Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 28
Bible en Swahili de l’est


Sur l’île de Malte

1 Tulipokwisha kuokoka, ndipo tulipojua ya kuwa kisiwa kile chaitwa Melita.
Actes 27.26 Actes 27.39 Actes 27.44 Actes 16.10
2 Wenyeji wakatufanyia fadhili zisizokuwa za kawaida. Kwa maana waliwasha moto, wakatukaribisha sote, kwa sababu ya mvua iliyonyesha na kwa sababu ya baridi.
Romains 1.14 1 Corinthiens 14.11 Colossiens 3.11 Actes 28.4 Actes 27.3
3 Paulo alipokuwa amekusanya mzigo wa kuni, na kuuweka motoni, nyoka akatoka kwa ajili ya ule moto akamzonga-zonga mkononi.
Actes 28.4 Matthieu 3.7 Matthieu 12.34 Esaïe 30.6 2 Corinthiens 6.9
4 Wenyeji walipomwona yule nyoka akilewa-lewa mkononi, wakaambiana, Hakosi mtu huyu ni mwuaji; ambaye ijapokuwa ameokoka katika bahari haki haimwachi kuishi.
Luc 13.2 Luc 13.4 Matthieu 23.35 Jean 9.1-9.2 Matthieu 27.25
5 Lakini yeye akamtukusia motoni asipate madhara.
Luc 10.19 Marc 16.18 Psaumes 91.13 Romains 16.20 Jean 3.14-3.15
6 Wao wakadhani ya kuwa atavimba au kuanguka chini kwa kufa ghafula; na wakiisha kumwangalia sana, na kuona kwamba halimpati dhara lo lote, wakageuka, wakasema kwamba yeye ni mungu.
Matthieu 21.9 Matthieu 27.22 Actes 14.11-14.13 Actes 12.22
7 Karibu na mahali pale palikuwa na mashamba ya mkuu wa kisiwa, jina lake Publio; mtu huyu akatukaribisha kwa moyo wa urafiki, akatufanya wageni wake kwa muda wa siku tatu.
Actes 23.24 Matthieu 10.40-10.41 Actes 18.12 Actes 13.7 Actes 28.2
8 Ikawa babaake Publio alikuwa hawezi homa na kuhara damu. Paulo akaingia kwake, akaomba, akaweka mikono yake juu yake, na kumpoza.
Actes 9.40 Marc 6.5 Matthieu 9.18 1 Rois 17.20-17.22 Marc 16.18
9 Yalipokwisha kutendeka hayo wengine waliokuwa na magonjwa katika kisiwa wakaja wakapozwa;
Actes 5.15 Marc 6.54-6.56 Actes 5.12 Matthieu 4.24
10 nao wakatuheshimu kwa heshima nyingi; basi tulipoabiri wakatupakilia vitu vile tulivyokuwa na haja navyo.
Philippiens 4.11-4.12 2 Corinthiens 8.2-8.6 Matthieu 15.5-15.6 Philippiens 4.19 1 Timothée 5.3-5.4

L’Évangile à Rome

11 Baada ya miezi mitatu tukasafiri katika merikebu ya Iskanderia iliyokuwa imekaa pale kisiwani wakati wa baridi; na alama yake ni Ndugu Pacha.
Actes 27.6 Actes 6.9 Jonas 1.5 Esaïe 45.20 Jonas 1.16
12 Tukafika Sirakusa, tukakaa siku tatu.
13 Kutoka huko tukazunguka tukafikia Regio; baada ya siku moja upepo wa kusi ukavuma, na siku ya pili tukawasili Puteoli.
Actes 27.13
14 Huko tukakuta ndugu, wakatusihi tukae nao siku saba; na hivi tukafika Rumi.
Actes 20.6 Jean 21.23 Genèse 7.4 Psaumes 119.63 Actes 21.4
15 Na kutoka huko ndugu, waliposikia habari zetu, wakaja kutulaki mpaka Soko la Apio na Mikahawa Mitatu. Paulo alipowaona alimshukuru Mungu, akachangamka.
Galates 4.14 1 Corinthiens 12.21-12.22 Actes 21.5 Josué 1.9 1 Samuel 30.6
16 Tulipoingia Rumi Paulo alipewa ruhusa kukaa kwake mwenyewe pamoja na askari aliyemlinda.
Actes 27.3 Actes 24.23 Romains 15.22-15.29 Actes 19.21 Actes 27.43
17 Ikawa baada ya siku tatu akawaita wakuu wa Wayahudi wakutane, hata walipokutanika akawaambia, Ndugu zangu, ningawa sikufanya neno kinyume cha watu wetu wala neno lililopingamana na desturi za baba zetu, nalitiwa katika mikono ya Warumi, hali nimefungwa, tokea Yerusalemu.
Actes 25.8 Actes 24.10-24.16 Actes 6.14 Actes 21.33-21.40 Actes 25.10
18 Na hao walipokwisha kuniuliza-uliza walitaka kunifungua, kwa maana hapakuwa na sababu yo yote kwangu ya kuuawa.
Actes 26.31-26.32 Actes 24.22 Actes 25.7-25.8 Actes 23.29 Actes 22.30
19 Lakini Wayahudi walipotoa hoja juu ya shauri hili nalishurutishwa kutaka rufani kwa Kaisari. Si kwamba nalikuwa na neno la kuwashitaki watu wa taifa langu.
Actes 26.32 Actes 25.21 Actes 25.25 1 Pierre 2.22-2.23 Actes 25.10-25.12
20 Basi kwa ajili ya hayo, nimewaita mje kunitazama na kusema nami; kwa maana nimefungwa kwa mnyororo huu kwa ajili ya tumaini la Israeli.
Ephésiens 6.20 Actes 26.6-26.7 Actes 26.29 Actes 23.6 Actes 21.33
21 Wale wakamwambia, Sisi hatukupata nyaraka zenye habari zako kutoka Uyahudi, wala hapana ndugu hata mmoja aliyefika hapa na kutupasha habari, au kunena neno baya juu yako.
Actes 22.5 Esaïe 41.11 Esaïe 54.17 Exode 11.7 Esaïe 50.8
22 Lakini tunataka kusikia kwako uonavyo wewe; kwa maana katika habari za madhehebu hiyo imejulikana kwetu kwamba inanenwa vibaya kila mahali.
1 Pierre 2.12 Actes 24.14 1 Pierre 3.16 Actes 17.6-17.7 Luc 2.34
23 Wakiisha kuagana naye siku, wakamjia katika nyumba aliyokaa, watu wengi sana, akawaeleza kwa taratibu na kuushuhudia ufalme wa Mungu, akiwaonya mambo yake Yesu, kwa maneno ya sheria ya Musa na ya manabii, tangu asubuhi hata jioni.
Actes 19.8 Actes 17.2-17.3 Luc 24.26-24.27 Actes 8.35 Jean 4.34
24 Wengine waliamini yale yaliyonenwa, wengine hawakuyaamini.
Actes 14.4 Actes 17.4-17.5 Romains 3.3 Romains 11.4-11.6 Actes 13.48-13.50
25 Na walipokuwa hawapatani wao kwa wao, wakaenda zao, Paulo alipokwisha kusema neno hili moja, ya kwamba, Roho Mtakatifu alinena vema na baba zetu, kwa kinywa cha nabii Isaya,
Matthieu 15.7 Marc 7.6 2 Pierre 1.21
26 akisema, Enenda kwa watu hawa, ukawaambie, Kusikia, mtasikia wala hamtafahamu; Na kuona, mtaona wala hamtatambua;
Esaïe 6.9-6.10 Esaïe 42.19-42.20 Ezéchiel 12.2 Matthieu 13.14-13.15 Marc 4.12
27 Kwa maana mioyo ya watu hawa imepumbaa, Na masikio yao ni mazito ya kusikia, Na macho yao wameyafumba; Wasije wakaona kwa macho yao, Na kusikia kwa masikio yao, Na kufahamu kwa mioyo yao, Na kubadili nia zao, nikawaponya.
Esaïe 6.10
28 Basi ijulikane kwenu ya kwamba wokovu huu wa Mungu umepelekwa kwa Mataifa, nao watasikia!
Actes 26.17-26.18 Luc 3.6 Actes 11.18 Actes 22.21 Luc 2.30-2.32
29 Alipokwisha kusema hayo, Wayahudi wakaenda zao, wakiulizana mengi wao kwa wao.]
30 Akakaa muda wa miaka miwili mizima katika nyumba yake aliyokuwa ameipanga, akawakaribisha watu wote waliokuwa wakimwendea,
31 akihubiri habari za ufalme wa Mungu, na kuyafundisha mambo ya Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri mwingi, asikatazwe na mtu.
Actes 28.23 Matthieu 4.23 Actes 4.29 Actes 20.25 Actes 8.12

Cette Bible est dans le domaine public.