Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 15.24
Bible en Swahili de l’est


Guerre contre les Amalécites

1 Wakati huo Samweli akamwambia Sauli, Bwana alinipeleka nikutie mafuta, uwe mfalme wa watu wake Israeli; basi sasa, isikilize sauti na maneno ya Bwana.
1 Samuel 9.16 1 Samuel 10.1 1 Samuel 12.14 Psaumes 2.10-2.11 2 Samuel 23.2-23.3
2 Bwana wa majeshi asema hivi, Nimeyatia moyoni mwangu mambo hayo Amaleki waliyowatenda Israeli, jinsi walivyowapinga njiani, hapo walipopanda kutoka Misri.
Nombres 24.20 Deutéronome 25.17-25.19 Exode 17.8-17.16 Osée 7.2 Amos 8.7
3 Basi sasa enda ukawapige Amaleki, na kuviharibu kabisa vitu vyote walivyo navyo, wala msiwaachilie; bali waueni, mwanamume na mwanamke, mtoto naye anyonyaye, ng’ombe na kondoo, ngamia na punda.
Nombres 24.20 Deutéronome 20.16-20.18 Josué 6.17-6.21 1 Samuel 22.19 Nombres 31.17
4 Ndipo Sauli akawaita watu, akawahesabu huko Telemu, askari waliopanda farasi mia mbili elfu, na watu wa Yuda kumi elfu.
Josué 15.24 1 Samuel 13.15 1 Samuel 11.8
5 Sauli akaufikilia mji wa Amaleki, akauvizia bondeni.
6 Sauli akawaambia Wakeni, Haya! Enendeni zenu, mkashuke ili kujitenga na Waamaleki, nisije nikawaangamiza ninyi pamoja nao; maana mliwatendea wana wa Israeli mema, walipopanda kutoka Misri. Basi hao Wakeni wakaondoka, wakajitenga na Waamaleki.
Juges 1.16 Exode 18.19 Nombres 10.29-10.32 Juges 4.11 Nombres 24.21-24.22
7 Sauli akawapiga Waamaleki, toka Havila uendapo Shuri, unaokabili Misri.
Genèse 25.18 1 Samuel 14.48 Genèse 16.7 1 Samuel 27.8 Exode 15.22
8 Akamkamata Agagi, mfalme wa Waamaleki, yu hai, akawaangamiza hao watu wote kwa upanga.
1 Samuel 30.1 Nombres 24.7 Esther 3.1 1 Rois 20.30 1 Samuel 15.3
9 Lakini Sauli na watu wake wakamwacha Agagi hai, na katika kondoo walio wazuri, na ng’ombe, na vinono, na wana-kondoo, na cho chote kilicho chema, wala hawakukubali kuwaangamiza; bali cho chote kilichokuwa kibaya na kibovu, ndicho walichokiangamiza kabisa.
1 Samuel 15.15 1 Samuel 15.3 1 Samuel 15.19 Josué 7.21 2 Samuel 6.13
10 Ndipo neno la Bwana likamjia Samweli, kusema,
11 Najuta kwa sababu nimemtawaza Sauli awe mfalme; maana amerudi nyuma, asinifuate, wala hakufanya nilivyomwamuru. Samweli akasikitika, akamlilia Bwana usiku kucha.
1 Samuel 13.13 Genèse 6.6 2 Samuel 24.16 Josué 22.16 1 Samuel 15.3
12 Samweli akaondoka asubuhi na mapema ili aonane na Sauli; Samweli akaambiwa ya kwamba, Sauli alifika Karmeli, na tazama, akajisimamishia ukumbusho, akageuka, akapita, akatelemkia Gilgali.
Josué 15.55 2 Samuel 18.18 1 Samuel 25.2 1 Rois 18.42 Josué 4.8-4.9
13 Samweli akamwendea Sauli; naye Sauli akamwambia, Ubarikiwe na Bwana, nimeitimiza amri ya Bwana.
Ruth 3.10 Juges 17.2 Genèse 14.19 Proverbes 27.2 Luc 17.10
14 Samweli akasema, Maana yake nini, basi, hiki kilio cha kondoo masikioni mwangu, na huu mlio wa ng’ombe ninaousikia?
Jérémie 2.34-2.37 Malachie 3.13-3.15 Romains 3.19 Jérémie 2.22-2.23 Psaumes 50.16-50.21
15 Sauli akasema, Wamewaleta kutoka kwa Waamaleki; maana watu waliwaacha hai kondoo na ng’ombe walio wazuri, ili wawatoe dhabihu kwa Bwana, Mungu wako, nao waliosalia tumewaangamiza kabisa.
1 Samuel 15.9 1 Samuel 15.21 Exode 32.22-32.23 Genèse 3.12-3.13 Proverbes 28.13
16 Ndipo Samweli akamwambia Sauli, Ngoja, nami nitakuambia neno aliloniambia Bwana usiku huu. Naye akamwambia, Haya, sema.
1 Samuel 9.27 1 Samuel 12.7 1 Rois 22.16
17 Basi Samweli akasema, Ingawa ulikuwa mdogo machoni pako mwenyewe, je! Hukufanywa kuwa kichwa cha kabila za Israeli? Naye Bwana akakutia mafuta uwe mfalme wa Israeli.
1 Samuel 9.21 1 Samuel 10.22 1 Samuel 15.1-15.3 Juges 6.15 Matthieu 18.4
18 Kisha Bwana akakutuma safarini, akasema, Enenda ukawaangamize kabisa wale Waamaleki wenye dhambi, upigane nao hata watakapoangamia.
Proverbes 10.29 Nombres 16.38 Job 31.3 Genèse 15.16 Proverbes 13.21
19 Mbona, basi, hukuitii sauti ya Bwana, bali ukazirukia nyara ukafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana?
1 Samuel 14.32 2 Timothée 4.10 2 Chroniques 36.12 2 Chroniques 33.2 Proverbes 15.27
20 Sauli akamwambia Samweli, Hakika mimi nimeitii sauti ya Bwana, nami nimemleta Agagi, mfalme wa Waamaleki, tena nimewaangamiza Waamaleki kabisa.
1 Samuel 15.13 Job 35.2 Job 33.9 Job 34.5 Luc 10.29
21 Ila watu waliteka nyara, kondoo na ng’ombe walio wazuri, katika vitu vilivyowekwa wakfu, kusudi wavitoe dhabihu kwa Bwana, Mungu wako, huko Gilgali.
1 Samuel 15.15 Exode 32.22-32.23 Genèse 3.13
22 Naye Samweli akasema, je! Bwana huzipenda sadaka za kuteketezwa na dhabihu Sawasawa na kuitii sauti ya Bwana? Angalia, kutii ni bora kuliko dhabihu, Na kusikia kuliko mafuta ya beberu.
Osée 6.6 Psaumes 51.16-51.17 Matthieu 9.13 Proverbes 21.3 Marc 12.33
23 Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, Na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; Kwa kuwa umelikataa neno la Bwana, Yeye naye amekukataa wewe usiwe mfalme.
1 Samuel 13.14 Esaïe 8.19 Deutéronome 18.10-18.11 Deutéronome 9.7 Esaïe 19.3
24 Ndipo Sauli akamwambia Samweli, Nimefanya dhambi; maana nimeihalifu amri ya Bwana, pia na maneno yako; kwa sababu naliwaogopa wale watu, nikaitii sauti yao.
Esaïe 51.12-51.13 2 Samuel 12.13 Proverbes 29.25 Nombres 22.34 Exode 9.27
25 Basi sasa, nakuomba, unisamehe dhambi yangu; rudi pamoja nami, nipate kumwabudu Bwana.
Exode 10.17
26 Samweli akasema, Sitarudi pamoja nawe; kwa sababu umelikataa neno la Bwana, Bwana naye amekukataa wewe, usiwe mfalme wa Israeli.
1 Samuel 16.1 Osée 4.6 1 Samuel 13.14 1 Samuel 15.23 1 Samuel 2.30
27 Naye Samweli alipogeuka, aende zake, Sauli akaushika upindo wa vazi lake, nalo likararuka.
1 Rois 11.30-11.31
28 Basi Samweli akamwambia, Leo Bwana amekurarulia ufalme wa Israeli, naye amempa jirani yako, aliye mwema kuliko wewe.
1 Samuel 28.17-28.18 1 Samuel 13.14 Jean 19.11 Romains 13.1 Jérémie 27.5-27.6
29 Tena Yeye aliye Nguvu za Israeli hatanena uongo, wala hataona majuto; maana siye mwanadamu, hata ajute.
Nombres 23.19 Ezéchiel 24.14 Tite 1.2 Philippiens 4.13 1 Chroniques 29.11
30 Akasema, Nimekosa; lakini uniheshimu sasa, nakuomba, mbele ya wazee wa watu wangu, na mbele ya Israeli, rudi pamoja nami, nimwabudu Bwana, Mungu wako.
Jean 5.44 Jean 12.43 Esaïe 29.13 Luc 18.9-18.14 2 Timothée 3.5
31 Basi Samweli akarudi na kuandamana na Sauli; naye Sauli akamwabudu Bwana.
32 Ndipo Samweli akasema, Nileteeni hapa Agagi, mfalme wa Waamaleki. Basi Agagi akamwendea kwa utepetevu. Naye Agagi akasema, Bila shaka uchungu wa mauti umeondoka.
Jérémie 48.44 1 Thessaloniciens 5.3 Apocalypse 18.7
33 Lakini Samweli akamjibu, Kama upanga wako ulivyofanya wanawake kufiwa na watoto wao, vivyo hivyo mama yako atafiwa miongoni mwa wanawake. Basi Samweli akamkata Agagi vipande mbele za Bwana huko Gilgali.
Juges 1.7 Genèse 9.6 Matthieu 7.2 Exode 17.11 Apocalypse 18.6
34 Na baada ya hayo Samweli akaenda zake kule Rama; naye Sauli akakwea kwenda nyumbani kwake huko Gibea ya Sauli.
1 Samuel 11.4 1 Samuel 7.17
35 Wala Samweli hakuenda tena kuonana na Sauli hata siku ya kufa kwake; lakini Samweli alikuwa akimlilia Sauli; naye Bwana akaghairi ya kuwa amemtawaza Sauli awe mfalme juu ya Israeli.
1 Samuel 15.11 1 Samuel 19.24 1 Samuel 16.1 Genèse 6.6 Jérémie 9.1-9.2

Cette Bible est dans le domaine public.