Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Pierre 2.11
Bible en Swahili de l’est


1 Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.
Ephésiens 4.31 Jacques 1.21 Jacques 4.11 1 Pierre 4.2 1 Corinthiens 14.20
2 Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu;
Hébreux 5.12-5.13 Ephésiens 4.15 1 Corinthiens 3.1-3.2 Matthieu 18.3 2 Pierre 3.18
3 ikiwa mmeonja ya kwamba Bwana ni mwenye fadhili.
Psaumes 34.8 Psaumes 9.10 Zacharie 9.17 Psaumes 63.5 Psaumes 24.8

Christ, la pierre angulaire

4 Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima.
1 Pierre 2.7 Actes 4.11-4.12 Psaumes 118.22-118.23 Marc 12.10-12.11 2 Pierre 1.1
5 Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.
Ephésiens 2.20-2.22 1 Pierre 2.9 1 Corinthiens 3.9 Esaïe 61.6 Philippiens 4.18
6 Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika.
Esaïe 28.16 Ephésiens 2.20 Romains 9.32-9.33 1 Pierre 2.4 Zacharie 10.4
7 Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini, Jiwe walilolikataa waashi, Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
Psaumes 118.22-118.23 1 Pierre 2.8 Matthieu 21.42 Actes 4.11-4.12 Marc 12.10-12.11
8 Tena, Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha, Kwa maana hujikwaza kwa neno lile,wasiliamini,nao waliwekwa kusudi wapate hayo.
Esaïe 8.14 Romains 9.22 1 Corinthiens 1.23 Exode 9.16 2 Pierre 2.3
9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;
Exode 19.5-19.6 Deutéronome 7.6 Esaïe 61.6 Apocalypse 1.6 Apocalypse 5.10
10 ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.
Osée 2.23 Osée 1.9-1.10 Romains 9.25-9.26 1 Corinthiens 7.25 Romains 11.6-11.7

Les relations dans le monde

11 Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho.
1 Jean 2.15-2.17 1 Pierre 4.2 Galates 5.24 Romains 8.13 2 Timothée 2.22
12 Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.
Matthieu 5.16 1 Pierre 3.16 Philippiens 2.15-2.16 2 Corinthiens 8.21 Philippiens 1.27
13 Tiini kila kiamriwacho na watu, kwa ajili ya Bwana; ikiwa ni mfalme, kama mwenye cheo kikubwa;
Tite 3.1 Romains 13.1-13.7 1 Timothée 2.1-2.2 Luc 20.25 2 Pierre 2.10
14 ikiwa ni wakubwa, kama wanaotumwa naye ili kuwalipiza kisasi watenda mabaya na kuwasifu watenda mema.
Romains 13.3-13.4
15 Kwa sababu ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba kwa kutenda mema mzibe vinywa vya ujinga vya watu wapumbavu;
1 Pierre 2.12 1 Thessaloniciens 4.3 1 Pierre 3.17 Tite 2.8 1 Thessaloniciens 5.18
16 kama walio huru, ila wasioutumia uhuru huo kwa kusitiri ubaya, bali kama watumwa wa Mungu.
Romains 6.22 1 Corinthiens 7.22 Jacques 1.25 Galates 5.13 1 Thessaloniciens 2.5
17 Waheshimuni watu wote. Wapendeni ndugu. Mcheni Mungu. Mpeni heshima mfalme.
Proverbes 24.21 Romains 13.7 Romains 12.10 1 Samuel 15.30 1 Pierre 1.22
18 Enyi watumishi, watiini bwana zenu kwa hofu nyingi, sio wao walio wema na wenye upole tu, bali nao walio wakali.
Tite 2.9-2.10 1 Timothée 6.1-6.3 Colossiens 3.22-3.25 Ephésiens 6.5-6.7 Jacques 3.17
19 Maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki.
Romains 13.5 Luc 6.32 Matthieu 5.10-5.12 Psaumes 69.4 Psaumes 119.86
20 Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu.
1 Pierre 2.19 1 Pierre 3.17 Matthieu 26.67 Romains 12.1-12.2 Luc 6.32
21 Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.
1 Jean 2.6 Matthieu 16.24 Actes 14.22 1 Pierre 3.18 Ephésiens 5.2
22 Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.
Esaïe 53.9 2 Corinthiens 5.21 1 Jean 3.5 Hébreux 4.15 Hébreux 9.28
23 Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki.
Hébreux 12.3 Esaïe 53.7 Luc 23.46 Psaumes 37.5 2 Timothée 1.12
24 Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa.
Esaïe 53.4-53.6 Romains 6.11 Matthieu 8.17 Romains 6.2 Hébreux 9.28
25 Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu.
Ezéchiel 34.6 Esaïe 53.6 Esaïe 40.11 Luc 15.4-15.6 1 Pierre 5.4

Cette Bible est dans le domaine public.