Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 25.31
Bible en Swahili de l’est


Instructions pour la construction du tabernacle

Les offrandes

1 Bwana akanena na Musa, akamwambia,
2 Waambie wana wa Israeli kwamba wanitwalie sadaka; kila mtu ambaye moyo wake wampa kupenda mtatwaa kwake sadaka yangu.
Esdras 2.68 2 Corinthiens 9.7 Esdras 3.5 Néhémie 11.2 Esdras 7.16
3 Sadaka utakayopokea mikononi mwao ni hii; dhahabu, na fedha, na shaba,
Job 28.2 Deutéronome 8.9
4 na nyuzi za rangi ya samawi, na za rangi ya zambarau, na za rangi nyekundu, na nguo za kitani safi, na singa za mbuzi;
Genèse 41.42 Ezéchiel 16.10 Apocalypse 19.8
5 na ngozi za kondoo waume zilizotiwa rangi nyekundu, na ngozi za pomboo, na miti ya mshita,
Exode 26.14-26.15 Exode 36.20 Exode 26.37-27.1 Exode 26.26
6 na mafuta ya ile taa, na viungo vya manukato kwa yale mafuta ya kupaka, na kwa ule uvumba wenye harufu nzuri;
Exode 27.20 Exode 25.37 Exode 40.24-40.25 Exode 30.23-30.38
7 na vito vya shohamu, na vito vingine vya kutiwa kwa ile naivera, na kwa kile kifuko cha kifuani.
Exode 28.4 Exode 28.6-28.30
8 Nao na wanifanyie patakatifu; ili nipate kukaa kati yao.
2 Corinthiens 6.16 Exode 29.45 Apocalypse 21.3 1 Rois 6.13 Hébreux 9.1-9.2
9 Sawasawa na haya yote nikuonyeshayo, mfano wa maskani, na mfano wa vyombo vyake vyote, ndivyo mtakavyovifanya.
Exode 25.40 Hébreux 8.5 Hébreux 9.9 1 Chroniques 28.11-28.19 Actes 7.44

L’arche de l’alliance

10 Nao na wafanye sanduku la mti wa mshita; urefu wake na uwe dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu, na kwenda juu kwake dhiraa moja na nusu.
Hébreux 9.4 Exode 37.1-37.3 Deutéronome 10.1-10.3 2 Chroniques 8.11 Apocalypse 11.19
11 Nawe ulifunike kwa dhahabu safi, ulifunike ndani na nje, nawe tia na ukingo wa dhahabu kulizunguka pande zote.
Exode 30.3 Exode 25.24 2 Chroniques 3.4 1 Rois 6.20
12 Nawe subu vikuku vinne vya dhahabu kwa ajili yake, na kuvitia katika miguu yake minne; vikuku viwili upande mmoja, na vikuku viwili upande wake wa pili.
Exode 38.7 Exode 26.29 Exode 25.15 Exode 37.5 Exode 27.7
13 Nawe fanya miti mirefu ya mshita na kuifunika dhahabu.
Exode 40.20 Exode 37.4 Nombres 4.11 Nombres 4.14 1 Chroniques 15.15
14 Nawe tia hiyo miti katika vile vikuku vilivyo katika pande mbili za sanduku ili kulichukua hilo sanduku.
15 Hiyo miti itakaa katika vile vikuku vya sanduku; haitaondolewa.
1 Rois 8.8 2 Chroniques 5.9
16 Kisha tia ndani ya sanduku huo ushuhuda nitakaokupa.
Deutéronome 31.26 1 Rois 8.9 Hébreux 9.4 Exode 16.34 Nombres 17.4
17 Nawe fanya kiti cha rehema cha dhahabu safi; urefu wake utakuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu.
Exode 37.6 Hébreux 9.5 Romains 3.25 1 Jean 2.2 Lévitique 16.12-16.15
18 Nawe fanya makerubi mawili ya dhahabu; uyafanye ya kazi ya kufua, katika hiyo miisho ya kiti cha rehema, huku na huku.
Ezéchiel 10.2 1 Rois 8.6-8.7 Ezéchiel 41.18-41.19 Ezéchiel 10.20 Exode 37.7-37.9
19 Weka kerubi moja mwisho mmoja, na kerubi la pili mwisho wa pili; fanya hayo makerubi ya kitu kimoja na kiti cha rehema, mwisho huku na mwisho huku.
20 Na hayo makerubi yatainua mabawa yao juu, na kukifunika hicho kiti cha rehema kwa mabawa yao, na nyuso zao zitaelekeana hili na hili; nyuso za hayo makerubi zitaelekea kiti cha rehema.
1 Chroniques 28.18 1 Rois 8.7 Hébreux 9.5 Jean 1.51 1 Corinthiens 4.9
21 Weka kiti cha rehema juu ya hilo sanduku, kisha utie huo ushuhuda nitakaokupa ndani ya sanduku.
Exode 26.34 Romains 10.4 Exode 25.16-25.17
22 Nami nitaonana nawe hapo, na kuzungumza nawe pale nilipo juu ya kiti cha rehema, katikati ya hayo makerubi mawili yaliyo juu ya sanduku la ushuhuda, katika mambo yote nitakayokuagiza kwa ajili ya wana wa Israeli.
Exode 29.42-29.43 Esaïe 37.16 2 Rois 19.15 Lévitique 16.2 1 Samuel 4.4

La table des pains consacrés

23 Nawe fanya meza ya mti wa mshita; urefu wake utakuwa dhiraa mbili, na upana wake dhiraa moja, na kwenda juu kwake dhiraa moja na nusu.
Hébreux 9.2 Exode 37.10-37.16 1 Rois 7.48 2 Chroniques 4.8 2 Chroniques 4.19
24 Uifunike dhahabu safi, na kuifanyia ukingo wa dhahabu wa kuizunguka pande zote.
Exode 25.11 1 Rois 6.20-6.22
25 Kisha ifanyie upapi wa kuizunguka pande zote, upana wake utakuwa nyanda nne, nawe uufanyie ule upapi ukingo wa urembo wa dhahabu wa kuuzunguka pande zote.
Exode 37.2 Exode 30.3
26 Uifanyie vikuku vinne vya dhahabu, na kuvitia vile vikuku katika pembe zake nne, katika miguu yake minne.
27 Vile vikuku na viwe karibu na ule upapi, ili viwe mahali pa kutilia ile miti, ya kuichukulia meza.
Exode 25.28 Exode 25.14
28 Fanya ile miti ya mti wa mshita, na kuifunika dhahabu, kwamba ile meza ichukuliwe kwayo.
Exode 25.14 Exode 25.27 Actes 9.15 Nombres 10.17
29 Nawe fanya sahani zake, na miiko yake, na makopo yake, na vikombe vyake vya kumiminia; vifanye vyote vya dhahabu safi.
Nombres 4.7 Exode 37.16 Nombres 7.19 1 Rois 7.50 Esdras 1.9-1.11
30 Nawe utaiweka mikate ya wonyesho juu ya meza mbele yangu daima.
Exode 39.36 Lévitique 24.5-24.9 Exode 35.13 1 Chroniques 23.29 Malachie 1.7

Le chandelier en or

31 Nawe fanya kinara cha taa cha dhahabu safi; hicho kinara na kifanywe cha kazi ya kufua, tako lake, na mti wake, vikombe vyake, na matovu yake, na maua yake, vyote vitakuwa vya kitu kimoja nacho;
1 Rois 7.49 Zacharie 4.2 Exode 37.17-37.24 Apocalypse 1.12 Hébreux 9.2
32 nacho kitakuwa na matawi sita yenye kutoka ubavuni mwake; matawi matatu ya kinara upande wake mmoja, na matawi matatu ya kinara upande wake wa pili
33 vikombe vitatu vilivyofanywa mfano wa maua ya mlozi katika tawi moja; tovu na ua; na vikombe vitatu vilivyofanywa mfano wa maua ya mlozi katika tawi la pili, tovu na ua; vivyo hivyo hayo matawi yote sita yatokayo katika kile kinara;
Exode 37.19-37.20 Zacharie 4.3 Jérémie 1.11-1.12 Nombres 17.4-17.8
34 na katika hicho kinara vikombe vinne vilivyofanywa mfano wa maua ya mlozi, matovu yake, na maua yake;
35 na tovu chini ya matawi mawili la kitu kimoja nacho, na tovu chini ya matawi mawili la kitu kimoja nacho, na tovu chini ya matawi mawili la kitu kimoja nacho, kwa hayo matawi sita yatokayo katika kile kinara.
36 Matovu yake na matawi yake yatakuwa ya kitu kimoja nacho; kiwe chote pia kazi moja ya kufua, ya dhahabu safi.
2 Chroniques 9.15 Exode 25.18 Nombres 8.4 1 Rois 10.16-10.17
37 Nawe zifanye taa zake saba; nao wataziwasha hizo taa zake, zitoe nuru mbele yake.
Nombres 8.2 2 Chroniques 13.11 Exode 27.21 Lévitique 24.2-24.4 Zacharie 4.2
38 Na makoleo yake, na visahani vyake, vyote vitakuwa vya dhahabu safi.
Jérémie 52.18 1 Rois 7.50 Exode 37.23 2 Rois 12.13 2 Rois 25.14
39 Kitafanywa cha talanta moja ya dhahabu safi, pamoja na vyombo hivi vyote.
40 Nawe angalia ya kwamba uvifanye kama mfano wake, ulioonyeshwa mlimani.
Exode 26.30 Hébreux 8.5 Nombres 8.4 Actes 7.44 1 Chroniques 28.11

Cette Bible est dans le domaine public.