Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 89.31
Bible en Swahili de l’est


Alliance de Dieu avec David

1 Fadhili za Bwana nitaziimba milele; Kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako.
Psaumes 101.1 Psaumes 89.33 Psaumes 89.49 Psaumes 36.5 Psaumes 119.90
2 Maana nimesema, Fadhili zitajengwa milele; Katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako.
Psaumes 36.5 Psaumes 103.17 Nombres 23.19 Hébreux 6.18 Psaumes 89.5
3 Nimefanya agano na mteule wangu, Nimemuapia Daudi, mtumishi wangu.
Psaumes 132.11 Jérémie 30.9 1 Rois 8.16 2 Samuel 7.10-7.16 Jérémie 33.20-33.21
4 Wazao wako nitawafanya imara milele, Nitakijenga kiti chako cha enzi hata milele.
2 Samuel 7.12-7.16 Psaumes 132.12 Esaïe 9.6-9.7 1 Chroniques 22.10 1 Chroniques 17.10-17.14
5 Ee Bwana, mbingu zitayasifu maajabu yako, Uaminifu wako katika kusanyiko la watakatifu.
Psaumes 19.1 Psaumes 97.6 Psaumes 50.6 Apocalypse 7.10-7.12 2 Thessaloniciens 1.7
6 Maana ni nani katika mbingu awezaye kulinganishwa na Bwana? Ni nani afananaye na Bwana miongoni mwa malaika?
Psaumes 113.5 Psaumes 86.8 Psaumes 29.1 Jérémie 10.6 Psaumes 89.8
7 Mungu huogopwa sana barazani pa watakatifu, Ni wa kuhofiwa kuliko wote wanaomzunguka.
Psaumes 47.2 Jérémie 10.10 Matthieu 10.28 Apocalypse 15.3-15.4 Lévitique 10.3
8 Bwana, Mungu wa majeshi, Ni nani aliye hodari kama Wewe, Ee YAHU? Na uaminifu wako unakuzunguka.
Psaumes 35.10 Psaumes 71.19 Jérémie 32.17 1 Samuel 2.2 Psaumes 147.5
9 Wewe ndiwe ukitawalaye kiburi cha bahari. Mawimbi yake yainukapo wayatuliza Wewe.
Psaumes 65.7 Marc 4.41 Psaumes 93.3-93.4 Psaumes 107.25-107.29 Nahum 1.4
10 Ndiwe uliyemseta Rahabu akawa kama aliyeuawa, Kwa mkono hodari umewatawanya wakuchukiao.
Psaumes 144.6 Psaumes 105.27-105.45 Psaumes 87.4 Psaumes 78.43-78.72 Esaïe 24.1
11 Mbingu ni mali yako, nchi nayo ni mali yako, Ulimwengu na vyote viujazavyo Ndiwe uliyeupiga msingi wake.
1 Chroniques 29.11 Genèse 1.1 Psaumes 50.12 1 Corinthiens 10.28 1 Corinthiens 10.26
12 Kaskazini na kusini ndiwe uliyeziumba, Tabori na Hermoni hulifurahia jina lako.
Josué 19.22 Job 26.7 Josué 12.1 Deutéronome 3.8-3.9 Juges 4.6
13 Mkono wako ni mkono wenye uweza, Mkono wako una nguvu, Mkono wako wa kuume umetukuka.
Daniel 4.34-4.35 Psaumes 89.10 Matthieu 6.13 Psaumes 62.11
14 Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako, Fadhili na kweli zahudhuria mbele za uso wako.
Psaumes 97.2 Psaumes 85.13 Psaumes 145.17 Proverbes 16.12 Jean 1.17
15 Heri watu wale waijuao sauti ya shangwe, Ee Bwana, huenenda katika nuru ya uso wako.
Nahum 1.15 Esaïe 52.7-52.8 Actes 2.28 Lévitique 25.9 Psaumes 44.3
16 Kwa jina lako hufurahi mchana kutwa, Na kwa haki yako hutukuzwa.
Romains 1.17 Psaumes 71.15-71.16 Esaïe 46.13 Psaumes 44.8 Romains 3.21-3.26
17 Maana fahari ya nguvu zao ni Wewe, Na kwa radhi yako pembe yetu itatukuka.
Psaumes 75.10 Psaumes 148.14 Psaumes 92.10 1 Samuel 2.10 Psaumes 132.17
18 Maana ngao yetu ina Bwana, Na mfalme wetu ni wake Mtakatifu wa Israeli.
Psaumes 47.9 Psaumes 71.22 Psaumes 44.4 Esaïe 29.19 Psaumes 91.1-91.2
19 Ndipo ulipowaambia watakatifu wako kwa njozi, Ukasema, nimempa aliye hodari msaada; Nimemtukuza aliyechaguliwa miongoni mwa watu.
1 Rois 11.34 1 Samuel 16.18 2 Pierre 1.21 Hébreux 2.9-2.17 1 Samuel 16.1
20 Nimemwona Daudi, mtumishi wangu, Nimempaka mafuta yangu matakatifu.
1 Samuel 16.1 1 Samuel 16.12-16.13 Actes 13.22 Esaïe 61.1-61.3 Jean 3.34
21 Ambaye mkono wangu utakuwa thabiti kwake, Na mkono wangu utamtia nguvu.
Esaïe 41.10 Esaïe 49.8 Esaïe 42.1 Psaumes 18.32-18.39 Zacharie 10.12
22 Adui hatamwonea, Wala mwana wa uovu hatamtesa.
2 Samuel 7.10 Jean 17.12 1 Chroniques 17.9 2 Thessaloniciens 2.3 Matthieu 4.1-4.10
23 Bali nitawaponda watesi wake mbele yake, Nitawapiga wanaomchukia.
2 Samuel 7.9 2 Samuel 7.1 2 Samuel 3.1 2 Samuel 22.40-22.44 Luc 19.14
24 Uaminifu wangu na fadhili zangu atakuwa nazo, Na kwa jina langu pembe yake itatukuka.
Psaumes 20.1 Jean 17.26 Psaumes 61.7 Psaumes 89.28 1 Samuel 2.1
25 Nitaweka mkono wake juu ya bahari, Na mkono wake wa kuume juu ya mito.
Psaumes 2.8 Psaumes 80.11 Psaumes 72.8-72.11 1 Rois 4.21 Apocalypse 11.15
26 Yeye ataniita, Wewe baba yangu, Mungu wangu na mwamba wa wokovu wangu.
2 Samuel 7.14 2 Samuel 22.47 1 Chroniques 22.10 Marc 15.34 Psaumes 95.1
27 Nami nitamjalia kuwa mzaliwa wangu wa kwanza, Kuwa juu sana kuliko wafalme wa dunia.
Colossiens 1.15 Colossiens 1.18 Apocalypse 19.16 Psaumes 2.7 Romains 8.29
28 Hata milele nitamwekea fadhili zangu, Na agano langu litafanyika amini kwake.
Esaïe 55.3 Psaumes 111.5 2 Samuel 7.15-7.16 Psaumes 111.9 Actes 13.32-13.34
29 Wazao wake nao nitawadumisha milele, Na kiti chake cha enzi kama siku za mbingu.
Psaumes 89.4 Deutéronome 11.21 Psaumes 89.36 Esaïe 9.7 Psaumes 132.11
30 Wanawe wakiiacha sheria yangu, Wasiende katika hukumu zangu,
2 Samuel 7.14 1 Chroniques 28.9 Psaumes 119.53 Ezéchiel 18.17 Ezéchiel 20.19
31 Wakizihalifu amri zangu, Wasiyashike maagizo yangu,
Psaumes 55.20
32 Basi, nitawarudi makosa yao kwa fimbo, Na uovu wao kwa mapigo.
2 Samuel 7.14 Hébreux 12.6-12.11 1 Rois 11.31 1 Rois 11.6 Job 9.34
33 Lakini fadhili zangu sitamwondolea yeye, Wala sitafanya uaminifu wangu kuwa uongo.
2 Samuel 7.15 1 Samuel 15.29 Jérémie 33.20-33.26 Lamentations 3.31-3.32 Esaïe 54.8-54.10
34 Mimi sitalihalifu agano langu, Sitalibadili neno lililotoka midomoni mwangu.
Nombres 23.19 Matthieu 24.35 Jérémie 33.20 Malachie 3.6 Jacques 1.17
35 Neno moja nimeliapa kwa utakatifu wangu, Hakika sitamwambia Daudi uongo,
Psaumes 132.11 Hébreux 6.13 Tite 1.2 Amos 4.2 Hébreux 6.17
36 Wazao wake watadumu milele, Na kiti chake kitakuwa kama jua mbele zangu.
Psaumes 72.5 Psaumes 89.29 Luc 1.33 Psaumes 72.17 Esaïe 9.7
37 Kitathibitika milele kama mwezi; Shahidi aliye mbinguni mwaminifu.
Genèse 1.14-1.18 Esaïe 54.9-54.10 Genèse 9.13-9.16 Jérémie 31.35-31.36 Psaumes 104.19
38 Walakini Wewe umemtupa na kumkataa, Umemghadhibikia masihi wako.
Deutéronome 32.19 1 Chroniques 28.9 Psaumes 89.51 Zacharie 13.7 2 Samuel 1.21
39 Umechukizwa na agano la mtumishi wako, Umeinajisi taji yake na kuitupa chini.
Psaumes 74.7 Lamentations 5.16 Psaumes 89.34-89.36 Psaumes 77.10 Psaumes 89.44
40 Umeyabomoa maboma yake yote, Umezifanya ngome zake kuwa magofu.
Psaumes 80.12 Lamentations 2.2 Lamentations 2.5 2 Chroniques 12.2-12.5 2 Chroniques 15.5
41 Wote wapitao njiani wanateka mali zake; Amekuwa laumu kwa jirani zake;
Psaumes 79.4 Néhémie 5.9 Deutéronome 28.37 Ezéchiel 5.14-5.15 Psaumes 44.10-44.14
42 Umeutukuza mkono wa kuume wa watesi wake; Umewafurahisha wote wanaomchukia.
Psaumes 80.6 Apocalypse 11.10 Lamentations 2.17 Deutéronome 28.43 Deutéronome 28.25
43 Pia umeurudisha nyuma ukali wa upanga wake; Wala hukumsimamisha vitani.
Josué 7.8-7.12 Josué 7.4-7.5 Lévitique 26.36-26.37 Nombres 14.42 2 Chroniques 25.8
44 Umeikomesha fahari yake; Kiti chake cha enzi umekitupa chini.
2 Thessaloniciens 2.3-2.10 1 Rois 14.25-14.28 Daniel 7.20-7.25 1 Rois 12.16-12.20 Psaumes 89.39
45 Umezipunguza siku za ujana wake; Umemvika aibu.
Psaumes 109.29 Psaumes 44.15 Psaumes 71.13 2 Chroniques 10.19 Michée 7.10
46 Ee Bwana, hata lini? Utajificha hata milele? Ghadhabu yako itawaka kama moto?
Psaumes 79.5 Psaumes 78.63 Psaumes 90.13 Esaïe 8.17 Psaumes 88.14
47 Ukumbuke jinsi mimi nisivyo wa kudumu; Kwa ubatili gani umeiumba jamii ya wanadamu!
Job 7.7 Job 10.9 Job 14.1 Job 9.25-9.26 Psaumes 119.84
48 Ni mwanamume gani atakayeishi asione mauti, Atakayejiokoa nafsi yake na mkono wa kuzimu?
Psaumes 49.15 Hébreux 11.5 Actes 2.27 Jean 8.51 Ecclésiaste 12.7
49 Bwana, zi wapi fadhili zako za kwanza, Ulizomwapia Daudi kwa uaminifu wako?
2 Samuel 7.15 Psaumes 89.35 Esaïe 63.7-63.15 Psaumes 89.3-89.4 2 Samuel 3.9
50 Ee Bwana, ukumbuke, Wanavyosimangwa watumishi wako; Jinsi ninavyostahimili kifuani mwangu Masimango ya watu wengi.
Psaumes 74.18 Psaumes 74.22 Psaumes 69.9 Psaumes 69.19-69.20 Romains 15.3
51 Ambayo adui zako wamesimanga, Ee Bwana, Naam, wamezisimanga hatua za masihi wako.
1 Pierre 2.20-2.21 Psaumes 56.5-56.6 Hébreux 10.33 Matthieu 26.61 Jean 8.48
52 Na ahimidiwe Bwana milele. Amina na Amina.
Psaumes 41.13 Psaumes 106.48 Psaumes 72.18-72.19 Matthieu 6.13 Néhémie 9.5

Cette Bible est dans le domaine public.