Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 22.8
Bible en Swahili de l’est


Parabole du festin des noces

1 Yesu akajibu, akawaambia tena kwa mithali, akisema,
Luc 14.16 Matthieu 12.43-12.45 Luc 8.10 Matthieu 20.1-20.16 Matthieu 21.28-21.46
2 Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanawe arusi.
Matthieu 13.24 Matthieu 22.2-22.14 Ephésiens 5.24-5.32 Apocalypse 19.7-19.9 Jean 3.29-3.30
3 Akawatuma watumwa wake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja.
Luc 19.27 Luc 15.28 Luc 14.15-14.17 1 Samuel 9.13 Luc 9.1-9.6
4 Akatuma tena watu kwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni, nimeandaa karamu yangu; ng’ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini.
Matthieu 21.36 Luc 10.1-10.16 Proverbes 9.1-9.2 Jean 6.50-6.57 Néhémie 9.17
5 Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake;
Hébreux 2.3 Proverbes 1.24-1.25 Psaumes 106.24-106.25 1 Jean 2.15-2.16 Proverbes 1.7
6 nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua.
Matthieu 21.35-21.39 Actes 5.40-5.41 Actes 7.51-7.57 Jean 15.19-15.20 Matthieu 23.34-23.37
7 Basi yule mfalme akaghadhibika; akapeleka majeshi yake, akawaangamiza wauaji wale, akauteketeza mji wao.
Luc 19.27 1 Pierre 4.17-4.18 Esaïe 10.5-10.7 Jérémie 51.20-51.23 1 Thessaloniciens 2.16
8 Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.
Luc 20.35 Apocalypse 3.4 Actes 13.46 Matthieu 10.37-10.38 Apocalypse 22.14
9 Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.
Luc 14.21-14.24 Luc 24.47 Esaïe 55.6-55.7 Apocalypse 22.17 Actes 13.47
10 Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni.
Matthieu 13.47-13.48 Matthieu 13.38 2 Corinthiens 12.21 Apocalypse 7.9 Matthieu 25.10
11 Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi.
Ephésiens 4.24 Colossiens 3.10-3.11 Zacharie 3.3-3.4 Galates 3.27 Apocalypse 19.8
12 Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa.
Matthieu 20.13 Matthieu 26.50 Matthieu 5.20 Psaumes 107.42 Romains 3.19
13 Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Matthieu 8.12 Matthieu 25.30 Matthieu 13.42 Matthieu 13.50 Luc 13.28
14 Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache.
Apocalypse 17.14 2 Pierre 1.10 Matthieu 7.13-7.14 Matthieu 20.16 Luc 13.23-13.24

Tentatives de piéger Jésus

15 Ndipo Mafarisayo wakaenda zao, wakafanya shauri, jinsi ya kumtega kwa maneno.
Marc 12.13-12.17 Luc 20.20-20.26 Hébreux 12.3 Psaumes 41.6 Psaumes 57.6
16 Wakatuma kwake wanafunzi wao pamoja na Maherodi, wakasema, Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, na njia ya Mungu waifundisha katika kweli, wala hujali cheo cha mtu awaye yote, kwa maana hutazami sura za watu.
Marc 3.6 Marc 8.15 Esaïe 59.13-59.15 Matthieu 26.49 Matthieu 22.24
17 Basi utuambie, Waonaje? Ni halali kumpa Kaisari kodi, ama sivyo?
Luc 2.1 Matthieu 17.25 Luc 3.1 Actes 28.22 Jean 19.12-19.15
18 Lakini Yesu akaufahamu uovu wao, akasema, Mbona mnanijaribu, enyi wanafiki?
Jean 2.25 Jean 8.6 Luc 5.22 Marc 12.5 Actes 5.9
19 Nionyesheni fedha ya kodi. Nao wakamletea dinari.
Matthieu 20.2 Apocalypse 6.6 Matthieu 18.28
20 Akawaambia, Ni ya nani sanamu hii, na anwani hii?
Luc 20.24
21 Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Akawaambia, Basi, mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu.
Romains 13.7 Malachie 1.6-1.8 Daniel 6.20-6.23 Matthieu 22.37 Matthieu 4.10
22 Waliposikia, walistaajabu, wakamwacha, wakaenda zao.
Marc 12.12 Matthieu 22.46 Luc 21.15 Luc 20.25-20.26 Actes 6.10
23 Siku ile Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza,
Matthieu 3.7 Actes 4.1 Luc 20.27-20.40 Actes 5.17 Marc 12.18-12.27
24 wakisema, Mwalimu, Musa alisema, Mtu akifa, akiwa hana watoto, ndugu yake na amwoe yule mkewe, ili ampatie nduguye mzao.
Luc 6.46 Matthieu 22.16 Luc 20.28 Genèse 38.8 Marc 12.19
25 Basi, kwetu kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akaoa, akafariki, na kwa kuwa hana mzao, akamwachia nduguye mke wake.
Marc 12.19-12.23 Luc 20.29-20.33 Hébreux 9.27
26 Vivyo hivyo wa pili naye, na wa tatu, hata wote saba.
27 Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.
28 Basi, katika kiyama, atakuwa mke wa yupi katika wale saba? Maana wote walikuwa naye.
29 Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.
Jean 20.9 Esaïe 26.19 Romains 15.4 Daniel 12.2-12.3 Jérémie 32.17
30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni.
Luc 20.34-20.36 Marc 12.24-12.25 Matthieu 24.38 Psaumes 103.20 1 Jean 3.1-3.2
31 Tena kwa habari ya kiyama ya watu, hamjalisoma neno lililonenwa na Mungu, akisema,
Matthieu 21.16 Matthieu 12.3 Matthieu 21.42 Matthieu 9.13 Matthieu 12.7
32 Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali wa walio hai.
Exode 3.6 Actes 7.32 Hébreux 11.16 Marc 12.26-12.27 Luc 20.37-20.38
33 Na makutano waliposikia, walishangaa kwa mafunzo yake.
Luc 20.39-20.40 Jean 7.46 Marc 6.2 Luc 4.22 Matthieu 22.22
34 Na Mafarisayo waliposikia ya kwamba amewafumba kinywa wale Masadukayo, walifanya shauri pamoja.
Marc 12.28-12.31 Actes 21.28-21.30 Jean 11.47-11.50 Esaïe 41.5-41.7 Matthieu 25.3-25.5
35 Mmoja wao, mwana-sheria, akamwuliza, akimjaribu;
Luc 7.30 Luc 11.52 Luc 14.3 Luc 11.45-11.46 Matthieu 22.18
36 Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?
Marc 12.28-12.33 Osée 8.12 Luc 11.42 Matthieu 15.6 Matthieu 5.19-5.20
37 Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
Deutéronome 6.5 Luc 10.27 Marc 12.29-12.30 Deutéronome 30.6 Deutéronome 10.12
38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
39 Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Lévitique 19.18 Matthieu 19.19 Galates 5.14 Marc 12.31 Jacques 2.8
40 Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii.
Matthieu 7.12 Romains 13.9 1 Jean 4.19-4.21 1 Jean 4.7-4.11 Jean 1.17

Reproches de Jésus aux chefs religieux

41 Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akisema, Mwaonaje katika habari za Kristo?
Marc 12.35-12.37 Luc 20.41-20.44 Matthieu 22.34 Matthieu 22.15
42 Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi.
Jean 6.68-6.69 Matthieu 1.1 1 Pierre 2.4-2.7 Jérémie 23.5-23.6 Esaïe 9.6-9.7
43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema,
Apocalypse 4.2 2 Samuel 23.2 2 Pierre 1.21 Apocalypse 1.10 Actes 2.30-2.31
44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako?
Psaumes 110.1 1 Corinthiens 15.25 Actes 2.34-2.35 Hébreux 1.13 Genèse 3.15
45 Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe?
Romains 1.3-1.4 Apocalypse 22.16 Jean 8.58 Philippiens 2.6-2.8 Hébreux 2.14
46 Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu ye yote tangu siku ile kumwuliza neno tena.
Luc 20.40 Marc 12.34 Luc 14.6 Esaïe 50.2-50.9 Actes 4.14

Cette Bible est dans le domaine public.