Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Rois 22.19
Bible en Swahili de l’est


Mort d’Achab

1 Wakakaa miaka mitatu pasipo vita kati ya Shamu na Israeli.
1 Rois 20.34
2 Ikawa, mwaka wa tatu Yehoshafati mfalme Wa Yuda akamshukia mfalme wa Israeli.
1 Rois 15.24 1 Rois 22.1 1 Rois 22.41 2 Rois 8.18 Matthieu 16.21
3 Mfalme wa Israeli akawaambia watumishi wake, Je! Hamjui ya kuwa Ramoth-Gileadi ni yetu? Nasi tumenyamaza tusiitwae mkononi mwa mfalme wa Shamu?
Deutéronome 4.43 1 Rois 4.13 Josué 21.38 2 Samuel 19.10 Josué 20.8
4 Akamwambia Yehoshafati, Je! Utakwenda nami tupigane na Ramoth-gileadi? Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli, Mimi ni kama wewe, na watu wangu ni kama watu wako na farasi zangu ni kama farasi zako.
2 Rois 3.7 2 Chroniques 19.2 1 Corinthiens 15.33 Psaumes 139.21-139.22 Apocalypse 2.26
5 Yehoshafati akamwambia mfalme wa Israeli, Uulize leo, nakusihi, kwa neno la Bwana.
2 Rois 3.11 Jérémie 42.2-42.6 2 Chroniques 18.4-18.5 1 Samuel 30.8 1 Samuel 23.2
6 Ndipo mfalme wa Israeli akawakusanya pamoja manabii, kama watu mia nne. Akawaambia Je! Niende juu ya Ramoth-Gileadi kuupiga vita, au ninyamaze? Wakasema Kwea; kwa kuwa Bwana atautia mkononi mwa mfalme.
1 Rois 18.19 Ezéchiel 13.22 Jérémie 23.14-23.17 Matthieu 7.15 1 Rois 22.15
7 Lakini Yehoshafati akasema, Je! Hayupo hapa nabii wa Bwana tena, ili tumwulize yeye?
2 Chroniques 18.6-18.7 2 Rois 3.11-3.13
8 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Yupo mtu mmoja, ambaye tungeweza kumwuliza Bwana kwa yeye, yaani Mikaya mwana wa Imla; lakini namchukia; kwa sababu hanibashirii mema, ila mabaya. Yehoshafati akasema, La! Mfalme asiseme hivi.
Jérémie 38.4 Michée 2.7 Amos 5.10 Jean 3.19-3.21 Jean 7.7
9 Ndipo mfalme wa Israeli akamwita akida, akamwambia, mlete hima Mikaya mwana wa Imla.
Daniel 1.18 Esaïe 39.7 2 Rois 9.32 2 Chroniques 18.8 1 Rois 22.26-22.27
10 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wakikaa kila mtu katika kiti chake cha enzi, wamevaa mavazi yao, katika sakafu langoni pa Samaria; na manabii wote wakafanya unabii mbele yao.
Jérémie 27.14-27.16 1 Rois 22.6 Esther 5.1 2 Chroniques 18.9-18.11 1 Rois 18.29
11 Na Zedekia mwana wa Kenaana akajifanyia pembe za chuma, akasema, Bwana asema hivi, Kwa hizo utawasukuma Washami, hata waharibike.
Zacharie 1.18-1.21 Deutéronome 33.17 Jérémie 23.25 Actes 19.13-19.16 Jérémie 28.10-28.14
12 Na manabii wote wakasema hivyo kwa unabii, wakisema, Kwea Ramoth-Gileadi, ukafanikiwe; kwa kuwa Bwana atautia mkononi mwa mfalme.
1 Rois 22.32-22.36 1 Rois 22.6-22.15 2 Chroniques 35.22
13 Na yule mjumbe, aliyekwenda kumwita Mikaya, akamwambia, akasema, Angalia sasa, maneno ya manabii kwa kinywa kimoja husema mema kwa mfalme; neno lako na liwe, nakusihi, kama neno la mmojawapo wao, ukaseme mema.
Osée 7.3 Psaumes 14.1 Michée 2.6-2.7 Psaumes 11.1 Amos 7.13-7.17
14 Mikaya akasema, Kama Bwana aishivyo, neno lile Bwana aniambialo, ndilo nitakalolinena.
Nombres 24.13 Nombres 22.18 Galates 1.10 Jérémie 42.4 1 Rois 18.10
15 Na alipokuja kwa mfalme, mfalme alimwambia, Je! Mikaya, tuende Ramoth-Gileadi kupiga vita, au tunyamaze? Akamwambia, Kwea, ufanikiwe; kwa kuwa Bwana atautia mkononi mwa mfalme.
1 Rois 18.27 Matthieu 26.45 2 Rois 3.13 Juges 10.14 2 Chroniques 18.14
16 Mfalme akamwambia, Mara ngapi nikuapishe usiniambie neno ila yaliyo kweli, kwa jina la Bwana?
1 Samuel 14.24 Actes 19.13 Matthieu 26.63 Matthieu 22.16-22.17 Jérémie 42.3-42.6
17 Akasema, Naliwaona Waisraeli wote wametawanyika milimani, kama kondoo wasio na mchungaji. Bwana akasema, Hawa hawana bwana; na warudi kila mtu nyumbani kwake kwa amani.
Matthieu 9.36 Nombres 27.17 1 Rois 22.34-22.36 Actes 10.11-10.17 Jérémie 50.6
18 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Je! Sikukuambia, hatanibashiria mema, ila mabaya?
1 Rois 22.8 Proverbes 10.24 Luc 11.45 Proverbes 27.22 Proverbes 29.1
19 Mikaya akasema, Sikia basi neno la Bwana; Nalimwona Bwana ameketi katika kiti chake cha enzi, na jeshi lote la mbinguni wamesimama upande wa mkono wake wa kuume na wa kushoto.
Job 1.6 Daniel 7.9-7.10 Job 2.1 Esaïe 6.1-6.3 Psaumes 103.20-103.21
20 Bwana akasema, Ni nani atakayemdanganya Ahabu, ili akwee Ramoth-Gileadi akaanguke? Basi huyu akasema hivi; na huyu hivi.
Ezéchiel 14.9 Job 12.16 Jérémie 4.10
21 Akatoka pepo, akasimama mbele za Bwana, akasema, Mimi nitamdanganya.
Job 2.1 Job 1.6-1.7 1 Rois 22.23
22 Bwana akamwambia, Jinsi gani? Akasema, Nitaondoka, na kuwa pepo wa uongo kinywani mwa manabii wake wote. Akasema, Utamdanganya, na kudiriki pia; ondoka ukafanye hivyo.
Juges 9.23 Ezéchiel 14.9 Apocalypse 20.10 Actes 5.3-5.4 Apocalypse 12.9-12.10
23 Basi angalia, Bwana ametia pepo wa uongo kinywani mwa manabii wako hawa wote; naye Bwana amenena mabaya juu yako.
Ezéchiel 14.9 Matthieu 13.13-13.15 1 Rois 22.8-22.11 Esaïe 3.11 Nombres 23.19-23.20
24 Ndipo akakaribia Zedekia, mwana wa Kenaana, akampiga Mikaya kofi la shavu, akasema, Roho ya Bwana alitokaje kwangu ili aseme na wewe?
Actes 23.2 Lamentations 3.30 Michée 5.1 Matthieu 5.39 Esaïe 50.5-50.6
25 Mikaya akamwambia, Angalia, utaona siku ile utakapoingia katika chumba cha ndani ili ujifiche.
1 Rois 20.30 Jérémie 28.16-28.17 Amos 7.17 Nombres 31.8 Esaïe 9.14-9.16
26 Mfalme wa Israeli akasema, Mchukueni Mikaya, mkamrudishe kwa Amoni mkuu wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme;
27 mkaseme, Mfalme asema hivi, Mtieni mtu huyu gerezani, mkamlishe kwa chakula cha shida, na maji ya shida, hata nitakaporudi kwa amani.
2 Chroniques 16.10 2 Chroniques 18.25-18.27 Jérémie 29.26 Psaumes 102.9 Psaumes 80.5
28 Mikaya akasema, Ukirudi kabisa kwa amani, Bwana hakusema kwa mimi. Akasema, Sikieni, enyi watu wote.
Michée 1.2 Nombres 16.29 1 Rois 18.36-18.37 Esaïe 44.26 Actes 13.10-13.11
29 Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakakwea mpaka Ramoth-Gileadi.
2 Chroniques 18.28 1 Rois 22.2-22.9
30 Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, Nitajibadilisha, na kuingia vitani; lakini wewe uvae mavazi yako. Mfalme wa Israeli akajibadilisha, akaingia vitani.
2 Chroniques 35.22 Jérémie 23.24 2 Samuel 14.2 Proverbes 21.30 Psaumes 12.2
31 Basi mfalme wa Shamu alikuwa amewaamuru wakuu wa magari yake thelathini na wawili, akisema, Msipigane na mdogo wala mkuu, ila na mfalme wa Israeli peke yake.
1 Rois 20.24 2 Chroniques 18.30 1 Rois 20.1 Genèse 19.11 1 Rois 20.33-20.42
32 Ikawa wakuu wa magari walipomwona Yehoshafati, wakasema, Huyo ndiye mfalme wa Israeli Wakageuka juu yake ili wapigane naye; naye Yehoshafati akapiga ukelele.
Proverbes 13.20 Jonas 2.1-2.2 Psaumes 91.15 Psaumes 130.1-130.4 Psaumes 50.15
33 Ikawa, wakuu wa magari walipoona ya kuwa siye mfalme wa Israeli, wakageuka nyuma wasimfuate.
1 Rois 22.31 Psaumes 76.10
34 Mtu mmoja akavuta upinde kwa kubahatisha, akampiga mfalme wa Israeli mahali pa kuungana mavazi yake ya chuma; kwa hiyo akamwambia mwendesha gari lake, Geuza mkono wako, unichukue kutoka katika majeshi; kwa kuwa nimejeruhiwa sana.
2 Chroniques 35.23 Apocalypse 9.9 Michée 6.13 2 Rois 9.24 2 Samuel 15.11
35 Pigano likazidi siku ile; mfalme akategemezwa garini mwake, kinyume cha Washami, hata jioni akafa; damu ikatoka katika jeraha yake ndani ya gari.
1 Rois 20.42 1 Rois 22.28
36 Ikapigwa mbiu jeshini, jua likichwa, kusema, Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake.
2 Rois 14.12 1 Rois 12.24 Juges 21.24 1 Rois 12.16 2 Samuel 19.8
37 Hivyo akafa mfalme, akachukuliwa Samaria, wakamzika mfalme huko Samaria.
38 Wakaliosha gari penye birika la Samaria, na mbwa wakaramba damu yake; (basi ndipo walipooga makahaba); sawasawa na neno la Bwana alilolinena.
1 Rois 21.19 Matthieu 24.35 Jérémie 44.21-44.23 Josué 23.14-23.15 Zacharie 1.4-1.6
39 Na mambo yote ya Ahabu yaliyosalia, na yote aliyoyafanya, na nyumba ya pembe aliyoijenga, na miji yote aliyoijenga, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Israeli?
Amos 3.15 1 Rois 15.23 Psaumes 45.8 1 Rois 14.19 Ezéchiel 27.6
40 Basi Ahabu akalala na baba zake; na Ahazia mwanawe akatawala mahali pake.
2 Samuel 7.12 1 Rois 14.31 1 Rois 22.51 2 Rois 1.2 2 Chroniques 20.35

Règne de Josaphat sur Juda

41 Yehoshafati mwana wa Asa alianza kutawala juu ya Yuda, katika mwaka wa nne wa Ahabu mfalme wa Israeli.
2 Chroniques 20.31 1 Chroniques 3.10 2 Chroniques 17.1 1 Rois 22.2
42 Yehoshafati alikuwa mwenye miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala; akatawala miaka ishirini na mitano huko Yerusalemu. Na jina la mamaye aliitwa Azuba binti Shilhi.
2 Rois 8.16 1 Rois 15.10 1 Rois 14.21 2 Rois 1.17 1 Rois 15.2
43 Akaiendea njia yote ya Asa babaye; wala hakugeuka, akifanya yaliyo mema machoni pa Bwana. Lakini mahali pa juu hapakuondolewa; watu wakaendelea kutoa dhabihu wakafukiza uvumba katika mahali pa juu.
1 Rois 15.14 2 Rois 12.3 2 Rois 14.3-14.4 Psaumes 101.3 2 Chroniques 19.3-19.4
44 Yehoshafati akafanya amani na mfalme wa Israeli.
2 Chroniques 19.2 1 Rois 22.2 2 Rois 8.18 2 Corinthiens 6.14 2 Chroniques 21.6
45 Na mambo yote ya Yehoshafati yaliyosalia, na uthabiti alioufanya, na jinsi alivyopiga vita, je! Hayakuandikwa katika kitabu-cha-tarehe cha wafalme wa Yuda?
1 Rois 11.41 1 Rois 14.29 2 Chroniques 20.34
46 Tena mahanithi waliosalia, hao waliosalia siku za Asa baba yake, akawaondoa katika nchi.
1 Rois 14.24 1 Rois 15.12 Deutéronome 23.17 Genèse 19.5 Jude 1.7
47 Wala hapakuwa na mfalme katika Edomu; naibu alikuwa ndiye mfalme.
2 Rois 3.9 2 Samuel 8.14 2 Rois 8.20 Genèse 25.23 Genèse 36.31-36.43
48 Yehoshafati akafanya merikebu za Tarshishi ziende Ofiri kuchukua dhahabu; walakini hazikuenda; kwa maana merikebu zilivunjika huko Esion-geberi.
1 Rois 9.26 1 Rois 10.22 1 Rois 9.28 2 Chroniques 20.21 2 Chroniques 9.21
49 Ndipo Ahazia mwana wa Ahabu akamwambia Yehoshafati, Watumishi wangu na waende pamoja na watumishi wako merikebuni. Lakini Yehoshafati hakukubali.
50 Basi Yehoshafati akalala na babaze, akazikwa pamoja na babaze mjini mwa Daudi baba yake; na Yehoramu mwanawe akatawala mahali pake.
2 Chroniques 21.1 1 Rois 11.43 1 Rois 22.40 2 Rois 8.16-8.18 1 Rois 2.10
51 Ahazia mwana wa Ahabu alianza kutawala juu ya Israeli huko Samaria, katika mwaka wa kumi na saba wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, akatawala miaka miwili juu ya Israeli.
2 Rois 1.17 1 Rois 15.25 1 Rois 22.40

Règne d’Achazia sur Israël

52 Akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, akaiendea njia ya babaye, na njia ya mamaye, na njia ya Yeroboamu mwana wa Nebati, aliyewakosesha Israeli.
1 Rois 15.26 1 Rois 21.25 1 Rois 15.34 2 Rois 8.27 2 Rois 3.3
53 Akamtumikia Baali, akamwabudu, akamghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kwa mfano wa mambo yote aliyoyafanya baba yake.
1 Rois 16.30-16.32 1 Rois 21.29 2 Rois 3.2 Juges 2.1-2.11 2 Rois 1.2

Cette Bible est dans le domaine public.