Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Ephésiens 4.3
Bible en Swahili de l’est


L’unité de l’Esprit

1 Kwa hiyo nawasihi, mimi niliye mfungwa katika Bwana, mwenende kama inavyoustahili wito wenu mlioitiwa;
Colossiens 1.10 Philippiens 1.27 1 Thessaloniciens 2.12 1 Thessaloniciens 4.1-4.2 2 Pierre 1.3
2 kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo;
Colossiens 3.12-3.13 1 Corinthiens 13.7 1 Pierre 3.15 1 Corinthiens 13.4-13.5 Matthieu 5.3-5.5
3 na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani.
Jean 17.21-17.23 1 Corinthiens 1.10 1 Corinthiens 12.12-12.13 Ephésiens 4.4 Hébreux 12.14
4 Mwili mmoja, na Roho mmoja, kama na mlivyoitwa katika tumaini moja la wito wenu.
1 Corinthiens 12.4-12.13 Romains 12.4-12.5 Ephésiens 2.18 Ephésiens 1.18 1 Corinthiens 12.20
5 Bwana mmoja, imani moja, ubatizo mmoja.
1 Corinthiens 8.6 1 Pierre 3.21 Romains 3.30 Matthieu 28.19 Jude 1.3
6 Mungu mmoja, naye ni Baba wa wote, aliye juu ya yote na katika yote na ndani ya yote.
Romains 11.36 1 Corinthiens 12.6 Malachie 2.10 Ephésiens 3.17 Galates 4.3-4.7
7 Lakini kila mmoja wetu alipewa neema kwa kadiri ya kipimo cha kipawa chake Kristo.
Romains 12.3 1 Pierre 4.10 Matthieu 25.15 Romains 12.6-12.8 1 Corinthiens 12.28-12.30
8 Hivyo husema, Alipopaa juu aliteka mateka, Akawapa wanadamu vipawa.
Psaumes 68.18 Colossiens 2.15 1 Samuel 30.26
9 Basi neno hilo, Alipaa, maana yake nini kama siyo kusema kwamba yeye naye alishuka mpaka pande zilizo chini za nchi?
Jean 3.13 Jean 6.33 Psaumes 63.9 Matthieu 12.40 Psaumes 139.15
10 Naye aliyeshuka ndiye yeye aliyepaa juu sana kupita mbingu zote, ili avijaze vitu vyote.
Hébreux 4.14 Hébreux 7.26 Colossiens 2.9 Matthieu 24.34 Actes 1.9
11 Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu;
Jérémie 3.15 1 Corinthiens 12.28-12.29 2 Timothée 4.5 Ephésiens 2.20 Ephésiens 3.5
12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe;
1 Corinthiens 12.27 Ephésiens 4.16 Romains 15.14 Hébreux 13.17 Romains 14.19
13 hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo;
Colossiens 1.28 Ephésiens 4.5 Ephésiens 4.3 Ephésiens 1.23 Jean 17.21
14 ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu.
Hébreux 13.9 1 Corinthiens 14.20 Jacques 1.6 Romains 16.17-16.18 2 Corinthiens 2.17
15 Lakini tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, Kristo.
Ephésiens 1.22 1 Jean 3.18 Ephésiens 4.25 Ephésiens 2.21 2 Pierre 3.18
16 Katika yeye mwili wote ukiungamanishwa na kushikanishwa kwa msaada wa kila kiungo, kwa kadiri ya utendaji wa kila sehemu moja moja, huukuza mwili upate kujijenga wenyewe katika upendo.
Colossiens 2.19 Jean 15.5 Ephésiens 4.12 1 Corinthiens 13.13-14.1 Ephésiens 4.15

La vie nouvelle en Christ

17 Basi nasema neno hili, tena nashuhudia katika Bwana, tangu sasa msienende kama Mataifa waenendavyo, katika ubatili wa nia zao;
Romains 1.21 Ephésiens 2.1-2.3 Colossiens 2.4 1 Pierre 4.3-4.4 1 Pierre 1.18
18 ambao; akili zao zimetiwa giza, nao wamefarikishwa na uzima wa Mungu, kwa sababu ya ujinga uliomo ndani yao, kwa sababu ya ugumu wa mioyo yao;
Ephésiens 2.12 Romains 1.21-1.23 1 Thessaloniciens 4.5 Colossiens 1.21 Galates 4.8
19 ambao wakiisha kufa ganzi wanajitia katika mambo ya ufisadi wapate kufanyiza kila namna ya uchafu kwa kutamani.
1 Timothée 4.2 Romains 1.24-1.26 Colossiens 3.5 Apocalypse 18.3 1 Pierre 4.3
20 Bali ninyi, sivyo mlivyojifunza Kristo;
Tite 2.11-2.14 Jean 6.45 Romains 6.1-6.2 Matthieu 11.29 Luc 24.47
21 ikiwa mlimsikia mkafundishwa katika yeye, kama kweli ilivyo katika Yesu,
Ephésiens 1.13 1 Jean 5.10-5.12 1 Jean 5.20 2 Corinthiens 1.20 Colossiens 2.7
22 mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unaoharibika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya;
Hébreux 12.1 Jacques 1.21 Romains 6.6 Hébreux 3.13 Ephésiens 4.25
23 na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu;
Romains 12.2 Romains 8.6 Ezéchiel 36.26 Colossiens 3.10 1 Pierre 1.13
24 mkavae utu mpya, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli.
Colossiens 3.10-3.14 Ephésiens 2.10 2 Corinthiens 5.17 Romains 13.14 Romains 6.4
25 Basi uvueni uongo, mkaseme kweli kila mtu na jirani yake; kwa maana tu viungo, kila mmoja kiungo cha wenzake.
Colossiens 3.9 Romains 12.5 Zacharie 8.16 Ephésiens 4.15 Proverbes 12.22
26 Mwe na hasira, ila msitende dhambi; jua lisichwe na uchungu wenu bado haujawatoka;
Psaumes 4.4 Jacques 1.19 Psaumes 37.8 Ecclésiaste 7.9 Ephésiens 4.31-4.32
27 wala msimpe Ibilisi nafasi.
Jacques 4.7 1 Pierre 5.8 Ephésiens 6.16 Ephésiens 6.11 Actes 5.3
28 Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo nzuri kwa mikono yake mwenyewe, apate kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji.
Exode 20.15 2 Thessaloniciens 3.11-3.12 1 Thessaloniciens 4.11-4.12 1 Timothée 6.18 2 Corinthiens 8.12
29 Neno lo lote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema la kumfaa mwenye kuhitaji, ili liwape neema wanaosikia.
Colossiens 4.6 Proverbes 15.7 Proverbes 12.13 Ecclésiaste 10.12 1 Thessaloniciens 5.11
30 Wala msimhuzunishe yule Roho Mtakatifu wa Mungu; ambaye kwa yeye mlitiwa muhuri hata siku ya ukombozi.
1 Thessaloniciens 5.19 Esaïe 63.10 Ephésiens 1.13-1.14 Psaumes 95.10 Romains 8.23
31 Uchungu wote na ghadhabu na hasira na kelele na matukano yaondoke kwenu, pamoja na kila namna ya ubaya;
Colossiens 3.8 Ecclésiaste 7.9 1 Pierre 2.1 Colossiens 3.19 Jacques 1.19
32 tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.
Colossiens 3.12-3.13 2 Corinthiens 2.10 1 Pierre 3.8-3.9 Matthieu 6.14-6.15 Ephésiens 5.1

Cette Bible est dans le domaine public.