Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 9.28
Bible en Swahili de l’est


Conversion de Saul

1 Lakini Sauli, akizidi kutisha na kuwaza kuwaua wanafunzi wa Bwana, akamwendea Kuhani Mkuu,
Actes 8.3 Psaumes 27.12 Actes 9.11-9.21 Actes 26.9-26.11 1 Corinthiens 15.9
2 akataka ampe barua za kuenda Dameski zilizoandikwa kwa masinagogi, ili akiona watu wa Njia hii, waume kwa wake, awafunge na kuwaleta Yerusalemu.
Actes 19.23 Actes 19.9 Actes 24.22 Actes 22.4-22.5 Actes 24.14
3 Hata alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafula ikamwangaza kote kote nuru kutoka mbinguni.
1 Corinthiens 15.8 Actes 22.6 Actes 26.12-26.13 Actes 9.17 Psaumes 104.2
4 Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona waniudhi?
Zacharie 2.8 Actes 26.14-26.15 Esaïe 63.9 Jean 18.6 Matthieu 25.45-25.46
5 Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe.
1 Samuel 3.4-3.10 1 Timothée 1.13 Esaïe 45.9 Job 40.9-40.10 Actes 5.39
6 Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda.
1 Samuel 28.5 Actes 26.16 Philippiens 2.12 Luc 3.10 Romains 9.15-9.24
7 Na wale watu waliosafiri pamoja naye wakasimama kimya, wakiisikia sauti, wasione mtu.
Actes 22.9 Daniel 10.7 Jean 12.29 Matthieu 24.40-24.41 Actes 26.13-26.14
8 Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski.
Actes 22.11 Actes 9.18 Actes 13.11 Genèse 19.11 Exode 4.11
9 Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi.
Esther 4.16 Actes 9.11-9.12 2 Chroniques 33.12-33.13 Jonas 3.6-3.8 2 Chroniques 33.18-33.19
10 Basi palikuwapo Dameski mwanafunzi jina lake Anania. Bwana akamwambia katika maono, Anania. Akasema, Mimi hapa, Bwana.
Esaïe 6.8 Actes 22.12 Actes 10.3 Genèse 22.1 1 Samuel 3.8-3.10
11 Bwana akamwambia, Simama, enenda zako katika njia iitwayo Nyofu, ukaulize katika nyumba ya Yuda mtu aitwaye Sauli, wa Tarso; maana, angalia, anaomba;
Actes 22.3 Actes 21.39 Actes 9.30 Actes 11.25 Actes 11.13
12 naye amemwona mtu, jina lake Anania, akiingia, na kumwekea mikono juu yake, apate kuona tena.
Marc 5.23 Actes 9.10 Actes 9.17-9.18
13 Lakini Anania akajibu, Bwana, nimesikia habari za mtu huyu kwa watu wengi, mabaya mengi aliyowatenda watakatifu wako Yerusalemu;
Actes 8.3 Actes 22.19-22.20 Actes 9.1 1 Samuel 16.2 Jonas 1.2-1.3
14 hata hapa ana amri itokayo kwa wakuu wa makuhani awafunge wote wakuitiao Jina lako.
Actes 9.21 Actes 7.59 Actes 22.16 1 Corinthiens 1.2 2 Timothée 2.22
15 Lakini Bwana akamwambia, Nenda tu; kwa maana huyu ni chombo kiteule kwangu, alichukue Jina langu mbele ya Mataifa, na wafalme, na wana wa Israeli.
Ephésiens 3.7-3.8 Galates 1.15-1.16 Actes 13.2 Romains 1.5 Romains 11.13
16 Maana nitamwonyesha yalivyo mengi yatakayompasa kuteswa kwa ajili ya Jina langu.
Actes 21.11 2 Corinthiens 11.23-11.27 Jean 15.20 1 Thessaloniciens 3.3 1 Pierre 4.14
17 Anania akaenda zake, akaingia mle nyumbani; akamwekea mikono akisema, Ndugu Sauli, Bwana amenituma, Yesu, yeye aliyekutokea katika njia uliyoijia, upate kuona tena, ukajazwe Roho Mtakatifu.
Actes 8.17 Actes 6.6 Actes 2.4 Actes 22.12-22.14 2 Timothée 1.6
18 Mara vikaanguka machoni pake vitu kama magamba, akapata kuona, akasimama, akabatizwa;
Actes 2.38 Actes 22.16 2 Corinthiens 3.14 Actes 2.41 Actes 13.37-13.38
19 akala chakula, na kupata nguvu. Akawa huko siku kadha wa kadha pamoja na wanafunzi walioko Dameski.
Actes 26.20 Galates 1.17 Ecclésiaste 9.7 Actes 11.26 1 Samuel 30.12
20 Mara akamhubiri Yesu katika masinagogi, kwamba yeye ni Mwana wa Mungu.
Matthieu 27.54 Psaumes 2.7 Galates 1.23-1.24 1 Jean 4.14-4.15 Apocalypse 2.18
21 Na wote waliosikia wakashangaa, wakasema, Siye huyu aliyewaharibu walioliitia Jina hili huko Yerusalemu? Na hapa alikuwa amekuja kwa kusudi hilo, awafunge na kuwapeleka kwa wakuu wa makuhani?
Actes 9.13-9.14 Actes 8.3 Matthieu 13.54-13.55 Actes 4.13 Actes 2.12
22 Sauli akazidi kuwa hodari, akawatia fadhaa Wayahudi waliokaa Dameski, akithibitisha ya kuwa huyu ndiye Kristo.
Actes 18.5 Actes 18.27-18.28 Actes 28.23 Luc 21.15 Esaïe 40.29
23 Hata siku nyingi zilipopita, Wayahudi wakafanya shauri ili wamwue;
Actes 14.2 Actes 22.21-22.23 1 Thessaloniciens 2.15-2.16 Galates 1.17-1.18 Matthieu 10.16-10.23
24 lakini hila yao ikajulikana na Sauli. Wakamvizia malangoni mchana na usiku wapate kumwua.
2 Corinthiens 11.32 Actes 25.3 Actes 20.19 Actes 20.3 Actes 9.29-9.30
25 Wanafunzi wake wakamtwaa usiku wakamshusha ukutani, wakimtelemsha katika kapu.
2 Corinthiens 11.33 Josué 2.15 1 Samuel 19.11-19.12
26 Na Sauli alipofika Yerusalemu, alijaribu kujiunga na wanafunzi, nao walikuwa wakimwogopa wote, wasisadiki ya kuwa yeye ni mwanafunzi.
Actes 26.20 Galates 2.4 Actes 4.23 Actes 22.17-22.20 Matthieu 10.17-10.19
27 Lakini Barnaba akamtwaa, akampeleka kwa mitume, akawaeleza jinsi alivyomwona Bwana njiani, na ya kwamba alisema naye, na jinsi alivyohubiri kwa ushujaa katika Dameski kwa jina la Yesu.
Actes 4.36 Actes 4.29 Galates 1.18-1.19 Actes 4.13 Actes 15.25-15.26
28 Naye akawa pamoja nao katika Yerusalemu akiingia na kutoka.
Actes 1.21 1 Rois 3.7 Galates 1.18 Nombres 27.16-27.17 Psaumes 121.8
29 Akahubiri kwa jina la Bwana kwa ushujaa, akinena na kuhojiana na Wayahudi wa Kiyunani. Nao wakajaribu kumwua.
Actes 6.1 2 Corinthiens 11.26 Actes 17.17 Actes 11.20 Actes 19.8
30 Lakini ndugu walipopata habari wakamchukua mpaka Kaisaria, wakampeleka aende Tarso.
Actes 8.40 Actes 9.11 Actes 11.25 Matthieu 10.23 Actes 17.15

Miracles à Lydde et Jaffa

31 Basi kanisa likapata raha katika Uyahudi wote na Galilaya na Samaria, likajengwa, likiendelea na kuongezeka katika kicho cha Bwana, na faraja ya Roho Mtakatifu.
Actes 8.1 Romains 5.5 Esaïe 33.6 Psaumes 111.10 Proverbes 8.13
32 Hata Petro alipokuwa akizunguka-zunguka pande zote akawatelemkia na watakatifu waliokaa Lida.
Actes 9.13 Actes 8.25 Galates 2.7-2.9 Philippiens 1.1 Actes 26.10
33 Akamwona mtu mmoja huko, jina lake Ainea, mtu huyo amelala kitandani miaka minane; maana alikuwa amepooza.
Marc 2.3-2.11 Marc 9.21 Jean 5.5 Actes 14.8 Luc 13.16
34 Petro akamwambia, Ainea, Yesu Kristo akuponya; ondoka, ujitandikie. Mara akaondoka.
Actes 3.6 Actes 3.16 Actes 4.10 Matthieu 8.3 Actes 16.18
35 Na watu wote waliokaa Lida na Sharoni wakamwona, wakamgeukia Bwana.
1 Chroniques 5.16 Actes 11.21 Actes 9.42 2 Corinthiens 3.16 Esaïe 35.2
36 Na mwanafunzi mmoja alikuwako Yafa, jina lake Tabitha, tafsiri yake ni Dorkasi (yaani paa); mwanamke huyu alikuwa amejaa matendo mema na sadaka alizozitoa.
Jonas 1.3 Esdras 3.7 2 Chroniques 2.16 Jean 15.5 Josué 19.46
37 Ikawa siku zile akaugua, akafa; hata walipokwisha kumwosha, wakamweka orofani.
Actes 1.13 Actes 20.8 Actes 9.39 Marc 14.15 Jean 11.36-11.37
38 Na kwa kuwa mji wa Lida ulikuwa karibu na Yafa, nao wanafunzi wamesikia ya kwamba Petro yuko huko, wakatuma watu wawili kwake, kumsihi na kusema, Usikawie kuja kwetu.
Actes 9.36 2 Rois 4.28-4.30 Actes 9.32 Actes 11.26
39 Petro akaondoka akafuatana nao. Alipofika, wakampeleka juu orofani wajane wote wakasimama karibu naye, wakilia na kumwonyesha zile kanzu na nguo alizozishona Dorkasi wakati ule alipokuwa pamoja nao.
1 Thessaloniciens 4.13 Proverbes 10.7 Proverbes 31.30-31.31 1 Thessaloniciens 1.3 Marc 14.8
40 Petro akawatoa nje wote, akapiga magoti, akaomba, kisha akaelekea yule maiti, akanena, Tabitha, ondoka. Naye akafumbua macho yake, na alipomwona Petro akajiinua, akaketi.
Matthieu 9.25 Actes 7.60 2 Rois 4.32-4.36 Jean 11.43-11.44 Marc 9.25
41 Akampa mkono, akamwinua; hata akiisha kuwaita wale watakatifu na wajane akamweka mbele yao, hali yu hai.
Actes 6.1 Genèse 45.26 Job 29.13 1 Rois 17.23 Luc 7.12
42 Ikajulikana katika mji mzima wa Yafa; watu wengi wakamwamini Bwana.
Jean 12.11 Actes 9.35 Jean 11.45 Jean 12.44 Actes 19.17-19.18
43 Basi Petro akakaa siku kadha wa kadha huko Yafa, nyumbani mwa mtu mmoja, jina lake Simoni, mtengenezaji wa ngozi.
Actes 10.6 Actes 10.32

Cette Bible est dans le domaine public.