Fermer le panneau de recherche

Appuyez sur Entrée pour rechercher ou ESC pour annuler.

Actes 5.31
Bible en Swahili de l’est


1 Lakini mtu mmoja jina lake Anania, pamoja na Safira mkewe, aliuza mali,
Lévitique 10.1-10.3 Josué 6.1 Matthieu 13.47-13.48 2 Timothée 2.20 Jean 6.37
2 akazuia kwa siri sehemu ya thamani yake, mkewe naye akijua haya, akaleta fungu moja akaliweka miguuni pa mitume.
Actes 4.37 Malachie 1.14 Matthieu 23.5 2 Pierre 2.14-2.15 Matthieu 6.2-6.3
3 Petro akasema, Anania, kwa nini Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho Mtakatifu, na kuzuia kwa siri sehemu ya thamani ya kiwanja?
Actes 5.9 Jean 13.2 Jean 13.27 Luc 22.3 Apocalypse 12.9-12.11
4 Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali Mungu.
Actes 5.3 Exode 35.21-35.22 Actes 8.21-8.22 1 Chroniques 29.5 Psaumes 139.4
5 Anania aliposikia maneno haya akaanguka, akafa. Hofu nyingi ikawapata watu wote walioyasikia haya.
Actes 5.10-5.11 Actes 2.43 Josué 22.20 2 Rois 1.10-1.14 Apocalypse 11.13
6 Vijana wakaondoka, wakamtia katika sanda, wakamchukua nje, wakamzika.
Jean 19.40 2 Samuel 18.17 Lévitique 10.4-10.6 Deutéronome 21.23
7 Hata muda wa saa tatu baadaye mkewe akaingia, naye hana habari ya hayo yaliyotokea.
8 Petro akamjibu, Niambie, Mlikiuza kiwanja kwa thamani hiyo? Akasema, Ndiyo, kwa thamani hiyo.
Actes 5.2
9 Petro akamwambia, Imekuwaje hata mkapatana kumjaribu Roho wa Bwana? Angalia, miguu yao waliomzika mumeo ipo mlangoni, nao watakuchukua nje wewe nawe.
1 Corinthiens 10.9 Actes 5.3-5.4 Psaumes 78.56 Psaumes 95.8-95.11 Psaumes 78.18-78.20
10 Mara akaanguka miguuni pake akafa; wale vijana wakaingia wakamkuta amekufa, wakamchukua nje, wakamzika pamoja na mumewe.
Actes 5.5
11 Hofu nyingi ikawapata kanisa lote na watu wote walioyasikia haya.
Actes 5.5 Actes 19.17 1 Corinthiens 10.11-10.12 Hébreux 4.1 1 Pierre 1.17

Arrestation des apôtres

12 Na kwa mikono ya mitume zikafanyika ishara na maajabu mengi katika watu; nao wote walikuwako kwa nia moja katika ukumbi wa Sulemani;
Actes 3.11 Hébreux 2.4 Actes 1.14 Marc 16.20 2 Corinthiens 12.12
13 na katika wote wengine hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao; ila watu waliwaadhimisha;
Actes 2.47 Actes 4.21 1 Samuel 16.4-16.5 Esaïe 33.14 1 Rois 17.18
14 walioamini wakazidi kuongezeka kwa Bwana, wengi, wanaume na wanawake;
Actes 2.47 Actes 4.4 Actes 9.2 Actes 9.42 1 Corinthiens 11.11-11.12
15 hata ikawa katika njia kuu hutoa nje wagonjwa, na kuwaweka juu ya majamvi na magodoro, ili Petro akija, ngawa kivuli chake kimwangukie mmojawapo wao.
Matthieu 14.36 Actes 19.11-19.12 Matthieu 9.21 Jean 14.12
16 Nayo makutano ya watu wa miji iliyoko kandokando ya Yerusalemu wakakutanika, wakileta wagonjwa, nao walioudhiwa na pepo wachafu; nao wote wakaponywa.
Marc 16.17-16.18 Matthieu 4.24 Jacques 5.16 1 Corinthiens 12.9 Luc 5.17
17 Akaondoka Kuhani Mkuu na wote waliokuwa pamoja naye, (hao ndio walio wa madhehebu ya Masadukayo), wamejaa wivu,
Actes 17.5 Actes 13.45 Actes 7.9 Ecclésiaste 4.4 1 Samuel 18.12-18.16
18 wakawakamata mitume wakawaweka ndani ya gereza;
Actes 4.3 Luc 21.12 Actes 8.3 Hébreux 11.36 Actes 12.5-12.7
19 lakini malaika wa Bwana akafungua milango ya gereza usiku, akawatoa, akasema,
Actes 8.26 Actes 16.26 Actes 27.23 Psaumes 105.17-105.20 Psaumes 146.7
20 Enendeni mkasimame hekaluni mkawaambie watu maneno yote ya Uzima huu.
Jean 6.63 Jean 6.68 Jean 12.50 Jérémie 36.10 Exode 24.3
21 Nao waliposikia wakaenda alfajiri hekaluni, wakaanza kufundisha. Akaja Kuhani Mkuu nao waliokuwa pamoja naye, wakawakutanisha watu wa baraza, na wazee wote wa wana wa Israeli, wakatuma watu gerezani ili wawalete.
Jean 8.2 Actes 5.41 Luc 21.37-21.38 Luc 22.66 Actes 5.34
22 Hata watumishi walipofika hawakuwaona gerezani, wakarudi wakatoa habari,
23 wakisema, Gereza tumeikuta imefungwa salama, nao walinzi wamesimama mbele ya mlango; lakini tulipoufungua hatukukuta mtu ndani.
Lamentations 3.55-3.58 Jean 8.59 Psaumes 2.4 Daniel 3.11-3.25 Matthieu 28.12-28.15
24 Basi jemadari wa hekalu na wakuu wa makuhani waliposikia haya, wakaingiwa na shaka kwa ajili yao, litakuwaje jambo hilo.
Actes 4.1 Actes 5.26 Marc 4.30-4.32 Zacharie 6.12-6.13 Actes 2.12
25 Mtu mmoja akaja akawapasha habari ya kwamba, Watu wale mliowaweka gerezani wako ndani ya hekalu, wamesimama wakiwafundisha watu.
26 Ndipo yule jemadari akaenda pamoja na watumishi, wakawaleta, lakini si kwa nguvu, kwa maana waliogopa watu wasije wakawapiga kwa mawe.
Actes 5.13 Actes 4.21 Matthieu 21.26 Matthieu 14.5 Luc 22.2
27 Walipowaleta, wakawaweka katika baraza. Kuhani Mkuu akawauliza,
Matthieu 5.22 Actes 4.7 Luc 22.66 Actes 22.30-23.1 Actes 6.12
28 akisema, Je! Hatukuwaamuru ninyi kwa nguvu, msifundishe kwa jina hili? Nanyi, tazameni, mmeijaza Yerusalemu mafundisho yenu, na mnataka kuileta damu ya mtu yule juu yetu.
Matthieu 27.25 Actes 7.52 Actes 4.10-4.11 1 Rois 21.20 Amos 7.10
29 Petro na mitume wakajibu, wakisema, Imetupasa kumtii Mungu kuliko wanadamu.
Actes 4.19 Marc 7.7-7.9 1 Samuel 15.24 Genèse 3.17 Apocalypse 14.8-14.12
30 Mungu wa baba zetu alimfufua Yesu, ambaye ninyi mlimwua mkimtundika katika mti.
Actes 10.39 Galates 3.13 1 Pierre 2.24 Luc 1.55 Actes 4.10-4.11
31 Mtu huyo Mungu amemtukuza kwa mkono wake wa kuume, awe Mkuu na Mwokozi, awape Waisraeli toba na msamaha wa dhambi.
Actes 2.33 Luc 24.47 Luc 2.11 Actes 11.18 Hébreux 2.10
32 Na sisi tu mashahidi wa mambo haya, pamoja na Roho Mtakatifu ambaye Mungu amewapa wote wamtiio.
Actes 2.4 Jean 15.26-15.27 Hébreux 2.3-2.4 2 Corinthiens 13.1 Actes 10.39-10.41
33 Wao waliposikia wakachomwa mioyo yao; wakafanya shauri kuwaua.
Actes 7.54 Actes 2.37 Jean 15.20 Genèse 4.5-4.8 Luc 6.11
34 Lakini mtu mmoja, Farisayo, jina lake Gamalieli, mwalimu wa torati, mwenye kuheshimiwa na watu wote, akasimama katika baraza, akaamuru mitume wawekwe nje kitambo kidogo,
Actes 22.3 Luc 2.46 Luc 5.17 Actes 23.7-23.9 Psaumes 76.10
35 akawaambia, Enyi waume wa Israeli, jihadharini jinsi mtakavyowatenda watu hawa.
Matthieu 27.19 Jérémie 26.19 Actes 19.36 Actes 22.26
36 Kwa sababu kabla ya siku hizi aliondoka Theuda, akijidai ya kuwa yeye ni mtu mkuu, watu wapata mia nne wakashikamana naye; naye aliuawa na wote waliomsadiki wakatawanyika wakawa si kitu.
Actes 8.9 Actes 21.38 2 Thessaloniciens 2.3-2.7 Jude 1.16 Apocalypse 17.5
37 Baada ya mtu huyo aliondoka Yuda Mgalilaya, siku zile za kuandikiwa orodha, akawavuta watu kadha wa kadha nyuma yake, naye pia akapotea na wote waliomsadiki wakatawanyika.
Luc 2.1-2.2 Psaumes 9.15-9.16 Luc 13.1-13.2 Job 20.5-20.9 Matthieu 26.52
38 Basi sasa nawaambia, Jiepusheni na watu hawa, waacheni; kwa kuwa shauri hili au kazi hii ikiwa imetoka kwa binadamu, itavunjwa,
Matthieu 15.13 Lamentations 3.37 Job 5.12-5.14 1 Corinthiens 3.19 Esaïe 7.5-7.7
39 lakini ikiwa imetoka kwa Mungu hamwezi kuivunja; msije mkaonekana kuwa mnapigana na Mungu.
Proverbes 21.30 Actes 7.51 1 Corinthiens 1.25 Matthieu 16.18 Actes 11.17
40 Wakakubali maneno yake; nao walipowaita mitume, wakawapiga, wakawaamuru wasinene kwa jina lake Yesu; kisha wakawaacha waende zao.
Matthieu 10.17 Marc 13.9 Matthieu 23.34 Amos 2.12 Actes 4.17-4.21
41 Nao wakatoka katika ile baraza, wakifurahi kwa sababu wamehesabiwa kuwa wamestahili kuaibishwa kwa ajili ya Jina hilo.
Jean 15.21 1 Pierre 4.13-4.16 Jacques 1.2 Philippiens 1.29 Hébreux 10.34
42 Na kila siku, ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kuhubiri habari njema za Yesu kwamba ni Kristo.
Actes 2.46 Actes 8.35 Actes 20.20 2 Timothée 4.2 Ephésiens 4.20-4.21

Cette Bible est dans le domaine public.