Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Marc 13.27
Bible en Swahili de l’est


Discours sur le mont des Oliviers

1 Hata alipokuwa akitoka hekaluni, mmoja wa wanafunzi wake alimwambia, Mwalimu, tazama, yalivyo mawe na majengo haya!
Malachie 3.1-3.2 Ezéchiel 10.19 Ezéchiel 7.20-7.22 Ezéchiel 10.4 Ezéchiel 8.6
2 Yesu akajibu, akamwambia, Wayaona majengo haya makubwa? Halitasalia hapa jiwe juu ya jiwe ambalo halitabomolewa.
2 Chroniques 7.20-7.21 Actes 6.14 Luc 19.41-19.44 Luc 21.6 Apocalypse 11.2
3 Hata alipokuwa ameketi katika mlima wa Mizeituni, kuelekea hekalu Petro, na Yakobo, na Yohana, na Andrea walimwuliza kwa faragha,
Marc 4.34 Matthieu 21.1 Marc 1.16-1.19 Marc 9.2 Marc 10.35
4 Tuambie, mambo hayo yatakuwa lini? Nayo ni nini dalili ya wakati, hayo yote yatakapokuwa karibu kutimia?
Actes 1.6-1.7 Matthieu 24.3 Jean 21.21-21.22 Daniel 12.8 Luc 21.7
5 Yesu akaanza kuwaambia, Jihadharini, mtu asiwadanganye.
Jérémie 29.8 Ephésiens 5.6 2 Thessaloniciens 2.3 Colossiens 2.8 Luc 21.8
6 Wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, Mimi ndiye, nao watadanganya wengi.
Marc 13.22 Jérémie 14.14 Matthieu 24.11 Actes 5.36-5.39 1 Jean 4.1
7 Nanyi mtakaposikia habari za vita na uvumi wa vita, msitishwe; hayo hayana budi kutukia, lakini ule mwisho bado.
Luc 21.9-21.11 Actes 17.3 Jean 14.27 Matthieu 18.7 Psaumes 46.1-46.3
8 Kwa maana taifa litaondoka kupigana na taifa, na ufalme kupigana na ufalme; kutakuwa na matetemeko ya nchi mahali mahali; kutakuwako na njaa; hayo ndiyo mwanzo wa utungu.
Actes 11.28 Apocalypse 6.4 Esaïe 19.2 Jérémie 6.24 2 Chroniques 15.6
9 Nanyi jihadharini nafsi zenu; maana watawapeleka ninyi mabarazani; na katika masinagogi mtapigwa; nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao.
Matthieu 10.17-10.18 Jean 16.2 Marc 13.5 Marc 6.11 Apocalypse 1.9
10 Na sharti Injili ihubiriwe kwanza katika mataifa yote.
Colossiens 1.6 Matthieu 24.14 Romains 10.18 Colossiens 1.23 Matthieu 28.18-28.19
11 Na watakapowachukua ninyi, na kuwasaliti, msitafakari kwanza mtakayosema, lakini lo lote mtakalopewa saa ile, lisemeni; kwa maana si ninyi msemao, bali ni Roho Mtakatifu.
Luc 21.14-21.15 Actes 6.10 Luc 12.11-12.12 Matthieu 10.19-10.21 Actes 4.31
12 Na ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe, na baba atamsaliti mtoto, na watoto watashambulia wazazi wao, na kuwafisha.
Matthieu 10.21 Luc 12.52-12.53 Michée 7.4-7.6 Luc 21.16 Ezéchiel 38.21
13 Nanyi mtakuwa mkichukiwa na watu wote kwa ajili ya jina langu; lakini mwenye kusaburi hata mwisho, ndiye atakayeokoka.
Jean 15.18-15.19 Matthieu 10.22 Jean 15.21 Luc 6.22 Matthieu 5.11-5.12
14 Lakini mlionapo chukizo la uharibifu likisimama pasipolipasa, (asomaye na afahamu), ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani;
Daniel 9.27 Daniel 12.11 Apocalypse 1.3 Daniel 11.31 Lamentations 1.10
15 na mtu aliye juu ya dari asishuke, wala asiingie kuchukua kitu nyumbani mwake;
Hébreux 11.7 Actes 27.38 Genèse 19.26 Luc 17.31-17.33 Genèse 19.22
16 naye aliye shambani asirudi nyuma kulichukua vazi lake.
17 Lakini ole wao wenye mimba, nao wanyonyeshao siku hizo!
Luc 23.29 Luc 21.23 Lamentations 2.19-2.20 Deutéronome 28.56-28.57 Osée 9.14
18 Ila ombeni yasitokee hayo wakati wa baridi.
19 Kwa maana siku hizo zitakuwa na dhiki, jinsi isivyokuwa tangu mwanzo wa kuumba alipoumba Mungu hata sasa, wala haitakuwa kamwe.
Daniel 12.1 Joël 2.2 Matthieu 24.21 Daniel 9.26 Luc 21.22-21.24
20 Na kama Bwana asingalizikatiza siku hizo, asingeokoka mtu ye yote; lakini kwa ajili ya wateule aliowateua amezikatiza siku hizo.
Esaïe 65.8-65.9 Romains 11.28-11.32 Zacharie 13.8-13.9 Matthieu 24.22 Romains 11.5-11.7
21 Na wakati huo mtu akiwaambia, Tazama, Kristo yupo hapa, au yuko kule, msisadiki;
Luc 17.23-17.24 Luc 21.8 Matthieu 24.23-24.25 Deutéronome 13.1-13.3 Matthieu 24.5
22 kwa maana wataondoka Makristo wa uongo, na manabii wa uongo, watatoa ishara na maajabu, wapate kuwadanganya, kama yamkini, hata hao wateule.
Matthieu 24.24 Apocalypse 13.13-13.14 Marc 13.6 Jean 4.48 1 Jean 2.19
23 Bali ninyi jihadharini; nimekwisha kuwaonya yote mbele.
2 Pierre 3.17 Jean 14.29 Marc 13.5 Matthieu 7.15 Marc 13.33
24 Lakini siku zile, baada ya dhiki hiyo, jua litatiwa giza, na mwezi hatautoa mwanga wake.
Ezéchiel 32.7 Esaïe 13.10 Amos 5.20 Joël 3.15 Jérémie 4.28
25 na nyota za mbinguni zitakuwa zikianguka, na nguvu zilizo mbinguni zitatikisika.
Esaïe 34.4 Apocalypse 6.13
26 Hapo ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija mawinguni kwa nguvu nyingi na utukufu.
Apocalypse 1.7 Matthieu 16.27 Marc 8.38 Matthieu 25.31 Matthieu 24.30
27 Ndipo atakapowatuma malaika na kuwakusanya wateule wake toka pepo nne, toka upande wa mwisho wa nchi hata upande wa mwisho wa mbingu.
Matthieu 24.31 Zacharie 2.6 Deutéronome 30.4 Matthieu 13.41 2 Thessaloniciens 2.1
28 Kwa mtini jifunzeni mfano; tawi lake liishapo kuwa laini, na kuchanua majani, mwatambua ya kuwa wakati wa mavuno ni karibu;
Luc 21.29-21.31 Matthieu 24.32-24.33
29 nanyi kadhalika, myaonapo mambo hayo yanaanza, tambueni ya kuwa yu karibu milangoni.
Jacques 5.9 Ezéchiel 12.25-12.28 Ezéchiel 7.10-7.12 1 Pierre 4.17-4.18 Hébreux 10.25-10.37
30 Amin, nawaambieni, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatimie.
Luc 21.32 Matthieu 24.34 Matthieu 16.28 Marc 9.1 Matthieu 23.36
31 Mbingu na nchi zitapita; lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Matthieu 5.18 Matthieu 24.35 Esaïe 40.8 Luc 21.33 Esaïe 51.6
32 Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba.
Actes 1.7 Apocalypse 3.3 1 Thessaloniciens 5.1-5.2 Matthieu 25.13 Matthieu 24.36-24.42
33 Angalieni, kesheni, [ombeni], kwa kuwa hamjui wakati ule utakapokuwapo.
Matthieu 25.13 Romains 13.11-13.12 Ephésiens 6.18 1 Corinthiens 16.13 1 Thessaloniciens 5.5-5.8
34 Mfano wake ni kama mtu mwenye kusafiri, ameiacha nyumba yake, amewapa watumwa wake amri, na kila mtu kazi yake, naye amemwamuru bawabu akeshe.
Jean 10.3 Matthieu 25.14-25.30 1 Corinthiens 15.58 Colossiens 3.24 Ezéchiel 33.2-33.9
35 Kesheni basi, kwa maana hamjui ajapo bwana wa nyumba, kwamba ni jioni, au kwamba ni usiku wa manane, au awikapo jimbi, au asubuhi;
Matthieu 24.42 Matthieu 24.44 Marc 13.33 Marc 14.30 Marc 6.48
36 asije akawasili ghafula akawakuta mmelala.
Romains 13.11-13.14 Matthieu 24.48-24.51 Marc 14.40 1 Thessaloniciens 5.6-5.7 Luc 21.34
37 Na hilo niwaambialo ninyi, nawaambia wote, Kesheni.
Marc 13.35 Marc 13.33 Luc 12.41-12.46

Cette Bible est dans le domaine public.