Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Genèse 41.42
Bible en Swahili de l’est


Joseph devant le pharaon

1 Ikawa, mwisho wa miaka miwili mizima, Farao akaota ndoto; na tazama, amesimama kando ya mto.
Genèse 20.3 Job 33.15-33.16 Exode 4.9 Daniel 7.1-7.8 Deutéronome 11.10
2 Na tazama, ng’ombe saba wazuri, wanono, walipanda kutoka mtoni, wakajilisha manyasini.
Esaïe 19.6
3 Na tazama, ng’ombe saba wengine wakapanda nyuma yao kutoka mtoni, wabaya, wamekonda, wakasimama karibu na wale ng’ombe wengine ukingoni mwa mto.
Genèse 41.20-41.21 Genèse 41.4
4 Kisha hao ng’ombe wabaya waliokonda wakawala wale ng’ombe saba wazuri, wanono. Basi Farao akaamka.
1 Rois 3.15
5 Akalala, akaota ndoto mara ya pili. Tazama, masuke saba yalimea katika bua moja, makubwa, mema.
Deutéronome 32.14
6 Na tazama, masuke saba membamba, yamekaushwa na upepo wa mashariki, yakatokeza baada yao.
Ezéchiel 19.12 Osée 13.15 Ezéchiel 17.10
7 Kisha hayo masuke membamba saba yakayala yale masuke saba makubwa yaliyojaa. Basi Farao akaamka, kumbe! Ni ndoto tu.
Genèse 20.3 Genèse 37.5
8 Hata asubuhi roho yake ikafadhaika; akapeleka watu kuwaita waganga wote wa Misri, na watu wote wenye hekima walioko. Farao akawahadithia ndoto yake, wala hakuna aliyeweza kumfasiria Farao mambo hayo.
Daniel 4.7 Exode 7.22 Exode 7.11 Daniel 1.20 Esaïe 29.14
9 Basi mkuu wa wanyweshaji akamwambia Farao akisema, Nayakumbuka makosa yangu leo.
Genèse 40.14 Genèse 40.23 Genèse 40.1-40.3
10 Farao aliwakasirikia watumwa wake, akanitia nifungwe nyumbani mwa mkuu wa askari, mimi na mkuu wa waokaji.
Genèse 39.20 Genèse 40.2-40.3 Genèse 37.36
11 Tukaota ndoto usiku mmoja, mimi na yeye; kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake tukaota.
Genèse 40.5-40.8
12 Na huko pamoja nasi palikuwa na kijana; Mwebrania, mtumishi wa mkuu wa askari, tukamhadithia, naye akatufasiria ndoto zetu; akamfasiria kila mtu kama ilivyokuwa ndoto yake.
Genèse 37.36 Genèse 40.12-40.19 Genèse 39.1 Genèse 39.20
13 Ikawa, kama vile alivyotufasiria ndivyo ilivyotokea; mimi nalirudishwa katika kazi yangu, na yeye alitundikwa.
Ezéchiel 43.3 Genèse 40.12 Jérémie 1.10 Genèse 40.20-40.22
14 Ndipo Farao akapeleka watu, akamwita Yusufu, wakamleta upesi kutoka gerezani. Akanyoa, akabadili nguo zake, na kuingia kwa Farao.
Daniel 2.25 Psaumes 113.7-113.8 Exode 10.16 2 Samuel 19.24 2 Rois 25.29
15 Farao akamwambia Yusufu, Nimeota ndoto, wala hakuna awezaye kunifasiria; nami nimesikia habari zako, ya kwamba, usikiapo ndoto, waweza kuifasiri.
Daniel 5.16 Daniel 5.12 Psaumes 25.14 Genèse 41.9-41.13
16 Yusufu akamjibu Farao, akisema, Si mimi; Mungu atampa Farao majibu ya amani.
Genèse 40.8 Actes 3.12 2 Corinthiens 3.5 Daniel 2.47 Nombres 12.6
17 Farao akamwambia Yusufu, Katika ndoto yangu nalikuwa nikisimama ukingoni mwa mto;
18 na tazama, ng’ombe saba wanatoka mtoni, wanono, wazuri, wakajilisha manyasini.
Jérémie 24.5 Jérémie 24.8 Jérémie 24.1-24.3
19 Kisha, tazama, ng’ombe saba wengine wakapanda baada yao, dhaifu, wabaya sana, wamekonda; katika nchi yote ya Misri sijaona kama hao kwa udhaifu.
20 Na hao ng’ombe waliokonda, wabaya, wakawala wale ng’ombe saba wa kwanza, wale wanono.
21 Na walipokwisha kuwala haikutambulikana ya kwamba wamewala, bali wakaonekana wabaya kama kwanza. Basi nikaamka.
Esaïe 9.20 Psaumes 37.19 Apocalypse 10.9-10.10 Ezéchiel 3.3
22 Kisha nikaona katika ndoto yangu, na tazama, masuke saba yanatokeza katika bua moja, mema, yamejaa.
23 Na tazama, masuke saba membamba, dhaifu, yamekaushwa na upepo wa mashariki, yakatokeza baada yao.
2 Rois 19.26 Osée 8.7 Psaumes 129.6-129.7 Osée 13.15 Osée 9.16
24 Na hayo masuke dhaifu yakameza yale masuke saba mema. Nami nikawaambia hao waganga, wala hakuna aliyeweza kunionyesha maana yake.
Genèse 41.8 Daniel 4.7 Exode 8.19
25 Yusufu akamwambia Farao, Ndoto ya Farao ni moja; Mungu amemwonyesha Farao atakayoyafanya hivi karibu.
Daniel 2.45 Daniel 2.28-2.29 Apocalypse 4.1 Amos 3.7 Josué 11.6
26 Wale ng’ombe saba wema ni miaka saba; na yale masuke saba mema ni miaka saba. Ndoto ni moja.
Genèse 41.2 1 Jean 5.7 Genèse 41.29 Genèse 41.47 Genèse 41.53
27 Na wale ng’ombe saba, dhaifu, wabaya, waliopanda baada yao, ni miaka saba; na yale masuke saba matupu yaliyokaushwa na upepo wa mashariki, yatakuwa miaka saba ya njaa.
2 Rois 8.1 2 Samuel 24.19
28 Ndivyo nilivyomwambia Farao, ya kwamba Mungu amemwonyesha Farao atakayoyafanya hivi karibu.
Genèse 41.25 Genèse 41.16
29 Tazama, miaka saba ya shibe inakuja, katika nchi yote ya Misri.
Genèse 41.26 Genèse 41.46-41.47 Genèse 41.49
30 Kisha kutakuja miaka saba ya njaa baada yake; na shibe ile yote itasahauliwa katika nchi ya Misri, na njaa itaiharibu nchi.
Genèse 47.13 Genèse 41.54 Psaumes 105.16 Jacques 5.17 Genèse 41.51
31 Wala shibe ile haitajulikana katika nchi kwa sababu ya njaa inayokuja baadaye, maana itakuwa nzito sana.
Esaïe 24.20 1 Samuel 5.6
32 Na ndoto ya Farao kwa vile ilivyokuja mara mbili, ni kwa sababu neno hilo Mungu amelithibitisha, na Mungu atalitimiza upesi.
Nombres 23.19 Esaïe 46.10-46.11 2 Corinthiens 13.1 Matthieu 25.41 Esaïe 14.24-14.27
33 Basi, Farao na ajitafutie mtu wa akili na hekima amweke juu ya nchi ya Misri.
Exode 18.19-18.22 Deutéronome 1.13 Genèse 41.39 Daniel 4.27 Actes 6.3
34 Farao na afanye hivi, tena akaweke wasimamizi juu ya nchi, na kutwaa sehemu ya tano katika nchi ya Misri, katika miaka hii saba ya kushiba.
Proverbes 6.6-6.8 Job 5.20 2 Rois 11.11-11.12 Nombres 31.14 Luc 16.5
35 Na wakusanye chakula chote cha miaka hii myema ijayo, wakaweke akiba ya nafaka mkononi mwa Farao wakakilinde kuwa chakula katika miji.
Genèse 45.6-45.7 Genèse 41.56 Genèse 41.48-41.49 Exode 4.13
36 Na hicho chakula kitakuwa akiba ya nchi kwa ajili ya miaka hiyo saba ya njaa, itakayokuwa katika nchi ya Misri, nchi isiharibike kwa njaa.
Genèse 47.13-47.25

Joseph gouverneur de l’Égypte

37 Neno hilo likawa jema machoni pa Farao, na machoni pa watumwa wake wote.
1 Rois 21.2 Actes 7.10 Proverbes 25.11 Psaumes 105.19 Proverbes 10.20
38 Farao akawaambia watumwa wake, Tupate wapi mtu kama huyu, mwenye roho ya Mungu ndani yake?
Daniel 5.14 Daniel 4.18 Daniel 5.11 Job 32.8 Nombres 27.18
39 Farao akamwambia Yusufu, Kwa kuwa Mungu amekufahamisha hayo yote, hapana mwenye akili na hekima kama wewe.
Genèse 41.33 Genèse 41.28 Genèse 41.25 Genèse 41.16
40 Basi wewe utakuwa juu ya nyumba yangu, na kwa neno lako watu wangu watatawaliwa. Katika kiti cha enzi tu nitakuwa mkuu kuliko wewe.
Psaumes 105.21-105.22 Proverbes 22.29 Actes 7.10 1 Samuel 10.1 Genèse 39.4-39.6
41 Farao akamwambia Yusufu, Tazama, nimekuweka juu ya nchi yote ya Misri.
Daniel 6.3 Genèse 42.6 Philippiens 2.9-2.11 Genèse 39.22 Daniel 4.2-4.3
42 Farao akavua pete yake ya muhuri mkononi mwake, akaitia mkononi mwa Yusufu; akamvika mavazi ya kitani nzuri, na kumtia mkufu wa dhahabu shingoni mwake.
Daniel 5.29 Daniel 5.7 Esther 3.10 Daniel 5.16 Esther 8.2
43 Akampandisha katika gari lake la pili alilokuwa nalo. Na watu wakapiga kelele mbele yake, Pigeni magoti. Hivyo akamweka juu ya nchi yote ya Misri.
Genèse 45.8 Genèse 45.26 Genèse 42.6 Esther 6.8-6.9 Philippiens 2.10
44 Farao akamwambia Yusufu, Mimi ni Farao, na bila amri yako, mtu asiinue mkono wala mguu katika nchi yote ya Misri.
Psaumes 105.22 Exode 11.7
45 Farao akamwita Yusufu, Safenath-panea; akamwoza Asenathi, binti Potifera, kuhani wa Oni, kuwa mkewe Yusufu akaenda huko na huko katika nchi yote ya Misri.
Genèse 46.20 Ezéchiel 30.17 Actes 11.28 Exode 2.16 Genèse 14.18
46 Naye Yusufu alikuwa mwenye miaka thelathini, aliposimama mbele ya Farao, mfalme wa Misri. Yusufu akatoka mbele ya uso wa Farao, akapita katika nchi yote ya Misri.
1 Rois 12.6 Nombres 4.3 Genèse 37.2 Daniel 1.19 2 Samuel 5.4
47 Ikawa katika miaka ile saba ya shibe, nchi ikazaa kwa wingi.
Genèse 26.12 Psaumes 72.16
48 Akakusanya chakula chote cha miaka ile saba katika nchi ya Misri. Akaweka chakula katika miji; chakula cha mashamba yaliyouzunguka kila mji, akakiweka ndani yake.
Genèse 41.34-41.36 Genèse 47.21
49 Yusufu akakusanya nafaka kama mchanga wa pwani, nyingi mno, hata akaacha kuhesabu, maana ilikuwa haina hesabu.
Psaumes 78.27 Juges 7.12 Juges 6.5 Genèse 22.17 1 Samuel 13.5

Naissance de Manassé et d’Éphraïm

50 Kabla ya kuja miaka ya njaa, Yusufu akazaliwa wana wawili, ambao Asenathi, binti Potifera, kuhani wa Oni, alimzalia.
Genèse 46.20 Genèse 48.5 2 Samuel 8.18 Genèse 41.45
51 Yusufu akamwita jina lake yule aliyezaliwa kwanza, Manase, maana alisema, Mungu amenisahaulisha taabu zangu zote, na nyumba yote ya baba yangu.
Genèse 48.13-48.14 Esaïe 57.16 Psaumes 30.11 Proverbes 31.7 Genèse 48.5
52 Na wa pili akamwita jina lake Efraimu, maana alisema, Mungu amenipa uzazi katika nchi ya mateso yangu.
Genèse 49.22 Genèse 17.6 Genèse 50.23 Genèse 30.6-30.13 Psaumes 105.17-105.18
53 Miaka ile saba ya shibe ikaisha katika nchi ya Misri,
Luc 16.25 Genèse 41.29-41.31 Psaumes 73.20
54 ikaanza kuja miaka ile saba ya njaa, kama vile Yusufu alivyosema. Kukawa na njaa katika nchi zote, bali katika nchi yote ya Misri palikuwa na chakula.
Actes 7.11 Psaumes 105.16 Genèse 45.11 Genèse 41.30 Genèse 47.13
55 Na nchi yote ya Misri ilipoona njaa, watu walimlilia Farao awape chakula. Farao akawaambia Wamisri wote, Enendeni kwa Yusufu; atakavyowaambia, fanyeni.
Jérémie 14.1-14.6 Psaumes 105.20-105.22 Lamentations 4.3-4.10 Colossiens 1.19 2 Rois 6.25-6.29
56 Njaa ikawa katika dunia yote pia. Yusufu akazifungua ghala zote, akawauzia Wamisri. Njaa ikawa nzito katika nchi ya Misri.
Genèse 42.6 Actes 17.26 Zacharie 5.3 Esaïe 23.17 Genèse 47.14-47.24
57 Watu wa nchi zote wakaja Misri kwa Yusufu; ili wanunue nafaka; kwa sababu njaa imekuwa nzito katika dunia yote.
Genèse 41.56 Genèse 41.54 Genèse 42.5 Deutéronome 9.28 Genèse 50.20

Cette Bible est dans le domaine public.