Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 18.28
Bible en Swahili de l’est


1 Ikawa Daudi alipokwisha kusema na Sauli, roho ya Yonathani, ikaambatana na roho ya Daudi, Yonathani akampenda kama roho yake mwenyewe.
2 Samuel 1.26 1 Samuel 20.17 Genèse 44.30 1 Samuel 19.2 Deutéronome 13.6
2 Sauli akamtwaa siku ile, wala hakumwacha arudi tena nyumbani kwa baba yake.
1 Samuel 17.15 1 Samuel 16.21-16.23
3 Nao Yonathani na Daudi wakaahidiana, kwa kuwa alimpenda kama roho yake mwenyewe.
1 Samuel 20.42 1 Samuel 20.8-20.17 1 Samuel 23.18 2 Samuel 9.1-9.3 2 Samuel 21.7
4 Ndipo Yonathani akalivua joho alilokuwa amelivaa, akampa Daudi, na mavazi yake, hata na upanga wake pia, na upinde wake, na mshipi wake.
Genèse 41.42 Esther 6.8-6.9 Luc 15.22 Philippiens 2.7-2.8 Esaïe 61.10

Jalousie et hostilité de Saül envers David

5 Basi Daudi akatoka kwenda kila mahali alikotumwa na Sauli, akatenda kwa akili; Sauli akamweka juu ya watu wa vita; jambo hili likawa jema machoni pa watu wote, na machoni pa watumishi wa Sauli pia.
1 Samuel 18.14-18.15 1 Samuel 18.30 Actes 7.10 Psaumes 1.3 1 Samuel 14.52
6 Hata ikawa, walipokuwa wakienda, hapo Daudi aliporudi baada ya kumwua yule Mfilisti, wanawake wakatoka katika miji yote ya Israeli, kwa kuimba na kucheza, ili kumlaki mfalme Sauli; wakatoka na matari, na shangwe, na vinanda.
Juges 11.34 Exode 15.20 Psaumes 68.25 Jérémie 31.11-31.13
7 Nao wale wanawake wakaitikiana wakicheza, wakasema, Sauli amewaua elfu zake, Na Daudi makumi elfu yake.
1 Samuel 21.11 1 Samuel 29.5 Exode 15.21 Psaumes 24.7-24.8
8 Basi Sauli akaghadhibika sana, na maneno haya yakamchukiza; akasema, Wamempa Daudi makumi elfu, na mimi wamenipa elfu tu; kuna nini tena awezayo kupata, isipokuwa ni ufalme?
1 Samuel 15.28 Nombres 11.1 Nombres 22.34 Proverbes 27.4 1 Samuel 20.31
9 Sauli akamwonea Daudi wivu tangu siku ile.
Genèse 31.2 Ephésiens 4.27 Genèse 4.5-4.6 Marc 7.22 Matthieu 20.15
10 Ikawa siku ya pili yake, roho mbaya kutoka kwa Mungu ikamjilia Sauli kwa nguvu, naye akatabiri ndani ya nyumba. Basi Daudi alikuwa akipiga kinubi kwa mkono wake kama siku zote; naye Sauli alikuwa na mkuki mkononi mwake.
1 Samuel 19.9 1 Rois 18.29 Actes 16.16 1 Samuel 16.23 1 Samuel 26.19
11 Mara Sauli akautupa ule mkuki; maana alisema, Nitampiga Daudi hata ukutani. Daudi akaepa, akatoka mbele yake, mara mbili.
1 Samuel 20.33 Esaïe 54.17 Psaumes 37.32-37.33 Jean 8.59 Jean 10.39
12 Sauli akamwogopa Daudi, kwa sababu Bwana alikuwa pamoja naye, ila amemwacha Sauli.
1 Samuel 18.29 1 Samuel 18.15 1 Samuel 28.15 1 Samuel 16.18 1 Samuel 16.13-16.14
13 Kwa ajili ya hayo Sauli akamwondosha kwake, akamfanya awe akida wake juu ya askari elfu; naye akatoka na kuingia mbele ya watu.
2 Samuel 5.2 1 Samuel 22.7 1 Samuel 18.25 Nombres 27.16-27.17 Psaumes 121.8
14 Naye Daudi akatenda kwa busara katika njia zake zote naye Bwana alikuwa pamoja naye.
Genèse 39.23 Josué 6.27 1 Samuel 16.18 Genèse 39.2-39.3 Matthieu 1.23
15 Sauli alipoona ya kwamba alitenda kwa busara sana, yeye alimwogopa.
Daniel 6.4-6.5 Jacques 3.17 Psaumes 112.5 Colossiens 4.5 Jacques 1.5
16 Lakini Israeli wote na Yuda wakampenda Daudi; kwa kuwa alitoka na kuingia mbele yao.
1 Samuel 18.5 Nombres 27.17 1 Rois 3.7 2 Samuel 5.2 Luc 20.19
17 Kisha Sauli akamwambia Daudi, Tazama, binti yangu mkubwa, Merabu, huyu nitakupa wewe ili umwoe; ila na wewe uniwie hodari wa vita, na kuvipiga vita vya Bwana. Maana Sauli alisema moyoni mwake, Mkono wangu usiwe juu yake, bali mkono wa Wafilisti na uwe juu yake.
1 Samuel 18.25 1 Samuel 17.25 1 Samuel 25.28 1 Samuel 18.21 1 Samuel 17.47
18 Naye Daudi akamwambia Sauli, Mimi ni nani, na jamaa zangu ni akina nani, au mbari ya babangu, katika Israeli, hata mimi niwe mkwewe mfalme?
2 Samuel 7.18 1 Samuel 18.23 1 Samuel 9.21 Ruth 2.10 Proverbes 15.33
19 Lakini ikawa, wakati ule, ilipopasa Daudi apewe Merabu, binti Sauli, aliolewa na Adrieli, Mmeholathi.
2 Samuel 21.8 Juges 7.22 Juges 14.20
20 Walakini Mikali, binti Sauli, alimpenda Daudi; watu wakamwambia Sauli, na neno hilo likampendeza.
1 Samuel 18.28
21 Naye Sauli akasema moyoni, Mimi nitamwoza huyu, awe mtego kwake, tena kwamba mkono wa Wafilisti uwe juu yake. Basi Sauli akamwambia Daudi mara ya pili, Leo utakuwa mkwe wangu.
1 Samuel 18.17 Exode 10.7 1 Samuel 18.26 Jérémie 5.26 Proverbes 29.5
22 Naye Sauli akawaagiza watumishi wake, Zungumzeni na Daudi kwa siri, na kusema, Angalia, mfalme anakuridhia, na watumishi wake wote wanakupenda; haya basi! Na uwe mkwewe mfalme.
Proverbes 29.12 Psaumes 55.21 Psaumes 36.1-36.3 2 Samuel 13.28-13.29
23 Nao watumishi wa Sauli wakanena maneno hayo masikioni mwa Daudi. Daudi akasema, Je! Ninyi mwaona kuwa ni shani mimi kuwa mkwewe mfalme, nami ni maskini, tena sina cheo?
1 Jean 3.1 Proverbes 19.6-19.7 Proverbes 14.20 1 Samuel 9.21 Ecclésiaste 9.15-9.16
24 Na hao watumishi wa Sauli wakampasha habari, wakisema, Ndivyo hivyo alivyosema Daudi.
25 Naye Sauli akasema, Mwambieni Daudi hivi, Mfalme hataki mahari yo yote, ila anataka govi mia za Wafilisti, ili ajilipize kisasi adui za mfalme. Basi Sauli alidhani kumwangamiza Daudi kwa mkono wa Wafilisti.
Genèse 34.12 1 Samuel 18.17 1 Samuel 14.24 2 Samuel 17.8-17.11 Genèse 17.11-17.14
26 Na watumishi wake walipomwambia Daudi; maneno hayo, ilimpendeza Daudi sana kuwa mkwewe mfalme. Na siku zilikuwa hazijaisha bado;
1 Samuel 18.21
27 basi Daudi akainuka, akaenda yeye na watu wake, akaua katika Wafilisti watu mia mbili; na Daudi akazileta govi zao, wakampa mfalme hesabu kamili, ili awe mkwewe mfalme. Naye Sauli akamwoza Mikali, binti yake.
2 Samuel 3.14 Juges 14.19 1 Samuel 18.13
28 Sauli akaona na kutambua ya kwamba Bwana alikuwa pamoja na Daudi; na huyo Mikali, binti Sauli, akampenda.
1 Samuel 26.25 Genèse 37.8-37.11 Apocalypse 3.9 Genèse 39.3 Genèse 30.27
29 Naye Sauli akazidi kumwogopa Daudi; Sauli akawa adui yake Daudi sikuzote.
Ecclésiaste 4.4 Jacques 2.19 Genèse 4.4-4.8 1 Jean 3.12-3.15 1 Samuel 18.15
30 Wakati huo wakuu wa Wafilisti wakatoka; kisha ikawa, kila mara walipotoka, Daudi akatenda kwa busara zaidi ya watumishi wote wa Sauli hivyo jina lake likawa na sifa kuu.
1 Samuel 18.5 2 Samuel 11.1 Luc 21.15 1 Samuel 26.21 1 Pierre 2.7

Cette Bible est dans le domaine public.