Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Deutéronome 29.14
Bible en Swahili de l’est


1 Haya ndiyo maneno ya agano Bwana alilomwamuru Musa alifanye na wana wa Israeli katika nchi ya Moabu, pamoja na agano alilofanya nao Horebu.
Deutéronome 5.2-5.3 Exode 19.3-19.5 Actes 3.25 Deutéronome 4.23 Jérémie 11.6
2 Musa akawaita Israeli wote akawaambia, Mmeyaona yote Bwana aliyomfanya Farao katika nchi ya Misri mbele ya macho yenu, yeye na watumwa wake wote, na nchi yake yote;
Exode 19.4 Psaumes 78.43-78.51 Psaumes 105.27-105.36 Josué 24.5-24.6 Exode 8.12
3 yale majaribu makuu yaliyoyaona macho yako; hizo ishara, na ile miujiza mikuu;
Néhémie 9.9-9.11 Deutéronome 7.18-7.19 Deutéronome 4.32-4.35
4 lakini Bwana hakuwapa moyo wa kujua, wala macho ya kuona, wala masikio ya kusikia, hata leo hivi.
Jean 8.43 Proverbes 20.12 Esaïe 6.9-6.10 Esaïe 63.17 2 Thessaloniciens 2.10-2.12
5 Nami miaka arobaini nimewaongoza jangwani; nguo zenu hazikuchakaa juu yenu, wala kiatu chako hakikuchakaa katika mguu wako.
Deutéronome 8.4 Deutéronome 1.3 Deutéronome 8.2 Néhémie 9.21 Matthieu 6.31-6.32
6 Hamkula mkate, wala hamkunywa divai, wala kileo; ili mpate kujua kwamba Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.
Deutéronome 8.3 Ephésiens 5.18 Nombres 20.8 Psaumes 78.24-78.25 Exode 16.12
7 Nanyi mlipokuja mahali hapa, walitutokea kupigana juu yetu Sihoni mfalme wa Heshboni, na Ogu mfalme wa Bashani, tukawapiga;
Nombres 21.21-21.35 Psaumes 135.10-135.12 Nombres 32.33-32.42 Deutéronome 2.24-3.17 Psaumes 136.17-136.22
8 tukaitwaa nchi yao, nayo tukawapa Wareubeni, na Wagadi, na nusu ya kabila ya Manase, iwe urithi.
Deutéronome 3.12-3.13 Nombres 32.33
9 Shikeni basi maneno ya agano hili myafanye, ili mfanikiwe katika yote mfanyayo.
Deutéronome 4.6 Josué 1.7 1 Rois 2.3 Luc 11.28 Jérémie 50.5
10 Leo mmesimama nyote mbele za Bwana, Mungu wenu; wakuu wenu, na kabila zenu, na wazee wenu, na maakida wenu, waume wote wa Israeli,
Néhémie 10.28 Deutéronome 4.10 2 Chroniques 23.16 Apocalypse 6.15 Néhémie 8.2
11 vijana vyenu, na wake wenu, na mgeni wako aliye kati ya kituo chako, tokea mchanjaji wa kuni zako hata mtekaji wa maji yako;
Exode 12.38 Exode 12.48-12.49 Josué 9.21-9.27 Nombres 11.4 Galates 3.28
12 ili uingie katika agano la Bwana, Mungu wako, na kiapo chake, afanyacho nawe Bwana, Mungu wako, hivi leo;
2 Chroniques 15.12-15.15 Deutéronome 5.2-5.3 Josué 24.25 Néhémie 10.28-10.29 2 Rois 11.17
13 apate kukuweka leo uwe taifa kwake naye apate kuwa Mungu kwako, kama alivyokuambia, na kama alivyowaapia baba zako, Ibrahimu, na Isaka, na Yakobo.
Exode 6.7 Genèse 17.7 Deutéronome 28.9 Jérémie 32.38 Genèse 26.3-26.4
14 Wala sifanyi na ninyi peke yenu agano hili na kiapo hiki;
Jérémie 31.31-31.34 Hébreux 8.7-8.12

Conséquences de la désobéissance

15 ila na yeye aliyesimama hapa nasi hivi leo mbele ya Bwana, Mungu wetu, na yeye naye asiyekuwapo pamoja nasi leo;
Actes 2.39 Deutéronome 5.3 Jérémie 32.39 Jérémie 50.5 1 Corinthiens 7.14
16 (kwani mwajua mlivyoketi nchi ya Misri, na tulivyo kuja katikati ya mataifa hayo mliyopita katikati yao;
Deutéronome 3.1-3.2 Deutéronome 2.4 Deutéronome 2.24 Deutéronome 2.9 Deutéronome 2.19
17 nanyi mliona machukizo yao, na sanamu zao, miti na mawe, fedha na dhahabu, zilizokuwako kwao;)
Deutéronome 28.36
18 asiwe mtu katikati yenu, mume wala mke, wala jamaa, wala kabila, ageukaye moyo wake leo amwache Bwana, Mungu wetu, kwenda kuitumikia miungu ya mataifa hayo; lisiwe katikati yenu shina lizaalo uchungu na pakanga;
Hébreux 12.15 Deutéronome 11.16-11.17 Deutéronome 13.1-13.15 Amos 6.12 Deutéronome 17.2-17.7
19 ikawa asikiapo maneno ya laana hii, ajibarikie mtu huyo moyoni mwake, na kusema, Nitakuwa katika amani, nijapotembea katika upotoe wa moyo wangu kwa kuangamiza mbichi na kavu;
Nombres 15.30 Ephésiens 4.17 Ephésiens 5.6 Psaumes 10.4-10.6 Ecclésiaste 11.9
20 Bwana hatamsamehe mtu huyo, lakini wakati huo hasira ya Bwana na wivu wake vitafuka moshi juu ya mtu yule, na laana yote iliyoandikwa katika kitabu hiki itamkalia juu yake, na Bwana atalifuta jina lake chini ya mbingu.
Psaumes 74.1 Deutéronome 9.14 Psaumes 79.5 Ezéchiel 23.25 Ezéchiel 14.7-14.8
21 Bwana atamtenga kwa uovu, kutoka kabila zote za Israeli, kwa laana zote za agano lililoandikwa katika chuo hiki cha torati.
Matthieu 24.51 Ezéchiel 13.9 Josué 7.1-7.26 Malachie 3.18 Matthieu 25.32
22 Na kizazi cha baadaye, wanenu watakaoinuka baada yenu, na mgeni atakayekuja kutoka nchi ya mbali, watasema, watakapoyaona mapigo ya nchi ile, na magonjwa aliyoitia Bwana;
Jérémie 19.8
23 ya kuwa nchi yake nzima ni kibiriti, na chumvi, na kuteketea, haipandwi, wala haizai, wala nyasi hazimei humo, kama mapinduko ya Sodoma na Gomora, Adma na Seboimu, aliyoipindua Bwana kwa ghadhabu yake na hasira zake;
Jérémie 17.6 Sophonie 2.9 Esaïe 34.9 Genèse 19.24-19.25 Ezéchiel 47.11
24 mataifa yote watasema, Mbona Bwana ameifanyia hivi nchi hii? Ni nini maana yake hari ya hasira hizi kubwa?
Jérémie 22.8-22.9 1 Rois 9.8-9.9 2 Chroniques 7.21-7.22 Romains 2.5 Ezéchiel 14.23
25 Ndipo watakaposema watu, Ni kwa kuwa waliacha agano la Bwana, Mungu wa baba zao, alilofanya nao hapo alipowatoa katika nchi ya Misri;
Jérémie 31.32 1 Rois 19.10-19.14 Jérémie 40.2-40.3 Jérémie 22.9 Hébreux 8.9
26 wakaenda wakatumikia miungu mingine, wakaiabudu miungu wasiyoijua, asiyowapa yeye;
Jérémie 19.3-19.13 Jérémie 44.2-44.6 Juges 5.8 2 Rois 17.7-17.18 Deutéronome 28.64
27 ndipo ikawashwa hasira ya Bwana juu ya nchi hii, kwa kuleta juu yake laana yote iliyoandikwa katika kitabu hiki;
Daniel 9.11-9.14 Deutéronome 28.15-28.68 Deutéronome 29.20-29.21 Lévitique 26.14-26.46 Deutéronome 27.15-27.26
28 Bwana akawang’oa katika nchi yao kwa hasira, na ghadhabu, na makamio makuu, akawatupa waende nchi nyingine, kama hivi leo.
2 Chroniques 7.20 Proverbes 2.22 1 Rois 14.15 Psaumes 52.5 Deutéronome 8.18
29 Mambo ya siri ni ya Bwana, Mungu wetu; lakini mambo yaliyofunuliwa ni yetu sisi na watoto wetu milele, ili tuyafanye maneno yote ya sheria hii.
Actes 1.7 Romains 11.33-11.34 Job 11.6-11.7 Matthieu 13.35 1 Corinthiens 2.16

Cette Bible est dans le domaine public.