Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Samuel 26.8
Bible en Swahili de l’est


Saül encore épargné par David

1 Basi hao Wazifi wakamwendea Sauli huko Gibea, wakasema, Je! Yule Daudi hakujificha katika kilima cha Hakila, kuelekea Yeshimoni?
1 Samuel 23.19 Psaumes 54.1-54.7 1 Samuel 26.3 Josué 15.55 Josué 15.24
2 Basi Sauli akaondoka, akashuka nyikani kwa Zifu, naye alikuwa na watu elfu tatu, wateule wa Israeli, pamoja naye, ili kumtafuta Daudi katika nyika ya Zifu.
1 Samuel 24.2 1 Samuel 23.23-23.25 1 Samuel 24.17 Psaumes 140.4-140.9 1 Samuel 13.2
3 Naye Sauli akapiga hema katika kilima cha Hakila, kilichoelekea Yeshimoni, barabarani; lakini Daudi alikuwa akikaa nyikani, akaona ya kwamba Sauli amemfuata mpaka nyikani.
1 Samuel 26.1 1 Samuel 23.19
4 Basi Daudi akatuma wapelelezi, akapata habari ya hakika ya kwamba Sauli amefika.
Josué 2.1 Matthieu 10.16
5 Daudi akainuka, akafika mahali pale alipotua Sauli; Daudi akapaangalia mahali alipolala Sauli, na Abneri, mwana wa Neri, jemadari wa jeshi lake; naye Sauli alikuwa amelala kati ya magari, na hao watu wamepiga hema zao wakimzunguka.
1 Samuel 17.55 1 Samuel 14.50-14.51 1 Samuel 17.20 1 Samuel 9.1 2 Samuel 2.8-2.12
6 Ndipo Daudi akajibu, akamwambia Ahimeleki, Mhiti, na Abishai, mwana wa Seruya, ndugu yake Yoabu, akisema, Ni nani atakayeshuka pamoja nami kwa Sauli kambini? Abishai akasema, Mimi nitashuka pamoja nawe.
Juges 7.10-7.11 2 Samuel 2.18 Genèse 10.15 2 Samuel 12.9 2 Samuel 23.18
7 Basi Daudi na Abishai wakawaendea watu usiku; na tazama, Sauli alikuwapo kati ya magari amelala usingizi, na fumo lake limechomekwa chini, karibu na kichwa chake; naye Abneri na watu wake wamelala wakimzunguka.
1 Thessaloniciens 5.2-5.3
8 Ndipo Abishai akamwambia Daudi, Mungu amemtia adui yako mikononi mwako leo; basi, niache nimpige kwa hilo fumo hata nchi kwa pigo moja, sitampiga mara ya pili.
1 Samuel 24.4 1 Samuel 26.23 Deutéronome 32.30 Juges 1.4 1 Samuel 24.18-24.19
9 Lakini Daudi akamwambia Abishai, Usimwangamize; kwani ni nani awezaye kuunyosha mkono wake juu ya masihi
2 Samuel 1.14 2 Samuel 1.16 1 Samuel 24.6-24.7 Psaumes 105.15
10 Daudi akasema, Aishivyo Bwana, Bwana atampiga; au siku yake ya kufa itampata; atashuka kwenda vitani na kupotea.
Deutéronome 31.14 1 Samuel 25.38 Genèse 47.29 Psaumes 37.13 Romains 12.19
11 Hasha! Nisiunyoshe mkono wangu juu ya masihi
1 Samuel 24.6 1 Samuel 24.12 2 Samuel 1.16 2 Samuel 1.14
12 Basi Daudi akalitwaa lile fumo, na lile gudulia la maji, kichwani pa Sauli; nao wakaenda zao, wala hapana mtu aliyeliona jambo hili wala kulijua, wala kuamka; maana wote walikuwa wamelala; kwa kuwa usingizi mzito kutoka kwa Bwana umewaangukia.
Genèse 15.12 Genèse 2.21 Esaïe 29.10 1 Samuel 26.7 1 Samuel 24.4
13 Kisha Daudi akaenda ng’ambo ya pili, akasimama juu ya kilima, mbali sana; palipokuwapo nafasi tele katikati yao;
1 Samuel 24.8 Juges 9.7
14 naye Daudi akawapigia kelele watu wale, na Abneri, mwana wa Neri, akasema, Abneri, hujibu? Ndipo Abneri akajibu, akasema, U nani wewe unayemlilia mfalme?
15 Naye Daudi akamwambia Abneri, Wewe si mtu shujaa? Tena ni nani aliye sawa na wewe katika Israeli? Mbona, basi, hukumlinda bwana wako, huyo mfalme? Kwa maana mtu mmoja aliingia ili amwangamize mfalme, bwana wako?
16 Jambo hili ulilolitenda si jema. Aishivyo Bwana, mmestahili kufa, kwa sababu hamkumlinda bwana wenu, masihi*fq* wa Bwana. Haya basi! Tazameni, liko wapi fumo la mfalme, na gudulia la maji lililokuwa kichwani pake?
1 Samuel 26.11 1 Samuel 20.31 Ephésiens 2.3 2 Samuel 12.5 2 Samuel 19.28
17 Naye Sauli akaitambua sauti ya Daudi, akasema, Hii ndiyo sauti yako, Daudi, mwanangu? Daudi akasema, Ndiyo, ni sauti yangu, bwana wangu, mfalme.
1 Samuel 24.16 1 Samuel 24.8
18 Akasema, Bwana wangu ananiwinda mimi mtumishi wake kwa sababu gani? Nimefanya nini mimi? Ni uovu gani nilio nao mkononi mwangu?
1 Samuel 24.9 1 Samuel 24.11-24.14 Psaumes 69.4 Psaumes 35.7 Jean 8.46
19 Basi sasa, nakusihi, bwana wangu, mfalme, na asikie maneno ya mtumishi wake. Ikiwa ni Bwana aliyekuondokesha juu yangu, na akubali sadaka; bali ikiwa ni wanadamu, na walaaniwe mbele za Bwana; kwa sababu wamenifukuza leo, nisishikamane na urithi wa Bwana, wakisema, Enenda, katumikie miungu mingine.
2 Samuel 14.16 2 Samuel 16.11 Psaumes 120.5 2 Samuel 20.19 Genèse 8.21
20 Basi sasa, isianguke damu yangu chini mbali na uso wa Bwana; maana mfalme wa Israeli ametoka ili kutafuta uhai wangu, kama vile mtu awindavyo kware mlimani.
1 Samuel 24.14 1 Samuel 25.29 Matthieu 26.47 Matthieu 26.55 1 Samuel 2.9
21 Ndipo Sauli akasema, Nimekosa; rudi, Daudi, mwanangu; maana sitakudhuru tena, kwa kuwa maisha yangu yalikuwa na thamani machoni pako leo; angalia, nimetenda upumbavu, nimekosa sana.
1 Samuel 24.17 1 Samuel 15.24 Exode 9.27 1 Samuel 15.30 Matthieu 27.4
22 Daudi akajibu, akasema, Litazame fumo hili, Ee mfalme! Kijana mmoja na avukie huku, alitwae.
23 Naye Bwana atamlipa kila mtu haki yake, na uaminifu wake; maana Bwana amekutia mikononi mwangu leo, nami nalikataa kuunyosha mkono wangu juu ya masihi wa BWANA.
1 Samuel 26.9 Psaumes 62.12 1 Rois 8.32 Néhémie 13.14 Psaumes 7.8-7.9
24 Tena, angalia, kama vile maisha yako yalivyokuwa na thamani machoni pangu, kadhalika na maisha yangu na yawe na thamani machoni pa Bwana, akaniokoe katika shida zote.
Genèse 48.16 Matthieu 5.7 Psaumes 18.1 Matthieu 7.2 2 Corinthiens 1.9-1.10
25 Ndipo Sauli akamwambia Daudi, Ubarikiwe, Daudi, mwanangu; utatenda mambo makuu, tena hakika yako utashinda. Basi, Daudi akaenda zake; Sauli naye akarudi kwao.
Nombres 24.9-24.10 1 Samuel 24.22 1 Samuel 24.19 Genèse 32.28 Proverbes 26.25

Cette Bible est dans le domaine public.