Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 51.45
Bible en Swahili de l’est


1 Bwana asema hivi, Angalia, nitaamsha juu ya Babeli, na juu yao wakaao Leb-kamai upepo uharibuo.
Jérémie 4.11-4.12 Osée 13.15 Jérémie 50.24 2 Rois 19.7 Jérémie 50.33
2 Nami nitapeleka wageni mpaka Babeli, watakaompepea; nao wataifanya nchi yake kuwa tupu; kwa kuwa katika siku ya taabu watakuwa juu yake pande zote.
Matthieu 3.12 Jérémie 15.7 Esaïe 41.16 Jérémie 50.32 Jérémie 50.29
3 Juu yake apindaye upinde, mwenye upinde na apinde upinde wake, na juu yake ajiinuaye katika dirii yake; msiwaachilie vijana wake; liangamizeni jeshi lake lote.
Jérémie 46.4 Jérémie 50.14 Jérémie 50.21 Esaïe 13.10-13.18 Jacques 2.13
4 Nao wataanguka, hali ya kuuawa, katika nchi ya Wakaldayo, hali ya kutumbuliwa katika njia kuu zake.
Jérémie 49.26 Esaïe 13.15 Jérémie 50.30 Esaïe 14.19 Jérémie 50.37
5 Kwa maana Israeli, wala Yuda, hakuachwa na Mungu wake, Bwana wa majeshi; ijapokuwa nchi yao imejaa hatia juu yake aliye Mtakatifu wa Israeli.
Osée 4.1 Jérémie 33.24-33.26 Osée 1.10 Romains 11.1-11.2 Jérémie 50.20
6 Kimbieni kutoka kati ya Babeli, kila mtu na ajiokoe nafsi yake; msikatiliwe mbali katika uovu wake; maana ni wakati wa kisasi cha Bwana, atamlipa malipo.
Jérémie 50.8 Jérémie 50.15 Jérémie 50.28 Jérémie 25.14 Nombres 16.26
7 Babeli umekuwa kikombe cha dhahabu mkononi mwa Bwana; kilicholevya dunia yote; mataifa wamekunywa mvinyo wake; kwa sababu hiyo mataifa wameingiwa na wazimu.
Apocalypse 14.8 Apocalypse 17.4 Apocalypse 18.3 Apocalypse 17.2 Apocalypse 18.23
8 Babeli umeanguka na kuangamia ghafula; mpigieni yowe; twaeni zeri kwa maumivu yake; ili labda apate kuponywa.
Esaïe 21.9 Jérémie 46.11 Apocalypse 14.8 Jérémie 50.2 Jérémie 48.20
9 Tungependa kuuponya Babeli, Lakini haukuponyeka; Mwacheni, nasi twendeni zetu, Kila mtu hata nchi yake mwenyewe; Maana hukumu yake inafika hata mbinguni, Nayo imeinuliwa kufikilia mawinguni.
Jérémie 50.16 Esaïe 13.14 Apocalypse 18.5 Jérémie 46.16 Esdras 9.6
10 Bwana ameitokeza haki yetu; Njoni, tutangaze katika Sayuni Habari za kazi ya Bwana, Mungu wetu.
Jérémie 50.28 Psaumes 37.6 Esaïe 40.2 Jérémie 31.6-31.9 Michée 7.9-7.10
11 Inoeni hiyo mishale; zishikeni ngao kwa nguvu; Bwana ameziamsha roho za wafalme wa Wamedi; kwa sababu shauri lake ni juu ya Babeli auangamize; maana ni kisasi cha Bwana, kisasi cha hekalu lake.
Jérémie 46.4 Jérémie 50.45 Jérémie 50.9 Jérémie 46.9 Esaïe 45.1
12 Twekeni bendera juu ya kuta za Babeli, yatieni malindo nguvu, wawekeni walinzi, tengenezeni waviziao; kwa maana Bwana ameazimia na kutenda yote aliyoyasema juu yao wakaao Babeli.
Esaïe 13.2 Jérémie 51.29 Jérémie 51.11 Nahum 2.1 Proverbes 21.30
13 Ewe ukaaye juu ya maji mengi, uliye na hazina nyingi, mwisho wako umewadia, kadiri ya tamaa zako.
Apocalypse 17.1 Esaïe 45.3 Apocalypse 17.15 Jérémie 51.36 Amos 8.2
14 Bwana wa majeshi ameapa kwa nafsi yake, akisema, Hakika nitakujaza watu, kama nzige, nao watapiga kelele juu yako.
Amos 6.8 Jérémie 49.13 Jérémie 50.15 Joël 2.25 Joël 2.3-2.4
15 Ameiumba dunia kwa uweza wake, Ameuthibitisha ulimwengu kwa hekima yake, Na kwa ufahamu wake amezitandika mbingu.
Job 9.8 Jérémie 10.12-10.16 Romains 1.20 Psaumes 104.2 Apocalypse 4.11
16 Atoapo sauti yake pana mshindo wa maji mbinguni, Naye hupandisha mawingu toka ncha za nchi; Huifanyia mvua umeme, Huutoa upepo katika hazina zake.
Psaumes 135.7 Jonas 1.4 Psaumes 18.13 Exode 14.21 Psaumes 147.18
17 Kila mtu amekuwa kama mnyama, hana maarifa; Kila mfua dhahabu amefedheheshwa na sanamu yake ya kuchonga; Maana sanamu yake ya kuyeyuka ni uongo, Wala hamna pumzi ndani yake.
Jérémie 10.14 Habakuk 2.18-2.19 Esaïe 44.18-44.20 Psaumes 115.8 Psaumes 53.1-53.2
18 Ni ubatili tu, ni kazi za udanganyifu; Wakati wa kujiliwa kwao watapotea.
Jérémie 43.12-43.13 Esaïe 19.1 Jérémie 48.7 Jérémie 10.15 Jérémie 10.8
19 Yeye, Fungu la Yakobo, siye kama hawa; Maana ndiye aliyeviumba vitu vyote; Na Israeli ni kabila ya urithi wake; Bwana wa majeshi ndilo jina lake.
Jérémie 10.16 Psaumes 73.26 1 Pierre 2.9 Jérémie 12.7-12.10 Lamentations 3.24
20 Wewe u rungu langu na silaha zangu za vita; kwa wewe nitawavunja-vunja mataifa; na kwa wewe nitaharibu falme;
Esaïe 41.15-41.16 Michée 4.13 Esaïe 10.5 Jérémie 50.23 Jérémie 27.5-27.7
21 na kwa wewe nitamvunja-vunja farasi, na yeye ampandaye; na kwa wewe nitalivunja-vunja gari la vita, na yeye achukuliwaye ndani yake;
Exode 15.1 Jérémie 50.37 Zacharie 12.4 Zacharie 10.5 Psaumes 76.6
22 na kwa wewe nitawavunja-vunja mwanamume na mwanamke; na kwa wewe nitawavunja-vunja mzee na mtoto; na kwa wewe nitawavunja-vunja kijana mwanamume na kijana mwanamke;
2 Chroniques 36.17 Esaïe 13.18 Esaïe 20.4 Esaïe 13.16 1 Samuel 15.3
23 na kwa wewe nitamvunja-vunja mchungaji na kundi lake; na kwa wewe nitamvunja-vunja mkulima na jozi yake ya ng’ombe; na kwa wewe nitawavunja-vunja maliwali na maakida.
Jérémie 51.57
24 Nami nitamlipa Babeli, na wote wakaao ndani ya Ukaldayo, mabaya yao yote, waliyoyatenda katika Sayuni mbele ya macho yenu, asema Bwana.
Jérémie 50.15 Jérémie 51.49 Psaumes 137.8-137.9 Apocalypse 18.24 Esaïe 66.6
25 Tazama, mimi ni juu yako, Ee mlima uharibuo, asema Bwana; wewe uiharibuye dunia nzima; nami nitaunyosha mkono wangu juu yako, na kukufingirisha chini toka majabalini; nami nitakufanya kuwa mlima ulioteketezwa.
Apocalypse 8.8 Zacharie 4.7 Jérémie 50.31 Esaïe 13.2 Jérémie 51.20-51.23
26 Wala hawatatwaa kwako jiwe moja liwe la pembeni, wala jiwe moja liwe msingi; bali wewe utakuwa ukiwa daima, asema Bwana.
Esaïe 13.19-13.22 Jérémie 51.43 Jérémie 50.12-50.13 Esaïe 14.23 Jérémie 51.37
27 Itwekeni bendera katika nchi, pigeni tarumbeta kati ya mataifa, yawekeni mataifa tayari juu yake; ziiteni juu yake falme za Ararati, na Mini, na Ashkenazi; agizeni jemadari juu yake; wapandisheni farasi, kama tunutu.
Genèse 10.3 Genèse 8.4 Jérémie 25.14 Jérémie 50.2 Jérémie 51.12
28 Wekeni mataifa tayari juu yake, wafalme wa Wamedi, na maliwali wake, na maakida wake, na nchi yote ya mamlaka yake.
Jérémie 51.11 Daniel 8.3-8.4 Esther 1.3 Genèse 10.2 Daniel 8.20
29 Nayo nchi yatetemeka, nayo ina utungu; maana makusudi ya Bwana juu ya Babeli yasimama, kuifanya nchi ya Babeli ukiwa, isikaliwe na mtu.
Jérémie 8.16 Jérémie 51.43 Esaïe 13.19-13.20 Jérémie 50.13 Amos 8.8
30 Mashujaa wa Babeli wameacha kupigana; Wanakaa katika ngome zao; Ushujaa wao umewapungukia; Wamekuwa kama wanawake; Makao yake yameteketea; Makomeo yake yamevunjika.
Nahum 3.13 Lamentations 2.9 Esaïe 13.7-13.8 Esaïe 19.16 Jérémie 50.36-50.37
31 Tarishi mmoja atapiga mbio kumlaki mwingine, Na mjumbe mmoja atapiga mbio kumlaki mwenziwe, Ili kumpasha habari mfalme wa Babeli, Ya kuwa mji wake umetwaliwa kila upande.
2 Samuel 18.19-18.31 2 Chroniques 30.6 Daniel 5.30 Esaïe 21.3-21.9 Job 9.25
32 Navyo vivuko vimeshambuliwa, Nayo makangaga wameyatia moto, Nao watu wa vita wameingiwa na hofu.
Esaïe 44.27 Jérémie 50.37-50.38 Jérémie 51.30
33 Kwa maana Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi; Binti Babeli amekuwa kama sakafu ya kufikichia wakati wa kukanyagwa kwake; bado kitambo kidogo na wakati wa mavuno utafika kwake.
Esaïe 21.10 Joël 3.13 Osée 6.11 Esaïe 41.15-41.16 Michée 4.13
34 Nebukadreza, mfalme wa Babeli, amenila, ameniseta, amenifanya kuwa chombo kitupu; amenimeza kama joka, amelijaza tumbo lake vitu vyangu vya anasa; amenitupa
Jérémie 50.17 Jérémie 51.44 Job 20.15 Esaïe 24.1-24.3 Lamentations 1.14-1.15
35 Udhalimu niliotendwa mimi, na uliotendwa mwili wangu, umpate Babeli; ndivyo atakavyosema yeye akaaye Sayuni; na Yerusalemu atasema, Damu yangu na iwe juu yao wakaao katika Ukaldayo.
Psaumes 137.8-137.9 Psaumes 12.5 Juges 9.20 Jacques 2.13 Jérémie 50.29
36 Basi, Bwana asema hivi, Tazama, nitakutetea, nami nitatwaa kisasi kwa ajili yako; nami nitaikausha bahari yake, nitaifanya chemchemi yake kuwa pakavu.
Jérémie 50.38 Romains 12.19 Psaumes 140.12 Esaïe 44.27 Deutéronome 32.35
37 Na Babeli utakuwa magofu, makao ya mbwa-mwitu, ajabu, na mazomeo, pasipo mtu wa kukaa huko.
Apocalypse 18.2 Jérémie 25.9 Jérémie 18.16 Jérémie 25.12 Michée 6.16
38 Watanguruma pamoja kama wana-simba; watanguruma kama simba wachanga.
Jérémie 2.15 Juges 16.20 Psaumes 34.10 Psaumes 58.6 Nahum 2.11-2.13
39 Wakiingiwa na ukali, nitawafanyizia karamu yao, nami nitawalevya, wapate kufurahi, na kulala usingizi wa milele, wasiamke tena, asema Bwana.
Jérémie 51.57 Jérémie 25.27 Daniel 5.1-5.4 Esaïe 21.4-21.5 Nahum 3.11
40 Nitawatelemsha kama wana-kondoo machinjoni, kama kondoo waume pamoja na mabeberu.
Jérémie 50.27 Esaïe 34.6 Psaumes 37.20 Psaumes 44.22 Ezéchiel 39.18
41 Jinsi Sheshaki alivyotwaliwa! Naye sifa ya dunia yote alivyoshambuliwa! Jinsi Babeli alivyokuwa ukiwa katikati ya mataifa.
Jérémie 25.26 Esaïe 13.19 Jérémie 49.25 Daniel 4.30 Jérémie 50.46
42 Bahari imefika juu ya Babeli, Umefunikwa kwa wingi wa mawimbi yake.
Esaïe 8.7-8.8 Daniel 9.26 Apocalypse 17.15-17.16 Ezéchiel 27.26-27.34 Psaumes 18.4
43 Miji yake imekuwa maganjo; Nchi ya ukame, na jangwa; Nchi asimokaa mtu ye yote, Wala hapiti mwanadamu huko.
Esaïe 13.20 Jérémie 2.6 Jérémie 51.29 Jérémie 50.39-50.40 Jérémie 50.12
44 Nami nitafanya hukumu juu ya Beli katika Babeli, nami nitavitoa katika kinywa chake alivyovimeza; wala mataifa hawatamwendea tena; naam, ukuta wa Babeli utaanguka.
Jérémie 51.34 Jérémie 51.58 Jérémie 50.2 Esaïe 2.2 Esaïe 46.1-46.2
45 Enyi watu wangu; tokeni katikati yake, mkajiokoe nafsi zenu na hasira kali ya Bwana, kila mmoja wenu.
Jérémie 51.6 Apocalypse 18.4 Jérémie 50.8 Esaïe 48.20 Genèse 19.12-19.16
46 Wala isizimie mioyo yenu, wala msiiogope habari itakayosikiwa katika nchi; maana habari itakuja mwaka mmoja, na baadaye mwaka wa pili habari itakuja, na udhalimu katika nchi, mwenye kutawala akishindana na mwenye kutawala.
2 Rois 19.7 Esaïe 13.3-13.5 Esaïe 19.2 2 Chroniques 20.23 Marc 13.7-13.8
47 Basi angalia, siku zitakuja, ambazo katika siku hizo, nitafanya hukumu juu ya sanamu za Babeli, na nchi yake yote itatahayarika; na watu wake wote waliouawa wataanguka katikati yake.
Jérémie 50.2 Jérémie 51.52 Esaïe 46.1-46.2 Esaïe 21.9 Jérémie 51.24
48 Ndipo mbingu, na nchi, na vitu vyote vilivyomo, vitaimba kwa furaha juu ya Babeli; kwa maana watu waangamizao watamjilia kutoka kaskazini, asema Bwana.
Apocalypse 18.20 Esaïe 44.23 Jérémie 50.3 Esaïe 48.20 Esaïe 49.13
49 Kama vile Babeli alivyowaangusha watu wa Israeli waliouawa, ndivyo watakavyoanguka katika Babeli watu wa nchi yake nzima waliouawa.
Jérémie 50.29 Jérémie 51.24 Apocalypse 18.5-18.6 Jacques 2.13 Jérémie 50.33-50.34
50 Ninyi mliojiepusha na upanga, Enendeni zenu, msisimame; Mkumbukeni Bwana tokea mbali, Na Yerusalemu ukatiwe mioyoni mwenu.
Jérémie 44.28 Deutéronome 4.29-4.31 Jérémie 51.45 Apocalypse 18.4 Psaumes 102.13-102.14
51 Twaona haya kwa kuwa tumesikia mashutumu; Fedheha imetufunikiza nyuso zetu; Kwa sababu wageni wamepaingia Patakatifu pa nyumba ya Bwana.
Lamentations 1.10 Psaumes 74.3-74.7 Psaumes 44.13-44.16 Psaumes 79.4 Ezéchiel 36.30
52 Kwa sababu hiyo siku zinakuja, asema Bwana, nitakapozihukumu sanamu zake; na katika nchi yake yote waliojeruhiwa wataugua.
Jérémie 51.47 Jérémie 50.38 Ezéchiel 30.24 Daniel 5.30-5.31 Esaïe 13.15-13.16
53 Babeli ujapopanda mbinguni, na ujapopafanya mahali pa juu penye nguvu zake kuwa ngome, hata hivyo toka kwangu wenye kuangamiza watamwendea, asema Bwana.
Jérémie 49.16 Genèse 11.4 Jérémie 51.25 Psaumes 139.8-139.10 Jérémie 50.25
54 Sauti ya kilio kutoka Babeli, Na ya uangamivu mkuu toka nchi ya Wakaldayo!
Jérémie 50.22 Jérémie 48.3-48.5 Jérémie 50.46 Apocalypse 18.17-18.19 Esaïe 13.6-13.9
55 Maana Bwana amwangamiza Babeli, Na kuikomesha sauti kuu ndani yake; Na mawimbi yake yavuma kama maji mengi, Mshindo wa sauti zao wafanya makelele;
Jérémie 25.10 Psaumes 18.4 Esaïe 17.13 Esaïe 24.8-24.11 Jérémie 51.42
56 Kwa maana mwenye kuangamiza amefika kwake; Naam, amefika Babeli; Na mashujaa wake wametwaliwa; Pinde zao zimevunjika kabisa; Maana Bwana ni Mungu wa kisasi; Hakika yake yeye atalipa.
Jérémie 51.6 Psaumes 46.9 Jérémie 51.48 Psaumes 94.1-94.2 Habakuk 2.8
57 Nami nitawalevya wakuu wake, na watu wake wenye hekima, maliwali wake, na maakida wake, na mashujaa wake; nao watalala usingizi wa milele, wasiamke, asema Mfalme, Bwana wa majeshi, ambaye jina lake ni Bwana.
Jérémie 46.18 Jérémie 25.27 Jérémie 48.15 Jérémie 51.39 Psaumes 76.5-76.6
58 Bwana wa majeshi asema hivi, Kuta pana za Babeli zitabomolewa kabisa, na malango yake marefu yatateketezwa; nao watu watajitaabisha kwa ubatili, na mataifa kwa moto; nao watachoka.
Habakuk 2.13 Jérémie 51.64 Jérémie 51.44 Jérémie 50.15 Esaïe 45.1-45.2
59 Neno ambalo Yeremia, nabii, alimwamuru Seraya, mwana wa Neria, mwana wa Maaseya, alipokwenda Babeli pamoja na Sedekia, mfalme wa Yuda, katika mwaka wa nne wa kumiliki kwake. Basi Seraya alikuwa msimamizi mkuu wa nyumba ya mfalme.
Jérémie 32.12 Jérémie 36.4 Jérémie 45.1 Jérémie 28.1 Jérémie 52.1
60 Naye Yeremia akaandika katika kitabu habari ya mabaya yote yatakayoupata Babeli, maneno hayo yote yaliyoandikwa juu ya Babeli.
Habakuk 2.2-2.3 Jérémie 30.2-30.3 Esaïe 30.8 Jérémie 36.32 Jérémie 36.2-36.4
61 Naye Yeremia akamwambia Seraya, Utakapofika Babeli, basi angalia uyasome maneno haya yote,
Jérémie 29.1-29.2 Colossiens 4.16 1 Thessaloniciens 5.27 Apocalypse 1.3 1 Thessaloniciens 4.18
62 ukaseme, Ee Bwana, umenena habari za mji huu kwamba utakatiliwa mbali, usikaliwe na awaye yote, wala wanadamu wala wanyama, lakini uwe ukiwa hata milele.
Jérémie 50.3 Jérémie 50.13 Apocalypse 18.20-18.23 Esaïe 14.22-14.23 Ezéchiel 35.9
63 Tena itakuwa utakapokwisha kukisoma kitabu hicho, utakifungia jiwe, na kukitupa katika mto Frati;
Apocalypse 18.21 Jérémie 19.10-19.11
64 nawe utasema, Hivyo ndivyo utakavyozama Babeli, wala hautazuka tena, kwa sababu ya mabaya yote nitakayoleta juu yake; nao watachoka. Maneno ya Yeremia yamefika hata hapa.
Jérémie 51.58 Job 31.40 Nahum 1.8-1.9 Apocalypse 18.21 Psaumes 72.20

Cette Bible est dans le domaine public.