Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Exode 12.10
Bible en Swahili de l’est


Institution de la Pâque

1 Bwana akanena na Musa na Haruni katika nchi ya Misri, akawaambia,
2 Mwezi huu utakuwa mwanzo wa miezi kwenu; utakuwa ni mwezi wa kwanza wa mwaka kwenu.
Deutéronome 16.1 Exode 13.4 Exode 23.15 Exode 34.18 Nombres 28.16
3 Semeni na mkutano wote wa Israeli, mkawaambie, Siku ya kumi ya mwezi huu kila mtu atatwaa mwana-kondoo, kwa hesabu ya nyumba ya baba zao, mwana-kondoo kwa watu wa nyumba moja;
Exode 20.19 Josué 7.14 2 Chroniques 35.7 Jean 1.29 Nombres 1.1-1.54
4 na ikiwa watu wa nyumba ni wachache kwa mwana-kondoo, basi yeye na jirani yake aliye karibu na nyumba yake na watwae mwana-kondoo mmoja, kwa kadiri ya hesabu ya watu; kwa kadiri ya ulaji wa kila mtu, ndivyo mtakavyofanya hesabu yenu kwa yule mwana-kondoo.
5 Mwana-kondoo wenu atakuwa hana ila, mume wa mwaka mmoja; mtamtwaa katika kondoo au katika mbuzi.
Deutéronome 17.1 Hébreux 9.13-9.14 1 Pierre 1.18-1.19 Lévitique 23.12 Malachie 1.14
6 Nanyi mtamweka hata siku ya kumi na nne ya mwezi ule ule; na kusanyiko lote la mkutano wa Israeli watamchinja jioni.
Lévitique 23.5 Exode 16.12 Nombres 28.16 Nombres 9.11 2 Chroniques 30.15-30.18
7 Nao watatwaa baadhi ya damu yake na kuitia katika miimo miwili na katika kizingiti cha juu, katika zile nyumba watakazomla.
Hébreux 11.28 Exode 12.22-12.23 Hébreux 9.22 Hébreux 9.13-9.14 Hébreux 10.29
8 Watakula nyama yake usiku ule ule, imeokwa motoni, pamoja na mkate usiotiwa chachu; tena pamoja na mboga zenye uchungu.
Exode 34.25 Deutéronome 16.7 Exode 13.3 Deutéronome 16.3-16.4 Nombres 9.11-9.12
9 Msiile mbichi, wala ya kutokoswa majini, bali imeokwa motoni; kichwa chake pamoja na miguu yake, na nyama zake za ndani.
Exode 12.8 Deutéronome 16.7 Lamentations 1.13
10 Wala msisaze kitu chake cho chote hata asubuhi, bali kitu kitakachosalia hata asubuhi mtakichoma kwa moto.
Exode 23.18 Exode 34.25 Lévitique 22.30 Exode 29.34 Lévitique 7.15-7.17
11 Tena mtamla hivi; mtakuwa mmefungwa viuno vyenu, mmevaa viatu vyenu miguuni, na fimbo zenu mikononi mwenu; nanyi mtamla kwa haraka; ni pasaka ya Bwana.
Ephésiens 6.15 Exode 12.27 Lévitique 23.5 1 Pierre 1.13 Luc 12.35
12 Maana nitapita kati ya nchi ya Misri usiku huo, nami nitawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, wa mwanadamu na wa mnyama; nami nitafanya hukumu juu ya miungu yote ya Misri; Mimi ndimi Bwana.
Nombres 33.4 Exode 6.2 Exode 12.23 Esaïe 19.1 Psaumes 82.1
13 Na ile damu itakuwa ishara kwenu katika zile nyumba mtakazokuwamo; nami nitakapoiona ile damu, nitapita juu yenu, lisiwapate pigo lo lote likawaharibu, nitakapoipiga nchi ya Misri.
Hébreux 11.28 1 Jean 1.7 Genèse 17.11 1 Thessaloniciens 1.10 Josué 2.12
14 Na siku hii itakuwa ukumbusho kwenu, nanyi mtaifanya iwe sikukuu kwa Bwana; mtaifanya iwe sikukuu katika vizazi vyenu vyote, kwa amri ya milele
Exode 13.9-13.10 Exode 12.17 2 Rois 23.21 Exode 12.24 Exode 12.43
15 Mtakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba; siku hiyo ya kwanza mtaondoa chachu yote isiwe katika nyumba zenu kabisa; kwa kuwa mtu ye yote atakayekula mkate uliochachwa tangu siku hiyo ya kwanza hata siku ya saba, nafsi hiyo atakatiliwa mbali na Israeli.
Deutéronome 16.3 Exode 23.15 Nombres 9.13 Genèse 17.14 Exode 34.18
16 Siku ya kwanza kutakuwa kwenu na kusanyiko takatifu, na siku ya saba kutakuwa kusanyiko takatifu; haitafanywa kazi yo yote katika siku hizo, isipokuwa kwa hiyo ambayo kila mtu hana budi kula, hiyo tu ifanyike kwenu.
Nombres 28.18 Lévitique 23.7-23.8 Nombres 28.25 Exode 16.5 Lévitique 23.24-23.25
17 Nanyi mtaitunza ile sikukuu ya mikate isiyochachwa; kwa kuwa katika siku iyo hiyo mimi nimeyatoa majeshi yenu katika nchi ya Misri; kwa hiyo mtaitunza siku hiyo katika vizazi vyenu vyote, kwa amri ya milele.
Exode 13.3 Exode 7.5 Nombres 20.16 Exode 12.41 Exode 13.8
18 Mwezi wa kwanza, siku ya mwezi kumi na nne, wakati wa jioni, mtakula mikate isiyochachwa, hata siku ya mwezi ishirini na moja jioni.
Lévitique 23.5-23.8 Exode 12.15 Nombres 28.16-28.25 Exode 12.1-12.2
19 Muda wa siku saba isionekane chachu katika nyumba zenu kabisa; kwa kuwa mtu ye yote atakayekula hiyo iliyotiwa chachu, nafsi hiyo atakatiliwa mbali na mkutano wa Israeli, akiwa mwenye kukaa hali ya ugeni, au akiwa mtu aliyezaliwa katika nchi.
Exode 12.15 Exode 12.48 Exode 23.15 Exode 12.43 Deutéronome 16.3
20 Msile kitu chochote kilichochachwa; mtakula mikate isiyochachwa katika makao yenu yote.
21 Hapo ndipo Musa akawaita wazee wa Israeli, na kuwaambia, Nendeni, mkajitwalie wana-kondoo kama jamaa zenu zilivyo mkamchinje pasaka.
Exode 12.3 Marc 14.12-14.16 Exode 3.16 2 Chroniques 35.5-35.6 Nombres 9.2-9.5
22 Nanyi twaeni tawi la hisopu, mkalichovye katika ile damu iliyo bakulini na kukipiga kizingiti cha juu, na miimo miwili ya mlango, kwa hiyo damu iliyo katika bakuli; tena mtu ye yote miongoni mwenu asitoke mlangoni mwa nyumba yake hata asubuhi.
Hébreux 11.28 Hébreux 9.19 Nombres 19.18 Exode 12.7 Psaumes 51.7
23 Kwa kuwa Bwana atapita ili awapige hao Wamisri; na hapo atakapoiona hiyo damu katika kizingiti cha juu, na katika ile miimo miwili, Bwana atapita juu ya mlango, wala hatamwacha mwenye kuharibu aingie nyumbani mwenu kuwapiga ninyi.
Apocalypse 7.3 Hébreux 11.28 Exode 12.12-12.13 1 Corinthiens 10.10 Apocalypse 9.4
24 Nanyi mtalitunza jambo hili kuwa ni amri kwako na kwa wanao milele.
Exode 12.14 Genèse 17.8-17.10
25 Itakuwa hapo mtakapoifikilia hiyo nchi, Bwana atakayowapa, kama alivyoahidi, ndipo mtakapoushika utumishi huu.
Exode 3.17 Exode 3.8 Deutéronome 12.8-12.9 Deutéronome 4.5 Psaumes 105.44-105.45
26 Kisha itakuwa, hapo watoto wenu watakapowauliza, N’nini maana yake utumishi huu kwenu?
Exode 13.14-13.15 Deutéronome 32.7 Josué 4.6-4.7 Josué 4.21-4.24 Psaumes 78.3-78.6
27 Ndipo mtawaambia, Ni dhabihu ya pasaka ya Bwana, kwa kuwa alipita juu ya nyumba za wana wa Israeli huko Misri, hapo alipowapiga Wamisri, akaziokoa nyumba zetu. Hao watu wakainama vichwa na kusujudia.
Exode 12.11 Exode 4.31 Exode 34.25 Deutéronome 16.2 Exode 12.23
28 Basi wana wa Israeli wakaenda na kufanya mambo hayo; vile vile kama Bwana alivyowaamuru Musa na Haruni, ndivyo walivyofanya.
Hébreux 11.28

Fléau n° 10 : la mort des aînés

29 Hata ikawa, usiku wa manane Bwana akawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, tangu mzaliwa wa kwanza wa Farao aliyeketi katika kiti chake cha enzi, hata mzaliwa wa kwanza wa mtu aliyefungwa katika nyumba ya wafungwa; na wazaliwa wa kwanza wote wa wanyama.
Exode 4.23 Psaumes 78.51 Nombres 33.4 Psaumes 135.8 Psaumes 136.10
30 Farao akaondoka usiku, yeye na watumishi wake wote, na Wamisri wote; pakawa na kilio kikuu katika Misri; maana hapakuwa na nyumba hata moja asimokufa mtu.
Exode 11.6 Amos 5.17 Matthieu 25.6 Proverbes 21.13 Jacques 2.13
31 Akawaita Musa na Haruni usiku, akasema, Ondokeni tokeni katika watu wangu, ninyi na wana wa Israeli; enendeni, kamtumikieni Bwana kama mlivyosema.
Exode 10.9 Psaumes 105.38 Exode 3.19-3.20 Exode 10.29-11.1 Exode 11.8
32 Twaeni kondoo zenu na ng’ombe zenu kama mlivyosema, enendeni zenu, mkanibariki mimi pia.
Exode 10.26 Exode 9.28 Genèse 27.38 Exode 10.9 Genèse 27.34
33 Wamisri nao wakawahimiza watu, kuwatoa katika nchi kwa haraka, maana walisema, Tumekwisha kufa sote.
Psaumes 105.38 Exode 11.1 Nombres 17.12-17.13 Genèse 20.3
34 Watu wakauchukua unga wa mikate yao kabla haijatiwa chachu, na vyombo vyao vya kukandia wakavitia ndani ya nguo zao mabegani.
Exode 8.3
35 Wana wa Israeli wakafanya kama neno lile la Musa; wakataka kwa Wamisri vyombo vya fedha na vyombo vya dhahabu, na mavazi.
Exode 11.2-11.3 Genèse 15.14 Exode 3.21-3.22 Psaumes 105.37
36 Bwana akawajalia kupendelewa na Wamisri hata wakawapa kila walichokitaka. Nao wakawateka Wamisri nyara.
Exode 11.3 Genèse 39.21 Psaumes 105.37 Exode 3.21-3.22 Genèse 15.14

Départ de l’Égypte et instructions pour la Pâque

37 Wana wa Israeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi, walipata hesabu yao kama watu sita mia elfu watu waume waliokwenda kwa miguu, bila kuhesabu watoto.
Nombres 33.5 Nombres 1.46 Nombres 11.21 Nombres 33.3 Exode 38.26
38 Na kundi kubwa la watu waliochangamana mno wakakwea pamoja nao; na kondoo na ng’ombe, wanyama wengi sana.
Nombres 11.4 Zacharie 8.23
39 Nao wakaoka mikate isiyochachwa ya ule unga waliouchukua walipotoka Misri, maana, haukutiwa chachu, kwa sababu walitolewa watoke Misri, wasiweze kukawia, nao walikuwa hawajajifanyia tayari chakula.
Exode 11.1 Exode 6.1 Exode 12.31-12.33
40 Basi wana wa Israeli kukaa kwao, maana, muda waliokaa ndani ya Misri, ulikuwa ni miaka mia nne na thelathini.
Genèse 15.13 Actes 7.6 Genèse 12.1-12.3 Actes 13.17 Hébreux 11.9
41 Ilikuwa mwisho wa miaka hiyo mia nne na thelathini, ilikuwa siku ile ile, ya kwamba majeshi yote ya Bwana yalitoka nchi ya Misri.
Daniel 9.24 Exode 12.51 Actes 1.7 Psaumes 102.13 Josué 5.14
42 Ni usiku wa kuangaliwa sana mbele za Bwana kwa sababu ya kuwatoa katika nchi ya Misri; huu ndio usiku wa Bwana, ambao wapasa kuangaliwa sana na wana wa Israeli wote katika vizazi vyao.
Deutéronome 16.1-16.6 Exode 12.14 Exode 13.10
43 Bwana akawaambia Musa na Haruni, Amri ya pasaka ni hii; mtu mgeni asimle;
Exode 12.48 Nombres 9.14 Lévitique 22.10 Exode 12.11 Ephésiens 2.12
44 lakini mtumishi wa mtu awaye yote aliyenunuliwa kwa fedha, ukiisha kumtahiri, ndipo hapo atamla pasaka.
Genèse 17.12-17.13 Genèse 17.23
45 Akaaye kwenu hali ya ugeni, na mtumishi aliyeajiriwa, wasimle pasaka.
Lévitique 22.10 Ephésiens 2.12
46 Na aliwe ndani ya nyumba moja; usiichukue nje ya nyumba nyama yake yo yote; wala msivunje mfupa wake uwao wote.
Nombres 9.12 Jean 19.36 Jean 19.33 1 Corinthiens 12.12 Ephésiens 2.19-2.22
47 Na wafanye jambo hili mkutano wa Israeli wote.
Exode 12.6 Nombres 9.13 Exode 12.3
48 Na mgeni atakapoketi pamoja nawe, na kupenda kumfanyia Bwana pasaka, waume wake wote na watahiriwe, ndipo hapo akaribie na kufanya pasaka; naye atakuwa mfano mmoja na mtu aliyezaliwa katika nchi; lakini mtu ye yote asiyetahiriwa asimle.
Nombres 9.14 Exode 12.43 Colossiens 3.11 Nombres 15.15-15.16 Genèse 17.12
49 Sheria ni hiyo moja kwa mtu aliyezaliwa kwenu, na kwa mgeni akaaye kati yenu ugenini.
Nombres 15.15-15.16 Nombres 15.29 Lévitique 24.22 Nombres 9.14 Galates 3.28
50 Ndivyo walivyofanya wana wa Israeli wote; kama Bwana alivyowaagiza Musa na Haruni, ndivyo walivyofanya.
Exode 7.4 Jean 13.17 Apocalypse 22.15 Deutéronome 4.1-4.2 Jean 2.5
51 Ilikuwa siku ile ile moja, Bwana akawatoa wana wa Israeli katika nchi ya Misri kwa majeshi yao.
Exode 12.41 Exode 6.26

Cette Bible est dans le domaine public.