Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Proverbes 18.6
Bible en Swahili de l’est


1 Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe; Hushindana na kila shauri jema.
Proverbes 2.1-2.6 Proverbes 20.3 Jude 1.19 Ephésiens 5.15-5.17 Proverbes 20.19
2 Mpumbavu hapendezwi na ufahamu; Ila moyo wake udhihirike tu.
Proverbes 12.23 Proverbes 13.16 Nombres 24.15-24.16 Psaumes 1.1-1.2 Proverbes 1.7
3 Ajapo asiye haki, huja dharau pia; Na pamoja na aibu huja lawama.
Psaumes 123.3-123.4 Matthieu 27.39-27.44 1 Pierre 4.4 Psaumes 69.20 Psaumes 69.9
4 Maneno ya kinywa cha mtu ni kama maji ya vilindi; Kijito kibubujikacho; chemchemi ya hekima.
Proverbes 20.5 Proverbes 13.14 Proverbes 10.11 Colossiens 4.6 Matthieu 12.34
5 Kukubali uso wake asiye haki si vizuri; Wala kumpotosha mwenye haki hukumuni.
Proverbes 24.23 Proverbes 28.21 Lévitique 19.15 Psaumes 82.2 Proverbes 17.15
6 Midomo ya mpumbavu huingia katika fitina, Na kinywa chake huita mapigo.
Proverbes 14.3 Proverbes 13.10 Proverbes 17.14 Proverbes 20.3 Proverbes 25.24
7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake, Na midomo yake ni mtego wa nafsi yake.
Proverbes 10.14 Proverbes 12.13 Proverbes 13.3 Psaumes 140.9 Psaumes 64.8
8 Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo; Nayo hushukia pande za ndani za tumbo.
Proverbes 16.28 Lévitique 19.16 Proverbes 12.18 Psaumes 52.2 Proverbes 26.20-26.22
9 Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake, Ni ndugu yake aliye mharabu.
Proverbes 28.24 Proverbes 10.4 Proverbes 23.20-23.21 Matthieu 25.26 Hébreux 6.12
10 Jina la Bwana ni ngome imara; Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.
2 Samuel 22.3 Esaïe 26.4 Psaumes 144.2 Psaumes 91.2 Psaumes 27.1
11 Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu; Ni kama ukuta mrefu katika mawazo yake.
Proverbes 10.15 Job 31.24-31.25 Psaumes 49.6-49.9 Psaumes 52.5-52.7 Deutéronome 32.31
12 Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna; Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.
Proverbes 15.33 Proverbes 11.2 Proverbes 16.18 Ezéchiel 28.9 Proverbes 29.23
13 Yeye ajibuye kabla hajasikia, Ni upumbavu na aibu kwake.
Jean 7.51 Deutéronome 13.14 Proverbes 20.25 2 Samuel 16.4 2 Samuel 19.24-19.30
14 Roho ya mtu itastahimili udhaifu wake; Bali roho iliyovunjika nani awezaye kuistahimili?
Proverbes 15.13 Proverbes 17.22 1 Pierre 1.6 Jacques 1.2 2 Corinthiens 12.9-12.10
15 Moyo wa mwenye busara hupata maarifa; Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.
Proverbes 15.14 Psaumes 119.97-119.104 2 Timothée 3.15-3.17 Proverbes 10.14 1 Rois 3.9
16 Zawadi ya mtu humpatia nafasi; Humleta mbele ya watu wakuu.
Genèse 32.20 1 Samuel 25.27 Proverbes 17.8 Genèse 43.11 Proverbes 19.6
17 Ajiteteaye kwanza huonekana kuwa ana haki; Lakini jirani yake huja na kumchunguza.
Proverbes 18.13 2 Samuel 19.24-19.27 2 Samuel 16.1-16.3 Actes 24.12-24.13
18 Kura hukomesha mashindano; Hukata maneno ya wakuu.
Proverbes 16.33 1 Chroniques 6.63 1 Samuel 10.21-10.27 Néhémie 11.1 1 Samuel 14.42
19 Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa nguvu; Na mashindano ni kama mapingo ya ngome.
Actes 15.39 1 Rois 12.16 Genèse 37.11 1 Rois 2.23-2.25 2 Samuel 13.28
20 Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake; Atashiba mazao ya midomo yake.
Proverbes 12.13-12.14 Proverbes 13.2 Proverbes 25.11-25.12
21 Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; Na wao waupendao watakula matunda yake.
Ephésiens 4.29 Matthieu 12.35-12.37 Colossiens 4.6 Proverbes 10.19-10.21 Jacques 3.6-3.9
22 Apataye mke apata kitu chema; Naye ajipatia kibali kwa Bwana.
Proverbes 19.14 Proverbes 12.4 Ecclésiaste 9.9 Proverbes 31.10-31.31 Proverbes 8.35
23 Maskini hutumia maombi; Bali tajiri hujibu kwa ukali.
Jacques 2.3 Ruth 2.7 Jacques 1.9-1.11 Matthieu 5.3 1 Samuel 2.36
24 Ajifanyiaye rafiki wengi ni kwa uangamivu wake mwenyewe; Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.
Proverbes 17.17 Proverbes 27.9 1 Chroniques 12.38-12.40 Matthieu 26.49-26.50 Jean 15.13-15.15

Cette Bible est dans le domaine public.