Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Colossiens 3.5
Bible en Swahili de l’est


La vie nouvelle en Christ

1 Basi mkiwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu.
Romains 8.6 Matthieu 6.33 Matthieu 6.20 Luc 12.33 2 Corinthiens 4.18
2 Yafikirini yaliyo juu, siyo yaliyo katika nchi.
1 Chroniques 22.19 Matthieu 16.23 1 Jean 2.15-2.17 Colossiens 3.1 Romains 8.4-8.6
3 Kwa maana mlikufa, na uhai wenu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu.
Colossiens 2.20 Romains 6.2 Galates 2.20 Romains 8.2 Jean 5.21
4 Kristo atakapofunuliwa, aliye uhai wetu, ndipo na ninyi mtafunuliwa pamoja naye katika utukufu.
1 Jean 3.2 Philippiens 3.21 Jean 11.25 1 Corinthiens 15.43 1 Jean 2.28
5 Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;
Galates 5.19-5.21 Romains 8.13 1 Corinthiens 6.18 Romains 6.13 2 Corinthiens 12.21
6 kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu.
Ephésiens 5.6 Romains 1.18 Esaïe 57.4 Apocalypse 22.15 2 Pierre 2.14
7 Katika hayo ninyi nanyi mlitembea zamani, mlipoishi katika hayo.
Ephésiens 2.2 1 Corinthiens 6.11 1 Pierre 4.3-4.4 Tite 3.3 Romains 6.19-6.20
8 Lakini sasa yawekeni mbali nanyi haya yote, hasira, na ghadhabu, na uovu, na matukano, na matusi vinywani mwenu.
Ephésiens 4.29 Ephésiens 4.22 Ephésiens 5.4 Proverbes 29.22 Ephésiens 4.26

Les relations dans l’Église

9 Msiambiane uongo, kwa kuwa mmevua kabisa utu wa kale, pamoja na matendo yake;
Ephésiens 4.22 Ephésiens 4.25 Lévitique 19.11 Apocalypse 22.15 Romains 6.6
10 mkivaa utu mpya, unaofanywa upya upate ufahamu sawasawa na mfano wake yeye aliyeuumba.
Ephésiens 4.23-4.24 Ephésiens 2.10 Romains 12.2 Colossiens 3.12 2 Corinthiens 5.17
11 Hapo hapana Myunani wala Myahudi, kutahiriwa wala kutokutahiriwa, mgeni wala mshenzi, mtumwa wala mwungwana, bali Kristo ni yote, na katika yote.
Romains 10.12 1 Corinthiens 12.13 Galates 5.6 1 Corinthiens 7.19 Galates 3.28-3.29
12 Basi, kwa kuwa mmekuwa wateule wa Mungu, watakatifu wapendwao, jivikeni moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole, uvumilivu,
Ephésiens 4.32 Ephésiens 4.2 2 Pierre 1.5-1.8 1 Jean 4.19 Colossiens 3.10
13 mkichukuliana, na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.
Ephésiens 4.32 Marc 11.25 Ephésiens 4.2 Romains 15.1-15.2 Matthieu 6.14-6.15
14 Zaidi ya hayo yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.
Ephésiens 4.3 Ephésiens 5.2 1 Pierre 4.8 Romains 13.8 1 Timothée 1.5
15 Na amani ya Kristo iamue mioyoni mwenu; ndiyo mliyoitiwa katika mwili mmoja; tena iweni watu wa shukrani.
Jean 14.27 Philippiens 4.6-4.7 1 Thessaloniciens 5.18 Ephésiens 5.20 Colossiens 3.17
16 Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.
Psaumes 119.11 Ephésiens 5.19 Jean 15.7 Ephésiens 1.17 1 Jean 2.24
17 Na kila mfanyalo, kwa neno au kwa tendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu, mkimshukuru Mungu Baba kwa yeye.
1 Corinthiens 10.31 Colossiens 3.23 Proverbes 3.6 Ephésiens 5.20 1 Pierre 4.11

Les relations à la maison

18 Ninyi wake, watiini waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana.
Ephésiens 5.22-6.9 1 Corinthiens 11.3 1 Pierre 3.1-3.6 1 Timothée 2.12 Tite 2.4-2.5
19 Ninyi waume, wapendeni wake zenu msiwe na uchungu nao.
1 Pierre 3.7 Ephésiens 5.25 Genèse 2.23-2.24 Ephésiens 4.31 Ephésiens 5.28-5.29
20 Ninyi watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote; maana jambo hili lapendeza katika Bwana.
Exode 20.12 Tite 2.9 Ephésiens 5.24 Ephésiens 6.1-6.3 Matthieu 15.4-15.6
21 Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.
Ephésiens 6.4 Proverbes 3.12 1 Thessaloniciens 2.11 Psaumes 103.13 Proverbes 4.1-4.4
22 Ninyi watumwa, watiini hao ambao kwa mwili ni bwana zenu, katika mambo yote, si kwa utumwa wa macho, kama wajipendekezao kwa wanadamu, bali kwa unyofu wa moyo, mkimcha Bwana.
Colossiens 3.20 Luc 6.46 Ephésiens 6.5-6.7 1 Thessaloniciens 2.4 1 Timothée 6.1-6.2
23 Lo lote mfanyalo, lifanyeni kwa moyo, kama kwa Bwana, wala si kwa wanadamu,
Colossiens 3.17 Ephésiens 6.6-6.7 Romains 14.8 Ecclésiaste 9.10 1 Pierre 2.15
24 mkijua ya kuwa mtapokea kwa Bwana ujira wa urithi. Mnamtumikia Bwana Kristo.
Ephésiens 6.8 1 Corinthiens 7.22 Actes 20.32 Hébreux 10.35 Romains 4.4-4.5
25 Maana adhulumuye atapata mapato ya udhalimu wake, wala hakuna upendeleo.
Actes 10.34 Romains 2.11 Deutéronome 10.17 1 Thessaloniciens 4.6 2 Chroniques 19.7

Cette Bible est dans le domaine public.