Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Matthieu 22
Bible en Swahili de l’est


Parabole du festin des noces

1 Yesu akajibu, akawaambia tena kwa mithali, akisema,
Luc 14.16 Matthieu 21.28-21.46 Matthieu 9.15-9.17 Marc 4.33-4.34 Matthieu 13.3-13.11
2 Ufalme wa mbinguni umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanawe arusi.
Matthieu 13.24 Matthieu 13.31-13.33 Luc 14.16-14.24 Psaumes 45.10-45.16 Matthieu 13.44-13.47
3 Akawatuma watumwa wake wawaite walioalikwa kuja arusini; nao wakakataa kuja.
Psaumes 81.10-81.12 Apocalypse 22.17 Romains 10.21 Jean 5.40 Actes 13.45
4 Akatuma tena watu kwa wengine, akisema, Waambieni wale walioalikwa, Tazameni, nimeandaa karamu yangu; ng’ombe zangu na vinono vimekwisha kuchinjwa, na vyote vimekuwa tayari, njoni arusini.
Matthieu 21.36 Psaumes 86.5 Cantique 5.1 Actes 28.17-28.31 Romains 8.32
5 Lakini hawakujali, wakaenda zao, mmoja shambani kwake, mmoja kwenye biashara yake;
Hébreux 2.3 2 Timothée 3.4 1 Timothée 6.9-6.10 Genèse 25.34 Proverbes 1.24-1.25
6 nao waliosalia wakawakamata watumwa wake, wakawatenda jeuri, na kuwaua.
Matthieu 5.10-5.12 Actes 4.1-4.3 Matthieu 10.12-10.18 Actes 8.1 Matthieu 21.35-21.39
7 Basi yule mfalme akaghadhibika; akapeleka majeshi yake, akawaangamiza wauaji wale, akauteketeza mji wao.
Luc 19.27 Luc 21.21 Joël 2.25 Matthieu 21.40-21.41 Zacharie 14.1-14.2
8 Kisha akawaambia watumwa wake, Arusi i tayari, lakini wale walioalikwa hawakustahili.
Luc 20.35 Apocalypse 3.4 Actes 13.46 Luc 21.36 Matthieu 10.37-10.38
9 Basi enendeni hata njia panda za barabara, na wote mwaonao waiteni arusini.
Luc 14.21-14.24 Ezéchiel 21.21 Proverbes 1.20-1.23 Proverbes 8.1-8.5 Luc 24.47
10 Watumwa wale wakatoka wakaenda njia kuu, wakakusanya wote waliowaona, waovu kwa wema; arusi ikajaa wageni.
Matthieu 13.47-13.48 Apocalypse 2.20-2.23 Apocalypse 19.6-19.9 Apocalypse 5.9 Matthieu 25.1-25.2
11 Lakini alipoingia yule mfalme ili kuwatazama wageni wake, akaona mle mtu mmoja asiyevaa vazi la arusi.
Apocalypse 19.8 Romains 13.14 Ephésiens 4.24 Colossiens 3.10-3.11 Zacharie 3.3-3.4
12 Akamwambia, Rafiki, uliingiaje humu nawe huna vazi la arusi? Naye akatekewa.
Matthieu 26.50 Matthieu 20.13 Matthieu 5.20 Tite 3.11 Job 5.16
13 Mfalme akawaambia watumishi, Mfungeni mikono na miguu, mchukueni mkamtupe katika giza la nje; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.
Matthieu 8.12 Matthieu 25.30 Luc 13.28 Matthieu 13.42 Matthieu 13.50
14 Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache.
Apocalypse 17.14 Matthieu 7.13-7.14 2 Pierre 1.10 Matthieu 20.16 Luc 13.23-13.24

Tentatives de piéger Jésus

15 Ndipo Mafarisayo wakaenda zao, wakafanya shauri, jinsi ya kumtega kwa maneno.
Luc 20.20-20.26 Marc 12.13-12.17 Jérémie 18.18 Psaumes 56.5-56.7 Luc 11.53-11.54
16 Wakatuma kwake wanafunzi wao pamoja na Maherodi, wakasema, Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, na njia ya Mungu waifundisha katika kweli, wala hujali cheo cha mtu awaye yote, kwa maana hutazami sura za watu.
Marc 3.6 Marc 8.15 Galates 2.6 1 Thessaloniciens 2.4 Psaumes 5.9
17 Basi utuambie, Waonaje? Ni halali kumpa Kaisari kodi, ama sivyo?
Luc 2.1 Matthieu 17.25 Néhémie 5.4 Néhémie 9.37 Esdras 7.24
18 Lakini Yesu akaufahamu uovu wao, akasema, Mbona mnanijaribu, enyi wanafiki?
Luc 5.22 Jean 2.25 Jean 8.6 Luc 20.23 Luc 9.47
19 Nionyesheni fedha ya kodi. Nao wakamletea dinari.
Apocalypse 6.6 Matthieu 18.28 Matthieu 20.2
20 Akawaambia, Ni ya nani sanamu hii, na anwani hii?
Luc 20.24
21 Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Akawaambia, Basi, mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu.
Romains 13.7 Malachie 1.6-1.8 Daniel 6.20-6.23 Matthieu 22.37 Actes 4.19
22 Waliposikia, walistaajabu, wakamwacha, wakaenda zao.
Marc 12.12 Matthieu 10.16 Colossiens 4.6 Matthieu 22.33 Proverbes 26.4-26.5
23 Siku ile Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza,
Matthieu 3.7 Actes 4.1 Actes 5.17 Marc 12.18-12.27 Luc 20.27-20.40
24 wakisema, Mwalimu, Musa alisema, Mtu akifa, akiwa hana watoto, ndugu yake na amwoe yule mkewe, ili ampatie nduguye mzao.
Luc 6.46 Deutéronome 25.5-25.10 Ruth 1.11 Matthieu 22.36 Matthieu 22.16
25 Basi, kwetu kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akaoa, akafariki, na kwa kuwa hana mzao, akamwachia nduguye mke wake.
Luc 20.29-20.33 Hébreux 9.27 Marc 12.19-12.23
26 Vivyo hivyo wa pili naye, na wa tatu, hata wote saba.
27 Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.
28 Basi, katika kiyama, atakuwa mke wa yupi katika wale saba? Maana wote walikuwa naye.
29 Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.
Jean 20.9 Esaïe 26.19 Daniel 12.2-12.3 Jérémie 32.17 Romains 15.4
30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni.
Luc 20.34-20.36 Marc 12.24-12.25 Matthieu 24.38 Luc 17.27 1 Corinthiens 7.29-7.31
31 Tena kwa habari ya kiyama ya watu, hamjalisoma neno lililonenwa na Mungu, akisema,
Matthieu 21.16 Matthieu 12.3 Matthieu 9.13 Matthieu 12.7 Matthieu 21.42
32 Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali wa walio hai.
Exode 3.6 Actes 7.32 Marc 12.26-12.27 Luc 20.37-20.38 Exode 3.15-3.16
33 Na makutano waliposikia, walishangaa kwa mafunzo yake.
Matthieu 22.22 Marc 12.17 Matthieu 7.28-7.29 Luc 2.47 Luc 20.39-20.40
34 Na Mafarisayo waliposikia ya kwamba amewafumba kinywa wale Masadukayo, walifanya shauri pamoja.
Marc 12.28-12.31 Actes 5.24-5.28 Actes 19.23-19.28 Matthieu 12.14 Actes 21.28-21.30
35 Mmoja wao, mwana-sheria, akamwuliza, akimjaribu;
Luc 7.30 Luc 14.3 Luc 11.52 Matthieu 22.18 Tite 3.13
36 Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?
Marc 12.28-12.33 Osée 8.12 Luc 11.42 Matthieu 23.23-23.24 Matthieu 15.6
37 Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
Deutéronome 6.5 Luc 10.27 Marc 12.29-12.30 Deutéronome 30.6 Deutéronome 10.12
38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
39 Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
Lévitique 19.18 Matthieu 19.19 Galates 5.14 Romains 13.9-13.10 Marc 12.31
40 Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii.
Matthieu 7.12 1 Jean 4.7-4.11 Romains 13.9 1 Jean 4.19-4.21 Jean 1.17

Reproches de Jésus aux chefs religieux

41 Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akisema, Mwaonaje katika habari za Kristo?
Marc 12.35-12.37 Luc 20.41-20.44 Matthieu 22.34 Matthieu 22.15
42 Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi.
Matthieu 1.1 Jean 6.68-6.69 Jean 20.28 Luc 1.69-1.70 Matthieu 14.33
43 Akawauliza, Imekuwaje basi Daudi katika Roho kumwita Bwana, akisema,
Apocalypse 4.2 2 Samuel 23.2 Luc 2.26-2.27 Actes 1.16 2 Pierre 1.21
44 Bwana alimwambia Bwana wangu, Uketi mkono wangu wa kuume, Hata niwawekapo adui zako Kuwa chini ya miguu yako?
Psaumes 110.1 1 Corinthiens 15.25 Actes 2.34-2.35 Hébreux 1.13 Genèse 3.15
45 Basi, Daudi akimwita Bwana, amekuwaje ni mwanawe?
Romains 1.3-1.4 Philippiens 2.6-2.8 Hébreux 2.14 1 Timothée 3.16 Apocalypse 22.16
46 Wala hakuweza mtu kumjibu neno; wala hakuthubutu mtu ye yote tangu siku ile kumwuliza neno tena.
Marc 12.34 Luc 20.40 Luc 14.6 Matthieu 21.27 Job 32.15-32.16

Cette Bible est dans le domaine public.