Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Corinthiens 8.23
Bible en Swahili de l’est


Instructions pour la collecte

Exemple des Églises de Macédoine et mission de Tite

1 Tena ndugu zetu, twawaarifu habari ya neema ya Mungu, waliyopewa makanisa ya Makedonia;
Actes 16.9 1 Thessaloniciens 4.10 Colossiens 1.29 Actes 11.23 Romains 15.26
2 maana walipokuwa wakijaribiwa kwa dhiki nyingi, wingi wa furaha yao na umaskini wao uliokuwa mwingi uliwaongezea utajiri wa ukarimu wao.
Jacques 2.5 2 Corinthiens 9.13 Proverbes 11.25 1 Thessaloniciens 1.6 Romains 12.8
3 Maana nawashuhudia kwamba, kwa uwezo wao, na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe walitoa vitu vyao;
Exode 35.29 1 Chroniques 29.9 Exode 35.5 1 Chroniques 29.5-29.6 1 Corinthiens 16.2
4 wakituomba sana pamoja na kutusihi kwa habari ya neema hii, na shirika hili la kuwahudumia watakatifu.
Actes 24.17 1 Corinthiens 16.3-16.4 2 Corinthiens 9.1 Romains 15.25-15.26 2 Corinthiens 9.12-9.14
5 Tena walitenda hivi si kama tulivyotumaini tu, bali kwanza walijitoa nafsi zao kwa Bwana; na kwetu pia, kwa mapenzi ya Mungu.
Romains 6.13 1 Samuel 1.28 2 Corinthiens 4.5 2 Chroniques 30.8 Romains 12.1
6 Hata tukamwonya Tito kuwatimilizia neema hii kwenu kama vile yeye alivyotangulia kuianzisha.
2 Corinthiens 12.18 2 Corinthiens 8.4 2 Corinthiens 8.19 2 Corinthiens 8.16-8.17 Philippiens 4.18
7 Lakini kama mlivyo na wingi wa mambo yote; imani, na usemi, na elimu, na bidii yote, na upendo wenu kwetu sisi; basi vivyo hivyo mpate wingi wa neema hii pia.
2 Corinthiens 9.8 1 Corinthiens 1.5 2 Pierre 1.5-1.8 Romains 15.14 Philippiens 1.9
8 Sineni ili kuwaamuru, bali kwa bidii ya watu wengine nijaribu unyofu wa upendo wenu.
1 Corinthiens 7.6 Romains 11.12-11.14 1 Corinthiens 7.12 Ezéchiel 33.31 2 Corinthiens 9.2
9 Maana mmejua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa maskini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri, ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake.
Matthieu 20.28 Philippiens 2.6-2.8 Romains 5.8 Romains 8.32 Jean 1.14
10 Nami katika neno hili natoa shauri langu; maana neno hili lawafaa ninyi mliotangulia, yapata mwaka, licha ya kutenda hata na kutaka pia.
1 Corinthiens 7.25 2 Corinthiens 9.2 1 Timothée 6.18-6.19 Hébreux 13.16 1 Corinthiens 7.40
11 Lakini sasa timizeni kule kutenda nako, ili kama vile mlivyokuwa tayari kutaka, vivyo hivyo mkawe tayari na kutimiza, kwa kadiri ya mlivyo navyo.
2 Corinthiens 9.2
12 Maana, kama nia ipo, hukubaliwa kwa kadiri ya alivyo navyo mtu, si kwa kadiri ya asivyo navyo.
2 Corinthiens 9.7 Luc 21.1-21.4 Marc 12.42-12.44 Luc 16.10 Marc 14.7-14.8
13 Maana sisemi hayo, ili wengine wapate raha nanyi mpate dhiki;
Actes 4.34 Romains 15.26-15.27
14 bali mambo yawe sawasawa; wakati huu wa sasa wingi wenu uwafae upungufu wao, ili na wingi wao uwafae ninyi mtakapopungukiwa; ili mambo yawe sawasawa.
2 Corinthiens 9.12 Actes 4.34
15 Kama ilivyoandikwa, Aliyekusanya vingi, hakuzidi, wala yeye aliyekusanya vichache hakupungukiwa.
Exode 16.18 Luc 22.35
16 Lakini ahimidiwe Mungu atiaye bidii ile ile kwa ajili yenu katika moyo wa Tito.
Apocalypse 17.17 Esdras 7.27 Jérémie 32.40 2 Corinthiens 7.7 2 Corinthiens 7.12
17 Maana aliyapokea kweli yale maonyo; tena, huku akizidi kuwa na bidii, alisafiri kwenda kwenu kwa hiari yake mwenyewe.
2 Corinthiens 8.6 Hébreux 13.22 2 Corinthiens 8.10 2 Corinthiens 8.8
18 Na pamoja naye tukamtuma ndugu yule ambaye sifa zake katika Injili zimeenea makanisani mwote.
2 Corinthiens 12.18 1 Corinthiens 7.17 2 Corinthiens 8.22-8.23 2 Corinthiens 2.12 2 Corinthiens 8.19
19 Wala si hivyo tu, bali alichaguliwa na makanisa asafiri pamoja nasi katika jambo la neema hii, tunayoitumikia, ili Bwana atukuzwe, ukadhihirike utayari wetu.
1 Corinthiens 16.3-16.4 2 Corinthiens 4.15 2 Corinthiens 9.8 1 Pierre 4.10-4.11 Actes 15.22
20 Tukijiepusha na neno hili, mtu asije akatulaumu kwa habari ya karama hii tunayoitumikia;
2 Corinthiens 11.12 1 Corinthiens 16.3 Ephésiens 5.15 Matthieu 10.16 1 Thessaloniciens 5.22
21 tukitangulia kufikiri yaliyo mema, si mbele za Bwana tu, ila na mbele ya wanadamu.
Romains 12.17 Philippiens 4.8 1 Pierre 2.12 Romains 14.18 Tite 2.5-2.8
22 Nasi pamoja nao tumemtuma ndugu yetu tuliyemwona mara nyingi katika mambo mengi kuwa ana bidii, na sasa ana bidii zaidi sana kwa sababu ya tumaini kuu alilo nalo kwenu.
Philippiens 2.20-2.22
23 Basi mtu akitaka habari za Tito, yeye ni mshirika wangu, na mtenda kazi pamoja nami kwa ajili yenu; tena akitaka habari za ndugu zetu, wao ni mitume wa makanisa, na utukufu wa Kristo.
Philippiens 2.25 Philémon 1.17 2 Corinthiens 8.6 1 Thessaloniciens 2.2 2 Corinthiens 8.19
24 Basi waonyesheni mbele ya makanisa hakika ya upendo wenu, na ya kujisifu kwetu kwa ajili yenu.
2 Corinthiens 7.14 2 Corinthiens 7.4 2 Corinthiens 8.8 2 Corinthiens 9.2-9.4

Cette Bible est dans le domaine public.