Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

2 Samuel 22.3
Bible en Swahili de l’est


Cantique de délivrance de David

1 Basi Daudi akamwambia Bwana maneno ya wimbo huu, siku ile Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake zote, na mkononi mwa Sauli;
Exode 15.1 Juges 5.1 Esaïe 12.1-12.6 1 Samuel 25.29 2 Corinthiens 1.10
2 akasema, Bwana ndiye jabali langu, na ngome yangu, na mwokozi wangu, naam, wangu;
Psaumes 71.3 Psaumes 31.3 Psaumes 18.2-18.50 Psaumes 144.2 Psaumes 91.2
3 Mungu wa mwamba wangu, nitamwamini yeye; Ngao yangu, na pembe ya wokovu wangu, mnara wangu, na makimbilio yangu; Mwokozi wangu, waniokoa na jeuri.
Psaumes 9.9 Genèse 15.1 Esaïe 32.2 Psaumes 46.7 Psaumes 46.11
4 Nitamwita Bwana astahiliye kusifiwa; Hivyo nitaokoka na adui zangu.
Romains 10.13 Psaumes 48.1 Psaumes 96.4 Psaumes 18.3 Psaumes 50.15
5 Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka, Mafuriko ya uovu yakanitia hofu.
Psaumes 69.14-69.15 Jonas 2.3 Esaïe 59.19 Psaumes 18.4 Apocalypse 12.15-12.16
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka; Mitego ya mauti ikanikabili.
Psaumes 116.3 Job 36.8 Jonas 2.2 Proverbes 13.14 Psaumes 140.5
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, Naam, nikamlalamikia Mungu wangu;
Psaumes 120.1 Psaumes 116.4 Psaumes 18.6 Psaumes 34.6 Jonas 2.4
8 Ndipo nchi ilipotikisika na kutetemeka, Misingi ya mbinguni ikasuka-suka Na kutikisika, kwa sababu alikuwa na ghadhabu.
Psaumes 97.4 Juges 5.4 Job 26.11 Psaumes 77.18 Matthieu 28.2
9 Kukapanda moshi kutoka puani mwake, Moto ukatoka kinywani mwake ukala; Makaa yakawashwa nao.
Hébreux 12.29 Job 4.9 Psaumes 18.15 2 Samuel 22.13 Esaïe 30.33
10 Aliziinamisha mbingu akashuka; Kukawa na giza kuu chini ya miguu yake.
1 Rois 8.12 Psaumes 97.2 Exode 20.21 Psaumes 144.5 Luc 23.44-23.45
11 Akapanda juu ya kerubi akaruka; Naam, alionekana juu ya mabawa ya upepo.
Psaumes 104.3 Psaumes 68.17 Exode 25.19 Genèse 3.24 Ezéchiel 9.3
12 Akafanya giza hema zake za kumzunguka, Makusanyiko ya maji, mawingu makuu ya mbinguni.
2 Samuel 22.10 Psaumes 97.2 Job 36.29 Psaumes 18.11-18.12 Psaumes 27.5
13 Toka mwangaza uliokuwa mbele zake Makaa ya moto yakawashwa.
2 Samuel 22.9
14 Bwana alipiga radi toka mbinguni, Naye Aliye juu akaitoa sauti yake.
1 Samuel 2.10 Job 37.2-37.5 Ezéchiel 10.5 1 Samuel 7.10 Psaumes 77.16-77.19
15 Akapiga mishale, akawatawanya; Umeme, naye akawatapanya.
Deutéronome 32.23 Josué 10.10 Habakuk 3.11 Psaumes 18.14 Psaumes 7.12-7.13
16 Ndipo ilipoonekana mikondo ya bahari, Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa, Kwa kukemea kwake Bwana, Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwake.
Nahum 1.4 Psaumes 106.9 Psaumes 74.1 Job 38.11 2 Samuel 22.9
17 Alipeleka kutoka juu, akanishika; Akanitoa katika maji mengi;
Psaumes 144.7 Psaumes 124.4-124.5 Psaumes 130.1 Exode 2.10 Psaumes 93.3-93.4
18 Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu, Na wale walionichukia; Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi.
2 Corinthiens 1.10 Psaumes 56.9 2 Timothée 4.17 Psaumes 3.7 2 Samuel 22.1
19 Walinikabili siku ya msiba wangu; Lakini Bwana alikuwa tegemeo langu.
Psaumes 118.10-118.13 Psaumes 23.4 1 Samuel 23.26-23.27 Psaumes 71.20-71.21 1 Samuel 19.11-19.17
20 Akanitoa akanipeleka panapo nafasi; Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami.
2 Samuel 15.26 Psaumes 31.8 Psaumes 118.5 Psaumes 22.8 Psaumes 149.4
21 Bwana alinitendea sawasawa na haki yangu; Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa.
1 Samuel 26.23 Psaumes 24.4 1 Rois 8.32 Psaumes 7.8 Job 17.9
22 Maana nimezishika njia za Bwana, Wala sikumwasi Mungu wangu.
Proverbes 8.32 Genèse 18.19 Psaumes 128.1 Psaumes 119.1 Psaumes 125.5
23 Maana hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu; Na kwa habari za amri zake, sikuziacha.
Psaumes 119.30 Psaumes 119.102 Psaumes 119.128 Psaumes 119.13 Jean 15.14
24 Nami nalikuwa mkamilifu kwake, Nikajilinda na uovu wangu.
Genèse 6.9 Job 1.1 Genèse 17.1 Psaumes 84.11 Proverbes 4.23
25 Basi Bwana amenilipa sawasawa na haki yangu; Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.
2 Samuel 22.21 Romains 2.7-2.8 2 Corinthiens 5.10 Proverbes 5.21 Esaïe 3.10
26 Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhili Kwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;
Matthieu 5.7 Jacques 2.13
27 Kwake ajitakasaye utajionyesha kuwa mtakatifu; Na kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi.
Matthieu 5.8 Psaumes 18.26 Esaïe 45.9 Deutéronome 28.58-28.61 Lévitique 26.23-26.28
28 Na watu wanaoonewa wewe utawaokoa; Ila macho yako ni juu ya wenye kiburi, uwadhili.
Psaumes 72.12-72.13 Esaïe 5.15 Esaïe 2.11-2.12 Exode 3.7-3.8 Esaïe 2.17
29 Kwa kuwa wewe u taa yangu, Ee Bwana; Na Bwana ataniangazia giza langu.
Psaumes 27.1 Job 29.3 Apocalypse 21.23 Psaumes 4.6 Jean 8.12
30 Maana kwa msaada wako nafuatia jeshi; Kwa msaada wa Mungu wangu naruka ukuta.
Psaumes 18.29 Philippiens 4.13 Romains 8.37 Psaumes 118.10-118.12
31 Mungu njia yake ni kamilifu; Ahadi ya Bwana imehakikishwa; Yeye ndiye ngao yao Wote wanaomkimbilia.
Deutéronome 32.4 Proverbes 30.5 Matthieu 5.48 Psaumes 119.140 Psaumes 12.6
32 Maana ni nani aliye Mungu, ila Bwana? Ni nani aliye mwamba, ila Mungu wetu?
1 Samuel 2.2 Esaïe 45.21 Jérémie 10.16 Jérémie 10.6-10.7 Deutéronome 32.39
33 Mungu ndiye ngome yangu yenye nguvu; Naye huwaongoza wakamilifu katika njia yake.
Esaïe 41.10 Psaumes 119.1 2 Samuel 22.2 Psaumes 101.2 Hébreux 13.21
34 Huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu; Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.
Deutéronome 32.13 Habakuk 3.19 Esaïe 58.14 2 Samuel 2.18 Esaïe 33.16
35 Ananifundisha mikono yangu vita; Hata mikono yangu yaupinda upinde wa shaba.
Psaumes 144.1 Psaumes 18.33-18.34 Ezéchiel 39.9-39.10 Psaumes 46.9 Ezéchiel 39.3
36 Nawe umenipa ngao ya wokovu wako; Na unyenyekevu wako umenikuza.
Ephésiens 6.16 Genèse 22.17 Psaumes 18.35 Genèse 15.1 Genèse 12.2
37 Umezifanyizia nafasi hatua zangu, Wala miguu yangu haikuteleza.
Proverbes 4.12 Psaumes 17.5 Psaumes 18.36 Psaumes 94.18 Psaumes 4.1
38 Nimewafuatia adui zangu, na kuwaangamiza; Wala sikurudi nyuma hata walipokomeshwa.
2 Samuel 8.13-8.14 Romains 8.37 2 Samuel 8.1-8.2 2 Samuel 10.14 Psaumes 21.8-21.9
39 Nami nimewakomesha na kuwapiga-piga wasiweze kusimama; Naam, wameanguka chini ya miguu yangu.
Malachie 4.3 Psaumes 110.5-110.6 Psaumes 118.10-118.12 Malachie 4.1 Psaumes 110.1
40 Maana umenifunga mshipi wa nguvu kwa vita; Umenitiishia chini yangu walioniondokea.
Psaumes 44.5 Colossiens 1.11 Psaumes 18.39 1 Samuel 17.49-17.51 Esaïe 60.14
41 Naam, adui zangu umewafanya wanipe visogo, Ili niwakatilie mbali wanaonichukia.
Exode 23.27 Josué 10.24 Psaumes 18.40-18.41 2 Thessaloniciens 1.8-1.9 Luc 19.14
42 Walitazama, lakini hakuna wa kuokoa; Walimwita Bwana, lakini hakuwajibu.
Esaïe 1.15 1 Samuel 28.6 Michée 3.4 Proverbes 1.28 Ezéchiel 20.3
43 Ndipo nikawaponda kama mavumbi ya nchi, Nikawakanyaga kama matope ya njiani, nikawatawanya.
Michée 7.10 Esaïe 10.6 2 Rois 13.7 Zacharie 10.5 Luc 21.24
44 Nawe umeniokoa na mashindano ya watu wangu; Umenihifadhi niwe kichwa cha mataifa; Watu nisiowajua watanitumikia.
2 Samuel 8.1-8.14 Esaïe 55.5 2 Samuel 3.1 Deutéronome 28.13 2 Samuel 19.9
45 Wageni watanijia wakinyenyekea; Kwa kusikia tu habari zangu, Mara watanitii.
Psaumes 81.15 Psaumes 66.3 Deutéronome 33.29 Esaïe 56.3 Esaïe 56.6
46 Wageni nao watatepetea, Watatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Michée 7.17 Amos 9.3 Esaïe 2.19 Jacques 1.11 Esaïe 2.21
47 Bwana ndiye aliye hai; Na ahimidiwe mwamba wangu; Na atukuzwe Mungu wa mwamba wa wokovu wangu;
Psaumes 89.26 Deutéronome 32.39-32.40 Job 19.25 2 Samuel 22.3 Luc 1.47
48 Naam, Mungu anipatiaye kisasi, Na kuwatweza watu chini yangu,
Psaumes 144.2 Psaumes 94.1 2 Samuel 18.19 1 Corinthiens 15.25 2 Samuel 18.31
49 Na kunileta nje nitoke kwa adui zangu; Naam, waniinua juu yao walioniinukia; Waniponya na mtu wa jeuri.
Psaumes 140.1 2 Samuel 5.12 Nombres 24.17-24.19 Nombres 24.7 Psaumes 52.1
50 Basi, Bwana, nitakushukuru kati ya mataifa, Nami nitaliimbia jina lako.
Romains 15.9 Psaumes 146.1-146.2 Psaumes 18.49 Psaumes 145.1-145.2 Esaïe 12.1-12.6
51 Ampa mfalme wake wokovu mkuu; Amfanyia fadhili masihi wake Daudi na mzao wake ,hata milele.
Psaumes 144.10 Psaumes 89.29 Psaumes 89.20 2 Samuel 7.12-7.13 Psaumes 18.50

Cette Bible est dans le domaine public.