Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jacques 2.8
Bible en Swahili de l’est


L’impartialité de la foi

1 Ndugu zangu, imani ya Bwana wetu Yesu Kristo, Bwana wa utukufu, msiwe nayo kwa kupendelea watu.
Lévitique 19.15 Proverbes 24.23 Jacques 2.9 Matthieu 22.16 Deutéronome 16.19
2 Maana akiingia katika sinagogi lenu mtu mwenye pete ya dhahabu na mavazi mazuri; kisha akiingia na maskini, mwenye mavazi mabovu;
Esther 8.2 Zacharie 3.3-3.4 Esther 3.10 Luc 15.22 Genèse 27.15
3 nanyi mkimstahi yule aliyevaa mavazi mazuri, na kumwambia, Keti wewe hapa mahali pazuri; na kumwambia yule maskini, Simama wewe pale, au keti miguuni pangu,
2 Corinthiens 8.9 Luc 7.44-7.46 Jude 1.16 Jacques 2.6 Esaïe 65.5
4 je! Hamkufanya hitilafu mioyoni mwenu, mkawa waamuzi wenye mawazo mabovu?
Jean 7.24 Jacques 4.11 Matthieu 7.1-7.5 Job 34.19 Malachie 2.9
5 Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa ufalme aliowaahidia wampendao?
Matthieu 5.3 Luc 12.21 Jacques 1.12 Luc 6.20 Luc 12.32
6 Bali ninyi mmemvunjia heshima maskini. Je! Matajiri hawawaonei ninyi na kuwavuta mbele ya viti vya hukumu?
1 Corinthiens 11.22 Actes 17.6 Actes 13.50 Actes 18.12 Psaumes 14.6
7 Hawalitukani jina lile zuri mliloitwa?
Philippiens 2.9-2.11 Actes 11.26 Apocalypse 13.5-13.6 Psaumes 111.9 Matthieu 1.23
8 Lakini mkiitimiza ile sheria ya kifalme kama ilivyoandikwa, Mpende jirani yako kama nafsi yako, mwatenda vema.
Lévitique 19.18 Galates 5.14 Jacques 2.12 Jonas 4.9 Galates 6.2
9 Bali mkiwapendelea watu, mwafanya dhambi na kuhukumiwa na sheria kuwa wakosaji.
Lévitique 19.15 Jean 8.9 Jean 8.46 1 Jean 3.4 Jude 1.15
10 Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote.
Galates 3.10 Deutéronome 27.26 Matthieu 5.18-5.19
11 Kwa maana yeye aliyesema, Usizini, pia alisema, Usiue. Basi ijapokuwa hukuzini, lakini umeua, umekuwa mvunja sheria.
Exode 20.13-20.14 Deutéronome 5.17-5.18 Matthieu 5.21-5.28 Romains 13.9 Psaumes 130.3-130.4
12 Semeni ninyi, na kutenda kama watu watakaohukumiwa kwa sheria ya uhuru.
Jacques 1.25 Jacques 2.8 2 Pierre 1.4-1.8 Colossiens 3.17 Philippiens 4.8
13 Maana hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma. Huruma hujitukuza juu ya hukumu.
Proverbes 21.13 Matthieu 6.15 Matthieu 5.7 Matthieu 18.28-18.35 Luc 6.37

Les œuvres de la foi

14 Ndugu zangu, yafaa nini, mtu akisema ya kwamba anayo imani, lakini hana matendo? Je! Ile imani yaweza kumwokoa?
Matthieu 7.26-7.27 Matthieu 7.21-7.23 Jacques 1.22-1.25 2 Pierre 1.5 Hébreux 13.9
15 Ikiwa ndugu mwanamume au ndugu mwanamke yu uchi na kupungukiwa na riziki,
Luc 3.11 Matthieu 25.35-25.40 Esaïe 58.10 Job 31.16-31.21 Jacques 2.5
16 na mtu wa kwenu akawaambia, Enendeni zenu kwa amani, mkaote moto na kushiba, lakini asiwape mahitaji ya mwili, yafaa nini?
1 Jean 3.16-3.18 Romains 12.9 Matthieu 25.42-25.45 Job 22.7-22.9 Proverbes 3.27-3.28
17 Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake.
Jacques 2.26 Jacques 2.14 1 Timothée 1.5 Jacques 2.19-2.20 2 Pierre 1.5-1.9
18 Lakini mtu atasema, Wewe unayo imani, nami ninayo matendo. Nionyeshe imani yako pasipo matendo, nami nitakuonyesha imani yangu kwa njia ya matendo yangu.
Jacques 3.13 Tite 2.7 Galates 5.6 Jacques 2.14 Tite 2.11-2.14
19 Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka.
Luc 4.34 Marc 1.24 Matthieu 8.29 Actes 16.17 Marc 5.7
20 Lakini wataka kujua, wewe mwanadamu usiye kitu, kwamba imani pasipo matendo haizai?
Proverbes 12.11 Galates 5.6 Romains 1.21 Jacques 2.26 1 Timothée 1.6
21 Je! Baba yetu Ibrahimu hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipomtoa Isaka mwanawe juu ya madhabahu?
Genèse 22.16-22.18 Genèse 22.9-22.12 Luc 1.73 Luc 16.30 Romains 4.16
22 Waona kwamba imani ilitenda kazi pamoja na matendo yake, na ya kwamba imani ile ilikamilishwa kwa njia ya matendo yale.
1 Thessaloniciens 1.3 Hébreux 11.17-11.19 Galates 5.6 Jacques 2.18 1 Jean 2.5
23 Maandiko yale yakatimizwa yaliyonena, Ibrahimu alimwamini Mungu, ikahesabiwa kwake kuwa ni haki; naye aliitwa rafiki wa Mungu.
Esaïe 41.8 2 Chroniques 20.7 Genèse 15.6 Galates 3.6 Romains 4.3-4.6
24 Mwaona kwamba mwanadamu huhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo yake; si kwa imani peke yake.
Jacques 2.21-2.22 Jacques 2.15-2.18 Psaumes 60.12
25 Vivyo hivyo na Rahabu, yule kahaba naye, je! Hakuhesabiwa kuwa ana haki kwa matendo, hapo alipowakaribisha wajumbe, akawatoa nje kwa njia nyingine?
Hébreux 11.31 Josué 2.1 Josué 2.4 Josué 6.22-6.25 Josué 2.19-2.21
26 Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa.
Jacques 2.20 Jacques 2.17 Ecclésiaste 12.7 Psaumes 146.4 Psaumes 104.29

Cette Bible est dans le domaine public.