Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Chroniques 2.10
Bible en Swahili de l’est


Les fils de Jacob et la descendance de Juda

1 Hawa ndio wana wa Israeli; Reubeni, na Simeoni, na Lawi, na Yuda, na Isakari, na Zabuloni;
Genèse 29.32-29.35 Genèse 35.22-35.26 Exode 1.2-1.4 Nombres 1.5-1.15 Genèse 46.8-46.27
2 na Dani, na Yusufu, na Benyamini, na Naftali, na Gadi, na Asheri.
3 Wana wa Yuda; Eri, na Onani, na Shela; ambao hao watatu alizaliwa na binti Shua, Mkanaani. Naye Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mbaya machoni pa Bwana; naye akamwua.
Genèse 38.2-38.10 Nombres 26.19 Genèse 46.12 1 Chroniques 9.5
4 Na Tamari, mkwewe, akamzalia Peresi, na Zera. Wana wote wa Yuda ni watano.
Matthieu 1.3 Genèse 38.13-38.30 Ruth 4.12 Néhémie 11.4 Genèse 38.11
5 Wana wa Peresi; Hesroni, na Hamuli.
Genèse 46.12 Ruth 4.18 Nombres 26.21 Luc 3.33 Matthieu 1.3
6 Na wana wa Zera; Zabdi, na Ethani, na Hemani, na Kalkoli, na Darda; hao wote ni watano.
1 Rois 4.31 Josué 7.1 Josué 7.17-7.18
7 Na wana wa Karmi; Akani, yule mwenye kutaabisha Israeli, aliyekosa katika kitu kilichowekwa wakfu.
Josué 6.18 Josué 7.25 Deutéronome 7.26 Josué 7.1-7.5 Josué 7.11-7.15
8 Na wana wa Ethani; Azaria.
9 Tena wana wa Hesroni aliozaliwa; Yerameeli, na Ramu, na Kalebu.
Ruth 4.19 1 Chroniques 2.42 Matthieu 1.3 1 Chroniques 2.18-2.19 1 Chroniques 2.24
10 Na Ramu akamzaa Aminadabu; na Aminadabu akamzaa Nashoni, mkuu wa wana wa Yuda;
Matthieu 1.4 Nombres 1.7 Luc 3.32-3.33 Ruth 4.19-4.20 Nombres 2.3
11 na Nashoni akamzaa Salmoni; na Salmoni akamzaa Boazi;
Ruth 4.21 Matthieu 1.4-1.5 Luc 3.32
12 na Boazi akamzaa Obedi; na Obedi akamzaa Yese;
1 Samuel 16.1 Actes 13.22 Esaïe 11.10 Esaïe 11.1 Romains 15.12
13 na Yese akamzaa Eliabu, mzaliwa wake wa kwanza, na wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama;
1 Samuel 17.13 1 Chroniques 27.18 1 Samuel 16.6-16.13 1 Chroniques 20.7 1 Samuel 17.28
14 na wa nne Nethaneli, na wa tano Radai;
15 na wa sita Ozemu, na wa saba Daudi;
1 Samuel 17.12-17.14 1 Samuel 16.10-16.11
16 na maumbu yao ni Seruya, na Abigaili. Na wana wa Seruya walikuwa, Abishai, na Yoabu, na Asaheli; hao watatu.
1 Samuel 26.6 2 Samuel 3.39 2 Samuel 16.9-16.11 2 Samuel 2.18-2.23 2 Samuel 19.22
17 Na Abigaili akamzaa Amasa; na babaye Amasa ni Yetheri, Mwishmaeli.
2 Samuel 17.25 1 Rois 2.32 2 Samuel 19.13 2 Samuel 20.4-20.12 1 Rois 2.5
18 Basi Kalebu, mwana wa Hesroni, akazaliwa wana na mkewe Azubu, na Yeriothi, na hawa ndio wanawe wa kiume; Yesheri, na Shobabu, na Ardoni.
19 Akafa Azuba, naye Kalebu akamtwaa Efrathi, aliyemzalia Huri.
1 Chroniques 2.50 Michée 5.2 1 Chroniques 4.4 1 Chroniques 2.24
20 Naye Huri akamzaa Uri; na Uri akamzaa Besaleli.
Exode 31.2 Exode 37.1 Exode 38.22 Exode 36.1-36.2 2 Chroniques 1.5
21 Na baadaye Hesroni akamwingilia binti wa Makiri, babaye Gileadi; ambaye alimtwaa alipokuwa mwenye miaka sitini; naye akamzalia Segubu.
Nombres 27.1 Nombres 26.29 Deutéronome 3.15 Genèse 50.23 Nombres 32.39-32.40
22 Na Segubu akamzaa Yairi, aliyekuwa mwenye miji ishirini na mitatu katika nchi ya Gileadi.
Josué 13.30 Deutéronome 3.14 Nombres 32.41
23 Na Geshuri na Aramu wakawapokonya miji ya Yairi, pamoja na Kenathi na miji yake, jumla yote miji sitini. Hao wote ni wana wa Makiri, babaye Gileadi.
Nombres 32.41-32.42 Josué 13.13 Josué 13.30 2 Samuel 13.38 Deutéronome 3.14
24 Tena, baada ya kufa kwake Hesroni huko Kalebu-Efrata, ndipo Abia, mkewe Hesroni, alipomzalia Ashuri, babaye Teboa.
1 Chroniques 4.5 2 Samuel 14.2 Amos 1.1 1 Chroniques 2.18-2.19 1 Chroniques 2.9
25 Na wana wa Yerameeli, mzaliwa wa kwanza wa Hesroni, walikuwa Ramu, mzaliwa wa kwanza, na Buna, na Oreni, na Ozemu; kwa Ahiya.
26 Naye Yerameeli alikuwa na mke mwingine, jina lake Atara; yeye alikuwa mamaye Onamu.
27 Na wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, na Yamini, na Ekeri.
28 Na wana wa Onamu walikuwa Shamai, na Yada; na wana wa Shamai; Nadabu, na Abishuri.
29 Na mkewe Abishuri aliitwa jina lake Abihaili; naye akamzalia Abani, na Molidi.
30 Na wana wa Nadabu; Seledi, na Apaimu; walakini Seledi alikufa hana watoto.
31 Na wana wa Apaimu; Ishi. Na wana wa Ishi; Sheshani. Na wana wa Sheshani; Alai.
1 Chroniques 2.34-2.35
32 Na wana wa Yada, nduguye Shamai; Yetheri, na Yonathani; naye Yetheri akafa hana watoto.
33 Na wana wa Yonathani; Pelethi, na Zaza. Hao ndio wana wa Yerameeli.
34 Basi huyo Sheshani alikuwa hana wana wa kiume, ila binti. Naye Sheshani alikuwa na mtumwa, Mmisri, jina lake akiitwa Yarha.
35 Basi akamwoza binti yake aolewe na Yarha, mtumwa wake; naye akamzalia Atai.
36 Na Atai akamzaa Nathani; na Nathani akamzaa Zabadi;
1 Chroniques 11.41
37 na Zabadi akamzaa Eflali; na Eflali akamzaa Obedi;
38 na Obedi akamzaa Yehu; na Yehu akamzaa Azaria;
39 na Azaria akamzaa Helesi; na Helesi akamzaa Eleasa
40 na Eleasa akamzaa Sismai; na Sismai akamzaa Shalumu;
41 na Shalumu akamzaa Yekamia; na Yekamia akamzaa Elishama.
42 Na wana wa Kalebu, nduguye Yerameeli, walikuwa Mesha, mzaliwa wake wa kwanza, aliyekuwa babaye Zifu; na wana wa Maresha, babaye Hebroni.
1 Chroniques 2.18-2.19 1 Samuel 23.19 Hébreux 12.23 Josué 15.24 Romains 8.29
43 Na wana wa Hebroni; Kora, na Tapua, na Rekemu, na Shema.
44 Naye Shema akamzaa Rahamu, babaye Yorkeamu; na Rekemu akamzaa Shamai.
45 Na mwana wake Shamai alikuwa Maoni; na Maoni alikuwa babaye Bethsuri.
Josué 15.58
46 Naye Efa, suria yake Kalebu, alimzaa Harani, na Mosa, na Gazezi; naye Harani akamzaa Gazezi.
1 Chroniques 2.48 1 Chroniques 2.18-2.19
47 Na wana wa Yadai; Regemu, na Yothamu, na Geshani, na Peleti, na Efa, na Shaafu.
48 Naye Maaka, suria yake Kalebu, akamzalia Sheberi, na Tirhana.
1 Chroniques 2.46 Genèse 25.5-25.6
49 Tena akamzaa Shaafu, babaye Madmana; na Sheva babaye Makbena; na babaye Gibea; naye binti Kalebu alikuwa Aksa.
Josué 15.31 Josué 15.57 1 Chroniques 2.42 Esaïe 10.31 2 Samuel 21.6
50 Hao walikuwa wana wa Kalebu. Wana wa Huri, mzaliwa wa kwanza wa Efrathi; Shobali, babaye Kiriath-Yearimu;
Josué 15.9 1 Chroniques 2.19-2.20 1 Chroniques 2.53 1 Chroniques 13.5-13.6 1 Chroniques 4.4
51 Salma, babaye Bethlehemu; na Harefu, babaye Beth-gaderi.
1 Chroniques 4.4 Ruth 4.11 Jean 7.42 Ruth 1.19 Genèse 35.19
52 Naye Shobali, babaye Kiriath-Yearimu, alikuwa na wana; Haroe, na nusu ya Wamenuhothi.
1 Chroniques 4.2
53 Na jamaa za Kiriath-Yearimu; Waithri, na Waputhi, na Washumathi, na Wamishrai; katika hao walitoka Wasorathi, na Waeshtaoli.
Juges 13.25 Josué 15.33 Juges 13.2 2 Samuel 23.38 Josué 19.41
54 Na wana wa Salma; Bethlehemu, na Wanetofathi, Atroth-beth-Yoabu, na nusu ya Wamenuhothi, na Wazori.
Néhémie 12.28 Esdras 2.22 Néhémie 7.26 2 Samuel 23.29 Josué 16.2
55 Na jamaa za waandishi waliokaa Yabesi; Watirathi, na Washimeathi, na Wasukathi. Hao ndio Wakeni, waliotoka kwake Hamathi, babaye mbari ya Rekabu.
Juges 1.16 2 Rois 10.15 Jérémie 35.2-35.8 Jérémie 35.19 Juges 4.11

Cette Bible est dans le domaine public.