Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

1 Pierre 2.1
Bible en Swahili de l’est


1 Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote.
Ephésiens 4.31 Jacques 1.21 Jacques 4.11 Colossiens 3.5-3.8 1 Pierre 4.2
2 Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu;
Hébreux 5.12-5.13 Ephésiens 4.15 1 Corinthiens 3.1-3.2 Matthieu 18.3 1 Corinthiens 14.20
3 ikiwa mmeonja ya kwamba Bwana ni mwenye fadhili.
Psaumes 34.8 Cantique 2.3 Psaumes 9.10 Zacharie 9.17 Psaumes 63.5

Christ, la pierre angulaire

4 Mmwendee yeye, jiwe lililo hai, lililokataliwa na wanadamu, bali kwa Mungu ni teule, lenye heshima.
1 Pierre 2.7 Actes 4.11-4.12 Psaumes 118.22-118.23 Jean 6.57 Zacharie 4.7
5 Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa mwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.
Ephésiens 2.20-2.22 1 Pierre 2.9 1 Corinthiens 3.9 Esaïe 61.6 Philippiens 4.18
6 Kwa kuwa imeandikwa katika maandiko Tazama, naweka katika Sayuni jiwe kuu la pembeni, teule, lenye heshima, Na kila amwaminiye hatatahayarika.
Esaïe 28.16 Ephésiens 2.20 Romains 9.32-9.33 1 Pierre 2.4 Zacharie 10.4
7 Basi, heshima hii ni kwenu ninyi mnaoamini. Bali kwao wasioamini, Jiwe walilolikataa waashi, Limekuwa jiwe kuu la pembeni.
Psaumes 118.22-118.23 1 Pierre 2.8 Marc 12.10-12.11 Matthieu 21.42 Actes 4.11-4.12
8 Tena, Jiwe la kujikwaza mguu, na mwamba wa kuangusha, Kwa maana hujikwaza kwa neno lile,wasiliamini,nao waliwekwa kusudi wapate hayo.
Esaïe 8.14 Romains 9.22 1 Corinthiens 1.23 Romains 9.32-9.33 Exode 9.16
9 Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu;
Exode 19.5-19.6 Deutéronome 7.6 Esaïe 61.6 Apocalypse 1.6 Apocalypse 5.10
10 ninyi mliokuwa kwanza si taifa, bali sasa ni taifa la Mungu; mliokuwa hamkupata rehema, bali sasa mmepata rehema.
Osée 1.9-1.10 Osée 2.23 Romains 9.25-9.26 1 Corinthiens 7.25 Romains 11.6-11.7

Les relations dans le monde

11 Wapenzi, nawasihi kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho.
1 Jean 2.15-2.17 1 Pierre 4.2 Galates 5.24 Hébreux 11.13 Romains 8.13
12 Mwe na mwenendo mzuri kati ya Mataifa, ili, iwapo huwasingizia kuwa watenda mabaya, wayatazamapo matendo yenu mazuri, wamtukuze Mungu siku ya kujiliwa.
Matthieu 5.16 1 Pierre 3.16 Philippiens 2.15-2.16 2 Corinthiens 8.21 Philippiens 1.27
13 Tiini kila kiamriwacho na watu, kwa ajili ya Bwana; ikiwa ni mfalme, kama mwenye cheo kikubwa;
Tite 3.1 Romains 13.1-13.7 1 Timothée 2.1-2.2 Luc 20.25 2 Pierre 2.10
14 ikiwa ni wakubwa, kama wanaotumwa naye ili kuwalipiza kisasi watenda mabaya na kuwasifu watenda mema.
Romains 13.3-13.4
15 Kwa sababu ndiyo mapenzi ya Mungu, kwamba kwa kutenda mema mzibe vinywa vya ujinga vya watu wapumbavu;
1 Thessaloniciens 4.3 1 Pierre 2.12 1 Thessaloniciens 5.18 1 Pierre 3.17 Tite 2.8
16 kama walio huru, ila wasioutumia uhuru huo kwa kusitiri ubaya, bali kama watumwa wa Mungu.
Romains 6.22 1 Corinthiens 7.22 Jacques 1.25 Galates 5.13 Ephésiens 6.6
17 Waheshimuni watu wote. Wapendeni ndugu. Mcheni Mungu. Mpeni heshima mfalme.
Proverbes 24.21 Romains 13.7 Romains 12.10 1 Samuel 15.30 1 Pierre 1.22
18 Enyi watumishi, watiini bwana zenu kwa hofu nyingi, sio wao walio wema na wenye upole tu, bali nao walio wakali.
Tite 2.9-2.10 1 Timothée 6.1-6.3 Colossiens 3.22-3.25 Ephésiens 6.5-6.7 Jacques 3.17
19 Maana huu ndio wema hasa, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo isivyo haki.
Romains 13.5 2 Corinthiens 1.12 1 Pierre 3.14-3.17 Luc 6.32 Matthieu 5.10-5.12
20 Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, huu ndio wema hasa mbele za Mungu.
1 Pierre 2.19 1 Pierre 3.17 Matthieu 26.67 Matthieu 5.10-5.12 Romains 12.1-12.2
21 Kwa sababu ndio mlioitiwa; maana Kristo naye aliteswa kwa ajili yenu, akawaachia kielelezo, mfuate nyayo zake.
1 Jean 2.6 Matthieu 16.24 Actes 14.22 1 Pierre 3.18 Jean 13.15
22 Yeye hakutenda dhambi, wala hila haikuonekana kinywani mwake.
Esaïe 53.9 2 Corinthiens 5.21 1 Jean 3.5 Hébreux 4.15 Luc 23.41
23 Yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa, hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki.
Hébreux 12.3 Esaïe 53.7 Luc 23.46 Psaumes 37.5 Psaumes 10.14
24 Yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; na kwa kupigwa kwake mliponywa.
Esaïe 53.4-53.6 Romains 6.11 Matthieu 8.17 Romains 6.2 Hébreux 9.28
25 Kwa maana mlikuwa mnapotea kama kondoo; lakini sasa mmemrudia Mchungaji na Mwangalizi wa roho zenu.
Ezéchiel 34.6 Esaïe 53.6 Esaïe 40.11 Luc 15.4-15.6 Actes 20.28

Cette Bible est dans le domaine public.