Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 25.27
Bible en Swahili de l’est


Mort d’Abraham

1 Ibrahimu alioa mke mwingine jina lake akiitwa Ketura.
Genèse 28.1 1 Chroniques 1.32-1.33 Genèse 23.1-23.2
2 Akamzalia Zimrani, na Yokshani, na Medani, na Midiani, na Ishbaki, na Sua.
1 Chroniques 1.32-1.33 Jérémie 25.25 Genèse 37.36 Genèse 37.28 Genèse 36.35
3 Yokshani akamzaa Sheba, na Dedani; na wana wa Dedani walikuwa Waashuri na Waletushi, na Waleumi.
Ezéchiel 25.13 2 Samuel 2.9 Psaumes 72.10 Ezéchiel 27.20 Jérémie 25.23
4 Na wana wa Midiani walikuwa, Efa, na Eferi, na Hanoki, na Abida, na Eldaa. Hao wote walikuwa ni wana wa Ketura.
Esaïe 60.6
5 Ibrahimu akampa Isaka yote aliyokuwa nayo.
Genèse 24.36 Matthieu 11.27 Colossiens 1.19 Psaumes 68.18 Galates 4.28
6 Lakini wana wa masuria aliokuwa nao Ibrahimu, Ibrahimu akawapa zawadi, naye akawaondoa katika mahali alipokaa Isaka mwanawe, wakati wa uhai wake, waende pande za mashariki, mpaka nchi ya Kedemu.
Genèse 21.14 Juges 6.3 Genèse 30.4 Matthieu 5.45 Genèse 32.22
7 Hizi ndizo siku za miaka ya maisha ya Ibrahimu alizoishi, miaka mia, na sabini na mitano.
Genèse 12.4
8 Ibrahimu akafariki, naye akafa katika uzee mwema, mzee sana, ameshiba siku, akakusanyika kwa watu wake.
Genèse 49.33 Genèse 25.17 Genèse 15.15 Genèse 49.29 Genèse 47.8-47.9
9 Isaka na Ishmaeli wanawe wakamzika katika pango ya Makpela, katika shamba la Efroni bin Sohari Mhiti, lielekealo Mamre.
Genèse 35.29 Genèse 50.13 Genèse 49.29-49.30 Genèse 23.9-23.20 Genèse 21.9-21.10
10 Katika lile shamba alilolinunua Ibrahimu kwa wazawa Hethi, huko ndiko alikozikwa Ibrahimu na Sara mkewe.
Genèse 23.16 Genèse 49.31
11 Ikawa, baada ya kufa kwake Ibrahimu, Mungu akambariki Isaka mwanawe. Naye Isaka akakaa karibu ya Beer-lahai-roi.
Genèse 16.14 Genèse 24.62 Genèse 12.2 Genèse 22.17 Genèse 50.24

Descendance d’Ismaël

12 Hivi ndivyo vizazi vya Ishmaeli, mwana wa Ibrahimu, ambaye Hajiri, Mmisri, mjakazi wa Sara, alimzalia Ibrahimu.
Genèse 17.20 Genèse 21.13 Psaumes 83.6 Genèse 16.10-16.15
13 Na haya ndiyo majina ya wana wa Ishmaeli, kwa majina yao, na kwa vizazi vyao. Mzaliwa wa kwanza wa Ishmaeli, ni Nebayothi, na Kedari, na Abdeeli, na Mibsamu,
1 Chroniques 1.29-1.31 Esaïe 60.7 Cantique 1.5 Psaumes 120.5 Esaïe 21.16-21.17
14 na Mishma, na Duma, na Masa,
Esaïe 21.16 Esaïe 21.11
15 na Hadadi, na Tema, na Yeturi, na Nafishi, na Kedema.
1 Chroniques 5.19 Job 2.11
16 Hao ndio wana wa Ishmaeli, na hayo ni majina yao, katika miji yao, na katika vituo vyao, maseyidi kumi na wawili kwa kufuata jamaa zao.
Genèse 17.20 Genèse 17.23
17 Na hii ndiyo miaka ya maisha ya Ishmaeli, miaka mia na thelathini na saba. Akakata roho, akafa, akakusanyika kwa watu wake.
Genèse 15.15 Genèse 25.7-25.8
18 Wakakaa toka Havila mpaka Shuri, unaoelekea Misri, kwa njia ya kwenda Ashuru. Akakaa katikati ya ndugu zake wote.
Genèse 16.12 Genèse 20.1 Psaumes 78.64 Genèse 14.10 Esaïe 19.23-19.24

Histoire d’Isaac

Naissance d’Ésaü et Jacob

19 Na hivi ndivyo vizazi vya Isaka, mwana wa Ibrahimu. Ibrahimu alimzaa Isaka.
Matthieu 1.2 1 Chroniques 1.32 Luc 3.34 Actes 7.8
20 Isaka akawa mwenye miaka arobaini alipomtwaa Rebeka binti Bethueli, Mshami, wa Padan-aramu, ndugu wa Labani, Mshami, kuwa mke wake.
Genèse 24.29 Genèse 24.67 Genèse 22.23 Genèse 31.24 Genèse 28.5-28.6
21 Isaka akamwomba Bwana kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye Bwana akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba.
Esdras 8.23 2 Chroniques 33.13 1 Chroniques 5.20 Genèse 11.30 Romains 9.10-9.12
22 Watoto wakashindana tumboni mwake. Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda kumwuliza Bwana.
1 Samuel 9.9 1 Samuel 10.22 Ezéchiel 36.37 Ezéchiel 20.31 1 Samuel 22.15
23 Bwana akamwambia,Mataifa mawili yamo tumboni mwako,Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako.Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili,Na mkubwa atamtumikia mdogo.
Genèse 27.29 Genèse 27.40 2 Samuel 8.14 Nombres 20.14 Genèse 24.60
24 Siku zake za kuzaa zilipotimia, tazama! Mapacha walikuwamo tumboni mwake.
25 Wa kwanza akatoka, naye alikuwa mwekundu mwili wote kama vazi la nywele. Wakamwita jina lake Esau.
Genèse 27.11 Genèse 27.16 Genèse 27.23
26 Baadaye ndugu yake akatoka, na mkono wake unamshika Esau kisigino. Akaitwa jina lake Yakobo. Isaka alikuwa mwenye miaka sitini mkewe alipowazaa.
Genèse 27.36 Osée 12.3 Genèse 38.28-38.30
27 Watoto wakakua, Esau alikuwa mtu ajuaye kuwinda wanyama, mtu wa nyikani, na Yakobo alikuwa mtu mtulivu, mwenye kukaa hemani.
Hébreux 11.9 Genèse 21.20 Genèse 46.34 Job 2.3 Job 1.8
28 Basi Isaka akampenda Esau, kwa sababu alikula mawindo yake, na Rebeka akampenda Yakobo.
Genèse 27.19 Genèse 27.4 Genèse 27.31 Genèse 27.6-27.7 Genèse 27.25
29 Yakobo akapika chakula cha dengu. Esau akaja kutoka nyikani, naye alikuwa amechoka sana.
Juges 8.4-8.5 1 Samuel 14.31 Proverbes 13.25 Esaïe 40.30-40.31 1 Samuel 14.28
30 Esau akamwambia Yakobo, Tafadhali, unipe hicho chakula chekundu nile, kwa kuwa ninazimia mimi. Kwa hiyo walimwita jina lake Edomu.
Genèse 36.1 Genèse 36.9 Exode 15.15 Genèse 36.43 Deutéronome 23.7
31 Yakobo akamwambia, Kwanza niuzie leo haki yako ya mzaliwa wa kwanza.
32 Esau akasema, Tazama, mimi ni karibu kufa, itanifaa nini haki hii ya uzazi?
Exode 22.9 Job 21.15 Malachie 3.14 Job 34.9 Job 22.17
33 Yakobo akamwambia, Uniapie kwanza. Naye akamwapia, akamwuzia Yakobo haki yake ya mzaliwa wa kwanza.
Hébreux 12.16 Genèse 27.36 Marc 6.23 Genèse 36.6-36.7 Genèse 14.22
34 Yakobo akampa Esau mkate na chakula cha dengu, naye akala, akanywa, kisha akaondoka, akaenda zake. Hivyo Esau akaidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.
Hébreux 12.16-12.17 Psaumes 106.24 Zacharie 11.13 Matthieu 26.15 Matthieu 22.5

Cette Bible est dans le domaine public.