Genèse 29.11 Matthieu 26.48
46 Hukunipaka kichwa changu mafuta; bali huyu amenipaka miguu yangu marhamu.
Psaumes 23.5 Ecclésiaste 9.8 Daniel 10.3 Matthieu 6.17 Psaumes 104.15
47 Kwa ajili ya hayo nakuambia, Amesamehewa dhambi zake ambazo ni nyingi, kwa kuwa amependa sana; lakini asamehewaye kidogo, huyo hupenda kidogo.
1 Jean 4.19 Jean 21.15-21.17 Esaïe 1.18 1 Corinthiens 6.9-6.11 Esaïe 55.7
48 Kisha alimwambia mwanamke, Umesamehewa dhambi zako.
Matthieu 9.2 Marc 2.5 Luc 5.20
49 Ndipo wale walioketi chakulani pamoja naye walianza kusema mioyoni mwao, Ni nani huyu hata asamehe dhambi?
Matthieu 9.3 Marc 2.7 Luc 5.20-5.21
50 Akamwambia yule mwanamke, Imani yako imekuokoa, enenda zako kwa amani.
Marc 5.34 Matthieu 9.22 Luc 8.48 Luc 18.42 Marc 10.52

Cette Bible est dans le domaine public.