Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 9.12
Bible en Swahili de l’est


1 Akawaambia, Amin, nawaambia, Pana watu katika hawa wasimamao hapa, ambao hawataonja mauti kabisa, hata watakapouona ufalme wa Mungu umekuja kwa nguvu.
Matthieu 25.31 Matthieu 24.30 Matthieu 16.28 Hébreux 2.9 Luc 9.27

La transfiguration

2 Hata baada ya siku sita Yesu akawatwaa Petro, na Yakobo, na Yohana, akawaleta juu ya mlima mrefu faraghani, peke yao; akageuka sura yake mbele yao;
Luc 9.28-9.36 Matthieu 17.1-17.8 Marc 5.37 Marc 14.33 Exode 24.13
3 mavazi yake yakimeta-meta, meupe mno, jinsi asivyoweza dobi duniani kuyafanya meupe.
Matthieu 28.3 Daniel 7.9 Malachie 3.2-3.3 Esaïe 1.18 Actes 10.30
4 Wakatokewa na Eliya pamoja na Musa, nao walikuwa wakizungumza na Yesu.
Luc 9.30-9.31 Actes 3.21-3.24 Jean 5.39 Jean 5.45-5.47 Matthieu 11.13
5 Petro akajibu, akamwambia Yesu, Rabi, ni vizuri sisi kuwapo hapa; na tufanye vibanda vitatu, kimoja chako wewe, kimoja cha Musa, na kimoja cha Eliya.
Exode 33.17-33.23 Philippiens 1.23 1 Jean 3.2 Apocalypse 22.3-22.4 Jean 14.21-14.23
6 Maana, hakujua la kunena, kwa kuwa waliingiwa na hofu nyingi.
Daniel 10.15-10.19 Apocalypse 1.17 Marc 16.5-16.8
7 Kisha likatokea wingu, likawatia uvuli; sauti ikatoka katika lile wingu, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, msikieni yeye.
Matthieu 3.17 2 Pierre 1.17 Marc 1.11 Matthieu 17.5-17.7 Psaumes 97.2
8 Mara hiyo walipotazama huku na huku, hawakuona mtu pamoja nao ila Yesu peke yake.
Luc 9.36 Actes 10.16 Luc 24.31 Actes 8.39-8.40
9 Na walipokuwa wakishuka mlimani aliwakataza wasimweleze mtu waliyoyaona, hata Mwana wa Adamu atakapokuwa amefufuka katika wafu.
Matthieu 17.9-17.13 Marc 5.43 Marc 10.32-10.34 Marc 8.29-8.31 Matthieu 16.21
10 Wakalishika neno lile, wakiulizana wao kwa wao, Huko kufufuka katika wafu maana yake nini?
Luc 24.25-24.27 Jean 2.19-2.22 Marc 9.32 Matthieu 16.22 Luc 24.7-24.8
11 Wakamwuliza, wakisema, Mbona waandishi hunena ya kwamba imempasa Eliya kuja kwanza?
Malachie 4.5 Malachie 3.1 Matthieu 11.14 Marc 9.4 Matthieu 17.10-17.11
12 Akajibu akawaambia, Ni kweli Eliya yuaja kwanza, na kurejeza upya yote; lakini, pamoja na haya, ameandikiwaje Mwana wa Adamu ya kwamba atateswa mengi na kudharauliwa?
Luc 23.11 Esaïe 53.1-53.12 Zacharie 13.7 Matthieu 3.1-3.12 Luc 1.16-1.17
13 Lakini nawaambia, Eliya amekwisha kuja, nao wakamtenda yote waliyoyataka kama alivyoandikiwa.
Matthieu 11.14 Actes 7.52 Matthieu 14.3-14.11 Luc 3.19-3.20 Marc 6.14-6.28

Guérison d’un démoniaque

14 Hata walipowafikia wanafunzi, waliona mkutano mkuu wakiwazunguka, na waandishi wakijadiliana nao;
Matthieu 17.14-17.20 Luc 9.37-9.42 Luc 11.53-11.54 Marc 12.14 Hébreux 12.3
15 mara mkutano wote walipomwona walishangaa, wakamwendea mbio, wakamsalimu.
Exode 34.30 Marc 9.2-9.3
16 Akawauliza, Mnajadiliana nini nao?
Marc 8.11 Luc 5.30-5.32
17 Mtu mmoja katika mkutano akamjibu, Mwalimu, nimemleta mwanangu kwako, ana pepo bubu;
Luc 11.14 Marc 9.25 Marc 7.26 Marc 10.13 Matthieu 12.22
18 na kila ampagaapo, humbwaga chini, naye hutoka povu na kusaga meno na kukonda; nikasema na wanafunzi wako wamtoe pepo, wasiweze.
Actes 7.54 Marc 9.20 Marc 11.23 Marc 9.28-9.29 Matthieu 17.19-17.20
19 Akawajibu, akasema, Enyi kizazi kisichoamini, nikae nanyi hata lini? Nichukuliane nanyi hata lini? Mleteni kwangu.
Jean 20.27 Nombres 14.22 Nombres 14.11 Psaumes 106.21-106.25 Nombres 32.13-32.14
20 Wakamleta kwake; hata alipomwona, mara yule pepo alimtia kifafa; naye akaanguka chini, akagaa-gaa, akitokwa na povu.
Marc 1.26 Job 2.6-2.8 Job 1.10-1.12 Marc 5.3-5.5 Marc 9.26
21 Akamwuliza babaye, Amepatwa na haya tangu lini? Akasema, Tangu utoto.
Actes 9.33 Jean 5.5-5.6 Jean 9.20-9.21 Job 14.1 Luc 8.43
22 Na mara nyingi amemtupa katika moto, na katika maji, amwangamize; lakini ukiweza neno lo lote, utuhurumie, na kutusaidia.
Matthieu 9.28 Matthieu 14.31 Matthieu 15.22-15.28 Matthieu 20.34 Luc 7.13
23 Yesu akamwambia, Ukiweza! Yote yawezekana kwake aaminiye.
Jean 11.40 Matthieu 17.20 Marc 11.23 Hébreux 11.6 Luc 17.6
24 Mara babaye yule kijana akapaza sauti, akasema, Naamini, nisaidie kutokuamini kwangu.
Luc 17.5 Hébreux 12.2 2 Thessaloniciens 1.3 Ephésiens 2.8 Philippiens 1.29
25 Naye Yesu akiona ya kuwa mkutano unakusanyika mbio, akamkemea yule pepo mchafu, akamwambia, Ewe pepo bubu na kiziwi, mimi nakuamuru, mtoke huyu, wala usimwingie tena.
Actes 16.18 Marc 9.15 Luc 4.35 Luc 9.42 Marc 1.25-1.27
26 Akalia, akamtia kifafa sana, akamtoka; naye akawa kama amekufa; hata wengi wakasema, Amekufa.
Marc 9.20 Marc 1.26 Exode 5.23 Marc 9.18 Apocalypse 12.12
27 Lakini Yesu akamshika mkono akamwinua naye akasimama.
Marc 1.31 Actes 3.7 Actes 9.41 Marc 8.23 Marc 1.41
28 Hata alipoingia nyumbani, wanafunzi wake wakamwuliza kwa faragha, Mbona sisi hatukuweza kumtoa?
Marc 7.17 Matthieu 17.19-17.20 Matthieu 13.10 Marc 4.10 Marc 4.34
29 Akawaambia, Namna hii haiwezi kutoka kwa neno lo lote, isipokuwa kwa kuomba.
Jacques 5.15 Matthieu 17.20 2 Corinthiens 12.8 2 Corinthiens 11.27 Daniel 9.3
30 Wakatoka huko, wakapita katikati ya Galilaya; naye hakutaka mtu kujua.
Matthieu 27.22-27.23 Marc 6.31-6.32 Matthieu 17.22-17.23 Luc 9.43-9.45
31 Kwa sababu alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake, akawaambia, Mwana wa Adamu yuaenda kutiwa katika mikono ya watu, nao watamwua; hata akiisha kuuawa, baada ya siku tatu atafufuka.
Matthieu 16.21 Marc 8.31 Marc 9.12 Matthieu 20.18-20.19 Actes 2.23-2.24
32 Lakini hawakulifahamu neno lile, wakaogopa kumwuliza.
Luc 2.50 Luc 18.34 Luc 9.45 Jean 12.16 Jean 16.19

Petits et grands dans le royaume de Dieu

33 Wakafika Kapernaumu; hata alipokuwamo nyumbani, akawauliza, Mlishindania nini njiani?
Matthieu 18.1-18.5 Matthieu 17.24 Luc 9.46-9.48 Jean 21.17 Marc 2.8
34 Wakanyamaza; kwa maana njiani walikuwa wakibishana wao kwa wao, ni nani aliye mkubwa.
Luc 22.24-22.30 Matthieu 18.1-18.5 Romains 12.10 Marc 9.50 Philippiens 2.3-2.7
35 Akaketi chini, akawaita wale Thenashara akawaambia, Mtu atakaye kuwa wa kwanza atakuwa wa mwisho kuliko wote, na mtumishi wa wote.
Marc 10.42-10.45 Luc 22.26 Matthieu 23.11 Luc 18.14 Luc 14.10-14.11
36 Akatwaa kitoto, akamweka katikati yao, akamkumbatia, akawaambia,
Marc 10.16 Matthieu 18.2 Matthieu 19.14-19.15
37 Mtu akimpokea mtoto mmoja wa namna hii kwa jina langu, anipokea mimi; na mtu akinipokea mimi, humpokea, si mimi, bali yeye aliyenituma.
Matthieu 18.3-18.5 Luc 10.16 Luc 9.48 Jean 10.30 Matthieu 10.40-10.42
38 Yohana akamjibu, akamwambia, Mwalimu, tulimwona mtu akitoa pepo kwa jina lako, ambaye hafuatani nasi; tukamkataza, kwa sababu hafuatani nasi.
Luc 9.49-9.50 Luc 11.19 Nombres 11.26-11.29
39 Yesu akasema, Msimkataze, kwa kuwa hakuna mtu atakayefanya mwujiza kwa jina langu akaweza mara kuninenea mabaya;
1 Corinthiens 12.3 Actes 19.13-19.16 1 Corinthiens 13.1-13.2 Marc 10.13-10.14 Matthieu 7.22-7.23
40 kwa sababu asiye kinyume chetu, yu upande wetu.
Luc 11.23 Matthieu 12.30
41 Kwa kuwa ye yote atakayewanywesha ninyi kikombe cha maji, kwa kuwa ninyi ni watu wa Kristo, amin, nawaambia, hatakosa thawabu yake.
Matthieu 10.42 Galates 3.29 2 Corinthiens 10.7 1 Corinthiens 3.23 Romains 8.9
42 Na ye yote atakayemkosesha mmojawapo wa wadogo hawa waniaminio, afadhali afungiwe jiwe la kusagia shingoni mwake, na kutupwa baharini.
Matthieu 18.6 Luc 17.1-17.2 Matthieu 18.10 1 Corinthiens 8.10-8.13 2 Thessaloniciens 1.6-1.9
43 Na mkono wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima u kigutu, kuliko kuwa na mikono miwili, na kwenda zako jehanum, kwenye moto usiozimika;
Matthieu 5.29-5.30 Matthieu 25.41 Matthieu 3.12 Matthieu 18.8-18.9 Matthieu 5.22
44 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.
45 Na mguu wako ukikukosesha, ukate; ni afadhali kuingia katika uzima, u kiwete, kuliko kuwa na miguu miwili, na kutupwa katika jehanum;
Marc 9.43 Matthieu 18.8 Matthieu 5.22
46 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.
47 Na jicho lako likikukosesha, ling’oe, ulitupe; ni afadhali kuingia katika ufalme wa Mungu, una chongo, kuliko kuwa na macho mawili, na kutupwa katika jehanum;
Matthieu 18.9 Matthieu 5.22 Marc 9.43 Luc 14.26 Galates 4.15
48 ambamo humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki.
Esaïe 66.24 Marc 9.43-9.45 Matthieu 25.41
49 Kwa sababu kila mtu atatiwa chumvi kwa moto.
Lévitique 2.13 Ezéchiel 43.24
50 Chumvi ni njema; lakini chumvi ikiwa si chumvi tena, mtaitia nini ikolee? Mwe na chumvi ndani yenu, mkakae kwa amani ninyi kwa ninyi.
Romains 12.18 Colossiens 4.6 2 Corinthiens 13.11 Matthieu 5.13 Hébreux 12.14

Cette Bible est dans le domaine public.