Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Daniel 3.23
Bible en Swahili de l’est


Dans la fournaise

1 Nebukadreza, mfalme, alifanya sanamu ya dhahabu, ambayo urefu wake ulikuwa ni dhiraa sitini, na upana wake dhiraa sita; akaisimamisha katika uwanda wa Dura, katika wilaya ya Babeli.
Esaïe 46.6 Jérémie 16.20 Habakuk 2.19 Osée 8.4 1 Rois 12.28
2 Ndipo Nebukadreza akatuma watu kuwakusanya maamiri, na manaibu, na maliwali, na makadhi, na watunza hazina, na mawaziri, na mawakili, na wakuu wa wilaya zote, ili wahudhurie wakati wa kuizindua ile sanamu, mfalme Nebukadneza aliyoisimamisha.
Daniel 3.27 Exode 32.4-32.6 Proverbes 29.12 Nombres 25.2 Juges 16.23
3 Ndipo maamiri, na manaibu, na maliwali, na makadhi, na watunza hazina, na mawaziri, na mawakili, na wakuu wa wilaya zote, wakakusanyika ili kuizindua ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha; wakasimama mbele ya ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha.
Apocalypse 17.17 Actes 19.34-19.35 Apocalypse 13.13-13.16 1 Corinthiens 1.24-1.26 Romains 1.21-1.28
4 Ndipo mpiga mbiu akapiga kelele akisema, Enyi watu wa kabila zote, na taifa, na lugha, mmeamriwa hivi,
Daniel 6.25 Daniel 4.1 Daniel 4.14 Esaïe 40.9 Osée 5.11
5 wakati mtakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, lazima kuanguka na kuiabudu sanamu ya dhahabu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha.
Daniel 3.15 Daniel 3.10 Daniel 3.7
6 Na kila mtu asiyeanguka na kuabudu atatupwa saa iyo hiyo katika tanuru ya moto uwakao.
Jérémie 29.22 Daniel 3.15 Matthieu 13.42 Matthieu 13.50 Daniel 3.11
7 Basi wakati huo, watu wa kabila zote walipoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, watu wote na mataifa na lugha wakaanguka, wakaiabudu ile sanamu, mfalme Nebukadreza aliyoisimamisha.
Apocalypse 13.3 Actes 14.16 Apocalypse 17.8 Apocalypse 13.14 Apocalypse 12.9
8 Basi baadhi ya Wakaldayo wakakaribia, wakaleta mashitaka juu ya Wayahudi.
Esdras 4.12-4.16 Daniel 6.12-6.13 Esther 3.8-3.9 1 Pierre 4.3-4.4 Actes 28.22
9 Wakajibu, wakamwambia mfalme Nebukadreza, Ee mfalme, uishi milele.
Daniel 5.10 Daniel 6.6 Daniel 2.4 Daniel 6.21 Daniel 3.4-3.5
10 Wewe, Ee mfalme, ulitoa amri ya kwamba kila mtu atakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, ni lazima aanguke na kuiabudu ile sanamu ya dhahabu;
Daniel 6.12 Daniel 3.4-3.7 Esther 3.12-3.14 1 Chroniques 16.5-16.6 Exode 1.16
11 na kila mtu asiyeanguka na kuabudu atatupwa katika tanuru ya moto uwakao.
12 Wako Wayahudi kadha wa kadha uliowaweka juu ya mambo ya wilaya ya Babeli, yaani, Shadraka, na Meshaki, na Abednego; watu hawa, Ee mfalme, hawakukujali wewe; hawaitumikii miungu yako, wala kuiabudu ile sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.
Daniel 2.49 Daniel 6.13 Esther 3.8 Proverbes 27.4 1 Samuel 18.7-18.11
13 Basi Nebukadreza akatoa amri kwa hasira na ghadhabu, waletwe hao Shadraka, na Meshaki, na Abednego. Basi wakawaleta watu hao mbele ya mfalme.
Daniel 3.19 Daniel 2.12 Actes 24.24 Proverbes 29.22 Proverbes 17.12
14 Nebukadreza akajibu, akawaambia, Enyi Shadraka, na Meshaki, na Abednego, je! Ni kwa makusudi hata hammtumikii mungu wangu wala kuisujudia sanamu ya dhahabu niliyoisimamisha?
Jérémie 50.2 Daniel 3.1 Esaïe 46.1 Daniel 4.8 Exode 21.13-21.14
15 Basi sasa, kama mkiwa tayari wakati mtakapoisikia sauti ya panda, na filimbi, na kinubi, na zeze, na santuri, na zomari, na namna zote za ngoma, kuanguka na kuisujudia sanamu niliyoisimamisha, ni vema; bali msipoisujudia, mtatupwa saa iyo hiyo katika tanuru iwakayo moto; naye ni nani Mungu yule atakayewaokoa ninyi na mikono yangu?
Exode 5.2 2 Rois 18.35 Luc 21.14-21.15 Actes 5.29 Marc 13.11
16 Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakajibu, wakamwambia mfalme, Ee Nebukadreza, hamna haja kukujibu katika neno hili.
Daniel 1.7 Daniel 3.12
17 Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia aweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto; naye atatuokoa na mkono wako, Ee mfalme.
Psaumes 27.1-27.2 Actes 20.24 Luc 1.37 Hébreux 7.25 Romains 8.31
18 Bali kama si hivyo, ujue, Ee mfalme, ya kuwa sisi hatukubali kuitumikia miungu yako, wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.
Luc 12.3-12.9 Matthieu 10.39 Josué 24.15 Apocalypse 2.10-2.11 Matthieu 10.32-10.33
19 Ndipo Nebukadreza akajaa ghadhabu, na sura ya uso wake ikabadilika juu ya Shadraka, na Meshaki, na Abednego, basi akatoa amri watie moto ile tanuru mara saba kuliko desturi yake ya kutiwa moto.
Daniel 3.13 Lévitique 26.28 Lévitique 26.21 Lévitique 26.24 Lévitique 26.18
20 Kisha akawaamuru baadhi ya watu mashujaa wa jeshi lake kuwafunga Shadraka, na Meshaki, na Abednego, na kuwatupa katika ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.
Actes 16.25 Daniel 3.15 Actes 12.4-12.5 Actes 16.23
21 Basi watu hao wakafungwa, hali wamevaa suruali zao, na kanzu zao, na joho zao, na mavazi yao mengine, wakatupwa katikati ya ile tanuru iliyokuwa ikiwaka moto.
22 Basi kwa sababu amri ya mfalme ilikuwa ni kali, na ile tanuru ilikuwa ina moto sana, mwako wa ule moto ukawaua wale watu waliowashika Shadraka, na Meshaki, na Abednego.
Exode 12.33 Proverbes 21.18 Proverbes 11.8 Matthieu 27.5 Daniel 1.7
23 Na watu hao watatu, Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakaanguka, hali wamefungwa, katikati ya ile tanuru iliyokuwa inawaka moto.
Psaumes 124.1-124.5 Jérémie 38.6 Psaumes 34.19 Psaumes 66.11-66.12 Daniel 6.16-6.17
24 Ndipo Nebukadreza akastaajabu, akainuka kwa haraka; akanena, akawaambia mawaziri wake, Je! Hatukutupa watu watatu, hali wamefungwa, katikati ya moto? Wakajibu, wakamwambia mfalme, Kweli, Ee mfalme.
Daniel 6.7 Actes 12.13 Daniel 4.27 Actes 5.23-5.25 Actes 9.6
25 Akajibu, akasema, Tazama, mimi naona watu wanne, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu.
Esaïe 43.2 Actes 28.5 Psaumes 91.3-91.9 Psaumes 34.7 Job 1.6
26 Kisha Nebukadreza akaukaribia mdomo wa ile tanuru iliyokuwa inawaka moto. Akanena, akasema, Enyi Shadraka, na Meshaki, na Abednego, watumishi wa Mungu Aliye juu, tokeni, mje huku. Ndipo Shadraka, na Meshaki, na Abednego, wakatoka katika ule moto.
Daniel 3.17 Esaïe 52.12 Galates 1.10 Daniel 4.2 Actes 16.17
27 Na maamiri, na manaibu, na maliwali, na mawaziri, waliokuwa wamekusanyika pamoja, wakawaona watu hao, ya kuwa ule moto ulikuwa hauna nguvu juu ya miili yao, wala nywele za vichwa vyao hazikuteketea, wala suruali zao hazikubadilika, wala harufu ya moto haikuwapata hata kidogo.
Hébreux 11.34 Esaïe 43.2 Actes 27.34 Luc 21.17-21.18 Matthieu 10.30
28 Nebukadreza akanena, akasema, Na ahimidiwe Mungu wa Shadraka, na Meshaki, na Abednego; aliyemtuma malaika wake, akawaokoa watumishi wake waliomtumaini, wakaligeuza neno la mfalme, na kujitoa miili yao ili wasimtumikie mungu mwingine, wala kumwabudu, ila Mungu wao wenyewe.
Actes 5.19 Psaumes 34.7-34.8 Esaïe 26.3-26.4 Daniel 3.25 Psaumes 147.11
29 Basi mimi naweka amri ya kuwa kila kabila ya watu, na kila taifa, na kila lugha, watakaonena neno lo lote lisilopasa juu ya huyo Mungu wa Shadraka, na Meshaki, na Abednego, watakatwa vipande vipande, na nyumba zao zitafanywa jaa; kwa kuwa hakuna Mungu mwingine awezaye kuokoa namna hii.
Daniel 2.5 Daniel 6.26-6.27 Deutéronome 32.31 Psaumes 76.10 Daniel 3.15
30 Kisha mfalme akawakuza Shadraka, na Meshaki, na Abednego, katika wilaya ya Babeli.
Daniel 2.49 Daniel 3.12 Psaumes 1.3 Jean 12.26 Romains 8.31

Cette Bible est dans le domaine public.