Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Amos 5
Bible en Swahili de l’est


Appel à revenir à Dieu

1 Lisikieni neno hili nilitamkalo liwe maombolezo juu yenu, enyi nyumba ya Israeli.
Ezéchiel 19.1 Jérémie 9.17 Jérémie 7.29 Jérémie 9.10 Ezéchiel 27.27-27.32
2 Bikira wa Israeli ameanguka; hatainuka tena; Ameangushwa katika nchi yake; hakuna mtu wa kumwinua.
Jérémie 14.17 Jérémie 4.20 Ezéchiel 16.36-16.37 Jérémie 50.32 Amos 9.11
3 Kwa kuwa Bwana MUNGU asema hivi; Mji uliotoka nje wenye watu elfu, utasaziwa watu mia, na mji uliotoka wenye watu mia, utasaziwa watu kumi, kwa nyumba ya Israeli.
Esaïe 6.13 Esaïe 1.9 Amos 6.9 Romains 9.27 Deutéronome 4.27
4 Maana Bwana awaambia hivi nyumba ya Israeli, Nitafuteni mimi, nanyi mtaishi;
2 Chroniques 15.2 Sophonie 2.3 Esaïe 55.3 Esaïe 55.6-55.7 1 Chroniques 28.9
5 bali msitafute Betheli, wala msiingie Gilgali, wala msipite kwenda Beer-sheba; kwani Gilgali hakika yake itakwenda utumwani, na Betheli itakuwa ubatili.
Amos 4.4 Amos 8.14 Osée 4.15 Genèse 21.33 Osée 10.14-10.15
6 Mtafuteni Bwana, nanyi mtaishi; asije akawaka kama moto katika nyumba ya Yusufu, nao ukateketeza, asiwepo mtu awezaye kuuzima katika Betheli.
Amos 5.4 Marc 9.43-9.48 Amos 5.14 Josué 18.5 2 Samuel 19.20
7 Ninyi mnaogeuza hukumu kuwa uchungu, na kuiangusha haki chini,
Amos 6.12 Osée 10.4 Sophonie 1.6 Ezéchiel 3.20 Amos 5.11-5.12
8 mtafuteni yeye afanyaye Kilimia na Orioni, na kukigeuza kivuli cha mauti kuwa asubuhi, na kuufanya mchana kuwa giza kwa usiku; yeye ayaitaye maji ya bahari, na kuyamwaga juu ya uso wa nchi; Bwana, ndilo jina lake;
Amos 4.13 Job 9.9 Psaumes 104.20 Amos 9.6 Amos 8.9
9 yeye aletaye uharibifu wa ghafula juu yao walio hodari, hata uharibifu uipate ngome.
Jérémie 37.10 2 Rois 13.17 Hébreux 11.34 Michée 5.11 2 Rois 13.25
10 Wao humchukia yeye akemeaye langoni, nao humzira anenaye maneno ya adili.
Esaïe 29.21 1 Rois 22.8 Jérémie 17.16-17.17 1 Rois 18.17 Amos 7.10-7.17
11 Basi, kwa kuwa mnamkanyaga maskini, na kumtoza ngano; ninyi mmejenga nyumba za mawe yaliyochongwa, lakini hamtakaa ndani yake; ninyi mmepanda mashamba mazuri ya mizabibu, lakini hamtakunywa divai yake.
Michée 6.15 Deutéronome 28.30 Jacques 2.6 Sophonie 1.13 Michée 3.1-3.3
12 Maana mimi najua jinsi maasi yenu yalivyo mengi, na jinsi dhambi zenu zilivyo kubwa; ninyi mnaowaonea wenye haki, mnaopokea rushwa, na kuwageuza wahitaji langoni wasipate haki yao.
Amos 2.6-2.7 Amos 5.10 1 Samuel 8.3 Esaïe 1.23 Esaïe 29.21
13 Kwa ajili ya hayo mwenye busara atanyamaza kimya wakati kama huo; kwa kuwa ni wakati mbaya.
Michée 2.3 Ecclésiaste 3.7 Osée 4.4 Ecclésiaste 9.12 2 Timothée 3.1
14 Tafuteni mema, wala si mabaya, mpate kuishi; hivyo Bwana, Mungu wa majeshi, atakuwa pamoja nanyi, kama msemavyo.
Josué 1.9 Philippiens 4.8-4.9 Michée 3.11 1 Chroniques 28.20 Amos 3.3
15 Yachukieni mabaya; yapendeni mema; mkaithibitishe haki langoni; yamkini kwamba Bwana, Mungu wa majeshi, atawafanyia fadhili mabaki ya Yusufu.
Romains 12.9 Joël 2.14 Psaumes 97.10 Michée 5.7-5.8 Exode 32.30
16 Kwa ajili ya hayo, asema Bwana, Mungu wa majeshi, aliye Bwana; Kutakuwako maombolezo katika njia kuu zote; nao watasema katika njia zote, Ole! Ole! Nao watamwita mkulima aje kuombolea, na hao walio hodari wa kulia waje kuomboleza.
Joël 1.11 Jérémie 9.17-9.20 Jérémie 9.10 Esaïe 15.2-15.5 Joël 1.14
17 Tena katika mashamba yote ya mizabibu kutakuwako kulia; kwa maana mimi nitapita katikati yako, asema Bwana.
Exode 12.12 Jérémie 48.33 Esaïe 16.10 Exode 12.23 Nahum 1.15
18 Ole wenu! Ninyi mnaoitamani siku ya Bwana; kwani kuitamani siku ya Bwana? Ni giza, wala si nuru.
Joël 1.15 Joël 2.1-2.2 Esaïe 5.30 Esaïe 5.19 Jérémie 30.7
19 Ni kama mtu aliyemkimbia simba, akakutana na dubu; au aliingia katika nyumba akauegemeza mkono wake ukutani, nyoka akamwuma.
Esaïe 24.17-24.18 Jérémie 15.2-15.3 Jérémie 48.43-48.44 Amos 9.1-9.2 Job 20.24-20.25
20 Je! Siku ya Bwana haitakuwa giza, wala si nuru? Naam, yenye giza sana, wala haina mwanga.
Esaïe 13.10 Sophonie 1.15 Ezéchiel 34.12 Job 3.4-3.6 Apocalypse 16.10
21 Mimi nazichukia sikukuu zenu, nazidharau, nami sitapendezwa na makutano yenu ya dini.
Esaïe 1.11-1.16 Jérémie 6.20 Lévitique 26.31 Esaïe 66.3 Proverbes 15.8
22 Naam, ijapokuwa mnanitolea sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za unga, sitazikubali; wala sitaziangalia sadaka zenu za amani, na za wanyama walionona.
Michée 6.6-6.7 Esaïe 66.3 Lévitique 7.12-7.15 Amos 4.4-4.5 Psaumes 50.8-50.14
23 Niondoleeni kelele za nyimbo zenu; kwa maana sitaki kuzisikia sauti za vinanda vyenu.
Amos 6.5 Amos 8.3 Amos 8.10
24 Lakini hukumu na itelemke kama maji, na haki kama maji makuu.
Michée 6.8 Proverbes 21.3 Amos 5.7 Marc 12.32-12.34 Job 29.12-29.17
25 Je! Mliniletea dhabihu na sadaka jangwani muda wa miaka arobaini, enyi nyumba ya Israeli?
Actes 7.42-7.43 Néhémie 9.21 Josué 24.14 Néhémie 9.18 Zacharie 7.5
26 Naam, mtamchukua Sikuthi, mfalme wenu, na Kiuni, sanamu zenu, nyota ya mungu wenu, mliojifanyizia wenyewe.
1 Rois 11.33 2 Rois 23.12-23.13 Lévitique 18.21 Lévitique 20.2-20.5
27 Kwa sababu hiyo nitawahamisha, hali ya kufungwa, mwende mbali kupita Dameski, asema Bwana, ambaye jina lake ni Mungu wa majeshi.
Actes 7.43 2 Rois 17.6 Amos 4.13 2 Rois 15.29

Cette Bible est dans le domaine public.