Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Hébreux 10.15
Bible en Swahili de l’est


Le sacrifice de la nouvelle alliance

1 Basi torati, kwa kuwa ni kivuli cha mema yatakayokuwa, wala si sura yenyewe ya mambo hayo, kwa dhabihu zile zile wanazozitoa kila mwaka daima, haiwezi wakati wo wote kuwakamilisha wakaribiao.
Hébreux 8.5 Colossiens 2.17 Hébreux 9.11 Hébreux 7.18-7.19 Hébreux 9.23
2 Kama ndivyo, je! Dhabihu hazingekoma kutolewa; kwa maana waabuduo, wakiisha kusafishwa mara moja, wasingejiona tena kuwa na dhambi?
Esaïe 43.25 Esaïe 44.22 Michée 7.19 Psaumes 103.12 Hébreux 10.17
3 Lakini katika dhabihu hizo liko kumbukumbu la dhambi kila mwaka.
Hébreux 9.7 Lévitique 16.6-16.11 Exode 30.10 Matthieu 26.28 Lévitique 23.27-23.28
4 Maana haiwezekani damu ya mafahali na mbuzi kuondoa dhambi.
Hébreux 10.11 Hébreux 9.9 Michée 6.6-6.8 Romains 11.27 Hébreux 10.8
5 Kwa hiyo ajapo ulimwenguni, asema, Dhabihu na toleo hukutaka, Lakini mwili uliniwekea tayari;
Psaumes 40.6-40.8 Hébreux 1.6 Esaïe 1.11 Esaïe 7.14 Luc 1.35
6 Sadaka za kuteketezwa na sadaka za dhambi hukupendezwa nazo;
Lévitique 1.1-1.6 Malachie 1.10 Hébreux 10.4 Matthieu 3.17 Ephésiens 5.2
7 Ndipo niliposema, Tazama, nimekuja (katika gombo la chuo nimeandikiwa) Niyafanye mapenzi yako, Mungu.
Psaumes 40.7-40.8 Jean 4.34 Hébreux 10.9-10.10 Jean 6.38 Proverbes 8.31
8 Hapo juu asemapo, Dhabihu na matoleo na sadaka za kuteketezwa na hizo za dhambi hukuzitaka, wala hukupendezwa nazo (zitolewazo kama ilivyoamuru torati),
Hébreux 10.5 Marc 12.33
9 ndipo aliposema, Tazama, nimekuja niyafanye mapenzi yako. Aondoa la kwanza, ili kusudi alisimamishe la pili.
Hébreux 10.7 Hébreux 12.27-12.28 Hébreux 9.11-9.14 Hébreux 7.18-7.19 Hébreux 8.7-8.13
10 Katika mapenzi hayo mmepata utakaso, kwa kutolewa mwili wa Yesu Kristo mara moja tu.
Hébreux 7.27 Hébreux 13.12 Hébreux 10.14 Hébreux 10.12 Hébreux 9.28
11 Na kila kuhani husimama kila siku akifanya ibada, na kutoa dhabihu zile zile mara nyingi; ambazo haziwezi kabisa kuondoa dhambi.
Hébreux 10.4 Hébreux 5.1 Nombres 28.3 Ezéchiel 45.4 Esaïe 1.11
12 Lakini huyu, alipokwisha kutoa kwa ajili ya dhambi dhabihu moja idumuyo hata milele, aliketi mkono wa kuume wa Mungu;
Hébreux 1.3 Hébreux 9.12 Actes 2.33-2.34 Romains 8.34 Colossiens 3.1
13 tangu hapo akingojea hata adui zake wawekwe kuwa chini ya miguu yake.
Hébreux 1.13 Psaumes 110.1 Luc 20.43 1 Corinthiens 15.25 Actes 2.35
14 Maana kwa toleo moja amewakamilisha hata milele hao wanaotakaswa.
Hébreux 10.1 Romains 15.16 Hébreux 7.25 Jude 1.1 Actes 26.13
15 Na Roho Mtakatifu naye amshuhudia; kwa maana, baada ya kusema,
Hébreux 3.7 Apocalypse 2.17 Apocalypse 2.7 Hébreux 9.8 Jean 15.26
16 Hili ni agano nitakaloagana nao baada ya siku zile, anena Bwana, Nitatia sheria zangu mioyoni mwao, Na katika nia zao nitaziandika; ndipo anenapo,
Hébreux 8.8-8.12 Jérémie 31.33-31.34 Romains 11.27
17 Dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kabisa.
Hébreux 8.12 Jérémie 31.34
18 Basi, ondoleo la hayo likiwapo, hapana toleo tena kwa ajili ya dhambi.
Hébreux 10.14 Hébreux 10.2
19 Basi, ndugu, kwa kuwa tuna ujasiri wa kupaingia patakatifu kwa damu ya Yesu,
Hébreux 4.16 Ephésiens 2.18 Hébreux 9.12 Romains 8.15 Hébreux 9.3
20 njia ile aliyotuanzia iliyo mpya, iliyo hai, ipitayo katika pazia, yaani, mwili wake;
Hébreux 9.3 Jean 14.6 Hébreux 9.8 Hébreux 6.19 Jean 10.9
21 na kuwa na kuhani mkuu juu ya nyumba ya Mungu;
Hébreux 2.17 1 Timothée 3.15 Hébreux 3.1 Hébreux 7.26 Hébreux 3.3-3.6
22 na tukaribie wenye moyo wa kweli, kwa utimilifu wa imani, hali tumenyunyiziwa mioyo tuache dhamiri mbaya, tumeoshwa miili kwa maji safi.
Ezéchiel 36.25 1 Corinthiens 6.11 Hébreux 7.19 Ephésiens 5.26 2 Corinthiens 7.1

Persévérance dans la foi

Persévérer dans l’espérance

23 Na mlishike sana ungamo la tumaini letu, lisigeuke; maana yeye aliyeahidi ni mwaminifu;
1 Corinthiens 1.9 Hébreux 3.6 1 Corinthiens 10.13 1 Thessaloniciens 5.24 Hébreux 11.11
24 tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri;
1 Thessaloniciens 5.11 Hébreux 13.1 1 Jean 3.18 Galates 5.13 Colossiens 3.16
25 wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.
Actes 2.42 Hébreux 3.13 Matthieu 18.20 1 Thessaloniciens 5.11 Hébreux 10.24
26 Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi;
2 Pierre 2.20-2.22 Jean 9.41 Hébreux 6.4-6.6 Luc 12.47 1 Jean 5.16
27 bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao.
Esaïe 26.11 Sophonie 1.18 Hébreux 12.25 Ezéchiel 36.5 Sophonie 3.8
28 Mtu aliyeidharau sheria ya Musa hufa pasipo huruma, kwa neno la mashahidi wawili au watatu.
Hébreux 2.2 Matthieu 18.16 Jean 8.17 Deutéronome 19.15 Romains 9.15
29 Mwaonaje? Haikumpasa adhabu iliyo kubwa zaidi mtu yule aliyemkanyaga Mwana wa Mungu, na kuihesabu damu ya agano aliyotakaswa kwayo kuwa ni kitu ovyo, na kumfanyia jeuri Roho wa neema?
Ephésiens 4.30 Hébreux 6.6 Hébreux 13.20 Hébreux 9.13 Hébreux 2.3
30 Maana twamjua yeye aliyesema, Kupatiliza kisasi ni juu yangu, mimi nitalipa. Na tena, Bwana atawahukumu watu wake.
Deutéronome 32.35-32.36 Romains 12.19 Psaumes 135.14 Psaumes 50.4 Nahum 1.2
31 Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai.
Matthieu 10.28 Esaïe 33.14 Hébreux 12.29 Luc 12.5 Matthieu 16.16
32 Lakini zikumbukeni siku za kwanza, ambazo, mlipokwisha kutiwa nuru, mlistahimili mashindano makubwa ya maumivu;
Hébreux 6.4 Galates 3.3-3.4 Philippiens 1.29-1.30 Apocalypse 3.3 Philippiens 3.16
33 pindi mlipotwezwa kwa mashutumu na dhiki, na pindi mliposhirikiana na wale waliotendewa hayo.
1 Corinthiens 4.9 Philippiens 4.14 1 Thessaloniciens 2.14 Psaumes 69.9 Hébreux 11.26
34 Maana mliwaonea huruma wale waliokuwa katika vifungo, tena mkakubali kwa furaha kunyang’anywa mali zenu, mkijua kwamba nafsini mwenu mna mali iliyo njema zaidi, idumuyo.
1 Pierre 1.4 Hébreux 13.3 2 Timothée 1.16 2 Timothée 4.8 Ephésiens 3.1
35 Basi msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kuu.
Galates 6.8-6.10 Hébreux 3.6 Hébreux 11.26 Hébreux 2.2 Matthieu 5.12
36 Maana mnahitaji saburi, ili kwamba mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu mpate ile ahadi.
Luc 21.19 Hébreux 12.1 Hébreux 6.15 Matthieu 10.22 1 Jean 2.17
37 Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia.
Habakuk 2.3-2.4 Esaïe 26.20 Apocalypse 22.20 Luc 18.8 Jacques 5.7-5.9
38 Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye.
Romains 1.17 Galates 3.11 Hébreux 6.4-6.6 2 Pierre 2.19-2.22 Habakuk 2.4
39 Lakini sisi hatumo miongoni mwao wasitao na kupotea, bali tumo miongoni mwa hao walio na imani ya kutuokoa roho zetu.
1 Jean 5.16 Luc 11.26 1 Samuel 15.11 1 Thessaloniciens 5.9 1 Jean 5.5

Cette Bible est dans le domaine public.