Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 14.4
Bible en Swahili de l’est


L’Évangile à Iconium, Lystre et Derbe

1 Ikawa huko Ikonio wakaingia pamoja katika sinagogi la Wayahudi; na kwa vile walivyonena, kundi kubwa la Wayahudi na la Wayunani wakaamini.
Actes 18.4 Actes 13.46 Actes 13.51 Actes 14.21 Jean 7.35
2 Walakini Wayahudi wasioamini wakawataharakisha watu wa Mataifa na kuwatia nia mbaya juu ya ndugu.
Actes 13.50 Actes 13.45 1 Thessaloniciens 2.15-2.16 Actes 14.19 Actes 21.27-21.30
3 Basi wakakaa huko wakati mwingi, wakinena kwa ushujaa katika Bwana, aliyelishuhudia neno la neema yake, akiwajalia ishara na maajabu yatendeke kwa mikono yao.
Hébreux 2.4 Actes 20.32 Actes 4.29-4.30 Ephésiens 6.18-6.20 Marc 16.20
4 Lakini jamii ya watu wa mjini wakafarakana; hawa walikuwa upande wa Wayahudi, na hawa upande wa Mitume.
Actes 28.24 Actes 14.14 Luc 12.51-12.53 Matthieu 10.34-10.36 Luc 2.34
5 Hata palipotokea shambulio la watu wa Mataifa na Wayahudi pamoja na wakubwa wao juu yao, kuwatenda jeuri na kuwapiga kwa mawe,
Actes 14.19 Psaumes 83.5 Matthieu 5.44 Luc 6.28 Psaumes 2.1-2.3
6 wao wakapata habari wakakimbilia Listra na Derbe, miji ya Likaonia, na nchi zilizo kando kando;
2 Timothée 3.11 Matthieu 10.23 Actes 14.20-14.21 Actes 23.12-23.22 Actes 9.24
7 wakakaa huko, wakiihubiri Injili.
Actes 14.21 Actes 16.10 Actes 14.15 Actes 8.4 Actes 17.2
8 Na huko Listra palikuwa na mtu mmoja, dhaifu wa miguu, kiwete tangu tumboni mwa mamaye, ambaye hajaenda kabisa.
Actes 3.2 Jean 5.7 Jean 5.3-5.5 Jean 9.1-9.2 Actes 4.9
9 Mtu huyo alimsikia Paulo alipokuwa akinena; ambaye akamkazia macho na kuona ya kuwa ana imani ya kuponywa,
Matthieu 9.28-9.29 Actes 3.4 Marc 2.11-2.12 Matthieu 15.28 Marc 1.40-1.41
10 akasema kwa sauti kuu, Simama kwa miguu yako sawasawa. Akasimama upesi akaenda.
Esaïe 35.6 Luc 13.11-13.13 Actes 9.33-9.34 Jean 5.8-5.9 Jean 14.12
11 Na makutano walipoona aliyoyafanya Paulo wakapaza sauti zao, wakisema kwa Kilikaonia, Miungu wametushukia kwa mifano ya wanadamu.
Actes 28.6 Actes 8.10 Actes 12.22
12 Wakamwita Barnaba, Zeu, na Paulo, Herme, kwa sababu ndiye aliyekuwa mnenaji.
Actes 19.35
13 Kuhani wa Zeu ambaye hekalu lake lilikuwa mbele ya mji, akaleta ng’ombe na taji za maua hata malangoni, akitaka kutoa dhabihu pamoja na makutano.
Daniel 2.46 Actes 10.25
14 Walakini mitume Barnaba na Paulo, walipopata habari, wakararua nguo zao, wakaenda mbio wakaingia katika makutano, wakipiga kelele,
Matthieu 26.65 Actes 14.4 Jérémie 36.24 Esdras 9.3-9.5 2 Rois 18.37-19.2
15 wakisema, Akina bwana, mbona mnafanya haya? Sisi nasi tu wanadamu hali moja na ninyi; twawahubiri habari njema, ili mgeuke na kuyaacha mambo haya ya ubatili na kumwelekea Mungu aliye hai, aliyeumba mbingu na nchi na bahari na vitu vyote vilivyomo;
1 Samuel 12.21 Apocalypse 14.7 Jérémie 14.22 Actes 10.26 1 Corinthiens 8.4
16 ambaye zamani zilizopita aliwaacha mataifa yote waende katika njia zao wenyewe.
Actes 17.30 Psaumes 81.12 1 Pierre 4.3 Psaumes 147.20 Michée 4.5
17 Lakini hakujiacha pasipo ushuhuda, kwa kuwa alitenda mema, akiwapeni mvua kutoka mbinguni, na nyakati za mavuno, akiwashibisha mioyo yenu chakula na furaha.
Job 5.10 Deutéronome 11.14 Romains 1.19-1.20 Lévitique 26.4 Deutéronome 28.12
18 Na kwa maneno hayo wakawazuia makutano kwa shida, wasiwatolee dhabihu.
Jean 6.15 Genèse 11.6 Jérémie 44.16-44.17 Exode 32.21-32.23 Genèse 19.9
19 Lakini Wayahudi wakafika toka Antiokia na Ikonio, wakawashawishi makutano hata wakampiga kwa mawe Paulo, wakamburuta nje ya mji, wakidhania ya kuwa amekwisha kufa.
2 Timothée 3.11 2 Corinthiens 11.25 Actes 13.45 Actes 13.50-13.51 Actes 14.5
20 Lakini wanafunzi walipokuwa wakimzunguka pande zote, akasimama, akaingia ndani ya mji; na siku ya pili yake akatoka, akaenda zake pamoja na Barnaba mpaka Derbe.
Actes 14.6 Actes 16.1 Apocalypse 11.7-11.12 Actes 12.17 2 Corinthiens 1.9-1.10
21 Hata walipokwisha kuihubiri Injili katika mji ule, na kupata wanafunzi wengi, wakarejea mpaka Listra na Ikonio na Antiokia,
Actes 13.51 Actes 14.19 Actes 14.1 Matthieu 28.19 Actes 13.14
22 wakifanya imara roho za wanafunzi na kuwaonya wakae katika ile Imani, na ya kwamba imetupasa kuingia katika ufalme wa Mungu kwa njia ya dhiki nyingi.
2 Timothée 3.12 Jean 16.33 1 Pierre 5.10 Colossiens 1.23 1 Thessaloniciens 3.2-3.4
23 Na walipokwisha kuwachagulia wazee katika kila kanisa, na kuomba pamoja na kufunga, wakawaweka katika mikono ya Bwana waliyemwamini.
Tite 1.5 Actes 11.30 Actes 20.17 Jacques 5.14 Actes 20.32
24 Wakapita kati ya Pisidia wakaingia Pamfilia.
Actes 13.13-13.14 Actes 15.38
25 Na baada ya kuhubiri lile neno katika Perge wakatelemka mpaka Atalia.
26 Na kutoka huko wakaabiri kwenda Antiokia. Huko ndiko walikoombewa neema ya Mungu kwa ile kazi waliyokwisha kuitimiza.
Actes 15.40 Actes 11.19 Galates 2.11 Actes 13.1-13.3 Colossiens 4.17
27 Hata walipofika wakalikutanisha kanisa, wakawaeleza mambo yote aliyoyafanya Mungu pamoja nao, na ya kwamba amewafungulia Mataifa mlango wa imani.
1 Corinthiens 16.9 Actes 15.12 2 Corinthiens 2.12 Colossiens 4.3 1 Corinthiens 5.4
28 Wakaketi huko wakati usiokuwa mchache, pamoja na wanafunzi.
Actes 11.26 Actes 15.35

Cette Bible est dans le domaine public.