Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Joël 2.20
Bible en Swahili de l’est


1 Pigeni tarumbeta katika Sayuni, Pigeni na kelele katika mlima wangu mtakatifu; Wenyeji wote wa nchi na watetemeke; Kwa maana siku ya Bwana inakuja. Kwa sababu inakaribia;
Joël 2.15 Abdias 1.15 Joël 1.15 Jérémie 4.5 Amos 3.6
2 siku ya giza na weusi, siku ya mawingu na giza kuu. Kama mapambazuko yakitandazwa juu ya milima, hao ni wakuu, tena wenye nguvu, mfano wao haukuwako kamwe, wala hautakuwako baada ya hao, hata katika miaka ya vizazi vingi.
Joël 1.6 Sophonie 1.14-1.15 Amos 5.18-5.20 Joël 2.25 Joël 2.10-2.11
3 Moto unakula mbele yao; na nyuma yao miali ya moto inateketeza; hiyo nchi inafanana na bustani ya Adeni mbele yao, na nyuma yao imekuwa jangwa tupu; naam, hakuna aliyeokoka asipatikane nao.
Esaïe 51.3 Genèse 2.8 Zacharie 7.14 Joël 1.19-1.20 Exode 10.5
4 Kuonekana kwao ni kama kuonekana kwa farasi; na kama wapanda farasi ndivyo wanavyopiga mbio.
Apocalypse 9.7
5 Kama mshindo wa magari ya vita juu ya vilele vya milima, ndivyo warukavyo; kama mshindo wa miali ya moto ilapo mabua makavu, kama mashujaa waliopangwa tayari kwa vita.
Apocalypse 9.9 Esaïe 5.24 Esaïe 30.30 Matthieu 3.12 Nahum 3.2-3.3
6 Mbele yao watu wanahangaika; nyuso zote zimegeuka kuwa nyeupe kwa hofu.
Nahum 2.10 Esaïe 13.8 Jérémie 30.6 Psaumes 119.83 Jérémie 8.21
7 Hupiga mbio kama mashujaa; huupanda ukuta kama watu wa vita; nao huendelea mbele kila mmoja katika njia zake, wala hawapotoshi safu zao.
Proverbes 30.27 Esaïe 5.26-5.29 Joël 2.9 Jérémie 5.10 2 Samuel 2.18-2.19
8 Wala hapana mmoja amsukumaye mwenzake; huendelea mbele kila mmoja katika njia yake; hujifanyizia njia kwa nguvu kati ya silaha, wala hawaachi kuifuata njia yao.
2 Chroniques 23.10 2 Chroniques 32.5 Cantique 4.13 Job 36.12 Job 33.18
9 Huurukia mji; hupiga mbio juu ya ukuta; hupanda na kuingia ndani ya nyumba; huingia madirishani kama aingiavyo mwivi.
Jérémie 9.21 Jean 10.1 Exode 10.6
10 Nchi inatetemeka mbele yao; mbingu zinatetemeka; jua na mwezi hutiwa giza, na nyota huacha kuangaza;
Matthieu 24.29 Esaïe 13.10 Psaumes 18.7 Joël 3.15-3.16 Apocalypse 8.12
11 naye Bwana anatoa sauti yake mbele ya jeshi lake; maana matuo yake ni makubwa sana; kwa maana yeye ni hodari atekelezaye neno lake; kwa kuwa siku ya Bwana ni kuu, yenye kitisho sana; naye ni nani awezaye kuistahimili?
Apocalypse 18.8 Malachie 3.2 Apocalypse 6.17 Joël 3.16 Esaïe 13.4

Appel à revenir à Dieu

12 Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea;
Osée 12.6 Jérémie 4.1 1 Samuel 7.6 Deutéronome 4.29-4.30 Jacques 4.8-4.9
13 rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie Bwana, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya.
Psaumes 34.18 Jonas 4.2 Esaïe 57.15 Psaumes 86.15 Psaumes 86.5
14 N’nani ajuaye kwamba hatarudi na kugeuka, na kutuachia baraka nyuma yake, naam, sadaka ya unga, na sadaka ya kinywaji, kwa Bwana, Mungu wenu?
Jonas 3.9 Aggée 2.19 Joël 1.13 Joël 1.9 2 Samuel 12.22
15 Pigeni tarumbeta katika Sayuni, Takaseni saumu, kusanyeni kusanyiko kuu;
Joël 1.14 Joël 2.1 2 Rois 10.20 Jérémie 36.9 Nombres 10.3
16 Kusanyeni watu, litakaseni kusanyiko, Kusanyeni wazee, kusanyeni watoto, Na hao wanyonyao maziwa; Bwana arusi na atoke chumbani mwake, Na bibi arusi katika hema yake.
2 Chroniques 20.13 1 Corinthiens 7.5 2 Chroniques 29.5 1 Samuel 16.5 Exode 19.22
17 Hao makuhani, wahudumu wa Bwana, na walie Kati ya patakatifu na madhabahu, Na waseme, Uwaachilie watu wako, Ee Bwana, Wala usiutoe urithi wako upate aibu, Hata mataifa watawale juu yao; Kwani waseme kati ya watu, Yuko wapi Mungu wao?
Ezéchiel 8.16 Psaumes 115.2 Psaumes 79.10 1 Rois 6.3 Amos 7.5
18 Hapo ndipo Bwana alipoona wivu kwa ajili ya nchi yake, akawahurumia watu wake.
Zacharie 1.14 Zacharie 8.2 Psaumes 103.13 Esaïe 63.9 Esaïe 63.15
19 Bwana akajibu, akawaambia watu wake; Tazameni, nitawaletea nafaka, na divai, na mafuta, nanyi mtashiba kwa vitu hivyo; wala sitawafanya tena kuwa aibu kati ya mataifa;
Joël 1.10 Ezéchiel 34.29 Matthieu 6.33 Malachie 3.10-3.12 Ezéchiel 36.15
20 lakini jeshi lililotoka kaskazini nitaliondolea mbali nanyi, nami nitalifukuza mpaka nchi ya ukame na ukiwa; sehemu yake iliyo mbele itaingia katika bahari ya mashariki, na sehemu yake iliyo nyuma itaingia katika bahari ya magharibi; na uvundo wake utapanda juu, na harufu yake mbaya itapanda juu, kwa sababu ametenda mambo makubwa.
Zacharie 14.8 Deutéronome 11.24 Esaïe 34.3 Ezéchiel 47.18 Exode 10.19
21 Ee nchi, usiogope; furahi na kushangilia; kwa kuwa Bwana ametenda mambo makuu.
Sophonie 3.16-3.17 Esaïe 54.4 Jérémie 30.9-30.10 Psaumes 126.1-126.3 Osée 2.21
22 Msiogope, enyi wanyama wa kondeni; maana malisho ya jangwani yanatoa miche, na huo mti unazaa matunda yake, mtini na mzabibu inatoa nguvu zake.
Psaumes 65.12 Joël 1.18-1.20 Zacharie 8.12 Ezéchiel 34.26-34.27 Aggée 2.16
23 Furahini, basi, enyi wana wa Sayuni, mkamfurahie Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa yeye huwapa ninyi mvua ya masika, kwa kipimo cha haki, naye huwanyeshea mvua, mvua ya masika, na mvua ya vuli, kama kwanza.
Lévitique 26.4 Esaïe 12.2-12.6 Osée 6.3 Deutéronome 11.14 Esaïe 41.16
24 Na sakafu za kupepetea zitajaa ngano, na mashinikizo yatafurika kwa divai na mafuta.
Amos 9.13 Malachie 3.10 Lévitique 26.10 Joël 3.18 Proverbes 3.9-3.10
25 Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu.
Zacharie 10.6 Joël 1.4-1.7 Joël 2.2-2.11
26 Nanyi mtakula chakula tele na kushiba, na kulihimidi jina la Bwana, Mungu wenu, aliyewatendea mambo ya ajabu; na watu wangu hawatatahayari kamwe.
Esaïe 25.1 Lévitique 26.5 Esaïe 45.17 Deutéronome 12.7 Psaumes 126.2-126.3
27 Nanyi mtajua ya kuwa mimi ni katikati ya Israeli, na ya kuwa mimi ndimi Bwana, Mungu wenu, wala hakuna mwingine; na watu wangu hawatatahayari kamwe.
Joël 3.17 Lévitique 26.11-26.12 Ezéchiel 37.26-37.28 2 Corinthiens 6.16 Sophonie 3.17
28 Hata itakuwa, baada ya hayo, ya kwamba nitamimina roho yangu juu ya wote wenye mwili; na wana wenu, waume kwa wake, watatabiri, wazee wenu wataota ndoto, na vijana wenu wataona maono;
Actes 2.16-2.21 Ezéchiel 39.29 Esaïe 32.15 Actes 2.39 Actes 2.2-2.4
29 tena juu ya watumishi wenu, wanaume kwa wanawake, katika siku zile, nitamimina roho yangu.
1 Corinthiens 12.13 Galates 3.28 Colossiens 3.11
30 Nami nitaonyesha mambo ya ajabu katika mbingu na katika dunia, damu, na moto, na minara ya moshi.
Luc 21.11 Matthieu 24.29 Luc 21.25-21.26 Actes 2.19-2.20 Juges 20.40
31 Jua litageuzwa kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla haijaja hiyo siku ya Bwana iliyo kuu na itishayo.
Joël 2.10 Apocalypse 6.12-6.13 Malachie 4.5 Matthieu 24.29 Esaïe 13.9-13.10
32 Na itakuwa ya kwamba mtu awaye yote atakayeliita jina la Bwana ataponywa; kwa kuwa katika mlima Sayuni na katika Yerusalemu watakuwako watu watakaookoka, kama Bwana alivyosema; na katika mabaki, hao awaitao Bwana.
Abdias 1.17 Esaïe 46.13 Romains 9.27 Jérémie 31.7 Esaïe 11.11

Cette Bible est dans le domaine public.