Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 2.46
Bible en Swahili de l’est


Venue de l’Esprit à la Pentecôte

1 Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja.
Actes 20.16 Romains 15.6 1 Corinthiens 16.8 Philippiens 1.27 Actes 4.32
2 Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi.
Actes 4.31 Esaïe 65.24 Cantique 4.16 Actes 16.25-16.26 Ezéchiel 3.12-3.13
3 Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao.
Matthieu 3.11 Actes 2.4 Jean 1.32-1.33 Apocalypse 11.3 Esaïe 11.2-11.3
4 Wote wakajazwa Roho Mtakatifu, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama Roho alivyowajalia kutamka.
Actes 13.52 Actes 4.31 Actes 9.17 Ephésiens 5.18 Marc 16.17
5 Na walikuwako Yerusalemu Wayahudi wakikaa, watu watauwa, watu wa kila taifa chini ya mbingu.
Actes 8.2 Luc 2.25 Actes 10.2 Actes 22.12 Actes 2.1
6 Basi sauti hii iliposikiwa makutano walikutanika, wakashikwa na fadhaa, kwa kuwa kila mmoja aliwasikia wakisema kwa lugha yake mwenyewe.
1 Corinthiens 16.9 2 Corinthiens 2.12 Matthieu 2.3 Actes 3.11 Actes 2.2
7 Wakashangaa wote, wakastaajabu wakiambiana, Tazama, hawa wote wasemao si Wagalilaya?
Actes 1.11 Actes 2.12 Jean 7.52 Matthieu 4.18-4.22 Actes 14.11-14.12
8 Imekuwaje basi sisi kusikia kila mtu lugha yetu tuliyozaliwa nayo?
9 Warparthi na Wamedi na Waelami, nao wakaao Mesopotamia, Uyahudi na Kapadokia, Ponto na Asia,
1 Pierre 1.1 Actes 18.2 Actes 16.6 Esaïe 11.11 Daniel 8.2
10 Frigia na Pamfilia, Misri na pande za Libia karibu na Kirene, na wageni watokao Rumi, Wayahudi na waongofu,
Actes 16.6 Actes 18.23 Actes 15.38 Actes 13.13 Romains 1.15
11 Wakrete na Waarabu; tunawasikia hawa wakisema kwa lugha zetu matendo makuu ya Mungu.
Exode 15.11 1 Corinthiens 12.10 Tite 1.5 Jérémie 3.2 2 Chroniques 17.11
12 Wakashangaa wote wakaingiwa na shaka, wakiambiana, Maana yake nini mambo haya?
Actes 2.7 Actes 17.20 Luc 18.36 Luc 15.26 Actes 10.17
13 Wengine walidhihaki, wakisema, wamelewa kwa mvinyo mpya.
1 Corinthiens 14.23 Zacharie 9.15 Zacharie 9.17 Cantique 7.9 Ephésiens 5.18
14 Lakini Petro akasimama pamoja na wale kumi na mmoja, akapaza sauti yake, akawaambia, Enyi watu wa Uyahudi, na ninyi nyote mkaao Yerusalemu, lijueni jambo hili, mkasikilize maneno yangu.
Actes 13.16 Esaïe 51.4 Esaïe 52.8 Esaïe 51.7 Osée 8.1
15 Sivyo mnavyodhani; watu hawa hawakulewa, kwa maana ni saa tatu ya mchana;
1 Samuel 1.15 1 Thessaloniciens 5.5-5.8 Matthieu 20.3
16 lakini jambo hili ni lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Yoeli,
Joël 2.28-2.32
17 Itakuwa siku za mwisho, asema Mungu, nitawamwagia watu wote Roho yangu, na wana wenu na binti zenu watatabiri; na vijana wenu wataona maono; na wazee wenu wataota ndoto.
Esaïe 44.3 Actes 10.45 Actes 21.9 Jean 7.39 Tite 3.4-3.6
18 Naam, na siku zile nitawamwagia watumishi wangu wanaume na wanawake Roho yangu, nao watatabiri.
Galates 3.28 Colossiens 3.11 Actes 21.10 1 Corinthiens 7.21-7.22
19 Nami nitatoa ajabu katika mbingu juu, na ishara katika nchi chini, damu na moto, na mvuke wa moshi.
Joël 2.30-2.31 Malachie 4.1-4.6 Sophonie 1.14-1.18
20 Jua litageuka kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja ile siku ya Bwana iliyo kuu na iliyo dhahiri.
Matthieu 24.29 2 Pierre 3.10 1 Thessaloniciens 5.2 Amos 8.9 Luc 21.25
21 Na itakuwa kila atakayeliitia jina la Bwana ataokolewa.
Romains 10.12-10.13 Joël 2.32 Matthieu 28.19 Actes 22.16 Psaumes 86.5
22 Enyi waume wa Israeli, sikilizeni maneno haya: Yesu wa Nazareti, mtu aliyedhihirishwa kwenu na Mungu kwa miujiza na ajabu na ishara, ambazo Mungu alizifanya kwa mkono wake kati yenu, kama ninyi wenyewe mnavyojua;
Jean 3.2 Jean 14.10-14.11 Matthieu 12.28 Hébreux 2.4 Matthieu 9.8
23 mtu huyu alipotolewa kwa shauri la Mungu lililokusudiwa, na kwa kujua kwake tangu zamani, ninyi mkamsulibisha kwa mikono ya watu wabaya, mkamwua;
Actes 3.18 Actes 4.28 Luc 22.22 Psaumes 76.10 Matthieu 26.24
24 ambaye Mungu alimfufua, akiufungua uchungu wa mauti, kwa sababu haikuwezekana ashikwe nao.
Actes 2.32 1 Pierre 1.21 2 Corinthiens 4.14 1 Corinthiens 6.14 Colossiens 2.12
25 Maana Daudi ataja habari zake, Nalimwona Bwana mbele yangu siku zote, Kwa kuwa yuko upande wa mkono wangu wa kuume, nisitikisike.
Psaumes 16.8-16.11 Esaïe 50.7-50.9 Psaumes 62.6 Esaïe 41.13 Psaumes 109.31
26 Kwa hiyo moyo wangu ukapendezewa, ulimi wangu ukafurahi; Tena mwili wangu nao utakaa katika matumaini.
Psaumes 71.23 Psaumes 16.9 Psaumes 30.11 Psaumes 63.5 Psaumes 22.22-22.24
27 Kwa maana hutaiacha roho yangu katika kuzimu; Wala hutamtoa Mtakatifu wako aone uharibifu.
Actes 2.31 Apocalypse 20.13 Psaumes 86.13 Psaumes 49.15 Luc 1.35
28 Umenijuvisha njia za uzima; Utanijaza furaha kwa uso wako.
Psaumes 21.6 Psaumes 16.11 Jean 11.25-11.26 Jean 14.6 Proverbes 2.19
29 Waume, ndugu zangu, mniwie radhi, niseme kwa ujasiri mbele yenu habari za baba yetu mkuu, Daudi, ya kuwa alifariki akazikwa, na kaburi lake liko kwetu hata leo.
Actes 13.36 Hébreux 7.4 Actes 7.8-7.9 1 Rois 2.10 Néhémie 3.16
30 Basi kwa kuwa ni nabii, akijua ya kuwa Mungu amemwapia kwa kiapo, ya kwamba katika uzao wa viuno vyake atamketisha mmoja katika kiti chake cha enzi;
2 Samuel 7.11-7.16 2 Samuel 23.2 Psaumes 132.11-132.18 2 Pierre 1.21 Psaumes 89.3-89.4
31 yeye mwenyewe akitangulia kuyaona haya, alitaja habari za kufufuka kwake Kristo, ya kwamba roho yake haikuachwa kuzimu, wala mwili wake haukuona uharibifu.
Psaumes 16.10 Actes 2.27 Actes 13.35 1 Pierre 1.11-1.12
32 Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.
Actes 2.24 Actes 1.8 Actes 3.15 Actes 4.33 Actes 1.22
33 Basi yeye, akiisha kupandishwa hata mkono wa kuume wa Mungu, na kupokea kwa Baba ile ahadi ya Roho Mtakatifu, amekimwaga kitu hiki mnachokiona sasa na kukisikia.
Actes 1.4 Actes 2.17 Marc 16.19 Actes 10.45 Actes 5.31
34 Maana Daudi hakupanda mbinguni; bali yeye mwenyewe anasema, Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti upande wa mkono wangu wa kuume.
Psaumes 110.1 Matthieu 22.42-22.45 Hébreux 1.13 Ephésiens 1.22 Luc 20.42-20.43
35 Hata nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.
Esaïe 59.18 Genèse 3.15 Apocalypse 20.8-20.15 Josué 10.24-10.25 Esaïe 49.23
36 Basi nyumba yote ya Israeli na wajue yakini ya kwamba Mungu amemfanya Yesu huyo mliyemsulibisha kuwa Bwana na Kristo.
2 Thessaloniciens 1.7-1.10 2 Corinthiens 5.10 Jérémie 9.26 Matthieu 28.18-28.20 Ezéchiel 34.30
37 Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?
Luc 3.10 Actes 7.54 Actes 5.33 Jean 8.9 Actes 24.25-24.26
38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
Actes 22.16 Actes 10.48 Luc 24.47 Actes 8.12 Actes 3.19
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie.
Joël 2.32 Romains 8.30 Ephésiens 4.4 Actes 15.8 1 Corinthiens 7.14
40 Akawashuhudia kwa maneno mengine mengi sana na kuwaonya, akisema, Jiokoeni na kizazi hiki chenye ukaidi.
Matthieu 17.17 Deutéronome 32.5 1 Timothée 4.16 1 Thessaloniciens 2.11 Philippiens 2.15
41 Nao waliolipokea neno lake wakabatizwa; na siku ile wakaongezeka watu wapata elfu tatu.
Actes 4.4 Actes 2.47 Actes 2.37 Actes 16.31-16.34 Actes 8.6-8.8
42 Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.
Actes 1.14 Actes 20.7 Hébreux 10.25 Actes 2.46 Hébreux 10.39
43 Kila mtu akaingiwa na hofu; ajabu nyingi na ishara zikafanywa na mitume.
Osée 3.5 Actes 3.6-3.9 Luc 7.16 Luc 8.37 Actes 9.40
44 Na wote walioamini walikuwa mahali pamoja, na kuwa na vitu vyote shirika,
Actes 4.32 1 Jean 3.16-3.18 2 Corinthiens 9.6-9.15 2 Corinthiens 8.14-8.15 2 Corinthiens 8.9
45 wakiuza mali zao, na vitu vyao walivyokuwa navyo, na kuwagawia watu wote kama kila mtu alivyokuwa na haja.
Actes 11.29 Actes 4.34-5.2 1 Timothée 6.18-6.19 1 Jean 3.17 Esaïe 58.7-58.12
46 Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,
Actes 5.42 Actes 20.7 Actes 2.42 Luc 24.53 Actes 16.34
47 wakimsifu Mungu, na kuwapendeza watu wote. Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale waliokuwa wakiokolewa.
Actes 2.41 Actes 16.5 Actes 11.24 Luc 2.52 Actes 2.39

Cette Bible est dans le domaine public.