Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jérémie 32.27
Bible en Swahili de l’est


Achat d’un champ par Jérémie

1 Neno hili ndilo lililomjia Yeremia, kutoka kwa Bwana, katika mwaka wa kumi wa Sedekia, mfalme wa Yuda, nao ulikuwa mwaka wa kumi na nane wa Nebukadreza.
Jérémie 39.1-39.2 2 Rois 25.1-25.2 Jérémie 25.1 Jérémie 52.4-52.5 2 Chroniques 36.11
2 Basi, wakati huo jeshi la mfalme wa Babeli liliuzunguka Yerusalemu; na Yeremia, nabii, alikuwa amefungwa ndani ya uwanda wa walinzi, uliokuwa katika nyumba ya mfalme wa Yuda.
Jérémie 37.21 Néhémie 3.25 Jérémie 33.1 Jérémie 38.6 Jérémie 32.8
3 Kwa maana Sedekia, mfalme wa Yuda, alikuwa amemfunga, akisema, Kwa nini unatabiri, na kusema, Bwana asema hivi, Angalia, nitatia mji huu katika mikono ya mfalme wa Babeli, naye atautwaa;
Jérémie 34.2-34.3 Jérémie 21.4-21.7 Jérémie 26.8-26.9 Jérémie 32.28-32.29 Amos 7.13
4 tena, Sedekia, mfalme wa Yuda, hatapona kutoka katika mikono ya Wakaldayo, lakini hakika yake atatiwa katika mikono ya mfalme wa Babeli, atanena naye mdomo kwa mdomo, na macho yake yatatazama macho yake;
Jérémie 38.18 Jérémie 38.23 Jérémie 39.4-39.7 2 Rois 25.4-25.7 Jérémie 37.17
5 naye atamchukua Sedekia mpaka Babeli, naye atakuwako huko hata nitakapomjilia, asema Bwana; mjapopigana na Wakaldayo hamtafanikiwa.
Jérémie 27.22 Ezéchiel 17.15 Jérémie 39.7 Ezéchiel 17.9-17.10 Jérémie 33.5
6 Yeremia akasema, Neno la Bwana limenijia, kusema,
7 Tazama, Hanameli, mwana wa Shalumu, mjomba wako, atakujia, akisema, Jinunulie shamba langu lililoko Anathothi; maana haki ya ukombozi ni yako, ulinunue.
Jérémie 1.1 Jérémie 11.21 Lévitique 25.25 Lévitique 25.23 Nombres 35.2
8 Basi Hanameli, mwana wa mjomba wangu, akanijia ndani ya uwanda wa walinzi, sawasawa na lile neno la Bwana, akaniambia, Tafadhali, ulinunue shamba langu lililoko Anathothi, katika nchi ya Benyamini; maana haki ya urithi ni yako, na haki ya ukombozi ni yako; ujinunulie. Ndipo nikajua kama neno hili ni neno la Bwana.
Jérémie 32.7 Jérémie 32.2 Jérémie 33.1 1 Rois 22.25 1 Samuel 10.3-10.7
9 Basi nikalinunua shamba lile lililoko Anathothi kwa Hanameli, mwana wa mjomba wangu, nikampimia fedha yake, shekeli kumi na saba za fedha.
Esther 3.9 Genèse 37.28 1 Rois 20.39 Genèse 23.15-23.16 Zacharie 11.12-11.13
10 Nami nikaitia sahihi ile hati, na kuipiga muhuri, nikawaita mashahidi, nikampimia ile fedha katika mizani.
Jérémie 32.44 Jérémie 32.12 Deutéronome 32.34 Esaïe 44.5 Jérémie 32.25
11 Nikaitwaa ile hati ya kununua, ile iliyopigwa muhuri kama ilivyo sheria na ada, na ile nayo iliyokuwa wazi;
Luc 2.27 Actes 26.3 1 Corinthiens 11.16
12 na ile hati ya kununua nikampa Baruku, mwana wa Neria, mwana wa Maaseya, mbele ya uso wa Hanameli, mwana wa mjomba wangu, na mbele ya mashahidi wale walioitia sahihi hati ya kununua, mbele ya Wayahudi wote walioketi katika uwanda wa walinzi.
Jérémie 32.16 Jérémie 51.59 Jérémie 36.26 Jérémie 36.4-36.5 Jérémie 36.16-36.19
13 Nami nikamwagiza Baruku mbele yao, nikisema,
14 Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Twaa hati hizi, hati hii ya kununua, hati hii iliyopigwa muhuri, na hii iliyo wazi pia, ukazitie katika chombo cha udongo, zipate kukaa siku nyingi.
15 Maana Bwana wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi, Nyumba na mashamba na mashamba ya mizabibu yatanunuliwa tena katika nchi hii.
Jérémie 32.43-32.44 Amos 9.14-9.15 Jérémie 30.18 Jérémie 31.5 Jérémie 31.12
16 Hata nikiisha kumpa Baruku, mwana wa Neria, hati ile ya kununua, nalimwomba Bwana, nikisema,
Philippiens 4.6-4.7 Jérémie 12.1 Genèse 32.9-32.12 2 Samuel 7.18-7.25 Ezéchiel 36.35-36.37
17 Aa! Bwana MUNGU, tazama, wewe umeziumba mbingu na nchi, kwa uweza wako mkuu na kwa mkono wako ulionyoshwa; hapana neno lililo gumu usiloliweza;
Jérémie 27.5 Genèse 18.14 Luc 1.37 2 Rois 19.15 Jérémie 32.27
18 wewe uwarehemuye watu elfu nyingi, uwalipaye baba za watu uovu wao vifuani mwa watoto wao baada yao; Mungu aliye mkuu, aliye hodari, Bwana wa majeshi ndilo jina lake;
Jérémie 10.16 Deutéronome 5.9-5.10 Exode 34.7 Matthieu 23.32-23.36 Esaïe 9.6
19 mkuu wa mashauri, mweza katika kutenda; ambaye macho yake yamefumbuka juu ya njia zote za wanadamu, kumpa kila mtu kwa kadiri ya njia zake, na kwa kadiri ya matunda ya matendo yake,
Jérémie 17.10 Esaïe 28.29 Matthieu 16.27 Jérémie 16.17 Proverbes 5.21
20 wewe uliyeweka ishara na ajabu katika nchi ya Misri hata siku hii ya leo, katika Israeli na kati ya watu wengine; na kujifanyia jina kama ilivyo leo;
Néhémie 9.10 Exode 9.16 Esaïe 63.12 2 Samuel 7.23 Daniel 9.15
21 ukawatoa watu wako, Israeli, katika nchi ya Misri, kwa ishara, na kwa ajabu, na kwa mkono hodari, na kwa mkono ulionyoshwa, na kwa utisho mkuu;
Exode 6.6 Deutéronome 26.8 1 Chroniques 17.21 Psaumes 136.11-136.12 Exode 13.9
22 ukawapa nchi hii, uliyowaapia baba zao kwamba utawapa, nchi iliyojaa maziwa na asali;
Exode 3.8 Exode 13.5 Jérémie 11.5 Exode 3.17 Psaumes 105.9-105.11
23 nao wakaingia, wakaimiliki; lakini hawakuitii sauti yako, wala hawakuenda katika sheria yako; hawakutenda neno lo lote katika haya uliyowaagiza wayatende; basi, kwa sababu hii umeleta juu yao mabaya haya yote;
Esdras 9.7 Psaumes 78.54-78.55 Daniel 9.10-9.14 Psaumes 44.2-44.3 Lamentations 1.18
24 angalia maboma haya; wameujia mji huu ili kuutwaa; na mji huu umetiwa katika mikono ya Wakaldayo wanaopigana nao, kwa sababu ya upanga, na njaa, na tauni; na hayo uliyosema yamekuwa; na, tazama, wewe unayaona.
Josué 23.15-23.16 Deutéronome 4.26 Jérémie 32.36 Jérémie 33.4 Ezéchiel 14.21
25 Nawe, Ee Bwana MUNGU, umeniambia, Jinunulie shamba lile kwa fedha, ukawaite mashahidi; iwapo mji huu umetiwa katika mikono ya Wakaldayo; je! Itakuwaje?
Jérémie 32.24 Romains 11.33-11.34 Psaumes 97.2 Psaumes 77.19 Jean 13.7
26 Ndipo neno la Bwana likamjia Yeremia, kusema,
27 Tazama, mimi ni Bwana, Mungu wa wote wenye mwili; je! Kuna neno gumu lo lote nisiloliweza?
Jérémie 32.17 Matthieu 19.26 Nombres 16.22 Esaïe 64.8 Nombres 27.16
28 Basi, Bwana asema hivi, Tazama, nitautia mji huu katika mikono ya Wakaldayo, na katika mikono ya Nebukadreza, mfalme wa Babeli, naye atautwaa;
Jérémie 32.3 Jérémie 32.24 Jérémie 32.36 Jérémie 19.7-19.12 2 Chroniques 36.17
29 na Wakaldayo, wanaopigana na mji huu, watakuja, na kuutia moto mji huu, na kuuteketeza, pamoja na nyumba zake, ambazo juu ya dari zake wamemfukizia Baali uvumba, na kuwamiminia miungu mingine vinywaji, ili kunikasirisha.
Jérémie 19.13 Jérémie 21.10 Jérémie 52.13 2 Chroniques 36.19 Jérémie 44.17-44.19
30 Maana wana wa Israeli, na wana wa Yuda, wametenda yaliyo mabaya tu mbele za uso wangu, tangu ujana wao; maana wana wa Israeli wamenichokoza tu kwa matendo ya mikono yao, asema Bwana.
Jérémie 7.22-7.26 Jérémie 25.7 Jérémie 2.7 Esaïe 63.10 Jérémie 22.21
31 Kwa kuwa mji huu umekuwa sababu ya kunitia hasira, na sababu ya ghadhabu yangu, tangu siku ile walipoujenga hata siku hii ya leo; ili niuondoe usiwe mbele za uso wangu;
2 Rois 23.27 2 Rois 21.4-21.7 2 Rois 21.16 Jérémie 6.6-6.7 Jérémie 27.10
32 kwa sababu ya mabaya yote ya wana wa Israeli, na ya wana wa Yuda, waliyoyatenda ili kunitia hasira, wao, na wafalme wao, na wakuu wao, na makuhani wao, na manabii wao, na watu wa Yuda, na wenyeji wa Yerusalemu.
Esaïe 1.4-1.6 Daniel 9.8 Jérémie 2.26 Esdras 9.7 Esaïe 1.23
33 Tena wamenigeuzia visogo vyao, wala si nyuso zao; ingawa naliwafundisha, niliondoka mapema na kuwafundisha, lakini hawakusikiliza ili wapate mafundisho.
Ezéchiel 8.16 Jérémie 2.27 Jérémie 7.13 Jérémie 7.24 Jérémie 35.15
34 Bali waliweka machukizo yao ndani ya nyumba iliyoitwa kwa jina langu, ili kuinajisi.
Jérémie 7.30 Jérémie 23.11 2 Rois 21.4-21.7 2 Rois 23.6 2 Chroniques 33.4-33.7
35 Tena walijenga mahali palipoinuka kwa Baali, palipo katika bonde la mwana wa Hinomu, ili kuwapitisha wana wao na binti zao katika moto kwa ajili ya Moleki, jambo nisilowaagiza; wala halikuingia moyoni mwangu kwamba walitende chukizo hilo; wapate kumkosesha Yuda.
Jérémie 7.31 Lévitique 18.21 2 Chroniques 33.6 Lévitique 20.2-20.5 2 Rois 23.10
36 Basi sasa, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi, katika habari za mji huu, ambao ninyi mnasema juu yake maneno haya, Umetiwa katika mikono ya mfalme wa Babeli, kwa upanga, na kwa njaa, na kwa tauni;
Jérémie 32.24 Jérémie 32.3 Jérémie 16.12-16.15 Osée 2.14 Romains 5.20
37 Tazama, nitawakusanya, na kuwatoa katika nchi zote nilikowafukuza, katika hasira yangu, na uchungu wangu, na ghadhabu yangu nyingi; nami nitawaleta tena hata mahali hapa, nami nitawakalisha salama salimini;
Jérémie 23.3 Jérémie 23.6 Jérémie 23.8 Ezéchiel 11.17 Zacharie 14.11
38 nao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao;
Jérémie 24.7 Ezéchiel 37.27 Jérémie 30.22 Hébreux 8.10 Apocalypse 21.7
39 nami nitawapa moyo mmoja na njia moja, wapate kunicha sikuzote; kwa mema yao, na ya watoto wao baada yao;
Ezéchiel 11.19-11.20 Jean 17.21 Actes 4.32 2 Chroniques 30.12 Deutéronome 11.18-11.21
40 nami nitafanya agano la milele pamoja nao, kwamba sitageuka wala kuwaacha, ili niwatendee mema; nami nitatia kicho changu mioyoni mwao, ili wasiniache.
Esaïe 55.3 1 Pierre 1.5 Jacques 1.17 Ezéchiel 39.29 Hébreux 6.13-6.18
41 Naam, nitafurahi juu yao niwatendee mema, nami nitawapanda katika nchi hii kweli kweli, kwa moyo wangu wote, na kwa roho yangu yote.
Jérémie 24.6 Osée 2.19-2.20 Deutéronome 30.9 Sophonie 3.17 Esaïe 62.5
42 Maana Bwana asema hivi, Kama nilivyoleta mabaya makuu haya yote juu ya watu hawa, vivyo hivyo nitaleta juu yao mema hayo yote niliyowaahidia.
Jérémie 31.28 Zacharie 8.14-8.15 Josué 23.14-23.15 Jérémie 33.10-33.11 Matthieu 24.35
43 Na mashamba yatanunuliwa katika nchi hii, mnayoitaja, mkisema, Ni ukiwa, haina mwanadamu wala mnyama; imetiwa katika mikono ya Wakaldayo.
Ezéchiel 37.11-37.14 Jérémie 32.15 Jérémie 33.10 Jérémie 32.36
44 Watu watanunua mashamba kwa fedha, watazitia sahihi hati zake, na kuzipiga muhuri, na kuwaita mashahidi, katika nchi ya Benyamini, na katika mahali palipo pande zote za Yerusalemu, na katika miji ya Yuda, na katika miji ya nchi yenye vilima, na katika miji ya nchi tambarare, na katika miji ya Negebu; kwa maana nitawarudisha wafungwa wao, asema Bwana.
Jérémie 17.26 Jérémie 33.11 Jérémie 33.7 Jérémie 33.26 Jérémie 32.10

Cette Bible est dans le domaine public.