Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Luc 23.13
Bible en Swahili de l’est


Jésus devant le gouverneur romain et le roi Hérode

1 Wakasimama mkutano wote, wakampeleka kwa Pilato.
Matthieu 27.11-27.14 Luc 22.66 Marc 15.1-15.5 Matthieu 27.1-27.2 Jean 18.28-18.38
2 Wakaanza kumshitaki, wakisema, Tumemwona huyu akipotosha taifa letu, na kuwazuia watu wasimpe Kaisari kodi, akisema kwamba yeye mwenyewe ni Kristo, mfalme.
Jean 19.12 Actes 17.6-17.7 Luc 23.14 Jérémie 38.4 1 Pierre 3.16-3.18
3 Pilato akamwuliza, akisema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Akajibu akamwambia, Wewe wasema.
1 Timothée 6.13 Marc 15.2 Luc 22.70 Jean 1.49 Marc 15.32
4 Pilato akawaambia wakuu wa makuhani na makutano, Sioni neno lililo ovu katika mtu huyu.
Jean 18.38 Luc 23.22 1 Pierre 2.22 Marc 15.14 Matthieu 27.23-27.24
5 Nao walikaza sana, wakisema, Huwataharakisha watu, akifundisha katika Uyahudi yote, tokea Galilaya mpaka huku.
Marc 1.14 Jean 2.11 Matthieu 4.23 Jean 1.43 Luc 11.53
6 Pilato aliposikia hayo aliuliza kama huyu ni mtu wa Galilaya.
Actes 5.37 Luc 13.1
7 Na alipopata habari ya kuwa yu chini ya mamlaka ya Herode, alimpeleka kwa Herode, kwa kuwa yeye naye alikuwapo Yerusalemu siku zile.
Luc 3.1 Luc 13.31 Matthieu 14.1
8 Na Herode alipomwona Yesu alifurahi sana, kwa sababu alikuwa akitaka sana kumwona tangu siku nyingi, maana amesikia habari zake, akataraji kuona ishara iliyofanywa na yeye.
Marc 6.14 Matthieu 14.1 Luc 4.23 2 Rois 5.3-5.6 Actes 8.19
9 Akamwuliza maneno mengi, yeye asimjibu lo lote.
Matthieu 27.14 1 Pierre 2.23 Esaïe 53.7 Matthieu 7.6 Psaumes 39.1-39.2
10 Wakuu wa makuhani na waandishi wakasimama wakamshitaki kwa nguvu sana.
Luc 23.14-23.15 Luc 23.5 Luc 23.2 Luc 11.53 Actes 24.5
11 Basi Herode akamfanya duni, pamoja na askari zake, akamdhihaki, na kumvika mavazi mazuri; kisha akamrudisha kwa Pilato.
Marc 9.12 Luc 22.64-22.65 Actes 4.27-4.28 Jean 19.5 Esaïe 53.3
12 Basi siku ile ile Herode na Pilato walipatana kwa urafiki kwa maana hapo kwanza walikuwa na uadui wao kwa wao.
Actes 4.27 Apocalypse 17.13-17.14 Matthieu 16.1 Psaumes 83.4-83.6
13 Na Pilato akawakutanisha wakuu wa makuhani, na wakubwa, na watu,
Marc 15.14 Jean 18.38 Matthieu 27.21-27.23 Jean 19.4
14 akawaambia, Mtu huyu mmemleta kwangu kana kwamba anapotosha watu; nami, tazama, nimeamua mambo yake mbele yenu, ila sikuona kwake kosa lo lote katika mambo hayo mliyomshitaki;
Actes 13.28 Matthieu 27.4 Luc 23.4-23.5 Luc 23.1-23.2 Matthieu 27.19
15 wala hata Herode, kwa maana amemrudisha kwetu; basi tazama, hakuna neno lo lote alilolitenda lipasalo kufa.
16 Kwa hiyo nitamrudi, kisha nitamfungua. [
Matthieu 27.26 Luc 23.22 Marc 15.15 Esaïe 53.5 Jean 19.1-19.4
17 Maana ilimlazimu kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa sikukuu.]
18 Wakapiga kelele wote pamoja, wakisema, Mwondoe huyu, utufungulie Baraba.
Actes 3.14 Actes 21.36 Actes 22.22 Marc 15.6-15.15 Jean 18.39-18.40
19 Naye ni mtu aliyetupwa gerezani kwa ajili ya fitina iliyotokea mjini, na kwa uuaji
Actes 3.14 Luc 23.5 Luc 23.2
20 Basi Pilato alisema nao mara ya pili, kwa vile alivyotaka kumfungua Yesu.
Jean 19.12 Matthieu 14.8-14.9 Matthieu 27.19 Marc 15.15
21 Lakini wakapiga kelele, wakisema, Msulibishe. Msulibishe.
Luc 23.23 Jean 19.15 Matthieu 27.22-27.25 Marc 15.13
22 Akawaambia mara ya tatu, Kwa sababu gani? Huyu ametenda uovu gani? Sikuona kwake hata neno lipasalo kufa. Basi nikiisha kumrudi nitamfungua.
Luc 23.16 Luc 23.14 1 Pierre 3.18 Luc 23.20 1 Pierre 1.19
23 Lakini wakatoa sauti zao kwa nguvu sana, wakitaka asulibiwe. Sauti zao zikashinda.
Zacharie 11.8 Psaumes 57.4 Psaumes 22.12-22.13 Luc 23.5
24 Pilato akahukumu kwamba haja yao ifanyike.
Exode 23.2 Marc 15.15 Jean 19.1 Proverbes 17.15 Matthieu 27.26
25 Akamfungua yule aliyetupwa gerezani kwa ajili ya fitina na uuaji, yule waliyemtaka, akamtoa Yesu wamfanyie watakavyo.
Actes 3.14 Luc 23.5 Marc 15.6-15.7 Luc 23.2 Jean 18.40

Crucifixion et mort de Jésus

26 Na walipokuwa wakimwondoa walimkamata mtu mmoja, Simoni Mkirene, aliyekuwa ametoka shamba, wakamtwika msalaba, auchukue nyuma yake Yesu.
Actes 13.1 Matthieu 27.32-27.44 Actes 6.9 Actes 2.10 Actes 6.6
27 Mkutano mkubwa wa watu wakamfuata, na wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea.
Luc 8.52 Matthieu 27.55 Marc 15.40 Luc 8.2 Luc 23.55
28 Yesu akawageukia, akasema, Enyi binti za Yerusalemu, msinililie mimi, bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu.
Cantique 2.7 Cantique 8.4 Cantique 3.10 Cantique 3.5 Cantique 5.16
29 Kwa maana tazama, siku zitakuja watakaposema, Heri walio tasa, na matumbo yasiyozaa, na maziwa yasiyonyonyesha.
Matthieu 24.19 Osée 13.16 Osée 9.12-9.16 Deutéronome 28.53-28.57 Marc 13.17-13.19
30 Ndipo watakapoanza kuiambia milima, Tuangukieni, na vilima, Tufunikeni.
Apocalypse 6.16 Esaïe 2.19 Osée 10.8 Apocalypse 9.6
31 Kwa kuwa kama wakitenda mambo haya katika mti mbichi, itakuwaje katika mkavu?
Jean 15.6 Matthieu 3.12 Jérémie 25.29 Ezéchiel 15.2-15.7 Proverbes 11.31
32 Wakapelekwa na wawili wengine, wahalifu, wauawe pamoja naye.
Marc 15.27 Matthieu 27.38 Jean 19.18 Esaïe 53.12 Luc 22.37
33 Na walipofika mahali paitwapo Fuvu la Kichwa, ndipo walipomsulibisha yeye, na wale wahalifu, mmoja upande wa kuume, na mmoja upande wa kushoto.
Marc 15.22-15.23 Matthieu 27.33-27.34 Jean 19.17-19.18 Jean 18.32 Psaumes 22.16
34 Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui watendalo. Wakagawa mavazi yake, wakipiga kura.
Matthieu 5.44 Psaumes 22.18 1 Pierre 3.9 Actes 7.60 1 Pierre 2.20-2.23
35 Watu wakasimama wakitazama. Wale wakuu nao walikuwa wakimfanyia mzaha, wakisema, Aliokoa wengine; na ajiokoe mwenyewe, kama ndiye Kristo wa Mungu, mteule wake.
Esaïe 42.1 Psaumes 22.17 Luc 16.14 1 Pierre 2.4 Matthieu 12.18
36 Wale askari nao wakamfanyia dhihaka, wakimwendea na kumletea siki,
Matthieu 27.48 Psaumes 69.21 Marc 15.36 Jean 19.28-19.30 Luc 23.11
37 huku wakisema, Kama wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi, ujiokoe mwenyewe.
38 Na juu yake palikuwa na anwani; HUYU NDIYE MFALME WA WAYAHUDI.
Marc 15.26 Matthieu 27.37 Marc 15.32 Jean 19.3 Marc 15.18
39 Na mmoja wa wale wahalifu waliotungikwa alimtukana, akisema, Je! Wewe si Kristo? Jiokoe nafsi yako na sisi.
Matthieu 27.44 Marc 15.32 Luc 23.35 Luc 23.37 Luc 17.34-17.35
40 Lakini yule wa pili akamjibu akamkemea, akisema, Wewe humwogopi hata Mungu, nawe u katika hukumu iyo hiyo?
Apocalypse 16.11 Psaumes 36.1 Apocalypse 15.4 2 Chroniques 28.22 Jérémie 5.3
41 Nayo ni haki kwetu sisi, kwa kuwa tunapokea malipo tuliyostahili kwa matendo yetu; bali huyu hakutenda lo lote lisilofaa.
Esdras 9.13 Matthieu 27.54 Josué 7.19-7.20 Matthieu 27.19 Matthieu 27.24
42 Kisha akasema, Ee Yesu, nikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.
Romains 10.9-10.14 Actes 16.31 1 Pierre 2.6-2.7 1 Jean 5.11-5.13 Esaïe 9.6-9.7
43 Yesu akamwambia, Amin, nakuambia, leo hivi utakuwa pamoja nami peponi.
Apocalypse 2.7 Philippiens 1.23 Luc 19.10 1 Timothée 1.15-1.16 Hébreux 7.25
44 Hapo ilikuwa yapata saa sita, kukawa giza juu ya nchi yote hata saa kenda,
Matthieu 27.45 Amos 8.9 Actes 2.20 Marc 15.33-15.34 Exode 10.21-10.23
45 jua limepungua nuru yake; pazia la hekalu likapasuka katikati.
Matthieu 27.51 2 Chroniques 3.14 Marc 15.38 Hébreux 10.19-10.22 Exode 26.31-26.33
46 Yesu akalia kwa sauti kuu, akasema, Ee Baba, mikononi mwako naiweka roho yangu.
Psaumes 31.5 Jean 19.30 Actes 7.59 1 Pierre 2.23 Marc 15.34-15.41
47 Alipokwisha kusema hayo alikata roho. Yule akida alipoona yaliyotukia, alimtukuza Mungu, akisema, Hakika yake, mtu huyu alikuwa mwenye haki.
Marc 15.39 Matthieu 27.54 Luc 23.41
48 Na makutano yote ya watu waliokuwa wamekutanika kutazama mambo hayo, walipoona yaliyotendeka, wakaenda zao kwao, wakijipiga-piga vifua.
Luc 18.13 Jérémie 31.19 Actes 2.37
49 Na wote waliojuana naye, na wale wanawake walioandamana naye toka Galilaya, wakasimama kwa mbali, wakitazama mambo hayo.
Luc 8.2 Psaumes 38.11 Matthieu 27.55-27.56 Luc 23.55 Jean 19.21-19.27

Mise au tombeau du corps de Jésus

50 Na tazama, akatoka mtu mmoja, jina lake Yusufu, ambaye ni mtu wa baraza, mtu mwema, mwenye haki;
Marc 15.42-15.47 Actes 11.24 Jean 19.38-19.42 Matthieu 27.57-27.61 Actes 10.2
51 (wala hakulikubali shauri na tendo lao), naye ni mtu wa Arimathaya, mji mmoja wa Wayahudi, tena anautazamia ufalme wa Mungu;
Luc 2.25 Luc 2.38 Marc 15.43 1 Samuel 1.1 Genèse 37.21-37.22
52 mtu huyo alikwenda kwa Pilato, akataka kupewa mwili wa Yesu.
Jean 19.38-19.42
53 Akaushusha, akauzinga sanda ya kitani, akauweka katika kaburi lililochongwa mwambani, ambalo hajalazwa mtu bado ndani yake.
Esaïe 53.9 Marc 15.46 Matthieu 27.59-27.60
54 Na siku ile ilikuwa siku ya Maandalio, na sabato ikaanza kuingia.
Matthieu 27.62 Jean 19.31 Jean 19.14 Jean 19.42 Marc 15.42
55 Na wale wanawake waliokuja naye toka Galilaya walifuata, wakaliona kaburi, na jinsi mwili wake ulivyowekwa.
Luc 23.49 Matthieu 27.61 Luc 8.2 Marc 15.47
56 Wakarudi, wakafanya tayari manukato na marhamu. Na siku ya sabato walistarehe kama ilivyoamriwa.
Luc 24.1 Marc 16.1 Deutéronome 5.14 Exode 20.8-20.10 Esaïe 58.13-58.14

Cette Bible est dans le domaine public.