Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 15.11
Bible en Swahili de l’est


Jésus devant le gouverneur romain

1 Mara kulipokuwa asubuhi wakuu wa makuhani walifanya shauri pamoja na wazee na waandishi na baraza nzima, wakamfunga Yesu, wakamchukua, wakamleta mbele ya Pilato.
Matthieu 27.1-27.2 Luc 22.66 Actes 3.13 Luc 23.1-23.5 Jean 18.28-18.38
2 Pilato akamwuliza, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Akajibu, akamwambia, Wewe wasema.
Matthieu 2.2 1 Timothée 6.13 Matthieu 27.11-27.14 Luc 23.2-23.3 Marc 15.12
3 Nao wakuu wa makuhani walikuwa wakimshitaki mambo mengi.
Esaïe 53.7 Jean 19.6-19.7 Marc 14.60-14.61 Marc 15.5 Jean 19.12
4 Pilato akamwuliza tena akisema, Hujibu neno? Tazama ni mambo mangapi wanayokushitaki!
Jean 19.10 Matthieu 26.62 Matthieu 27.13
5 Wala Yesu hakujibu neno tena, hata Pilato akastaajabu.
Matthieu 27.14 Esaïe 8.18 Zacharie 3.8 1 Corinthiens 4.9 Jean 19.9
6 Basi wakati wa sikukuu huwafungulia mfungwa mmoja, wamwombaye.
Jean 18.39-18.40 Actes 24.27 Jean 19.16 Matthieu 27.15-27.26 Actes 25.9
7 Palikuwa na mtu aitwaye Baraba, amefungwa pamoja na watu waliofanya fitina, na kufanya uuaji katika fitina ile.
Luc 23.18-23.19 Luc 23.25 Matthieu 27.16
8 Makutano wakaja, wakaanza kuomba awafanyie kama vile alivyozoea.
9 Pilato akawajibu, akisema, Je! Mnataka niwafungulie mfalme wa Wayahudi?
Jean 18.39 Jean 19.4-19.5 Actes 3.13-3.15 Matthieu 27.17-27.21 Jean 19.14-19.16
10 Kwa maana alitambua ya kuwa wakuu wa makuhani wamemtoa kwa husuda.
1 Samuel 18.8-18.9 Proverbes 27.4 Actes 13.45 1 Jean 3.12 Genèse 37.11
11 Lakini wakuu wa makuhani wakawataharakisha makutano, kwamba afadhali awafungulie Baraba.
Actes 3.14 Osée 5.1 Matthieu 27.20 Jean 18.40
12 Pilato akajibu tena akawaambia, Basi nimtendeje huyu mnayemnena kuwa ni mfalme wa Wayahudi?
Luc 23.2 Actes 5.31 Luc 23.20-23.24 Proverbes 2.6-2.7 Zacharie 9.9
13 Wakapiga kelele tena, Msulibishe.
14 Pilato akawaambia, Kwani, ni ubaya gani alioutenda? Wakazidi sana kupiga kelele, Msulibishe.
Luc 23.41 Actes 22.22-22.23 Matthieu 27.19 Matthieu 27.4 Jean 19.12-19.15
15 Pilato akipenda kuwaridhisha makutano, akawafungulia Baraba; akamtoa Yesu, baada ya kumpiga mijeledi, ili asulibiwe.
Matthieu 27.26 Jean 19.1 Esaïe 50.6 Marc 10.34 Matthieu 20.19
16 Nao askari wakamchukua ndani ya behewa, ndiyo Praitorio (yaani, nyumba ya uliwali), wakakusanya pamoja kikosi kizima.
Jean 19.9 Jean 18.28 Matthieu 26.3 Matthieu 27.27-27.31 Actes 10.1
17 Wakamvika vazi la rangi ya zambarau, wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani;
Luc 23.11 Jean 19.2-19.5 Matthieu 27.28-27.30
18 wakaanza kumsalimu, Salamu, Mfalme wa Wayahudi!
Matthieu 27.42-27.43 Marc 15.2 Marc 15.29-15.32 Luc 23.36-23.37 Genèse 37.20
19 Wakampiga mwanzi wa kichwa, wakamtemea mate, wakapiga magoti, wakamsujudia.
Marc 14.65 Genèse 24.52 Michée 5.1 Luc 23.36 Esaïe 49.7
20 Hata wakiisha kumdhihaki, wakamvua lile vazi la rangi ya zambarau, wakamvika mavazi yake mwenyewe; wakamchukua nje ili wamsulibishe.
Jean 19.16 Matthieu 27.31

Crucifixion et mort de Jésus

21 Wakamshurutisha mtu aliyekuwa akipita, akitoka mashamba, Simoni Mkirene, baba yao Iskanda na Rufo, ili auchukue msalaba wake.
Matthieu 27.32 Luc 23.26 Romains 16.13 Luc 14.27 Actes 13.1
22 Wakamleta mpaka mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa.
Matthieu 27.33-27.44 Luc 23.27-23.38 Jean 19.17-19.27
23 Wakampa mvinyo iliyotiwa manemane, asiipokee.
Matthieu 27.34 Jean 19.28-19.30 Marc 14.25 Matthieu 26.19 Luc 23.36
24 Wakamsulibisha, wakagawa mavazi yake, wakayapigia kura kila mtu atwae nini.
Galates 3.13 Psaumes 22.16-22.18 1 Pierre 2.24 Matthieu 27.35-27.36 Actes 5.30
25 Basi ilikuwa saa tatu, nao wakamsulibisha.
Jean 19.14 Marc 15.33 Actes 2.15 Luc 23.44 Matthieu 27.45
26 Palikuwa na anwani ya mashitaka yake iliyoandikwa juu, MFALME WA WAYAHUDI.
Matthieu 27.37 Jean 19.18-19.22 Marc 15.2 Luc 23.37-23.38 Psaumes 76.10
27 Na pamoja naye walisulibisha wanyang’anyi wawili, mmoja mkono wake wa kuume na mmoja mkono wake wa kushoto. [
Matthieu 27.38 Luc 23.32-23.33 Jean 19.18
28 Basi andiko likatimizwa linenalo, Alihesabiwa pamoja na waasi.]
29 Nao waliokuwa wakipita njiani wakamtukana, wakitikisa-tikisa vichwa, wakisema, Ahaa! Wewe mwenye kulivunja hekalu na kulijenga katika siku tatu,
Marc 14.58 Psaumes 109.25 Lamentations 1.12 Lamentations 2.15 Psaumes 35.15-35.21
30 jiponye nafsi yako, ushuke msalabani.
31 Kadhalika na wakuu wa makuhani wakamdhihaki wao kwa wao, pamoja na waandishi, wakisema, Aliponya wengine; hawezi kujiponya mwenyewe.
Luc 23.35-23.37 Jean 11.47-11.52 1 Pierre 3.17-3.18 Matthieu 27.41-27.43 Jean 12.23-12.24
32 Kristo, mfalme wa Israeli, na ashuke sasa msalabani tupate kuona na kuamini. Hata wale waliosulibiwa pamoja naye wakamfyolea.
Luc 23.39-23.43 Matthieu 27.44 Jean 12.13 Jean 20.25-20.29 2 Timothée 2.18
33 Na ilipokuwa saa sita, palikuwa na giza juu ya nchi yote, hata saa tisa.
Matthieu 27.45 Marc 15.25 Luc 23.44-23.45 Amos 8.9-8.10 Psaumes 105.28
34 Na saa tisa Yesu akapaza sauti yake kwa nguvu, Eloi, Eloi, lama sabakthani? Maana yake, Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?
Psaumes 22.1 Luc 23.46 Hébreux 5.7 Psaumes 27.9 Psaumes 42.9
35 Na baadhi yao waliosimama pale, walisema, Tazama, anamwita Eliya.
Matthieu 27.47-27.49 Matthieu 17.11-17.13 Marc 9.11-9.13
36 Na mmoja akaenda mbio, akajaza sifongo siki, akaitia juu ya mwanzi, akamnywesha, akisema, Acheni, na tuone kwamba Eliya anakuja kumtelemsha.
Psaumes 69.21 Marc 15.23 Luc 23.36 Jean 19.28-19.30
37 Naye Yesu akatoa sauti kuu, akakata roho.
Jean 19.30 Luc 23.46 Matthieu 27.50
38 Pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu hata chini.
Luc 23.45 2 Chroniques 3.8-3.14 Exode 26.31-26.34 Hébreux 6.19 Hébreux 9.3-9.12
39 Basi yule akida, aliyesimama hapo akimwelekea, alipoona ya kuwa alikata roho jinsi hii, akasema, Hakika mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu.
Matthieu 27.54 Luc 23.47-23.48 Matthieu 27.43 Actes 10.1 Actes 27.43
40 Palikuwako na wanawake wakitazama kwa mbali; miongoni mwao alikuwamo Mariamu Magdalene, na Mariamu mama yao Yakobo mdogo na Yose, na Salome;
Matthieu 27.55-27.56 Psaumes 38.11 Luc 23.49 Galates 1.19 Marc 16.9
41 hao ndio waliofuatana naye huko Galilaya, na kumtumikia; na wengine wengi waliopanda pamoja naye mpaka Yerusalemu.
Matthieu 27.55-27.56 Luc 8.2-8.3

Mise au tombeau du corps de Jésus

42 Hata ikiisha kuwa jioni, kwa sababu ni Maandalio, ndiyo siku iliyo kabla ya sabato,
Jean 19.31 Jean 19.38-19.42 Luc 23.50-23.56 Matthieu 27.57-27.62
43 akaenda Yusufu, mtu wa Arimathaya, mstahiki, mtu wa baraza ya mashauri, naye mwenyewe anautazamia ufalme wa Mungu; akafanya ujasiri, akaingia mbele ya Pilato akauomba mwili wake Yesu.
Luc 2.25 Luc 2.38 Luc 23.51 Actes 4.8-4.13 Matthieu 27.57
44 Lakini Pilato akastaajabu, kwamba amekwisha kufa. Akamwita yule akida, akamwuliza kwamba amekufa kitambo.
Jean 19.31-19.37
45 Hata alipokwisha kupata hakika kwa yule akida, alimpa Yusufu yule maiti.
Matthieu 27.58 Jean 19.38 Marc 15.39
46 Naye akanunua sanda ya kitani, akamtelemsha, akamfungia ile sanda, akamweka katika kaburi lililochongwa mwambani; akavingirisha jiwe mbele ya mlango wa kaburi.
Esaïe 53.9 Marc 16.3-16.4 Jean 11.38 Esaïe 22.16 Matthieu 28.2
47 Nao Mariamu Magdalene na Mariamu mamaye Yose wakapatazama mahali alipowekwa.
Marc 15.40 Marc 16.1 Matthieu 28.1 Luc 23.55-24.2 Matthieu 27.61

Cette Bible est dans le domaine public.