Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Psaumes 89.12
Bible en Swahili de l’est


Alliance de Dieu avec David

1 Fadhili za Bwana nitaziimba milele; Kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako.
Psaumes 101.1 Psaumes 36.5 Psaumes 89.33 Psaumes 89.49 Psaumes 89.8
2 Maana nimesema, Fadhili zitajengwa milele; Katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako.
Psaumes 36.5 Psaumes 103.17 Psaumes 42.1 Psaumes 146.6 Néhémie 9.17
3 Nimefanya agano na mteule wangu, Nimemuapia Daudi, mtumishi wangu.
Psaumes 132.11 2 Samuel 7.10-7.16 Jérémie 33.20-33.21 Jérémie 30.9 1 Rois 8.16
4 Wazao wako nitawafanya imara milele, Nitakijenga kiti chako cha enzi hata milele.
2 Samuel 7.12-7.16 1 Chroniques 17.10-17.14 Luc 1.32-1.33 Psaumes 132.12 Esaïe 9.6-9.7
5 Ee Bwana, mbingu zitayasifu maajabu yako, Uaminifu wako katika kusanyiko la watakatifu.
Psaumes 19.1 Psaumes 97.6 Apocalypse 7.10-7.12 Psaumes 50.6 Hébreux 12.22-12.23
6 Maana ni nani katika mbingu awezaye kulinganishwa na Bwana? Ni nani afananaye na Bwana miongoni mwa malaika?
Psaumes 29.1 Psaumes 113.5 Psaumes 86.8 Psaumes 89.8 Exode 15.11
7 Mungu huogopwa sana barazani pa watakatifu, Ni wa kuhofiwa kuliko wote wanaomzunguka.
Psaumes 47.2 Jérémie 10.7 Actes 5.11 Luc 12.4-12.5 Psaumes 76.7-76.11
8 Bwana, Mungu wa majeshi, Ni nani aliye hodari kama Wewe, Ee YAHU? Na uaminifu wako unakuzunguka.
Psaumes 71.19 Psaumes 35.10 1 Samuel 2.2 Jérémie 32.17 1 Samuel 15.19
9 Wewe ndiwe ukitawalaye kiburi cha bahari. Mawimbi yake yainukapo wayatuliza Wewe.
Psaumes 65.7 Marc 4.41 Psaumes 93.3-93.4 Psaumes 107.25-107.29 Nahum 1.4
10 Ndiwe uliyemseta Rahabu akawa kama aliyeuawa, Kwa mkono hodari umewatawanya wakuchukiao.
Psaumes 144.6 Esaïe 24.1 Deutéronome 4.34 Exode 3.19-3.20 Psaumes 59.11
11 Mbingu ni mali yako, nchi nayo ni mali yako, Ulimwengu na vyote viujazavyo Ndiwe uliyeupiga msingi wake.
1 Chroniques 29.11 Genèse 1.1 Genèse 2.1 Job 41.11 Psaumes 24.1-24.2
12 Kaskazini na kusini ndiwe uliyeziumba, Tabori na Hermoni hulifurahia jina lako.
Josué 19.22 Job 26.7 Josué 12.1 Psaumes 98.8 Psaumes 133.3
13 Mkono wako ni mkono wenye uweza, Mkono wako una nguvu, Mkono wako wa kuume umetukuka.
Daniel 4.34-4.35 Psaumes 89.10 Matthieu 6.13 Psaumes 62.11
14 Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chako, Fadhili na kweli zahudhuria mbele za uso wako.
Psaumes 97.2 Psaumes 85.13 Jean 1.17 Apocalypse 15.3 Psaumes 99.4
15 Heri watu wale waijuao sauti ya shangwe, Ee Bwana, huenenda katika nuru ya uso wako.
Psaumes 44.3 Nombres 10.10 Psaumes 4.6 Nahum 1.15 Esaïe 52.7-52.8
16 Kwa jina lako hufurahi mchana kutwa, Na kwa haki yako hutukuzwa.
Psaumes 29.7 Esaïe 45.24-45.25 Luc 1.47 Psaumes 105.3 Philippiens 4.4
17 Maana fahari ya nguvu zao ni Wewe, Na kwa radhi yako pembe yetu itatukuka.
Psaumes 75.10 Psaumes 92.10 Psaumes 148.14 1 Samuel 2.1 Philippiens 4.13
18 Maana ngao yetu ina Bwana, Na mfalme wetu ni wake Mtakatifu wa Israeli.
Psaumes 47.9 Psaumes 71.22 Psaumes 84.11 Psaumes 62.6 Genèse 15.1
19 Ndipo ulipowaambia watakatifu wako kwa njozi, Ukasema, nimempa aliye hodari msaada; Nimemtukuza aliyechaguliwa miongoni mwa watu.
1 Rois 11.34 1 Samuel 16.18 2 Samuel 17.10 Marc 1.24 Psaumes 89.3
20 Nimemwona Daudi, mtumishi wangu, Nimempaka mafuta yangu matakatifu.
1 Samuel 16.1 1 Samuel 16.12-16.13 Actes 13.22 Esaïe 61.1-61.3 Jean 3.34
21 Ambaye mkono wangu utakuwa thabiti kwake, Na mkono wangu utamtia nguvu.
Psaumes 18.32-18.39 Zacharie 10.12 2 Samuel 7.8-7.16 Psaumes 80.15-80.17 Psaumes 89.13
22 Adui hatamwonea, Wala mwana wa uovu hatamtesa.
2 Samuel 7.10 2 Thessaloniciens 2.3 Matthieu 4.1-4.10 Jean 17.12 1 Chroniques 17.9
23 Bali nitawaponda watesi wake mbele yake, Nitawapiga wanaomchukia.
2 Samuel 7.9 Psaumes 2.1-2.6 Psaumes 132.18 Psaumes 21.8-21.9 Jean 15.23
24 Uaminifu wangu na fadhili zangu atakuwa nazo, Na kwa jina langu pembe yake itatukuka.
Psaumes 20.5 Psaumes 89.33 Jean 1.17 2 Corinthiens 1.20 Jean 17.11
25 Nitaweka mkono wake juu ya bahari, Na mkono wake wa kuume juu ya mito.
1 Rois 4.21 Apocalypse 11.15 Psaumes 2.8 Psaumes 80.11 Psaumes 72.8-72.11
26 Yeye ataniita, Wewe baba yangu, Mungu wangu na mwamba wa wokovu wangu.
2 Samuel 7.14 2 Samuel 22.47 1 Chroniques 22.10 Marc 15.34 Psaumes 95.1
27 Nami nitamjalia kuwa mzaliwa wangu wa kwanza, Kuwa juu sana kuliko wafalme wa dunia.
Colossiens 1.18 Colossiens 1.15 Apocalypse 19.16 Psaumes 2.7 Romains 8.29
28 Hata milele nitamwekea fadhili zangu, Na agano langu litafanyika amini kwake.
Esaïe 55.3 Actes 13.32-13.34 Psaumes 89.33-89.34 Jérémie 33.20-33.21 2 Samuel 23.5
29 Wazao wake nao nitawadumisha milele, Na kiti chake cha enzi kama siku za mbingu.
Psaumes 89.4 Deutéronome 11.21 Psaumes 89.36 Esaïe 9.7 1 Chroniques 17.11-17.12
30 Wanawe wakiiacha sheria yangu, Wasiende katika hukumu zangu,
2 Samuel 7.14 1 Chroniques 28.9 Psaumes 119.53 Proverbes 28.4 Luc 1.6
31 Wakizihalifu amri zangu, Wasiyashike maagizo yangu,
Psaumes 55.20
32 Basi, nitawarudi makosa yao kwa fimbo, Na uovu wao kwa mapigo.
2 Samuel 7.14 Hébreux 12.6-12.11 Amos 3.2 1 Corinthiens 11.31-11.32 Proverbes 3.11-3.12
33 Lakini fadhili zangu sitamwondolea yeye, Wala sitafanya uaminifu wangu kuwa uongo.
2 Samuel 7.15 Hébreux 6.18 Psaumes 89.39 1 Rois 11.13 1 Rois 11.36
34 Mimi sitalihalifu agano langu, Sitalibadili neno lililotoka midomoni mwangu.
Nombres 23.19 Malachie 3.6 Matthieu 24.35 Jérémie 33.20 Romains 11.29
35 Neno moja nimeliapa kwa utakatifu wangu, Hakika sitamwambia Daudi uongo,
Psaumes 132.11 Amos 4.2 Hébreux 6.17 Hébreux 6.13 Tite 1.2
36 Wazao wake watadumu milele, Na kiti chake kitakuwa kama jua mbele zangu.
Psaumes 72.5 Luc 1.33 Psaumes 72.17 Psaumes 89.29 Esaïe 53.10
37 Kitathibitika milele kama mwezi; Shahidi aliye mbinguni mwaminifu.
Jérémie 31.35-31.36 Psaumes 104.19 Psaumes 72.7 Genèse 1.14-1.18 Esaïe 54.9-54.10
38 Walakini Wewe umemtupa na kumkataa, Umemghadhibikia masihi wako.
1 Chroniques 28.9 Deutéronome 32.19 Psaumes 89.51 Psaumes 60.1 Psaumes 106.40
39 Umechukizwa na agano la mtumishi wako, Umeinajisi taji yake na kuitupa chini.
Lamentations 5.16 Psaumes 74.7 Psaumes 89.44 Psaumes 143.3 Esaïe 43.28
40 Umeyabomoa maboma yake yote, Umezifanya ngome zake kuwa magofu.
Psaumes 80.12 Lamentations 2.2 Lamentations 2.5 Apocalypse 13.1-13.7 Esaïe 5.5-5.6
41 Wote wapitao njiani wanateka mali zake; Amekuwa laumu kwa jirani zake;
Psaumes 79.4 Psaumes 80.13 Jérémie 44.12 Daniel 9.16 Jérémie 50.17
42 Umeutukuza mkono wa kuume wa watesi wake; Umewafurahisha wote wanaomchukia.
Deutéronome 28.43 Deutéronome 28.25 Lévitique 26.17 Jean 16.20 Lévitique 26.25
43 Pia umeurudisha nyuma ukali wa upanga wake; Wala hukumsimamisha vitani.
Nombres 14.42 2 Chroniques 25.8 Ezéchiel 30.21-30.25 Nombres 14.45 Psaumes 44.10
44 Umeikomesha fahari yake; Kiti chake cha enzi umekitupa chini.
1 Rois 12.16-12.20 Psaumes 89.39 Lamentations 4.1-4.2 1 Samuel 4.21-4.22 2 Thessaloniciens 2.3-2.10
45 Umezipunguza siku za ujana wake; Umemvika aibu.
Psaumes 109.29 Psaumes 44.15 Michée 7.10 Psaumes 102.23 Esaïe 63.18
46 Ee Bwana, hata lini? Utajificha hata milele? Ghadhabu yako itawaka kama moto?
Psaumes 79.5 Psaumes 78.63 Psaumes 10.1 Psaumes 85.5 Hébreux 12.29
47 Ukumbuke jinsi mimi nisivyo wa kudumu; Kwa ubatili gani umeiumba jamii ya wanadamu!
Job 7.7 Job 10.9 Job 14.1 Psaumes 119.84 Psaumes 39.5-39.6
48 Ni mwanamume gani atakayeishi asione mauti, Atakayejiokoa nafsi yake na mkono wa kuzimu?
Psaumes 49.15 Hébreux 11.5 2 Corinthiens 4.14 Hébreux 9.27 Ecclésiaste 8.8
49 Bwana, zi wapi fadhili zako za kwanza, Ulizomwapia Daudi kwa uaminifu wako?
2 Samuel 7.15 2 Samuel 3.9 Psaumes 54.5 Psaumes 132.11-132.12 Psaumes 77.9-77.10
50 Ee Bwana, ukumbuke, Wanavyosimangwa watumishi wako; Jinsi ninavyostahimili kifuani mwangu Masimango ya watu wengi.
Psaumes 74.18 Psaumes 74.22 Psaumes 69.9 Psaumes 44.13-44.16 Psaumes 79.10-79.12
51 Ambayo adui zako wamesimanga, Ee Bwana, Naam, wamezisimanga hatua za masihi wako.
Matthieu 12.24 Actes 5.41 1 Pierre 3.16 1 Pierre 4.14-4.16 2 Samuel 16.7-16.8
52 Na ahimidiwe Bwana milele. Amina na Amina.
Psaumes 41.13 Psaumes 106.48 Matthieu 6.13 Néhémie 9.5 1 Timothée 1.17

Cette Bible est dans le domaine public.