Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Colossiens 2.5
Bible en Swahili de l’est


1 Maana nataka ninyi mjue jinsi ilivyo kuu juhudi yangu niliyo nayo kwa ajili yenu, na kwa ajili ya wale wa Laodikia, na wale wasioniona uso wangu katika mwili;
Colossiens 1.29 Philippiens 1.30 Colossiens 4.12-4.13 Apocalypse 1.11 Luc 22.44
2 ili wafarijiwe mioyo yao, wakiunganishwa katika upendo, wakapate utajiri wote wa kufahamu kwa hakika, wapate kujua kabisa siri ya Mungu, yaani, Kristo;
Colossiens 4.8 Colossiens 3.14 Ephésiens 6.22 Colossiens 1.27 Colossiens 1.15-1.17
3 ambaye ndani yake yeye hazina zote za hekima na maarifa zimesitirika.
1 Corinthiens 1.24 1 Corinthiens 1.30 Romains 11.33 2 Timothée 3.15-3.17 Proverbes 2.4
4 Nasema neno hili, mtu asije akawadanganya kwa maneno ya kuwashawishi.
Ephésiens 5.6 Romains 16.18-16.19 2 Timothée 2.16 2 Corinthiens 11.3 1 Jean 2.26
5 Maana nijapokuwa sipo kwa mwili, lakini nipo pamoja nanyi kwa roho, nikifurahi na kuuona utaratibu wenu na uthabiti wa imani yenu katika Kristo.
1 Pierre 5.9 1 Corinthiens 14.40 1 Corinthiens 16.13 1 Thessaloniciens 2.17 1 Thessaloniciens 3.8
6 Basi kama mlivyompokea Kristo Yesu, Bwana, enendeni vivyo hivyo katika yeye;
Colossiens 1.10 1 Thessaloniciens 4.1 1 Jean 2.6 2 Jean 1.8-1.9 Colossiens 3.17
7 wenye shina na wenye kujengwa katika yeye; mmefanywa imara kwa imani, kama mlivyofundishwa; mkizidi kutoa shukrani.
Ephésiens 3.17 Ephésiens 2.20-2.22 Colossiens 1.23 2 Thessaloniciens 2.17 Colossiens 1.12-1.13

L’œuvre de Christ et la liberté qui en découle

8 Angalieni mtu asiwafanye mateka kwa elimu yake ya bure na madanganyo matupu, kwa jinsi ya mapokeo ya wanadamu, kwa jinsi ya mafundisho ya awali ya ulimwengu, wala si kwa jinsi ya Kristo.
1 Timothée 6.20 Ephésiens 5.6 Colossiens 2.20 Romains 1.21-1.22 Galates 4.3
9 Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili.
Colossiens 1.19 Jean 1.14 Jean 10.30 1 Timothée 3.16 Jean 10.38
10 Na ninyi mmetimilika katika yeye aliye kichwa cha enzi yote na mamlaka.
Ephésiens 3.19 Colossiens 1.16-1.18 Ephésiens 1.20-1.23 Philippiens 2.9-2.11 1 Pierre 3.22
11 Katika yeye mmetahiriwa kwa tohara isiyofanyika kwa mikono, kwa kuuvua mwili wa nyama, kwa tohara ya Kristo.
Romains 2.29 Romains 6.6 Ephésiens 4.22 Philippiens 3.3 Actes 17.24
12 Mkazikwa pamoja naye katika ubatizo; na katika huo mkafufuliwa pamoja naye, kwa kuziamini nguvu za Mungu aliyemfufua katika wafu.
Romains 6.3-6.5 1 Pierre 3.21 Ephésiens 4.5 Romains 4.24 Actes 2.24
13 Na ninyi mlipokuwa mmekufa kwa sababu ya makosa yenu na kutokutahiriwa kwa mwili wenu, aliwafanya hai pamoja naye, akiisha kutusamehe makosa yote;
Ephésiens 2.1 1 Jean 1.7-1.9 Jacques 2.26 Psaumes 119.50 1 Corinthiens 15.36
14 akiisha kuifuta ile hati iliyoandikwa ya kutushitaki kwa hukumu zake, iliyokuwa na uadui kwetu; akaiondoa isiwepo tena, akaigongomea msalabani;
Hébreux 7.18 Ephésiens 2.14-2.16 Hébreux 10.8-10.9 1 Pierre 2.24 Hébreux 8.13
15 akiisha kuzivua enzi na mamlaka, na kuzifanya kuwa mkogo kwa ujasiri, akizishangilia katika msalaba huo.
Ephésiens 4.8 Hébreux 2.14 Esaïe 53.12 Matthieu 12.29 Jean 12.31-12.32
16 Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au sabato;
Romains 14.5-14.6 Galates 4.10 Romains 14.10 1 Chroniques 23.31 Romains 14.13-14.17
17 mambo hayo ni kivuli cha mambo yajayo; bali mwili ni wa Kristo.
Hébreux 10.1 Hébreux 8.5 Jean 1.17 Hébreux 9.9 Hébreux 4.1-4.11
18 Mtu asiwanyang’anye thawabu yenu, kwa kunyenyekea kwa mapenzi yake mwenyewe tu, na kuabudu malaika, akijitia katika maono yake na kujivuna bure, kwa akili zake za kimwili;
Colossiens 2.23 Colossiens 2.8 1 Timothée 1.7 Jacques 4.1-4.6 Daniel 11.38
19 wala hakishiki Kichwa, ambacho kwa yeye mwili wote ukiruzukiwa na kuungamanishwa kwa viungo na mishipa, hukua kwa maongeo yatokayo kwa Mungu.
Ephésiens 4.15-4.16 Job 19.9-19.12 Ephésiens 5.29 Romains 11.17 Jean 15.4-15.6
20 Basi ikiwa mlikufa pamoja na Kristo mkayaacha yale mafundisho ya awali ya ulimwengu, kwa nini kujitia chini ya amri, kama wenye kuishi duniani,
Galates 4.3 Colossiens 2.8 Colossiens 2.14 Colossiens 2.16 Galates 4.9-4.12
21 Msishike, msionje, msiguse;
1 Timothée 4.3 2 Corinthiens 6.17 Esaïe 52.11 Genèse 3.3
22 (mambo hayo yote huharibika wakati wa kutumiwa); hali mkifuata maagizo na mafundisho ya wanadamu?
Esaïe 29.13 Tite 1.14 1 Corinthiens 6.13 Marc 7.7-7.13 Matthieu 15.3-15.9
23 Mambo hayo yanaonekana kana kwamba yana hekima, katika namna ya ibada mliyojitungia wenyewe, na katika kunyenyekea, na katika kuutawala mwili kwa ukali; lakini hayafai kitu kwa kuzizuia tamaa za mwili.
Colossiens 2.18 1 Timothée 4.8 1 Timothée 4.3 Matthieu 23.27-23.28 Ephésiens 5.29

Cette Bible est dans le domaine public.