Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Daniel 3.6
Bible en Swahili de l’est


Dans la fournaise

1 Nebukadreza, mfalme, alifanya sanamu ya dhahabu, ambayo urefu wake ulikuwa ni dhiraa sitini, na upana wake dhiraa sita; akaisimamisha katika uwanda wa Dura, katika wilaya ya Babeli.
Habakuk 2.19 Esaïe 46.6 Jérémie 16.20 Osée 8.4 Actes 17.29
2 Ndipo Nebukadreza akatuma watu kuwakusanya maamiri, na manaibu, na maliwali, na makadhi, na watunza hazina, na mawaziri, na mawakili, na wakuu wa wilaya zote, ili wahudhurie wakati wa kuizindua ile sanamu, mfalme Nebukadneza aliyoisimamisha.
Daniel 3.27 Daniel 6.1-6.4 Daniel 6.6-6.7 1 Rois 12.32 Exode 32.4-32.6
3 Ndipo maamiri, na manaibu, na maliwali, na makadhi, na watunza hazina, na mawaziri, na mawakili, na wakuu wa wilaya zote, wakakusanyika ili kuizindua ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha; wakasimama mbele ya ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha.
Apocalypse 17.17 Psaumes 82.1-82.8 Apocalypse 17.13 Romains 3.11 Actes 19.34-19.35
4 Ndipo mpiga mbiu akapiga kelele akisema, Enyi watu wa kabila zote, na taifa, na lugha, mmeamriwa hivi,
Daniel 4.1 Daniel 6.25 Daniel 4.14 Michée 6.16 Esther 8.9
5 wakati mtakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, lazima kuanguka na kuiabudu sanamu ya dhahabu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha.
Daniel 3.15 Daniel 3.10 Daniel 3.7
6 Na kila mtu asiyeanguka na kuabudu atatupwa saa iyo hiyo katika tanuru ya moto uwakao.
Jérémie 29.22 Matthieu 13.50 Daniel 3.11 Daniel 3.15 Matthieu 13.42
7 Basi wakati huo, watu wa kabila zote walipoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, watu wote na mataifa na lugha wakaanguka, wakaiabudu ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha.
Apocalypse 19.20 Jérémie 51.7 Apocalypse 13.8 1 Jean 5.19 Apocalypse 13.3
8 Basi baadhi ya Wakaldayo wakakaribia, wakaleta mashitaka juu ya Wayahudi.
Esther 3.8-3.9 Esdras 4.12-4.16 Daniel 6.12-6.13 Esther 3.6 Actes 16.20-16.22
9 Wakajibu, wakamwambia mfalme Nebukadreza, Ee mfalme, uishi milele.
Daniel 5.10 Daniel 6.6 Daniel 6.21 Daniel 2.4 Romains 13.7
10 Wewe, Ee mfalme, ulitoa amri ya kwamba kila mtu atakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, ni lazima aanguke na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu;
Daniel 3.4-3.7 Daniel 6.12 Esther 3.12-3.14 Esaïe 10.1 Exode 1.22
11 na kila mtu asiyeanguka na kuabudu atatupwa katika tanuru ya moto uwakao.
12 Wako Wayahudi kadha wa kadha uliowaweka juu ya mambo ya wilaya ya Babeli, yaani, Shadraka, na Meshaki, na Abednego; watu hawa, Ee mfalme, hawakukujali wewe; hawaitumikii miungu yako, wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.
Daniel 2.49 Daniel 6.13 Actes 5.28 Actes 17.7 Esther 3.8
13 Basi Nebukadreza akatoa amri kwa hasira na ghadhabu, waletwe hao Shadraka, na Meshaki, na Abednego. Basi wakawaleta watu hao mbele ya mfalme.
Daniel 3.19 Daniel 2.12 Matthieu 10.18 1 Samuel 20.30-20.33 Luc 6.11
14 Nebukadreza akajibu, akawaambia, Enyi Shadraka, na Meshaki, na Abednego, je! Ni kwa makusudi hata hammtumikii mungu wangu wala kuisujudia sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha?
Daniel 3.1 Esaïe 46.1 Jérémie 50.2 Daniel 4.8 Exode 21.13-21.14
15 Basi sasa, kama mkiwa tayari wakati mtakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, kuanguka na kuisujudia sanamu niliyoisimamisha, ni vema; bali msipoisujudia, mtatupwa saa iyo hiyo katika tanuru iwakayo moto; naye ni nani Mungu yule atakayewaokoa ninyi na mikono yangu?
Exode 5.2 2 Rois 18.35 Marc 13.11 Luc 21.14-21.15 Actes 5.29
16 Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakajibu, wakamwambia mfalme, Ee Nebukadreza, hamna haja kukujibu katika neno hili.
Daniel 1.7 Daniel 3.12
17 Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme.
Psaumes 27.1-27.2 Hébreux 7.25 Romains 8.31 Actes 20.24 Luc 1.37
18 Bali kama si hivyo, ujue, Ee mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako, wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.
Matthieu 10.39 Josué 24.15 Luc 12.3-12.9 Lévitique 19.4 Proverbes 28.1
19 Ndipo Nebukadreza akajaa ghadhabu, na sura ya uso wake ikabadilika juu ya Shadraka, na Meshaki, na Abednego, basi akatoa amri watie moto ile tanuru mara saba kuliko desturi yake ya kutiwa moto.
Daniel 3.13 Lévitique 26.21 Lévitique 26.24 Lévitique 26.18 Lévitique 26.28
20 Kisha akawaamuru baadhi ya watu mashujaa wa jeshi lake kuwafunga Shadraka, na Meshaki, na Abednego, na kuwatupa katika ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.
Actes 12.4-12.5 Actes 16.23 Actes 16.25 Daniel 3.15
21 Basi watu hao wakafungwa, hali wamevaa suruali zao, na kanzu zao, na joho zao, na mavazi yao mengine, wakatupwa katikati ya ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.
22 Basi kwa sababu amri ya mfalme ilikuwa ni kali, na ile tanuru ilikuwa ina moto sana, mwako wa ule moto ukawaua wale watu waliowashika Shadraka, na Meshaki, na Abednego.
Proverbes 21.18 Proverbes 11.8 Exode 12.33 Actes 12.19 Zacharie 12.2-12.3
23 Na watu hao watatu, Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakaanguka, hali wamefungwa, katikati ya ile tanuru iliyokuwa inawaka moto.
Daniel 6.16-6.17 Psaumes 124.1-124.5 Jérémie 38.6 Psaumes 34.19 Psaumes 66.11-66.12
24 Ndipo Nebukadreza akastaajabu, akainuka kwa haraka; akanena, akawaambia mawaziri wake, Je! Hatukutupa watu watatu, hali wamefungwa, katikati ya moto? Wakajibu, wakamwambia mfalme, Kweli, Ee mfalme.
Daniel 6.7 Daniel 5.6 Daniel 3.17 Daniel 3.9-3.10 Actes 26.27
25 Akajibu, akasema, Tazama, mimi naona watu wanne, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu.
Esaïe 43.2 Actes 28.5 Psaumes 91.3-91.9 Psaumes 34.7 Daniel 3.28
26 Kisha Nebukadreza akaukaribia mdomo wa ile tanuru iliyokuwa inawaka moto. Akanena, akasema, Enyi Shadraka, na Meshaki, na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye juu, tokeni, mje huku. Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakatoka katika ule moto.
Daniel 3.17 Daniel 4.2 Actes 16.17 Daniel 2.47 Apocalypse 19.5
27 Na maamiri, na manaibu, na maliwali, na mawaziri, waliokuwa wamekusanyika pamoja, wakawaona watu hao, ya kuwa ule moto ulikuwa hauna nguvu juu ya miili yao, wala nywele za vichwa vyao hazikuteketea, wala suruali zao hazikubadilika, wala harufu ya moto haikuwapata hata kidogo.
Esaïe 43.2 Hébreux 11.34 Daniel 3.2-3.3 2 Rois 19.19 Esaïe 26.11
28 Nebukadreza akanena, akasema, Na ahimidiwe Mungu wa Shadraka, na Meshaki, na Abednego; aliyemtuma malaika wake, akawaokoa watumishi wake waliomtumaini, wakaligeuza neno la mfalme, na kujitoa miili yao ili wasimtumikie mungu mwingine, wala kumwabudu, ila Mungu wao wenyewe.
Psaumes 34.7-34.8 Esaïe 26.3-26.4 Actes 5.19 Daniel 4.34 Psaumes 22.4-22.5
29 Basi mimi naweka amri ya kuwa kila kabila ya watu, na kila taifa, na kila lugha, watakaonena neno lo lote lisilopasa juu ya huyo Mungu wa Shadraka, na Meshaki, na Abednego, watakatwa vipande vipande, na nyumba zao zitafanywa jaa; kwa kuwa hakuna Mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.
Daniel 6.26-6.27 Daniel 2.5 Daniel 3.15 Deutéronome 32.31 Psaumes 76.10
30 Kisha mfalme akawakuza Shadraka, na Meshaki, na Abednego, katika wilaya ya Babeli.
Daniel 2.49 1 Samuel 2.30 Daniel 3.12 Psaumes 1.3 Jean 12.26

Cette Bible est dans le domaine public.