Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Josué 10.3
Bible en Swahili de l’est


Conquêtes dans le centre et au sud

1 Basi ikawa hapo Adoni-sedeki, mfalme wa Yerusalemu, aliposikia jinsi Yoshua alivyoushika mji wa Ai na kuuharibu kabisa; kama alivyoufanyia mji wa Yeriko na mfalme wake, akaufanya vivyo Ai na mfalme wake; na jinsi wenyeji waliokaa Gibeoni walivyofanya amani na Israeli, na ya kwamba walikuwa kati yao;
Josué 8.2 Josué 6.21 Josué 9.15-9.27 Josué 11.19-11.20 Hébreux 7.1
2 ndipo wakacha mno, kwa sababu Gibeoni ulikuwa ni mji mkubwa, kama ilivyo miji ya kifalme mmojawapo, tena kwa sababu ulikuwa ni mji mkubwa kupita Ai, tena watu wake wote walikuwa ni mashujaa.
Exode 15.14-15.16 Josué 2.24 Deutéronome 11.25 Psaumes 48.4-48.6 Proverbes 1.26-1.27
3 Basi kwa hiyo Adoni-sedeki, mfalme wa Yerusalemu, akatuma ujumbe kwa Hohamu, mfalme wa Hebroni, na kwa Piramu, mfalme wa Yarmuthi, na kwa Yafia, mfalme wa Lakishi, na kwa Debiri, mfalme wa Egloni, akiwaambia,
2 Chroniques 11.9 Michée 1.13 Genèse 23.2 Josué 10.1 Josué 10.5
4 Haya, kweeni mje kwangu, mnisaidie, tuupige Gibeoni; kwa sababu umefanya mapatano ya amani pamoja na Yoshua na wana wa Israeli.
Josué 9.15 Josué 10.1 2 Timothée 3.12 Matthieu 16.24 1 Pierre 4.4
5 Ndipo hao wafalme watano wa Waamori, mfalme wa Yerusalemu, na mfalme wa Hebroni na mfalme wa Yarmuthi na mfalme wa Lakishi, na mfalme wa Egloni, wakakutana pamoja, kisha wakakwea, wao na jeshi zao zote, na kupanga marago yao kinyume cha Gibeoni, na kuupiga vita.
Josué 9.1-9.2 Genèse 15.16 Esaïe 8.9-8.10 Josué 10.6 Nombres 13.29
6 Ndipo watu wa Gibeoni wakatuma wajumbe kwenda kwa Yoshua huko Gilgali maragoni, wakamwambia, Usiulegeze mkono wako hata ukatuacha sisi watumishi wako; uje kwetu kwa upesi, utuokoe, na kutusaidia; kwa sababu wafalme wote wa Waamori wakaao katika nchi ya vilima wamekutana pamoja juu yetu.
Josué 5.10 Josué 9.6 Esaïe 33.22 Josué 21.11 2 Rois 4.24
7 Basi Yoshua akakwea kutoka Gilgali, yeye, na watu wa vita wote pamoja naye, na mashujaa wenye uwezo pia wote.
Josué 8.1 Esaïe 8.12 Esaïe 8.14
8 Bwana akamwambia Yoshua, Usiwache watu hao; kwa kuwa mimi nimekwisha kuwatia mikononi mwako; hapana mtu awaye yote miongoni mwao atakayesimama mbele yako.
Josué 11.6 Deutéronome 3.2 Psaumes 27.1-27.2 Esaïe 41.10-41.15 Josué 1.5-1.9
9 Basi Yoshua akawafikilia ghafula; kwani alikwea kutoka Gilgali kwenda usiku kucha.
2 Timothée 2.3 Proverbes 22.29 2 Timothée 4.2 Ecclésiaste 9.10 Proverbes 24.11-24.12
10 Bwana naye akawatapanya mbele ya Israeli, naye Israeli akawaua uuaji ulio mkuu hapo Gibeoni, akawafukuza waikimbilie hiyo njia ya kukwelea kwenda Beth-horoni, na kuwapiga hata kufikilia Azeka, tena hata kufikilia Makeda.
Josué 16.3 Josué 16.5 Juges 4.15 Psaumes 18.14 Esaïe 28.21
11 Kisha ikawa, hapo walipokuwa wakimbia mbele ya Israeli, hapo walipokuwa katika kutelemkia Beth-horoni, ndipo Bwana alipowatupia mawe makubwa kutoka mbinguni juu yao hata kufikilia Azeka, nao wakafa; hao waliokufa kwa kuuawa na hayo mawe ya barafu walikuwa ni wengi kuliko hao waliouawa na wana wa Israeli kwa upanga.
Esaïe 28.2 Psaumes 18.12-18.14 Apocalypse 16.21 Esaïe 30.30 Genèse 19.24
12 Ndipo Yoshua akanena na Bwana katika siku hiyo ambayo Bwana aliwatoa Waamori mbele ya wana wa Israeli; akasema mbele ya macho ya Israeli, Wewe Jua, simama kimya juu ya Gibeoni; Na wewe Mwezi, simama katika bonde la Aiyaloni.
Habakuk 3.11 Esaïe 38.8 Esaïe 60.20 Josué 10.13 Juges 12.12
13 Ndipo jua likasimama, na mwezi ukatulia, Hata hilo taifa lilipokuwa limekwisha jipatiliza juu ya adui zao.
2 Samuel 1.18 Esaïe 38.8 Habakuk 3.11 Apocalypse 16.8-16.9 Joël 2.10
14 Haikuwapo siku nyingine mfano wa siku hiyo katika siku zilizotangulia mbele yake wala katika hizo zilizoandama baada yake, hata ikawa yeye Bwana kuisikia sauti ya binadamu; kwa kuwa Bwana alipiga vita kwa ajili ya Israeli.
Josué 10.42 Deutéronome 1.30 Esaïe 38.8 Josué 23.3 Matthieu 21.21-21.22
15 Basi Yoshua akarudi, na Israeli wote wakarudi pamoja naye, mpaka maragoni hapo Gilgali.
Josué 10.43 Josué 10.6
16 Na hawa wafalme watano wakakimbia, wakajificha ndani ya pango la Makeda.
Esaïe 2.19-2.22 1 Samuel 24.3 Apocalypse 6.15 Esaïe 2.10-2.12 Juges 6.2
17 Kisha Yoshua aliambiwa habari hiyo, ya kwamba, Hao wafalme watano wameonekana, nao wa hali ya kujificha ndani ya pango la Makeda
18 Basi Yoshua akasema, Haya, vingirisheni mawe makubwa mdomoni mwa lile pango, kisha wekeni watu hapo ili kuwalinda;
Amos 5.19 Job 21.30 Amos 9.1 Matthieu 27.66 Juges 9.46-9.49
19 lakini msikae ninyi; wafuatieni adui zenu, mwapige hao walio nyuma; msiwaache wakaingia ndani ya miji yao; kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, amewatia mikononi mwenu.
2 Samuel 20.6 Jérémie 48.10 Esaïe 9.14-9.15 Jérémie 8.14 Psaumes 18.37-18.41
20 Kisha ikawa, hapo Yoshua, na wana wa Israeli, walipokuwa wamekwisha kuwaua watu wengi mno, hata wakaangamizwa, na hayo mabaki yao yaliyowasalia walipokuwa wamekwisha ingia katika miji yao yenye boma,
Josué 8.24 Jérémie 8.14 Deutéronome 20.16 2 Chroniques 13.17 2 Samuel 20.6
21 ndipo hao watu wote wakamrudia Yoshua maragoni huko Makeda salama; hakuna mtu awaye yote aliyetoa ulimi kinyume cha hao wana wa Israeli hata mmojawapo.
Exode 11.7 Esaïe 57.4 Esaïe 54.17
22 Kisha Yoshua akasema, Haya, funua mdomo wa pango, mniletee hao wafalme watano hapa nje ya pango.
1 Samuel 15.32
23 Nao wakafanya, wakamletea hao wafalme watano hapo nje ya pango, yaani, mfalme wa Yerusalemu, na mfalme wa Hebroni, na mfalme wa Yarmuthi, na mfalme wa Lakishi, na mfalme wa Egloni.
Josué 10.3 Josué 10.1 Josué 10.5
24 Kisha ikawa hapo walipomletea Yoshua hao wafalme watano hapo nje, Yoshua akawaita wanaume wote wa Israeli, akawaambia majemadari wa watu wa vita waliokwenda naye, Haya, jongeeni karibu, mweke nyayo za miguu yenu katika shingo za wafalme hawa. Nao wakajongea karibu, wakatia nyayo zao katika shingo zao.
Malachie 4.3 Psaumes 110.1 Apocalypse 2.26-2.27 Psaumes 110.5 Esaïe 26.5-26.6
25 Yoshua akawaambia, Msiche, wala msifadhaike; iweni hodari na wa mioyo ya ushujaa; kwa kuwa ndivyo Bwana atakavyowafanyia adui zenu wote ambao mwapigana nao.
Deutéronome 31.6-31.8 Deutéronome 7.19 Josué 1.9 Psaumes 77.11 Ephésiens 6.10
26 Baadaye Yoshua akawapiga, na kuwaua, akawatundika katika miti mitano; nao wakawa wakitundikwa katika hiyo miti hata jioni.
Josué 8.29 Esther 2.23 Nombres 25.4 Deutéronome 21.22-21.23 2 Samuel 21.9
27 Kisha wakati wa kuchwa jua, Yoshua akatoa amri, nao wakawatelemsha katika hiyo miti, na kuwatupa katika lile pango ambamo walikuwa walijificha kisha wakatia mawe makubwa mdomoni mwa pango, hata hivi leo.
Josué 8.29 Josué 7.26 2 Samuel 18.17 Deutéronome 21.22-21.23 Josué 4.9
28 Siku hiyo Yoshua akautwaa mji wa Makeda, akaupiga kwa makali ya upanga, na mfalme wake; akawaangamiza kabisa na wote pia waliokuwamo ndani yake, hakumwacha hata mmoja aliyesalia; naye akamfanyia huyo mfalme wa Makeda kama alivyomfanyia huyo mfalme wa Yeriko.
Josué 6.21 Josué 10.37 Psaumes 21.8-21.9 Josué 10.39 Josué 10.35
29 Kisha Yoshua akapita kutoka hapo Makeda, mpaka Libna, na Israeli wote pamoja naye, nao wakapiga Libna;
Josué 21.13 Josué 15.42 Josué 12.15 Josué 8.29 Josué 8.2
30 Bwana akautia na mji huo pia pamoja na mfalme wake mkononi mwa Israeli; naye akaupiga kwa makali ya upanga, na wote pia waliokuwamo ndani yake; hakumwacha hata mmoja aliyesalia ndani yake; naye akamtenda mfalme wake kama alivyomtenda huyo mfalme wa Yeriko.
31 Kisha Yoshua akapita kutoka hapo Libna, na Israeli wote pamoja naye, wakafika Lakishi, wakapanga marago mbele yake na kupigana nao;
Josué 10.3 2 Chroniques 11.9 Josué 12.11 Michée 1.13 Josué 15.39
32 Bwana akautia huo mji wa Lakishi mkononi mwa Israeli, naye akautwaa siku ya pili, akaupiga kwa makali ya upanga, na wote pia waliokuwamo ndani yake, sawasawa na hayo yote aliyoutenda Libna.
33 Wakati huo Horamu, mfalme wa Gezeri, akakwea ili kuusaidia Lakishi, lakini Yoshua akampiga yeye na watu wake, hata asimsazie hata mtu mmoja.
Juges 1.29 Josué 16.10 Josué 16.3 1 Chroniques 20.4 1 Rois 9.15-9.17
34 Kisha Yoshua akapita kutoka hapo Lakishi, na Israeli wote pamoja naye, hata wakafikilia Egloni; nao wakapanga marago mbele yake, na kupigana nao;
Josué 10.3 Josué 15.39 Josué 12.12
35 siku iyo hiyo wakautwaa, nao wakaupiga kwa makali ya upanga, na wote pia waliokuwamo ndani yake akawaangamiza kabisa siku hiyo, sawasawa na hayo yote aliyoufanyia mji wa Lakishi.
Josué 10.37 Job 19.10 Lévitique 26.44
36 Kisha Yoshua akakwea kutoka hapo Egloni, na Israeli wote pamoja naye, hata wakafikilia Hebroni; nao wakapigana nao;
Juges 1.10 Josué 15.13 Nombres 13.22 Josué 14.13-14.14 Josué 15.54
37 wakautwaa, na kuupiga kwa makali ya upanga, na mfalme wake, na miji yake yote, na wote waliokuwamo ndani yake; hakumwacha aliyesalia hata mtu mmoja, sawasawa na hayo yote aliyoufanyia huo mji wa Egloni; lakini akauangamiza kabisa, na wote pia waliokuwamo ndani yake.
38 Kisha Yoshua akarudi, na Israeli wote pamoja naye, hata Debiri; nao wakapigana nao;
Josué 15.15 Josué 21.15 Juges 1.11-1.15 Josué 12.13 Josué 15.49
39 kisha akautwaa, na mfalme wake, na miji yake yote; nao wakawapiga kwa makali ya upanga, wakawaangamiza kabisa wote pia waliokuwamo ndani yake; hakumwacha hata mmoja aliyesalia; kama alivyoufanyia Hebroni aliufanyia na Debiri vivyo, na mfalme wake; kama alivyoufanyia Libna, na mfalme wake.
Deutéronome 3.3 Josué 10.33 Josué 10.40 2 Rois 10.11 Abdias 1.18
40 Basi Yoshua akaipiga nchi hiyo yote, nchi ya vilima, na nchi ya Negebu, na nchi ya Shefela, na nchi ya matelemko, na wafalme wake wote; hakumwacha aliyesalia hata mmoja; lakini akawaharibu kabisa wote waliokuwa wavuta pumzi, kama Bwana, Mungu wa Israeli, alivyoamuru.
Deutéronome 7.2-7.16 Exode 34.12 Deutéronome 26.16-26.17 Deutéronome 20.16-20.17 Josué 18.21-19.8
41 Yoshua akawapiga kutoka Kadesh-barnea mpaka Gaza, na nchi yote ya Gosheni, hata Gibeoni.
Josué 11.16 Josué 15.51 Genèse 10.19 Deutéronome 9.23 Nombres 13.26
42 Na wafalme hao wote na nchi zao Yoshua akatwaa, wakati huo, kwa sababu yeye Bwana, Mungu wa Israeli, alipigana kwa ajili ya Israeli,
Josué 10.14 Psaumes 46.7 Deutéronome 20.4 Psaumes 46.1 Esaïe 8.9-8.10
43 Kisha Yoshua akarudi, na Israeli wote pamoja naye, hata marago yao huko Gilgali.
Josué 10.15 Josué 4.19 1 Samuel 11.14

Cette Bible est dans le domaine public.