Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 8.35
Bible en Swahili de l’est


Multiplication des pains pour quatre mille hommes

1 Katika siku zile, kwa vile ulivyokuwa mkuu tena ule mkutano, nao wamekosa kitu cha kula, akawaita wanafunzi wake, akawaambia,
Matthieu 15.32-15.39 Marc 6.34-6.44
2 Nawahurumia mkutano kwa sababu yapata siku tatu wamekaa nami, wala hawana kitu cha kula;
Matthieu 9.36 Matthieu 6.32-6.33 Psaumes 145.15 Marc 6.34 Matthieu 4.2-4.4
3 nami nikiwaaga waende zao nyumbani kwao hali wanafunga, watazimia njiani; na baadhi yao wametoka mbali.
Juges 8.4-8.6 Esaïe 40.31 1 Samuel 30.10-30.12 1 Samuel 14.28-14.31
4 Wanafunzi wake wakamjibu, Je! Ataweza wapi mtu kuwashibisha hawa mikate hapa nyikani?
2 Rois 7.2 Nombres 11.21-11.23 Psaumes 78.19-78.20 Marc 6.36-6.37 2 Rois 4.42-4.44
5 Akawauliza, Mnayo mikate mingapi? Wakasema, Saba,
Matthieu 14.15-14.17 Luc 9.13 Matthieu 15.34 Marc 6.38
6 Akawaagiza mkutano waketi chini; akaitwaa ile mikate saba, akashukuru, akaimega, akawapa wanafunzi wake wawaandikie; wakawaandikia mkutano.
Jean 2.5 Luc 12.37 Jean 6.10-6.11 Matthieu 26.26 1 Corinthiens 10.30-10.31
7 Walikuwa na visamaki vichache; akavibarikia, akasema wawaandikie na hivyo pia.
Matthieu 14.19 Luc 6.41 Luc 24.41-24.42 Jean 21.8-21.9 Jean 21.5
8 Wakala, wakashiba, wakakusanya mabaki ya vipande vya mikate makanda saba.
2 Rois 4.42-4.44 Jean 6.47-6.58 Jean 6.32-6.35 2 Rois 4.2-4.7 Jean 6.11-6.13
9 Na watu waliokula wapata elfu nne. Akawaaga.
10 Mara akapanda chomboni pamoja na wanafunzi wake, akaenda pande za Dalmanutha.
Matthieu 15.39
11 Wakatokea Mafarisayo, wakaanza kuhojiana naye; wakitafuta kwake ishara itokayo mbinguni; wakimjaribu.
Matthieu 12.38 Luc 11.16 1 Corinthiens 10.9 Matthieu 22.23 Exode 17.7
12 Akaugua rohoni mwake, akasema, Mbona kizazi hiki chatafuta ishara? Amin, nawaambieni, Hakitapewa ishara kizazi hiki.
Marc 7.34 Luc 16.29-16.31 Marc 3.5 Esaïe 53.3 Marc 9.19
13 Akawaacha, akapanda tena chomboni, akaenda zake hata ng’ambo.
Osée 9.12 Luc 8.37 Zacharie 11.8-11.9 Actes 13.45-13.46 Jean 8.21
14 Wakasahau kuchukua mikate, wala chomboni hawana ila mkate mmoja tu.
Matthieu 16.5
15 Akawaagiza, akasema, Angalieni, jihadharini na chachu ya Mafarisayo na chachu ya Herode.
1 Corinthiens 5.6-5.8 Marc 12.13 Matthieu 16.6 1 Timothée 6.13 1 Chroniques 28.9-28.10
16 Wakabishana wao kwa wao, kwa kuwa hawana mikate.
Luc 20.5 Matthieu 16.7-16.8 Luc 9.46
17 Naye Yesu akatambua, akawaambia, Mbona mnabishana kwa sababu hamna mikate? Hamfahamu bado, wala hamjaelewa? Je! Mioyo yenu ni mizito?
Marc 6.52 Matthieu 16.8-16.9 Marc 16.14 Hébreux 4.12-4.13 Jean 16.30
18 Mna macho, hamwoni; mna masikio, hamsikii? Wala hamkumbuki?
Marc 4.12 Jérémie 5.21 Actes 28.26-28.27 Matthieu 13.14-13.15 Ezéchiel 12.2
19 Nilipoivunja ile mikate mitano na kuwapa wale elfu tano, mlichukua vikapu vingapi vimejaa vipande? Wakamwambia, Kumi na viwili.
Marc 6.38-6.44 Jean 6.5-6.13 Luc 9.12-9.17 Matthieu 14.17-14.21
20 Na ile saba kuwapa wale elfu nne, mlichukua makanda mangapi yamejaa vipande? Wakamwambia, Saba.
Matthieu 15.34-15.38 Marc 8.1-8.9
21 Akawaambia, Hamjafahamu bado?
Marc 6.52 Jean 14.9 Matthieu 16.11-16.12 Psaumes 94.8 1 Corinthiens 6.5
22 Wakafika Bethsaida, wakamletea kipofu, wakamsihi amguse.
Matthieu 11.21 Marc 6.45 Matthieu 8.15 Matthieu 8.3 Marc 2.3
23 Akamshika mkono yule kipofu, akamchukua nje ya kijiji, akamtemea mate ya macho, akamwekea mikono yake, akamwuliza, Waona kitu?
Marc 7.33 Actes 9.8 Marc 5.23 Hébreux 8.9 Esaïe 44.2
24 Akatazama juu, akasema, Naona watu kama miti, inakwenda.
Juges 9.36 1 Corinthiens 13.9-13.12 Esaïe 32.3 Esaïe 29.18
25 Ndipo akaweka tena mikono yake juu ya macho yake, naye akatazama sana; akawa mzima, akaona vyote waziwazi.
Proverbes 4.18 1 Pierre 2.9 2 Pierre 3.18 Matthieu 13.12 Philippiens 1.6
26 Akampeleka nyumbani kwake, akisema, Hata kijijini usiingie.
Matthieu 8.4 Marc 7.36 Marc 5.43 Matthieu 9.30 Matthieu 12.16

Pierre reconnaît Jésus comme le Messie

27 Akatoka Yesu na wanafunzi wake, wakaenda kwenye vijiji vya Kaisaria-Filipi; na njiani akawauliza wanafunzi wake, akasema, Watu huninena mimi kuwa ni nani?
Luc 9.18-9.20 Matthieu 16.13-16.20
28 Wakamjibu, Yohana Mbatizaji; wengine, Eliya; wengine, Mmojawapo wa manabii.
Malachie 4.5 Matthieu 14.2 Jean 1.21 Marc 6.14-6.16 Marc 9.11-9.13
29 Naye akawauliza, Na ninyi mnasema ya kuwa mimi ni nani? Petro akamjibu, akamwambia, Wewe ndiwe Kristo.
Jean 6.69 Jean 11.27 Jean 1.41-1.49 1 Jean 4.15 Actes 8.36
30 Akawaonya wasimwambie mtu habari zake.
Matthieu 16.20 Luc 9.21 Marc 9.9 Matthieu 8.4 Marc 7.36
31 Akaanza kuwafundisha kwamba imempasa Mwana wa Adamu kupatikana na mateso mengi, na kukataliwa na wazee, na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na baada ya siku tatu kufufuka.
Jean 2.19 Marc 12.10 Osée 6.2 Matthieu 12.40 Luc 24.26
32 Naye alikuwa akinena neno hilo waziwazi. Petro akamchukua, akaanza kumkemea.
Jean 16.25 Jean 16.29 Matthieu 16.22 Marc 4.38 Luc 10.40
33 Akageuka, akawatazama wanafunzi wake, akamkemea Petro, akasema, Nenda nyuma yangu, Shetani; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.
Matthieu 4.10 1 Jean 2.15 Philippiens 3.19 Romains 8.5-8.8 Luc 9.55
34 Akawaita mkutano pamoja na wanafunzi wake, akawaambia, Mtu ye yote akitaka kunifuata na ajikane mwenyewe, ajitwike na msalaba wake, anifuate.
Matthieu 10.38 Luc 14.26-14.27 1 Rois 14.8 Nombres 14.24 Jean 10.27
35 Kwa kuwa mtu atakaye kuiponya nafsi yake, ataiangamiza, na mtu atakayeiangamiza nafsi yake kwa ajili yangu na kwa ajili ya Injili, huyu ataisalimisha.
2 Timothée 1.8 Luc 17.33 Matthieu 10.39 Matthieu 19.29 1 Corinthiens 9.23
36 Kwa kuwa itamfaidia mtu nini kuupata ulimwengu wote, akipata hasara ya nafsi yake?
Luc 9.25 Matthieu 16.26 Job 22.2 Romains 6.21 Psaumes 49.17
37 Ama mtu atoe nini badala ya nafsi yake?
Psaumes 49.7-49.8 1 Pierre 1.18-1.19
38 Maana kila mtu atakayenionea haya mimi, na maneno yangu, katika kizazi hiki cha uzinzi na dhambi, Mwana wa Adamu atamwonea haya mtu huyo, atakapokuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika watakatifu.
Matthieu 26.64 Matthieu 16.27 Matthieu 25.31 Daniel 7.13 Matthieu 24.30

Cette Bible est dans le domaine public.