Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Jean 10.25
Bible en Swahili de l’est


Jésus, le bon berger

1 Yesu aliwaambia, Amin, amin, nawaambieni, Yeye asiyeingia mlangoni katika zizi la kondoo, lakini akwea penginepo, huyo ni mwivi naye ni mnyang’anyi.
1 Jean 4.1 Romains 16.18 Hébreux 5.4 Jean 10.8-10.10 Matthieu 7.15
2 Aingiaye mlangoni ni mchungaji wa kondoo.
Jean 10.14 Actes 20.28 1 Pierre 5.4 Jean 10.11-10.12 Jean 10.7
3 Bawabu humfungulia huyo, na kondoo humsikia sauti yake; naye huwaita kondoo wake kwa majina yao, na kuwapeleka nje.
Jean 10.16 Jean 10.4 Jean 10.14 Esaïe 42.16 Psaumes 23.2-23.3
4 Naye awatoapo nje kondoo wake wote, huwatangulia; na wale kondoo humfuata, kwa maana waijua sauti yake.
Jean 10.16 1 Corinthiens 11.1 Jean 18.37 Jean 12.26 Deutéronome 1.30
5 Mgeni hawatamfuata kabisa, bali watamkimbia; kwa maana hawazijui sauti za wageni.
1 Jean 4.5-4.6 1 Jean 2.21 Ephésiens 4.11-4.15 Marc 4.24 Colossiens 2.6-2.10
6 Mithali hiyo Yesu aliwaambia, lakini wao hawakuelewa na mambo hayo aliyowaambia.
Jean 16.25 Esaïe 6.9-6.10 Matthieu 13.51 Psaumes 106.7 Daniel 12.10
7 Basi Yesu aliwaambia tena, Amin, amin, nawaambieni, Mimi ndimi mlango wa kondoo.
Jean 14.6 Jean 10.9 Ephésiens 2.18 Jean 10.1 Hébreux 10.19-10.22
8 Wote walionitangulia ni wevi na wanyang’anyi; lakini kondoo hawakuwasikia.
Ezéchiel 34.2 Ezéchiel 22.25-22.28 Jean 10.1 Zacharie 11.4-11.9 Zacharie 11.16
9 Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.
Jean 14.6 Ephésiens 2.18 Jean 10.1 Psaumes 23.1-23.6 Romains 5.1-5.2
10 Mwivi haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele.
Luc 19.10 Jean 6.51 Jean 12.47 Jean 3.17 Jean 6.33
11 Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
Esaïe 40.11 Jean 15.13 Ezéchiel 34.23 1 Pierre 5.4 Hébreux 13.20
12 Mtu wa mshahara, wala si mchungaji, ambaye kondoo si mali yake, humwona mbwa-mwitu anakuja, akawaacha kondoo na kukimbia; na mbwa-mwitu huwakamata na kuwatawanya.
2 Pierre 2.3 Ezéchiel 34.2-34.6 Zacharie 11.16-11.17 Esaïe 56.10-56.12 Matthieu 10.16
13 Yule hukimbia kwa kuwa ni mtu wa mshahara; wala mambo ya kondoo si kitu kwake.
Actes 18.17 Jean 12.6 Philippiens 2.20
14 Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi;
Jean 10.27 Esaïe 53.11 2 Timothée 2.19 Psaumes 1.6 1 Jean 5.20
15 kama vile Baba anijuavyo, nami nimjuavyo Baba. Nami nautoa uhai wangu kwa ajili ya kondoo.
Jean 10.11 Matthieu 11.27 Esaïe 53.10 Matthieu 20.28 1 Pierre 3.18
16 Na kondoo wengine ninao, ambao si wa zizi hili; na hao nao imenipasa kuwaleta; na sauti yangu wataisikia; kisha kutakuwako kundi moja na mchungaji mmoja.
Esaïe 56.8 1 Pierre 2.25 Ezéchiel 34.23 Jean 11.52 Ephésiens 2.13-2.18
17 Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena.
Jean 10.11 Hébreux 2.9 Jean 10.18 Jean 10.15 Esaïe 53.7-53.12
18 Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu.
Hébreux 2.9 Jean 10.17 Jean 14.31 Jean 15.10 Jean 6.38
19 Kukaingia tena matengano kati ya Wayahudi, kwa ajili ya maneno hayo.
Jean 9.16 Actes 14.4 Jean 7.40-7.43 Matthieu 10.34-10.35 Actes 23.7-23.10
20 Wengi wao wakasema, Ana pepo huyu, tena ana wazimu; mbona mnamsikiliza?
Marc 3.21 Jean 7.20 Jean 7.46-7.52 Matthieu 10.25 Actes 18.14-18.15
21 Wengine wakasema, Maneno hayo siyo ya mtu mwenye pepo. Je! Pepo aweza kuwafumbua macho vipofu?
Exode 4.11 Psaumes 146.8 Matthieu 4.24 Jean 9.6 Proverbes 20.12
22 Basi huko Yerusalemu ilikuwa Sikukuu ya Kutabaruku; ni wakati wa baridi.
23 Naye Yesu alikuwa akitembea hekaluni, katika ukumbi wa Sulemani.
Actes 3.11 Actes 5.12
24 Basi Wayahudi walimzunguka, wakamwambia, Hata lini utatuhangaisha nafsi zetu? Kama wewe ndiwe Kristo, utuambie waziwazi.
Matthieu 11.3 Jean 1.19 Luc 22.67-22.70 Jean 8.25 Luc 3.15
25 Yesu akawajibu, Naliwaambia, lakini ninyi hamsadiki. Kazi hizi ninazozifanya kwa jina la Baba yangu ndizo zinazonishuhudia.
Jean 10.38 Jean 8.58 Jean 5.17-5.43 Jean 8.12 Jean 11.47
26 Lakini ninyi hamsadiki, kwa sababu hammo miongoni mwa kondoo wangu.
Jean 8.47 Romains 11.7-11.8 2 Corinthiens 4.3-4.4 Jean 10.4 1 Jean 4.6
27 Kondoo wangu waisikia sauti yangu; nami nawajua, nao wanifuata.
Jean 10.14 Jean 10.16 Jean 10.3-10.4 Apocalypse 3.20 Galates 4.9
28 Nami nawapa uzima wa milele; wala hawatapotea kamwe; wala hakuna mtu atakayewapokonya katika mkono wangu.
Jean 6.39-6.40 Jean 6.37 Jean 18.9 Jean 17.2 Hébreux 7.25
29 Baba yangu aliyenipa hao ni mkuu kuliko wote; wala hakuna mtu awezaye kuwapokonya katika mkono wa Baba yangu.
Jean 14.28 Jean 6.37 Jean 17.2 Exode 18.11 Jean 17.6
30 Mimi na Baba tu umoja.
Matthieu 28.19 Tite 2.13 Jean 1.1-1.2 1 Timothée 3.16 Jean 14.9
31 Basi Wayahudi wakaokota mawe tena ili wampige.
Jean 8.59 Jean 5.18 Actes 7.52 Matthieu 23.35 Exode 17.4
32 Yesu akawajibu, Kazi njema nyingi nimewaonyesha, zitokazo kwa Baba; kwa ajili ya kazi ipi katika hizo mnanipiga kwa mawe?
2 Chroniques 24.20-24.22 Actes 10.38 Psaumes 35.12 Jean 10.37 Jean 5.36
33 Wayahudi wakamjibu, Kwa ajili ya kazi njema hatukupigi kwa mawe; bali kwa kukufuru, na kwa sababu wewe uliye mwanadamu wajifanya mwenyewe u Mungu.
Jean 5.18 Lévitique 24.16 Jean 10.30 1 Rois 21.10 Philippiens 2.6
34 Yesu akawajibu, Je! Haikuandikwa katika torati yenu ya kwamba, Mimi nimesema, Ndinyi miungu?
Psaumes 82.6-82.7 Psaumes 138.1 Exode 7.1 Psaumes 82.1 Jean 15.25
35 Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiliwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka);
Jean 19.28 Deutéronome 18.18-18.20 1 Samuel 15.1 2 Samuel 7.5 Jean 12.38-12.39
36 je! Yeye ambaye Baba alimtakasa, akamtuma ulimwenguni, ninyi mnamwambia, Unakufuru; kwa sababu nalisema, Mimi ni Mwana wa Mungu?
Jean 3.17 Jérémie 1.5 Jean 5.17-5.18 Jean 6.27 Jean 19.7
37 Kama sizitendi kazi za Baba yangu, msiniamini;
Jean 15.24 Jean 10.25 Jean 10.32 Jean 12.37-12.40 Jean 5.31
38 lakini nikizitenda, ijapokuwa hamniamini mimi, ziaminini zile kazi; mpate kujua na kufahamu ya kuwa Baba yu ndani yangu, nami ni ndani ya Baba.
Jean 14.20 Jean 17.21-17.23 Jean 10.25 Jean 3.2 Jean 5.36
39 Wakatafuta tena kumkamata; lakini akatoka mikononi mwao.
Jean 7.30 Jean 8.59 Jean 7.44 Luc 4.29-4.30 Jean 10.31
40 Akaenda zake tena ng’ambo ya Yordani, mpaka mahali pale alipokuwapo Yohana akibatiza hapo kwanza, akakaa huko.
Jean 1.28 Jean 11.54 Jean 7.1 Jean 3.26
41 Na watu wengi wakamwendea, wakasema, Yohana kweli hakufanya ishara yo yote, lakini yote aliyoyasema Yohana katika habari zake huyu yalikuwa kweli.
Jean 1.29-1.30 Jean 1.33-1.34 Luc 5.1 Jean 2.11 Matthieu 4.23-4.25
42 Nao wengi wakamwamini huko.
Jean 7.31 Jean 12.42 Jean 8.30 Jean 11.45 Jean 4.41

Cette Bible est dans le domaine public.